Waziri Jerry Silaa ana kitu, atafika mbali, abarikiwe

Waziri Jerry Silaa ana kitu, atafika mbali, abarikiwe

Kwenye suala la ardhi Mahakama sio msuluhishi wa kwanza, kesi zinaanzia kwenye mabaraza either ya kata na wilaya mahakamani unaenda kuappeal in case umeshindwa.

Silaa yupo sahihi sababu anaongozana na Commissioner wa ardhi na wasajili wa ardhi...ukisoma powers za Commissioner wa ardhi utaona pia wanayo haki ya kufanya Revokation of Right of Occupancy either customary or granted right of occupancy.

Endapo ulifanya forgery, hata ukifanya conveyance au unauza eneo commissioner ni lazima umpe notice kwahyo nakushauri usome sheria ya ardhi vizuri na pia usome power za Commissioner wa ardhi ambaye na yeye yupo chini ya waziri wa ardhi.Pia utambue Jerry ni msomi wa sheria na mimi ninae kuambia hivi ninaijua sheria ya ardhi Kwa uzuri zaidi hakuna jambo baya ambalo Jerry Silaa anafanya zaidi ni kumfanya Commissioner afanye kazi zake Kwa uweredi zaidi.
Kwenye kesi ya mmasi, hata hapakuitajika waziri aende, tayari mahakama ilishatoa hukumu. Angetuma timu yale iende, hio ni issue ndogo sana kwa level ya uwaziri.
Kuna kesi kama hiyo imetatuliwa arusha bila kuwepo order ya waziri.
Umeshajaribu kuwaza image ambayo hawa wanasiasa wanaitengeneza kwenye jamii kuhusu mahakama. Ilihali wakijua kabisa kuwa wao ndio vinara namba moja katika kuifanya mahakama isiwe huru.ifanye maamuzi kulingana na wanabyotala wao.
Sasa kama anasema kuwa mahakama inahongwa, haitoi haki, hao matapeli anawakamata wakashitakiwe wapi?
 
Tupambanie KATIBA mpya Ili waziri asitokane na wabunge.

Hapo mkabeni shati mbunge wa viti maalum akaimu vizuri nafasi ya mbunge awapo katika utumishi wa nje ya Bunge Kwa nafasi ya Uwaziri.
Tunaanzaje kuipambania katiba mpya na wakat wenye katiba yao hawataki wanajua ulaji utapotea tu
 
Ungejua power za Commissioner usinge andika hivi..nenda ukasome Quasi Judicial Tribunals ni nini ?
M

aha ndio mwamuzi wa mwisho wa mgogoro wowote hata makampuni huenda mahakamani kuishtaki serikali endapo inavunja mikataba pasipo utaratibu. Mgogoro wa ardhi baina ya pande mbili hutatuliwa mahakamani na sio wizarani!
 
Hao wote wanaompopoa Slaa wanamakandokanndo kwenye ardhi zao 🤣🤣🤣🤣🤣 chuma kipo njiani kuwafikia. Mtaongea Kijapani mwaka huu
 
Ungejua power za Commissioner usinge andika hivi..nenda ukasome Quasi Judicial Tribunals ni nini ?
Nilichogundua humu wengi hawatumii akili zao kufikiri, wanaendeshwa na uchama,

Ni bendera fuata upepo, hawezi toa maoni yake Hadi asikilizie wanachama wenzangu wanasema nini Kisha naye anaunga tera.

Anachokifanya Slaa na commissioner wa ardhi kipo kisheria kabisa,

Na ni njia nzuri kuwamulika maafisa ardhi walishiriki UOVU huo Ili watumbuliwe na kushtakiwa.
 
Huyo hamna kitu, ana-deal na kiki ambazo akikutana na mbabe anakwama, yaani uje mtaani umtoe mtu kwenye nyumba, hiyo ni kazi yako kama waziri? Anatafuta yale yaliyomkuta Mwamwindi wa Iringa.

Wizara ina mambo makubwa ya kisera ya kufanya, hayafanyii kazi.

Kuna tatizo kubwa la utawala wq ardhi (land administration) hasa kwa kuwa asilimia kubwa ya nchi yetu haijapimwa. Sheria ya ardhi namba 4/1999 inajishughulisha na ardhi yenye hati, lakini wangapi mjini wqna hati? Wale wasio na hati wanakuwa regulated vipi? Wizara imetoa muongozo kwa uhamishaji wa miliki ambazo hazina hati?

Wizara ina mpango gani kuunga mifumo ya kibenki na usajili wa ndoa ili mali za dhamana wakopeshaji wajue hali ya mkopaji?

Kulikuwa na mradi wa hati za kidigitali, umekwama wapi?

Benki ya dunia walitoa bilioni 350 kufadhili mradi wa wizara ya ardhi ambao unajumuisha ujenzi wa majengo ya taasisi za ardhi kila mkoa, mbona bajeti inaisha, majengo hayapo? Na hata vifaa walivyosema watanunua kwa ajili ya kila mkoa ili kupima ardhi havipo? Hizo hela zimeenda wapi?

Mamlaka zinapoingiza vijiji mjini, wizara imetoa muongozo kuhusu ardhi iliyokuwa ya vijiji? Kuna namna au mfumo wa vijiji kukabidhi ardhi kwa Halmashauri? Au ndio inaachwa kwa viongozi wa mitaa mipya wajiuzie wanavyotaka?

Hatumuoni katika migogoro ya hifadhi za taifa na wananchi, anazurura mijini tu. Kapima vijiji vingapi mwaka huu? Amegawa hati za kimila ngapi?

He is just a petty politician ambaye alitakiwa ajenge josho ili kuosha wanyama kwq maelfu, yeye kaamua kuchambua manyoya ya mnyama mmoja mmoja ili awe anatoa kupe
Hata hapo alipoanzia ni sawa.Watu wasio na pa kusemea wanadhulumiwa sana
 
Unajua hata mtaani watu wanauziana ardhi kwa kutumia mjumbe bila kumfahamisha Commissioner wala kwenda kwenye ofisi yake kuangalia kuwa is there any encumbrance? baadae ikitokea mgogoro wanalalamika lakini ni mambo ambayo yapo wazi kwenye sheria ila hawayatekelezi. Ila nawashauri unaponunua ardhi nenda katika ofisi za Ardhi kujiridhisha kwanza.
Hao wote wanaompopoa Slaa wanamakandokanndo kwenye ardhi zao [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] chuma kipo njiani kuwafikia. Mtaongea Kijapani mwaka huu
 
Hao wote wanaompopoa Slaa wanamakandokanndo kwenye ardhi zao 🤣🤣🤣🤣🤣 chuma kipo njiani kuwafikia. Mtaongea Kijapani mwaka huu
Na Kuna matajiri wengine matapeli pia wamulikwe,

Akishagundua eneo la wananchi au shamba halina hati, anakimbilia ardhi anapimiwa na kupewa hati bila kuuziwa eneo Hilo na wamiliki au Wana chi.

Hati za namna hiyo pia ni haramu, zifutwe, HAKI ya wananchi ziheshimiwe.
 
Huyo hamna kitu, ana-deal na kiki ambazo akikutana na mbabe anakwama, yaani uje mtaani umtoe mtu kwenye nyumba, hiyo ni kazi yako kama waziri? Anatafuta yale yaliyomkuta Mwamwindi wa Iringa.

Wizara ina mambo makubwa ya kisera ya kufanya, hayafanyii kazi.
hakuna shukurani kwa kila analofanya binadamu, hebu baadhi ya wakati tujaribu kupongeza lile jema linalofanyika.

Shida ya kuachia mfumo ufanye kazi unakuta hao waendesha mfumo (baadhi ya majaji, baraza la ardhi na hata maafisa wa ardhi wenyewe) ndiyo hao walioko mstari wa mbele kudhulumu.
 
Nilichogundua watu wengi wanamponda waziri kwasababu hawajui utaratibu wa case za ardhi zinavyoamuliwa...ukimiliki ardhi kimakosa haina haja ya kwenda mahakamani lakini Commissioner anayo hiyo nguvu ya kutengua umiliki wako. Nawashauri mkasome S.175 ya Tanzania Land Act Cap 113.

Silaa anamsaidia Commissioner kufanikisha majukumu yake kama Commissioner pia anaisaidia mahakama kufanya Execution order.
 
Hata hapo alipoanzia ni sawa.Watu wasio na pa kusemea wanadhulumiwa sana
Imagine maskini kiwanja ni chake kihalali, akiwa anadunduliza kuanza msingi, anasikia kuwa Kuna mtu amekuja anayo hati na amezungushia uzio tayari, ukienda baada ya wiki, unakuta nyumba imesimama tayari,

Ukimuuliza, anakwambia Nina hati na Kwa kuwa nimeshajenga, niuzie, anakupa Bei ya kukugalaliza akijua huna uwezo wa kuendesha case.

Asee Hawa watu wanaudhi,

Watu aina ya Slaa, waombewe sana.
 
Nilichogundua watu wengi wanamponda waziri kwasababu hawajui utaratibu wa case za ardhi zinavyoamuliwa...ukimiliki ardhi kimakosa haina haja ya kwenda mahakamani lakini Commissioner anayo hiyo nguvu ya kutengua umiliki wako. Nawashauri mkasome S.175 ya Tanzania Land Act Cap 113.

Silaa anamsaidia Commissioner kufanikisha majukumu yake kama Commissioner pia anaisaidia mahakama kufanya Execution order.
Swali ni kwamba, kazi ya waziri ni nini?
Sasa kamq hiyo ni kazi ya kamiahna wa ardhi, kwa nini hawapi nafasi pamoja na kuwajengea uwezo ili waweze kufanya kazi kikamilifu.
Kwa nini hatoi hiyo elimu kwa wananchi ili wajue namna bora ya kutatua migogoro ya ardhi.
Kama maafisa ardhi wana nguvu, na wao ndio wametengeneza hiyo migogoro, mbona hawachukuliwi hatua? Mbona inaonekana ni watu waina fulani tu ndio anaowalenga?
Mimi namuunga mkono kwenda site kwa lengo la kujenga uelewa, lakini napinga mfumo anaoutumia kitatua hiyo migogoro
 
Utanisamehe mkuu 'Abeltrainer', hili la "shell" sina ufahamu wowote juu yake. Nalo linahusu uongozi wa mtu asiyetetereka, na kuweka maslahi ya taifa mbele?
Pamoja na kwamba ni kama lipo nje ya mada, lakini unaweza kudokeza kidogo hii shell inahusikana vipi na mjadala huu.
Sorry shell nimemaanisha vituo vya kuuzia mafuta.
Wakati anaingia alianzia kwenye vituo vya mafuta. Kuna vingine akasema vivunjwe. Na akasimamisha ujenzi wa vituo vipya.
Sasa mimi huku mtaani bado naona vituo vinajengwa. Tena kwenye makazi ya watu.
Ni kweli tunahitaji viongozi watendaji, ila utendaji ambao ni SMART
Katika hali ya kawaida, huwezi ukatatua kesi iliyoshindikana miaka 20 ndani ya dakika. Halafu ukasema unetenda haki
 
Imagine maskini kiwanja ni chake kihalali, akiwa anadunduliza kuanza msingi, anasikia kuwa Kuna mtu amekuja anayo hati na amezungushia uzio tayari, ukienda baada ya wiki, unakuta nyumba imesimama tayari,

Ukimuuliza, anakwambia Nina hati na Kwa kuwa nimeshajenga, niuzie, anakupa Bei ya kukugalaliza akijua huna uwezo wa kuendesha case.

Asee Hawa watu wanaudhi,

Watu aina ya Slaa, waombewe sana.
Kabisa
 
Sorry shell nimemaanisha vituo vya kuuzia mafuta.
Wakati anaingia alianzia kwenye vituo vya mafuta. Kuna vingine akasema vivunjwe. Na akasimamisha ujenzi wa vituo vipya.
Sasa mimi huku mtaani bado naona vituo vinajengwa. Tena kwenye makazi ya watu.
Ni kweli tunahitaji viongozi watendaji, ila utendaji ambao ni SMART
Katika hali ya kawaida, huwezi ukatatua kesi iliyoshindikana miaka 20 ndani ya dakika. Halafu ukasema unetenda haki
Mwanzo nilipoanza kujibishana nawe sikujuwa kuwa ulikuwa na ajenda maalum unayoisukuma mbele humu JF. Ni ajenda ovu. Jitafakari.
 
N

Tanzania tumewapa wanasiasa mamlaka kubwa mno na ndio maana wanafanya watakavyo kwani wanajua wao wapo juu ya sheria na kwa bahati mbaya sana sisi wananchi tunawaunga mkono! Slaa hawezi kuwa mbadala wa mahakama hata rais hawezi kuwa mbadala wa mahakama kama ulivyoandika! Hamjui haki zenu na mtaendelea kudhulumiwa sana watanzania.
Hakuna mahali popote Jerry Silaa amefanya ionekane kuwa kazi yake ni "mbadala wa mahakama". Matatizo yote aliyoyashughulikia ni ya uonevu wa baadhi ya watu wanaojiona wao wana uwezo dhidi ya wengine wanaowaonea. Ni hawa hawa kila mara wanaoyatumia hayo mahakama kimakosa kuhalalisha uovu wao

Ukimwondoa Magufuli, na sasa Samia kwa njia tofauti anazotumia kulazimisha mahakama zifanye kazi zake kwa kuangalia wanayoyataka wao; hakuna viongozi wengine chini yao wanaoweza kulazimisha makhakama zifuate matakwa yao.

Haya mnayoyasisitiza hapa, ni yale yale ya utegemezi wa kufanyiana 'favor'. Hakimu anaamua kesi ili amfurahishe waziri, anayemtegemea naye arudishe 'favor' ile ile kwa hakimu katika mambo ambayo waziri anayasimamia.
Hapa mnahusisha hata mawaziri wasiopenda njia hizo, kwa sababu zenu mnazozijuwa wenyewe.
 
Marinda huna, unatembea mzigo unamwagika

Waziri anampamba tu, akienda mahakamani wanafuta, waziri hana maamuzi ya mwisho kuhusu haki, endelea kukenua masaburi tu

Achakukatisha tamaa watu wewe jamaa ndo Mana wazir anawachukua na kuwafungulia kes ya unyang’anyi wao mzee
 
Marinda huna, unatembea mzigo unamwagika

Waziri anampamba tu, akienda mahakamani wanafuta, waziri hana maamuzi ya mwisho kuhusu haki, endelea kukenua masaburi tu

Unaona mtu anashindwa kujieleza kiwanja kapataje mbele ya wazir sasa huko mahakaman anakwenda kueleza nn zaidi ya rushwa na uchawi we nae usipo angalia utakua mchawi ndan ya uzee wako aisee
 
Salaam, Shalom!!

Nimefuatilia Kwa ukaribu jinsi waziri Jerry Slaa anavyofanya katika utatuzi wa migogoro ya ardhi, japo Bado ni mapema sana kusema kuwa anafanya vizuri, lakini Kwa sasa itoshe kusema ana kitu kinachoonekana, na atafika mbali, tuendelee kumwombea.

Nimesikiliza Kwa Umakini jinsi alovyotatua case ya Tajiri aitwaye Mzee Mmassy aliyenunua nyumba Kwa marehemu aliyeko kaburini, yaani document zinaonyesha marehemu akiwa kaburini alisaini mauziano na kumuuzia nyumba tajiri Mmassy,na jinsi alivyotatua case Ile Kwa uwazi Kwa kutumia nyaraka halali katika ofisi ya ardhi, na jinsi alivyoweza kuwarudishia nyumba watoto na mke wa marehemu nyumba Yao, kiukweli Mungu aendelee kumjalia uhai na AFYA na baraka kiongozi huyu.

Nilifanikiwa pia kufuatilia jinsi alivyosaidia kutatua mgogoro ulioletwa na Msama, Kwa kutomtendea HAKI yake mama yule aliyedai kiwanja chake, pia nimeona ufuatiliaji, uthubutu na uchapakazi wa Waziri huyu kijana Jerry Slaa.

Ni maombi yangu, akae chini na viongozi wenzie katika wizara yake na kuja na mpango MIKAKATI wa kutatua migogoro ya ardhi Nchi nzima bila kuwepo haja ya kusafiri huku na huko, uwepo mfumo mzuri na WA haraka zaidi kuwafikia wananchi na kutatua migogoro hiyo ya ardhi.

So far, KAZI imeonekana inafanyika,

Mungu Mbariki Waziri huyu Jerry Slaa,

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Ameeen.

Source: Milard Ayo tv.

Karibuni🙏
Tanzania tunahitaji mawaziri kama hawa si watu kama January Makamba na Nape
 
Back
Top Bottom