Pre GE2025 Waziri Bashe: Wenye mamlaka ya kuniita na kunihoji kwenye nchi hii wapo wanne tu

Pre GE2025 Waziri Bashe: Wenye mamlaka ya kuniita na kunihoji kwenye nchi hii wapo wanne tu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huyo msomali alipewaje uwaziri? Tangu apewe hiyo wizara kafanya lipi la maana zaidi ya ufisadi, huyu si ndio anahusishwa na ile kampuni dhulumati ya tumbaku mkwawa? Hawa mawaziri shida sana
Mnataka kumkwamisha Mama na Bashe. Mama ndio kamteua Bshe
 
Alafu tusikie mnampigia kelele za kupanda kwa bei ya sukari.

Hakika huyu mwamba ameamua kuwaondolea uvivu nyinyi wapiga kelele mitaani.

Hii ni dharau sana kwa watanzania na wapiga kura wake.
 
Japo simfagilii kivile lakini kwa kauli hii nampongeza sana.
Wewe umesema jambo. Japo Bashe ni mmoja wa mawaziri wababaishaji, nampongeza kwa kutokuwa mnafiki na kuamua kusema ukweli. Waziri au mtumishi wa serikali hapaswi kuwajibika kwa Makonda.
 
Haya sasa makonda amepata mbabe 😂
Bashe awezi kuwa mbabe wa Makonda mbona jana alipigiwa simu akaeleza mbele ya wananchi? Au hakuwa yeye? Siamni kama kuna mtu amemwambia aondoe bei elekezi ! Zaidi yeye ameambiwa ahakikishe ana simamia swala la upatikanaji wa sukari na bei alizozisema …na amekubali mbele za watu….
Bashe asibabaishwe na mchecheto wa mitandao akapoteza kibarua chake…hawa watu wanaoshangilia kauli zake huwa wanawageuka kabisa halafu unakwenda kuhojiwa na katibu wa chama mkoa au tawi 😂😂😂😂😂

Hata Mpina ni jeuri zaidi yake lakini kahojiwa na chama mkoa sio hao wanne hahahaha😂😂😂 bashe ana jifurahisha wakimuita atakwenda mikono nyuma uku ana hema
 
kwahiyo anamaanisha BASHITE, DCI/RPC, TAKUKURU na wengine hawawezi kumuita na kuchukua maelezo yake?
Husichanganye mada, Bashe hayuko juu ya sheria. Akifanya makosa ya kijinai au rushwa atahojiwa na vyombo husika kama raia mwingine yoyote lakini hawajibiki kwa Makonda. JPM aliwapa kichwa Polepole na Bashiru kuwaengua wagombea wa nafasi za ubunge nk, hichi ndicho wanachokiogopa mawaziri wakidhani Samia atafanya kama alivyofanya JPM.
 
Kuna mkopo wa kilimo $600ml, bashe akazugia kwenye BBT,
November mwaka jana BBT ikahamishiwa wizara ya uvuvi. Vijana amewa wa dump jkt, pesa za BBT zimekwisha😲😂
 
Huyu dogo uwa anajisahau, pia mfumo haujawahi mwamini, ukamuwekea nhoka ndani kwake?

Vp CS , Polisi, Takukuru, Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Binge, Mahakama? Anauelewa mdogo sanaa Kama anaamini Hawa hawawezi kumuhoji!
 
Bashe kaniangusha hahahaha inasemekana kaandika hayo uko x lakini leo hii kapigiwa Simu na Makonda kaulizwa maswali na kajibu vizuri na kuahidi kusimamia maekekezo ya chama.

Hahaha kweli za kuambiwa changanya na zako…Jamani mihemko ya uko x angalieni isije kuwapotezea vibarua vyenu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwani Mwenez anatumia kifungu gani kujigeuza yeye ni Rais wa nchi?
ni wapi mwenezi amejigeuza Rais wa nchi!!huo u MC anaoufanya kwa watendaji mbali mbali mbele ya wananchi au kuna jingine!!!
Mbina Nchimbi katulia tu.Tanzania hatuna utawala wa sheria.Ni vurugu mechi tu kama tumelaaniwa.
nchimbi sio mwenezi,ni katibu mkuu wa chama.
 
Na kujiamini ...
Watanzania wengi hatujiamini .. Na uoga sana wa kutumia Mahakama pale unapokandamizwa...Kuna kipindi kama miaka 4 ...Mnyeti akiwa RC akifanya ziara vijijini huko Manyara alimfanyia kituko mkulima mmoja ..

Akaenda kuripoti polisi ..polisi wakamtimua ..akafunga safari Dodoma kwa IGP ..basi yule bwana akapigiwa simu na RC kwenda ofisini kwake na kuyamaliza japo aliambiwa chunga sana....ni wachache wana udhubutu huo
Safi sana kwa huyo mkulima.
 
Back
Top Bottom