DOKEZO Waziri Gwajima, hii anayofanya Lillian Mwasha kwa watoto siyo sawa

DOKEZO Waziri Gwajima, hii anayofanya Lillian Mwasha kwa watoto siyo sawa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Uko sahihi, Na hapa ndiyo ambapo changamoto itaibukia.

Nimempa mtaalamu wa huduma za ustawi wa jamii atuongoze Ili twende salama. Nia njema iende sahihi ili tufanikiwe
Mheshimiwa Gwajima asante sana kwa hili. Huyu mama anachofanya hakikubaliki hata kidogo. Kuna namna nzuri ya kushughulikia haya mambo na siyo huu ujinga anaofanya. Tafadhali sana chukueni hatua huu ujinga usiendelee
 
Imefunguka, nimempa kamishna wa ustawi wa jamii afanyie kazi. Ahsanteni sana kwa ushirikiano.
Hongera Waziri Gwajima kwa kuwa proactive. Nimefurahi kuona namna ulivyopata habari na kujielekeza katika kulitatua. Mungu akubariki latika juhudi zako za kujenga Tanzania yenye watoto wenye matumaini.
 
FaizaFoxy,
Kwamba Mh. Waziri ajue yajayo vichwani mwa Watanzania wenye kichaa..
Yani ilibidi ajue Anachoenda kufanya Lilian!!?

Alafu mbona keshachukua hatua.

At least she is the only Minister that has this live engagement with us. We mwanamke wewe..

Give Credit when it's due..

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
 
Anawauliza watoto wanaochukiwa na baba zao. Je amewaandaa kisaikolojia? Mbona yaonekankama ni udhalilishaji kwa watoto na wazazi wao. Angalia clip hapa


Sioni Kama udharirishaji,Kama huudumii mtoto na mtoto anajua tusemaje sasa? Au mtoto aseme vipi. Huo Ndio ukweli na ukweli usemwe wazi,Yaan nikojoe tu alafu niondoke mwanangu Aishi vipi.
 
FaizaFoxy, Habari za asubuhi FaizaFoxy. Utanisamehe Sana kwa kuwa sijaja humu JF kukubaliana na kila jambo ambalo litakupendeza wewe. Kwa upeo wangu huu huu, katika hili, diagnosis yangu ni kuwa, huyu Lilian Mwasha amekosea hiki alichofanya, hakifai. Na kwa upeo wangu huu huu sijalala hadi nikampata na kumwambia hapa umekosea na aondoe hizo video mitandao yake yote. Na kwa huu upeo wangu, nimemwagiza kamishna wa ustawi amwite kwa hatua zaidi na kufika kwenye hiyo shule waliko hao waalimu na watoto kwa hatua zaidi na tamko litolewe la marufuku kuhusu Kila mtu kuingia kwa watoto na kutoa huduma aina hizi na zingine. Na pia hatua zingine zaidi zichukuliwe kwa mujibu wa taratibu za ustawi. Haya, na wewe Sasa kwa kuwa unao upeo mkubwa kabisa, ongezea tufanye nini zaidi.

Ila acha chuki binafsi Ili twende sawa. Nakubariki, ubarikiwe [emoji1666][emoji120][emoji2969]

Sent from my CPH2207 using JamiiForums mobile app
Pokea maua yako Mheshimiwa Waziri kwa uthubutu wako
 
Anawauliza watoto wanaochukiwa na baba zao. Je amewaandaa kisaikolojia? Mbona yaonekankama ni udhalilishaji kwa watoto na wazazi wao. Angalia clip hapa

Namuunga mmono Lilian Mwasha.

Ujinga mwingi sana unafanyika majumbani na wanawake hawana pa kukimbilia wala pa kusemea kwa sababu hata hayo madawati yanahudumiwa na wengi wanaonyanyasa wanawake huko majumbani.


Dkt. Gwajima D naamini bado jamii inahitaji elimu ya familia kabla ya khinvia kwenye kuunda familia
 
Hili ni lifeminist tu linajikuta linamshirikisha Mungu kwenye mambo ya kipumbavu, mara nyingi au mara zote baba kukataa kuhudumia mtoto hapo ujue chanzo ni mama sema madingi hatunaga time ya kuzungumzia yanayotusibu tunakausha na Mungu ndo muamuzi.

Feminist huyu ni wa kupuuzwa hayo maombi yenyewe ukiyaangalia kwa jicho la tatu ni ya mchongo, maombi kashayafanyia rehearsal kayakariri mpuuzi mmoja wa kupuuzwa.
Ukishasikia Mwasha sijui Macha . Ujue ni mpunga tu unatafutwa. Manka kama Manka?
 
Back
Top Bottom