Waziri Aweso awasweka ndani wahandisi, mkandarasi Handeni

Kinuju

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2021
Posts
2,386
Reaction score
5,325
F8163470-667A-4BF2-9538-366A68A10E04.jpg

Handeni. Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ameliagiza jeshi la polisi wilayani Handeni kuwakamata na kuwaweka ndani watumishi wawili wa wizara hiyo na mkandarasi anayejenga bwawa la Kwenkambala kwa kushindwa kumpa taarifa sahihi kuhusu ujenzi wa bwawa hilo.

Waziri Aweso ametoa agizo hilo leo Jumanne April 12 kwenye ziara yake ya kukagua ujenzi wa bwawa la maji la Kwenkambala na miradi ya maji katika kijiji cha Msomera, ambapo wasimamizi wa mradi wa Kwenkambala kutoka Ruwasa na Mkandarsi walishindwa kutoa taarifa alizotaka waziri na kuagiza wakamatwe.

Waliokamatwa na jeshi la polisi ni mtaalamu wa bwawa kutoka Ruwasa Hamisi Matunguru, mkandarasi Robert Lupinda na Mhandisi Amos Mtweve mthibiti ubora kutoka makao makuu ya Ruwasa.

Waziri amesema kuwa fedha zilipelekwa watu wapate huduma ya maji ila kwa makusudi kuna waliohujumu fedha za mradi na kushindwa kuendelea mpaka sasa.

"Kwa wataalamu wetu ambao kwa makusudi wanaendeleza hizi hujuma sitasita kuwachukulia hatua, hata awe mkubwa vipi lazima atachukuliwa hatua, niombe radhi kwa wananchi na viongozi wa Handeni kwa hili lililotokea".

Mkandarasi Robert Lupinda kwa upande wake amesema amesimama kuendelea na ujenzi wa bwawa hilo baada ya kusimamishwa.

"Sasa hivi nimesimama kazi kwasababu nimepewa oda ya kusimama, tulifanya kikao mara ya mwisho Dar es Salaam nikaambiwa natakiwa kusimama," amesema mkandarasi.

Kwa upande wa viongozi kutoka Ruwasa alioagiza wakamatwe Waziri Aweso amesema kesho Jumatano atakaa kikao na wataalam wengine Dodoma ili kujua shida iko wapi na atachukua hatua.

Hata hivyo mwenyekiti halmashauri ya mji Handeni Mussa Mkombati ameongeza kuwa kuna suala la mkataba wa Tsh. Milioni 132 mwingine nje ya ule wa Bilioni 1.9 za mradi ambao ni tofauti, hivyo kumuomba waziri pia kuufuatilia.

Amesema pia wananchi wote ambao wamezungukwa na mradi hawajalipwa fidia zao mpaka sasa huku mkandarasi akilipwa asilimia zaidi ya 30 za fedha kwaajili ya kuanza kazi, jambo ambalo limefanya wananchi walalamike.

 
Inabidi ujitafakari sana waziri! Uzalendo ndo jambo la msingi! Sio kujipamba tu wa Rais lakini uhalisia ufanisi wa kazi mdogo!
Bwawa la Million 600 lakini uhalisia wa mradi na hicho kituko ni mbingu na ardhi! Kwa hali hii Rais awe mkali Kidogo!
 
Inabidi ujitafakari sana waziri! Uzalendo ndo jambo la msingi! Sio kujipamba tu wa Rais lakini uhalisia ufanisi wa kazi mdogo!
Bwawa la Million 600 lakini uhalisia wa mradi na hicho kituko ni mbingu na ardhi! Kwa hali hii Rais awe mkali Kidogo!

Kwanini kidogo awe mkali kwelikweli yupo hapo kusimamia maslahi ya umma wa watanzania.
 
Mkuu Jidula. Mpaka sasa hakuna hiyo civil case. Kuna issues contractual hazijakaa vizuri.
Sijui scope ya kazi Ila kama mradi ni water supply kwa wananchi., kutakuwa na raiser tanks, main supply and distribution pipes na draw off point( sehemu za kuchotea maji). Kwa mantiki hiyo kuna kazi zilishafanyika na kulipwa.
Kuhusu maendeleo ya bwawa unaweza kuta design haijakamilika ama ilibadilika au kutakuwa kubadilika hi yo kuna mvutano boda

Iss contractual ziwe handled contractual otherwise tutakuwa outlaw country
 
Miafrika bila fimbo hatuendi. Naona Waziri anajaribu kufoka kwa utulivu. Mkandarasi anaongea kwa kujiamini kabisa na kazi yake.
 
Huyu waziri anaanza kuwa mshamba.
Hizo ni civil cases na utatuzi wake uko kwenye mkataba.
Sasa hapo hao aliowaweka ndani anawafungulia mashtaka gani?
Its nonsense!

Ukifuata hizi technicalities wabongo watakutia hadi kidole cha macho. Miafrika bila fimbo hatuendi ukitaka kazi yako iharibike tupe wabongo afu jidai mtu wakufuata protocol.
 
Ukifuata hizi technicalities wabongo watakutia hadi kidole cha macho. Miafrika bila fimbo hatuendi ukitaka kazi yako iharibike tupe wabongo afu jidai mtu wakufuata protocol.
Basi akasimamie kwa fimbo huko Tanga aachane na mikataba!
 
Wabongo tumezoea kusimamiwa nyuma bila hivyo hakuna kitakacho enda mbele zaidi ya upigaji.

"Nchi yetu ni tajiri sana......ila tumechezewa na kuliwa sana........."
wapigaji na wpiga dili ndio wanao rudisha maendeleo ya wananchi nyuma
 
Wabongo tumezoea kusimamiwa nyuma bila hivyo hakuna kitakacho enda mbele zaidi ya upigaji.

"Nchi yetu ni tajiri sana......ila tumechezewa na kuliwa sana........."
wapigaji na wpiga dili ndio wanao rudisha maendeleo ya wananchi nyuma
Weeeeh [emoji15][emoji15][emoji15]tumeshaambiwa hakuna kusimamiana.
.
Hakuna mtumishi kukaripiwa maana Tutafanya Kazi Kwa Hofu Kubwa
 
Back
Top Bottom