Waziri Jerry Silaa ana kitu, atafika mbali, abarikiwe

Ni Kweli,

Njia ya maendeleo huacha maumivu Kwa wengi, lakini, hakuna namna.
 
Hata ingekuwa miezi sita, kazi inayoonekana, inatosha kabisa kiongozi kuheshimika na anaowatumikia.
Hata ingekuwa miezi sita, kazi inayoonekana, inatosha kabisa kiongozi kuheshimika na anaowatumikia.
Labda 2025 akagombee jimbo lingine, sio tena Ukonga
W Sawa lakini unajua watu wa kimara walionewa, hawakutendewa haki kabisa. Sisi tulibomoa nyumba, tanroad wamekuja wamepima nyumba ipo nje kabisa ya eneo wanalolitaka. Je huu ni uongozi unaozingumzia. Uongozi wa kutakujali haki za watu ilimradi unalolitaka litimie
 
Nisome vizuri hapo mkuu 'Abeltrainer'; mimi sijasema hivyo hata kidogo. Ndiyo maana nikauleta huo mfano ili kusisitiza uwepo wa ubinaadam katika uamzi wa kiongozi, hata kama anafanya kazi ndani ya sheria. Uelewa wangu ni kuwa mahakama ilikuwa imeweka zuio hao watu wasibomolewe nyumba bila ya kufidiwa, au nimekosea?
Kwa vyovyote hizo nyumba zingebomolewa kupisha mradi; lakini ilitakiwa watu wapewe haki yao. Kuna kitu kinaitwa 'eminent dominion'; kukisha kuwepo na hali hiyo hakuna namna nyingine bali kupisha, mradi tu upewe haki yako. Sasa sijui kama walipewa.
 
Hatukupewa chochote, ilibidi tuuze eneo lingine, ili tupate hela ya kujenga mji mwingine.huo ndio uongozi unaouzungumzia? Kipindi cha magufuli, ulikuwa unaenda mahakamani kufanya nini? Hiyo hela tumgeipata wapi? Nani alikuwa anadhubutu kwenda kusimamia kesi dhidi yake mahakamani?
Je huo ndio uongozi unaouzungumzia?
 
Pole sana Kwa kupoteza nyumba, Fungua case court sasa udai HAKI Yako,

Ikumbukwe pia kuwa, uongozi huo ndio umesaidia kupunguza foleni dar na zikajengwa barabara nyingi, flyovers nk nk.

Maendeleo Huwa na pande mbili, mchungu wa maumivu na sacrifice, na upande Ule mwingine.
 
Hapana, mkuu wangu 'Abeltrainer', huo siyo uongozi ninaouzungumzia hata kidogo, ninakusihi unielewe ninachoeleza hapa. Magufuli alikuwa na mapungufu sana kama binaadam, na hasa kama kiongozi. Hata siku moja hutasikia nikiunga mkono baadhi ya mambo machafu kabisa aliyokuwa akifanya. Yote niliyokwisha andika juu yake yamo humu humu JF, na wala sibadili kitu juu yake.
Baada ya kusema hayo, elewa nilicho eleza hapo juu; mlistahili kupata haki yenu, na hasa kwa vile mahakama ilikuwa upande wenu. Swala la kupisha barabara, hilo ni vigumu kulikana, lakini baada yenu kupewa haki mliyostahili kupata.

Sasa basi, inawezekana kwa uchungu huo wa kupoteza kwenu, inawezekana kabisa nyoyo zenu zikashindwa kuona lolote zuri lililotokana na baadhi ya mambo aliyoyasimamia Magufuli. Mimi naamini yapo; pamoja na kwamba hayawezi kufuta udhaifu mkubwa aliokuwa nao kwa upande wa pili.

Kamwe siwezi kukuhimiza 'usahau; lakini nadhani kusamehe kwa manufaa ya taifa inawezekana. kwa hayo mazuri anayohusishwa nayo.
 
Pamoja na mapungufu yake kibinadamu, Jerry anatatua migogoro kwa kutumia common sense na logic, tofauti na Kleruu kwa Mamwindi.
Changamoto ni kwamba majinga na mapuuzi ni mengi kwenye mifumo ya kiserikali.
 
Pamoja na mapungufu yake kibinadamu, Jerry anatatua migogoro kwa kutumia common sense na logic, tofauti na Kleruu kwa Mamwindi.
Changamoto ni kwamba majinga na mapuuzi ni mengi kwenye mifumo ya kiserikali.
Jerry angetimua viongozi kadhaa hapo wizarani Ili wapate Kutoka usingizini,

Wizara hiyo Ina Ujinga mwingi sana,

Lissu analalama, Manyara huko hivi karibuni wameuza open spaces Kwa ajili ya mikutano ya hadhara.

Sasa viongozi type hiyo wapo kazini!!
 
Pamoja na mapungufu yake kibinadamu, Jerry anatatua migogoro kwa kutumia common sense na logic, tofauti na Kleruu kwa Mamwindi.
Changamoto ni kwamba majinga na mapuuzi ni mengi kwenye mifumo ya kiserikali.
Ule msikiti wa kariakoo alitumia common sense gani? Yaani mtu ameshindwa mahakama zote, na pia anawadhulumu wenzake, wakamua wauze na waamishe wakfu sehemu ngingine kubwa zaidi na itakayokuwa inatumika na watoto wengi zaidi. Then unawaita matapeli. Sawa tuseme kwemye swala la wakfu walikosea, je alijioa muda wa kusoma hukumu ya hizo kesi ili ajue kwa nini huyo dada alishindwa?
Kutatua migogoro ni jambo jema sana, tatizo ni kwamba asiweke siasa kwenye utatuzi wa hiyo migogoro. Aache wataalamu wa wizara wafanye kazi. Yeye atengeneze paltform nzuri ya utatuzi wa migogoro
Kama kweli anatenda HAKI aje huku kimara atupe HAKI yetu sisi ambao tulibomolewa nyumba kinyume kabisa na order ya mahakama. Hapo ndio nitaamini anatenda haki
 
Swala la sheli limeishia wapi mbona kila uchao sheli mpya zinajengwa?
 
Silaa hajichukulii maamuzi kesi ya Mmasy ilifika mpaka High Court Mmasy akawa ameshindwa ikaja execution order atoke kwenye nyumba tangu mwaka jana mwez wa 8 akagoma, Jerry Silaa akamuuliza Mmasy kuwa wewe na huyu nani mshindi ? Mmasy akasema huyo mwenzake.

Kwahyo wazir hapo hajachukua maamuz yake mkononi bali amesaidia execution order ya mahakama na ndio anachokifanya. Ila hasolve case Kwa kuingilia kazi ya mahakama.
 
Sina details za matukio yote, kwa hiyo maoni yangu ni ya jumla tu. Nimeandika kasoro za kibinadamu lazima zihusike pia.
 
Kwenye kesi ya mmasi, hata hapakuitajika waziri aende, tayari mahakama ilishatoa hukumu. Angetuma timu yale iende, hio ni issue ndogo sana kwa level ya uwaziri.
Kuna kesi kama hiyo imetatuliwa arusha bila kuwepo order ya waziri.
Umeshajaribu kuwaza image ambayo hawa wanasiasa wanaitengeneza kwenye jamii kuhusu mahakama. Ilihali wakijua kabisa kuwa wao ndio vinara namba moja katika kuifanya mahakama isiwe huru.ifanye maamuzi kulingana na wanabyotala wao.
Sasa kama anasema kuwa mahakama inahongwa, haitoi haki, hao matapeli anawakamata wakashitakiwe wapi?
 
Mtu anadai haki yake mahakamani zaidi ya miaka 10 anazungushwa tu,anakuja waziri anamsaidia kupata haki yake WAPUMBAVU kama chiembe wanaanza kumtukana eti anatafuta kiki.
Unajiuliza hawa watu wana akili kweli?

Yaan Sijui wanawaza kwa kutumia nn aisee et mahakamani kuna haki mahakama hii iyowafunga kina yona na mramba kifungo cha nje na kumfunga maisha mama aliyekutwa na nyama pori llooh
 
Swala la sheli limeishia wapi mbona kila uchao sheli mpya zinajengwa?
Utanisamehe mkuu 'Abeltrainer', hili la "shell" sina ufahamu wowote juu yake. Nalo linahusu uongozi wa mtu asiyetetereka, na kuweka maslahi ya taifa mbele?
Pamoja na kwamba ni kama lipo nje ya mada, lakini unaweza kudokeza kidogo hii shell inahusikana vipi na mjadala huu.
 
Asalaleh!
Kumbe upo hivi?
Nimejibishana nawe nikidhani najibishana na mtu mwenye uelewa wa kutosha kumbe ni wale wale wapiga dili?

Jerry Silaa, sasa hivi anafanya kazi nzuri sana kutatua matatizo yaliyoletwa na hawa wenzenu wanaodhani kuwa na pesa ni kila kitu maishani mwao.

Sasa ukikomaria kutaka kunifuatafuata na majibu ya kipuuzi kama hili uliloweka hapa; nitakujibu kwa stahiki inayoendana na uhayawani kama huu unaojionyesha wenyewe kwenye andiko lako hapa juu.
Umeshajaribu kuwaza image ambayo hawa wanasiasa wanaitengeneza kwenye jamii kuhusu mahakama. Ilihali wakijua kabisa kuwa wao ndio vinara namba moja katika kuifanya mahakama isiwe huru.ifanye maamuzi kulingana na
Mahakama haihitaji kutengenezewa 'image' na yeyote; inajitengenezea 'image' yenyewe kwa kukumbatia ufisadi. Waziri hana mamlaka yoyote juu ya mahakama.
Tena naona ni kama umechanganyikiwa. Kama kesi ya Mmasi ilikwisha amriwa mahakamani, ni kipi kilichokuwa kikizuia utekelzaji wake, hadi waziri alipoingilia.

Sasa hata hiyo habari ya Kimara, naona siyo ya kweli, wewe ni tapeli tu, kama walivyo matapeli wengine.
Tunawahitaji mawaziri wengi wa aina ya Jerry Silaa kukomesha watu wenye tabia mbovu kama hizi zenu.
 
Wewe una ajenda mbovu, kutaka kumkatisha moyo waziri kwa juhudi zake nzuri anazofanya. Maandishi yako sasa yamekuonyesha wazi kuwa ni mtu ambaye ni mshiriki katika uovu na uonevu wanaofanyiwa watu wasiokuwa na uwezo wa kupigania haki zao. ,
Kwa mtu kama wewe simlaumu Magufuli. Hata hivyo, sasa nina mashaka na unayosema hapa kama ndilo tukio lililotokea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…