DOKEZO Waziri Gwajima, hii anayofanya Lillian Mwasha kwa watoto siyo sawa

DOKEZO Waziri Gwajima, hii anayofanya Lillian Mwasha kwa watoto siyo sawa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Hawa feminist harakati zao kubwa ni kujenga chuki kwa wanawake na watoto dhidi ya wanaume , huwa hawaangalii kusuluhisha wanapambana wanawake wachukie waume zao baadae ndoa zikivunjika watoto wa mtaani wakiwa wengi wanaanza kuwapandikiza chuki kuchukia baba zao
 
FaizaFoxy, Habari za asubuhi FaizaFoxy. Utanisamehe Sana kwa kuwa sijaja humu JF kukubaliana na kila jambo ambalo litakupendeza wewe. Kwa upeo wangu huu huu, katika hili, diagnosis yangu ni kuwa, huyu Lilian Mwasha amekosea hiki alichofanya, hakifai. Na kwa upeo wangu huu huu sijalala hadi nikampata na kumwambia hapa umekosea na aondoe hizo video mitandao yake yote. Na kwa huu upeo wangu, nimemwagiza kamishna wa ustawi amwite kwa hatua zaidi na kufika kwenye hiyo shule waliko hao waalimu na watoto kwa hatua zaidi na tamko litolewe la marufuku kuhusu Kila mtu kuingia kwa watoto na kutoa huduma aina hizi na zingine. Na pia hatua zingine zaidi zichukuliwe kwa mujibu wa taratibu za ustawi. Haya, na wewe Sasa kwa kuwa unao upeo mkubwa kabisa, ongezea tufanye nini zaidi.

Ila acha chuki binafsi Ili twende sawa. Nakubariki, ubarikiwe [emoji1666][emoji120][emoji2969]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Mh.huyu Faiza Fox ni kirusi ktk jamii usihangaike naye!
 
Yaani Kila kitu kinautaratibu, nikifanya langu mm hapa, watakuja waseme waziri kakurupuka. Wote huwa tunafuata utaratibu huu huu, kuwa kwa haraka waziri huwa nasema hili baya au hili liko hivi, na nimesema hapo tayari. Sasa, kinachofuata ni kuwa, ataitwa na kamishna, atahojiwa ilikuwaje kafikaje huko alikofika, atasema, huenda wengine wataunganishwa maana uelewa utakuwa sasa mpana. Inaweza gusa huko shuleni alikokuwa lakini pia watoto watahitaji huduma na wazazi pia watahitaji huduma, yaani mfumo mzima uliguswa utahusika kwenye hatua mbalimbali Kila mmoja kwa nafasi yake kama ni kupata unasihi au kuwajibika. Na hapo baada ya huo uchambuzi ndiyo wizara itasema ikaja ikaenda ikawa hivi na Sasa kilichofanyika hiki. Halafu Sasa maoni yatatolewa je nn kimesahaulika au kimeachwa wapi Ili hatua zaidi ziendelee juu eneo hilo. Nadhani huu ni utaratibu mzuri kabisa, au vipi ndugu zangu?

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Hapo umenena baada ya mchakato usisite kutupa majibu
 
Hapo umenena baada ya mchakato usisite kutupa majibu
Mtapata kabisa. Na hadi sasa kamishna wa ustawi ameshawasiliana na mhusika, katika hatua za awali kasikilizwa kapewa maelekezo. Na hatua zingine zinaendelea. Hili jambo linachukuliwa kwa uzito wote. Ahsante Sana

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
 
Ahsante Sana. Mambo mengi ya jamii yana dhamana ya wizara mbalimbali za kisekta, wizara yangu tunaendelea na uratibu wa wadau wa kisekta kama nilivyotamka tarehe 12 Sept 2023 tukiwa na BASATA, Cosota Bodi ya FILAMU wanaouhusika na udhibiti wa uzalishaji content.

Tunaendelea na ushirikiano na wenye dhamana ya hivi vyombo vya habari pia.... Shukrani kwa maoni yako.

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Wewe Sasa ndio Dr! Saaafi sana.
 
Sioni Kama udharirishaji,Kama huudumii mtoto na mtoto anajua tusemaje sasa? Au mtoto aseme vipi. Huo Ndio ukweli na ukweli usemwe wazi,Yaan nikojoe tu alafu niondoke mwanangu Aishi vipi.
Wakati tunazagamuana huyu lilian mwasha alitushikia miguu? Yeye haya baada ya kumhoji mtoto alimuuliza mamake hela ya kuhudumia mtoto anatoa wapi? Ulimhoji babake kujua ukweli? Baada ya kuwahoji aliwapa hata elfu kumi za kifuta machozi, sie huwa tunawaambia nenda shule ukileta div four katafute pa kuipeleka, huo ndio ukweli.
 
Its all about Wanaume?
Playing Gender card wont help hapa......
Kwa kuwa umesema kuhusu wanaume nitasema kuhusu wanawake.
Ili yasitokee hayo.
1. Mwanamke asikubali kubeba mimba ya mtu asiye eleweka.
2. Mwanamke asi " tegeshe" ipatikane mimba ili kulazimisha kuwa pamoja ( ndoa) hasa kama anajua mwanaume aliyenaye ana mipango mingine.
3. If mahusiano yalikufa , mtoto asilishwe "sumu" juu ya baba ake, baba ake apewe " access" ya mwanawe, pia mtoto asitumike kama ndio chanzo cha kupiga hela in a name of " Child support".
Vitu ni vingi aseee, ila kusema hili ni jambo la wanaume pekee aseee hii ni issue.
Na haitosaidia chochote.
Acha vijisababu
No 1 na 2 vaa condom... kwanini ufanye peku na mtu huna mpango? Take responsibility vaa condom hutokaa uache mbegu usipotarajia

No 3 kama una nia sheria zipo wazi, kuchunwa ni kuamua, toa child support kulingana na kipato chako na mtu kama hataki kuna njia za kisheria za kufata KAMA UNA NIA

inshort umetoa excuses za kitoto tu, VAENI CONDON MKIWA MNAKULANA NA WATU MSIO NA MALENGO NAO, otherwise ni kutafuta kutesa watoto duniani hapa
 
Mtapata kabisa. Na hadi sasa kamishna wa ustawi ameshawasiliana na mhusika, katika hatua za awali kasikilizwa kapewa maelekezo. Na hatua zingine zinaendelea. Hili jambo linachukuliwa kwa uzito wote. Ahsante Sana

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Absolutly i salute now you are talking as a professional Doctor, kwa taaluma yako unajua hatua za makuzi ya watoto, huyu Lilian ni ignorant kwa kile alichokuwa akifanya.

Mh, napendekeza ukae na waziri wa elimu muweke mwongozo wa maudhui ya watoto mashuleni, uwepo uratibu wa shughuli kama hizi na kama kuna haja ya kuwa puplic basi serikali ihusishwe na ibariki
 
Huyo nae anapenda cheap publicity,
Kuna njia sahihi ya kusaidia hao watoto na sio kuwaanika hivyo. Maombi hayaondoi chuki, angekuwa na nia ya dhati angewatafuta in private na kuwaunganisha kwa wabobezi wa hiyo fani wawasidie na sio HUO UPUUZI ANAOFANYA HAPO
Ifike hatua shule nazo ziwe zinaangalia nini cha kuongelewa kabla ya kuwapa watu wajinga wajinga platform.
 
kuna kina mama hapa Tz kazi yao kubwa ni kupandikiza chuki kwa watoto kuhusu baba zao hasa wanapokuwa wametengana hata baba ufanye nini inaonekana mama ndio ka-push...Na unajitahidi lakini unaona mtoto yupo mbali na wewe inafika kipindi unaacha kwanza unaendelea na mambo mengine.
 
Mtapata kabisa. Na hadi sasa kamishna wa ustawi ameshawasiliana na mhusika, katika hatua za awali kasikilizwa kapewa maelekezo. Na hatua zingine zinaendelea. Hili jambo linachukuliwa kwa uzito wote. Ahsante Sana

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Mhe. Kuomba radhi iwe ni miongoni mwa hatua zitakazochukuliwa, muhusika aombe radhi hadharani kama alivyodhalilisha hao watoto pamoja na familia zao kupitia mitandao aombe radhi pia na ikiwezekana arudi shuleni kuomba radhi na ajutie kosa lake.
Alichokifanya kitawaathiri hao watoto hapo shuleni.
 
Acha vijisababu
No 1 na 2 vaa condom... kwanini ufanye peku na mtu huna mpango? Take responsibility vaa condom hutokaa uache mbegu usipotarajia

No 3 kama una nia sheria zipo wazi, kuchunwa ni kuamua, toa child support kulingana na kipato chako na mtu kama hataki kuna njia za kisheria za kufata KAMA UNA NIA

inshort umetoa excuses za kitoto tu, VAENI CONDON MKIWA MNAKULANA NA WATU MSIO NA MALENGO NAO, otherwise ni kutafuta kutesa watoto duniani hapa
Ngoja nikujibu kistaarabu waziri kashusha munkari wangu, kuna wazazi jobless walishafukuzwa kazi mtoto hajui kama babake hana kipato, anaona baba hawajibiki kumbe mzee pesa hakuna,

Kuna madai ya kitoto huwa tunayakataa tu mfano mtoto anadai apewe iphone ajiunge tiktok, mie kwangu hiyo ni dhambi hatamamake hawezi thubutu kuomba achilia mtoto.

Kuhusu matumizi ya condom at age of 50 umeshakunywa kvant hainaga nafasi, hebu nikujibu hivyo kwa leo

Relationship ya binti na babake mkuu ukilegeza utakunywa breakfast na boyfriend wa mwanao sebuleni, ukiwachekea watakuomba mirathi bado unapumua
 
Back
Top Bottom