Wazazi Mnaosomesha Watoto Shule za Private jifunzeni kufanya tathmini ya Pesa mnayowekeza katika Elimu hiyo na matokeo yake (Hawatazeekea Nyumbani)?

Wazazi Mnaosomesha Watoto Shule za Private jifunzeni kufanya tathmini ya Pesa mnayowekeza katika Elimu hiyo na matokeo yake (Hawatazeekea Nyumbani)?

Maelezo meng ila umeandika pumba na utumbo

Kila mtu anafamilia yake na kila mtu anawatoto wake na kila mtu anauwezo wake kipesa so acha uswahili komaa na familia yako familia za wengne waachie wenye familia zao

Hii kampeni ya kupinga EM imekua kubwa sana na sioni ata cha maana mnachopinga au kuhoji
 
Sio aajiriwe kuja kunisaidia bali nimejenga generational wealth (utajiri unaohamia kizazi kimoja kwenda kingine)
Nimetoa hapa mifano ya wahindi pia, alichoanza nacho babu kinakua katika mikono ya mwanae, mwanae naye anamrithisha mikoba mtoto wake na kila hatua inakuja na maendeleo makubwa zaidi
Wakati nyinyi ndugu zangu hapa mnakazana kumkaririsha mtoto tu yale ya darasani afu eti mnaiita hiyo bookish education ndio urithi (hopeless kabisa) wenzenu wahindi na waarabu hiyo elimu ni brush tu ya mtoto kujifunza skills za usimamiaji wa miradi ya familia (urithi ni rasiliamali za familia na sio elimu )
Familia kama za kina Azam, Asas na wengine tutazitoa wapi sisi waafrika kwa mentality ya aina hii; yaani mtoto anasoma akimaliza chuo akaajiriwe huko mbali kabisa na miradi Yako kama mzazi na aanze upya kwenye msoto kama wako; yaani unasomesha mtoto kwa 20M afu adi aje kujitegemea na kazi akapata unakuta uwezo wa kununua hata kiwanja ajibangaize tena miaka 5 tena kwa pesa anayozalisha usishangae akafanya kazi Posta huku anaishia chalinze
Rithisheni watoto mali na Biashara , hivi visingizio vya kusema mnawarithisha elimu ni umaskini tu
Hao wahindi na waarabu hawasomeshi watoto wao? Kwa taarifa yako hao matajiri unaowajua wanasomesha watoto wao kwenye shule bora za gharama. Mo Dewji kasoma IST na chuo Georgetown University. Unadhani kuitoa biashara ya milioni hadi ifike bilioni itawezekana kwa hiyo elimu duni unayotaka kuwapa wanao?
 
Nunua kiwanja hata Kisarawe au chanika huko, huyo mtoto hadi amalize chuo kiwanja hicho hicho ulichonunua hata milioni 2 utauza hata 20M
Una akili duni mno bro. Hujui kuna kitu kinaitwa inflation? Mpe mtoto elimu bora huenda akawa na mawazo makubwa zaidi kuliko hayo ya kwako ya kijima.
 
Hao wahindi na waarabu hawasomeshi watoto wao? Kwa taarifa yako hao matajiri unaowajua wanasomesha watoto wao kwenye shule bora za gharama. Mo Dewji kasoma IST na chuo Georgetown University. Unadhani kuitoa biashara ya milioni hadi ifike bilioni itawezekana kwa hiyo elimu duni unayotaka kuwapa wanao?

Elimu lazima iendane na uchumi wa mtu husika kama mzazi wa mtoto

Mo Dewji alisoma shule ya gharama na pia alirithi biashara kubwa. ( alipewa elimu inayoondena na
biashara za familia yao ili aweze kuziendesha),

hakupelekwa IST na Georgetown kwa ajili ya kuzunguka na bahasha kugombea ajira za watu.

Mimi nadhani mtu ambae anasomesha mtu shule kwa gharama hafu hajaweka mazingira
yatakayo endena na hiyo elimu ya mwanae huyo anazingua.
unakuta Kuna Mtu anauza zake tu Viazi mbatata Sokoni pamoja na bidhaa zingine ndogondogo
ila yuko katika Vikundi vya Vicoba kama Saba hivi anawasomesha Watoto wake Shule za
Gharama wakati Yeye bado amepanga na hana hata Uwanja na Kwao shida hazibanduki.
 
Nampeleka mwanangu shule za EM Ili kumpa mazingira mazur ya kujifunza na uangalizi mzur si Kwa sababu aje aajiriwe serikalin hapana swala la ajira ni mapendekezo yangu mzaz nimuandaaje mwanangu anapokaribia kumaliza masomo yake mikakat ni mingi tofaut na hizo ajira
Kujifunza nn? Labda lugha ya kigeni kwa ufasaha, napo pana walakini.
Tusidanganyane.
 
Una akili duni mno bro. Hujui kuna kitu kinaitwa inflation? Mpe mtoto elimu bora huenda akawa na mawazo makubwa zaidi kuliko hayo ya kwako ya kijima.
Elimu Bora labda uwe na bajeti ya kumpeleka Feza au IST na sio hizi EM za kukaririshana ili kufaulu, pia Ushasema "huweza" , hivyo viwanja guaranteed; mwaga hizo pesa kwenye ardhi huku ukimpambania mwanao Saint Kayumba na tuition (tuition unaweza kuchukua Walimu hawahawa wa private) na ndani ya miaka 20 unakuwa na ubavu hata wa kumkabidhi mwanao cheki ya milioni 50 siku anaoa au kuolewa
Tatizo hapa naona ndugu zangu wala ishu sio elimu Bora bali uvivu na kutojiamini kwa mzazi kutake charge elimu ya mtoto wako
Aidha uchome 20 M afu mwisho wa siku azunguke na makaratasi kama kahaba kwenye ofisi za watu (tena akiwa anapishana na wenzake waliosoma Saint Kayumba ndani ya msululu huo huo ) au mpe double chance ya mafanikio kwa kuwekeza kwa kiasi kwenye elimu yake (narejea kwenye neno lako "huweza") wakati kiasi kingine kikiwa kimewekezwa guaranteed kabisa katika ardhi au uwekezeji mwingine wenye guarantee kubwa ya marejesho
 
Elimu Bora labda uwe na bajeti ya kumpeleka Feza au IST na sio hizi EM za kukaririshana ili kufaulu, pia Ushasema "huweza" , hivyo viwanja guaranteed; mwaga hizo pesa kwenye ardhi huku ukimpambania mwanao Saint Kayumba na tuition (tuition unaweza kuchukua Walimu hawahawa wa private) na ndani ya miaka 20 unakuwa na ubavu hata wa kumkabidhi mwanao cheki ya milioni 50 siku anaoa au kuolewa
Tatizo hapa naona ndugu zangu wala ishu sio elimu Bora bali uvivu na kutojiamini kwa mzazi kutake charge elimu ya mtoto wako
Aidha uchome 20 M afu mwisho wa siku azunguke na makaratasi kama kahaba kwenye ofisi za watu (tena akiwa anapishana na wenzake waliosoma Saint Kayumba ndani ya msululu huo huo ) au mpe double chance ya mafanikio kwa kuwekeza kwa kiasi kwenye elimu yake (narejea kwenye neno lako "huweza") wakati kiasi kingine kikiwa kimewekezwa guaranteed kabisa katika ardhi au uwekezeji mwingine wenye guarantee kubwa ya marejesho
Kama ada ya laki 8 inakushinda labda umwage mavi kupata hizo ardhi. Acha ku-justify umaskini wako ndugu. Elimu haina mbadala na kamwe haitakuwa na mbadala.
 
Ba
Katika kila jamii, elimu hupewa nafasi ya kipekee kama nyenzo ya kufanikisha maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla. Wazazi huwekeza kwa gharama kubwa kuhakikisha watoto wao wanapata elimu bora, wakiamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha bora. Lakini swali la msingi linabaki: Je, uwekezaji huu unatoa faida inayolingana na gharama zinazotumika?

Katika makala hii, nitachambua gharama za kumsomesha mtoto hadi chuo kikuu, nikiilinganisha na hali halisi ya soko la ajira nchini Tanzania. Pia, nitatoa tafakari mbadala kuhusu thamani ya ardhi kama uwekezaji, pamoja na mbinu ambazo mzazi anaweza kutumia kupunguza gharama za elimu bila kuathiri ubora wa maarifa anayoyapata mtoto wake.

GHARAMA ZA KUMSOMESHA MTOTO: TAKWIMU ZINASEMAJE?

Wazazi wengi hujitoa kwa hali na mali kugharamia elimu ya watoto wao. Kwa mujibu wa makadirio yafuatayo, mzazi anayemsomesha mtoto mmoja kutoka darasa la kwanza hadi chuo kikuu anahitaji angalau:

1. Elimu ya Msingi (Darasa la 1 - 7):

Tsh 800,000 kwa mwaka x 7 miaka = Tsh 5,600,000

2. Elimu ya Sekondari (Kidato cha 1 - 4):

Tsh 1,200,000 kwa mwaka x 4 miaka = Tsh 4,800,000

3. Elimu ya Juu ya Sekondari (Kidato cha 5 - 6):

Tsh 1,200,000 kwa mwaka x 2 miaka = Tsh 2,400,000

4. Chuo Kikuu (Mwaka wa 1 - 3):

Tsh 2,500,000 kwa mwaka x 3 miaka = Tsh 7,500,000

Jumla ya gharama kwa mtoto mmoja inakuwa Tsh 20,300,000, na kwa watoto watatu inafikia Tsh 60,900,000.

Lakini je, mzazi anayefanya uwekezaji huu ana uhakika wa kupata faida kupitia ajira ya mtoto wake baada ya kuhitimu?

HALI YA SOKO LA AJIRA: UHALISIA ULIOPO

Kwa mujibu wa takwimu za Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), mwaka wa masomo wa 2023/2024 uliona ongezeko la udahili wa wanafunzi wa shahada ya kwanza kufikia 186,289 (Mwananchi).

Hata hivyo, soko la ajira haliwezi kuwahudumia wote. Takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) zinaonyesha kuwa kila mwaka nafasi za kazi mpya serikalini na sekta binafsi hazizidi 50,000. Kwa hesabu rahisi:

Wahitimu wa vyuo kwa mwaka:
186,289

Nafasi za ajira zilizopo: 50,000

Wahitimu wasiopata ajira mara moja: ~136,289

Uwezekano wa kupata ajira mara moja: ~27%

Kwa maneno mengine, asilimia 73 ya wahitimu wa vyuo vikuu hawapati ajira mara moja.

Hili linaibua swali muhimu: Je, mzazi aliyelipa ada kwa miaka 16-20 anaweza kupata mrejesho wa uwekezaji wake ndani ya muda mfupi?

UWEKEZAJI MBADALA: THAMANI YA ARDHI JIJINI DAR ES SALAAM

Hebu tuchukulie mfano wa mzazi aliyekuwa akitumia wastani wa Tsh 3,000,000 kwa mwaka kwa mtoto mmoja katika elimu tangu miaka ya 1990s. Kama angewekeza pesa hii kwenye kununua viwanja jijini Dar es Salaam, leo hii thamani yake ingekuwa ya mamilioni.

Kwa mfano, mnamo 1995, viwanja katika maeneo kama Tegeta vilikuwa vinauzwa kwa kati ya Tsh 500,000 – 2,000,000. Leo hii, kiwanja cha ukubwa wa 1,200m² katika Mbweni kinauzwa kwa Tsh 85,000,000 (Jiji.co.tz).

Kwa maneno mengine, mzazi aliyenunua kiwanja miaka ya 1990s kwa Tsh 2,000,000 leo anaweza kuwa na mali yenye thamani ya zaidi ya Tsh 200,000,000.

Hii inaonyesha kuwa kuna uwezekano mkubwa wa mzazi kupata faida kubwa zaidi kwa kuwekeza katika ardhi badala ya kutegemea ajira za watoto wao kama njia ya kupata mrejesho wa gharama za elimu.

NJIA YA KUOKOA GHARAMA ZA ELIMU PASIPO KUPOTEZA UBORA

Je, kuna namna mzazi anaweza kumpa mtoto elimu bora kwa gharama nafuu?

Jibu ni ndiyo!

Njia mojawapo ni kumpeleka mtoto shule za serikali na kisha kuongeza maarifa kwa njia ya tuition.

Mfumo huu umefanikiwa katika nchi kama Kanada, ambako homeschooling na masomo ya ziada (tutoring) vimeongezeka kwa 36% kila mwaka, huku gharama ya elimu kwa mtoto mmoja ikiwa chini kwa 90% ukilinganisha na shule binafsi (Moe.go.tz).

Kwa hesabu rahisi, mzazi anaweza kutumia Tsh 120,000 kwa mwaka kwa tuition bora badala ya Tsh 1,200,000 kwa shule binafsi, hivyo kuokoa hadi Tsh 1,080,000 kwa mwaka kwa mtoto mmoja.

HITIMISHO: NI WAKATI WA KUHOJI UWEKEZAJI WETU KATIKA ELIMU

Hakuna anayepinga thamani ya elimu, lakini ni muhimu wazazi kuhoji kama njia wanazotumia kugharamia elimu zina manufaa makubwa kwa watoto na familia kwa ujumla.

Kwa kutumia shule za serikali pamoja na masomo ya ziada, mzazi anaweza kuokoa hadi 90% ya gharama za shule binafsi na kutumia fedha hizo kwa uwekezaji wa muda mrefu kama ardhi, biashara au hisa.

Uamuzi wa leo utaathiri maisha ya kesho. Je, ni busara kuwekeza zaidi ya Tsh 60,900,000 kwa watoto watatu bila uhakika wa faida, au ni heri kutumia kiasi hicho kwa uwekezaji wenye uhakika wa marejesho?
Badilisha headline ya uzi wako isomeke "JINSI YA KUFUGA POPOMA NA KUEPUKA KUPOTEZA PESA KWA KULIPA ADA YA KIJANA WAKO MZURI"
 
Elimu lazima iendane na uchumi wa mtu husika kama mzazi wa mtoto

Mo Dewji alisoma shule ya gharama na pia alirithi biashara kubwa. ( alipewa elimu inayoondena na
biashara za familia yao ili aweze kuziendesha),

hakupelekwa IST na Georgetown kwa ajili ya kuzunguka na bahasha kugombea ajira za watu.

Mimi nadhani mtu ambae anasomesha mtu shule kwa gharama hafu hajaweka mazingira
yatakayo endena na hiyo elimu ya mwanae huyo anazingua.
unakuta Kuna Mtu anauza zake tu Viazi mbatata Sokoni pamoja na bidhaa zingine ndogondogo
ila yuko katika Vikundi vya Vicoba kama Saba hivi anawasomesha Watoto wake Shule za
Gharama wakati Yeye bado amepanga na hana hata Uwanja na Kwao shida hazibanduki.
Yaani watu wana Vipaumbele vibovu sana, maofisini humu Kuna watu wanahangaika ada za mamilioni wakati hata hawajajenga
 
Kama ada ya laki 8 inakushinda labda umwage mavi kupata hizo ardhi. Acha ku-justify umaskini wako ndugu. Elimu haina mbadala na kamwe haitakuwa na mbadala.
Tatizo mna dharau sana, yaani waliosoma na kufanikiwa kupitia kayumba mnadhani sijui ni ushirikina
 
Tatizo mna dharau sana, yaani waliosoma na kufanikiwa kupitia kayumba mnadhani sijui ni ushirikina
Mimi nimesoma Kayumba mwanzo mwisho ila mzazi wangu hajawahi kuwa na akili za kipumbavu za kutaka nisisonge mbele kielimu ili nirithi vitu vyake. Kupitia elimu niliyopata hata mzazi anajivunia ninapomshauri kwenye shughuli zake. Na wala hajawahi kudai nimsaidie pesa ingawa huwa najiongeza na kumtumia. Ndugu maisha hayahitaji shortcut... vinginevyo utaendeleza tu generational poverty.
 
Mimi nimesoma Kayumba mwanzo mwisho ila mzazi wangu hajawahi kuwa na akili za kipumbavu za kutaka nisisonge mbele kielimu ili nirithi vitu vyake. Kupitia elimu niliyopata hata mzazi anajivunia ninapomshauri kwenye shughuli zake. Na wala hajawahi kudai nimsaidie pesa ingawa huwa najiongeza na kumtumia. Ndugu maisha hayahitaji shortcut... vinginevyo utaendeleza tu generational poverty.
Generational poverty mnaidumisha kwa kushindwa kukombolewa kifikra na hili jinamizi litawatafuna vizazi na vizazi
Kumpa mwanao investment kubwa ambayo guarantee ya return (kuajirika) ni chini ya 50% ni sawasawa Simba icheze na lipuli afu uchore mkeka kwamba Lipuli atashinda 5 - 0
Yaani hiyo mwanao bila hata kulipa ada kubwa hivyo unaweza ukashangaa ukamtafutia kadi ya maktaba ya mkoa akiwa kayumba huko huko tena akafanya vizuri zaidi ya hata wale wa kayumba
 
Hii kampeni ya kupinga EM imekua kubwa sana na sioni ata cha maana mnachopinga au kuhoji
Hatupingi ila tuna tafakari, yaani wazazi wanashinda njaa maofisini ili mtoto asome "ei, bi, si, di" badala ya "a, be, che, de"
Yaani lugha akuletee mkoloni afu eti ufuge acid tumboni kwa kushinda njaa ili mtoto aweze kuizungumza vizuri even though ukikuwa unaweza kuhakikisha mtoto anaiongea vizuri bila hata kushinda njaa
 
Kama una uwezo wa kumsomesha mtoto EM msomeshe, Hizi excuses za kutaka kupunguza gharama kwa lengo la investments hazina tija.

Kwenye mizunguko yetu ya maisha kwa siku, wiki, mwezi, mwaka tumekuwa tukipoteza pesa nyingi kwenye Anasa, Saluni hasa wanawake, Sadaka nono kwa watumishi feki, Kununua gari tusizomudu kugharimikia, Michango ya harusi, n.k

Kabla ya kufikiria kuingilia Utulivu wa Elimu kwa mtoto, Anza kubadiri lifestyle yako utakuta unasave kiasi kikubwa yawezekana kuzidi hicho cha EM, mnachopigia kelele kila siku.
 
Back
Top Bottom