Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri
Waziri mkuu unaongea ujinga as if maana ya elimu tanzania ni almost zero au haipo kabisa?

Unawwzqje kusema wenye degree wakasome VETA na at the same time vyuo vinavyotoa degree bado vipo havijafutwa kama kweli Tanzania degree haina maama tena.

Kweli Tanzania ni nchi ya ajabu sana na bado kuna vijana wanasema ccm mbele kwa mbele licha ya matusi haya kwenu?

So, studying for 3 years or 4 years getting degree is wastage of time in Twnzania

Karibuni Chadema tupambane
Waziri yupo sahihi asilimia zote mia
 
Ni wakati Sasa serikali ikubali wamewakosea sana maelfu ya vijana kwa kutokuwa na mpango wa kueleweka wa hatima zao Baada ya kuhitimu.

Sambamba na Hilo serikali iwaunganishe na mataifa yaliyo na upungufu na nguvukazi. Na hayo mataifa YAPO. Waache ukiritimba. Waziri wa Kenya wa masuala ya kazi yupoo very active. Huku kwetu ni kusifu na kuabudu na kuwalisha watu pilau na nyama!

Ujerumani Kuna kipindi walikuwa wanauhitaji wa nguvukazi kwenye sekta ya afya. India waliichangamkia fursa haraka.

Tuache propaganda ambazo hazitupeleki popote kama taifa kwa maslahi tu ya mtu mmoja.

TUSIONE NI FAHARI SANA VIJANA WETU KWA MAELFU WAKIWA BODABODA. HUKO NI KUWAJENGA WACHINA ZAIDI.
 
Umeona wapi waliohitimu VETA wanalalamika Ajira? By the way Bado Wilaya 60 Hazina VETA,Mkoa 1 hauna Veta na zile zilizokamilika ndani ya miaka 4 iliyopita Bado hazijawa well equiped.

Mambo yakishachangabya huko Veta wahitimu watapewa mikopo ya bila riba na Serikali Ili wakafanye kile wanachoona kinaweza wapate Fedha.

Mwisho Hakuna shule za ufundi ziliuwawa ,Kwa Sasa Samia ndio anazifufua na zinajengwa upya
Shule za ufundi ziliuwawa kivipi wakat watu tumesoma hizo shule! Af wasomi wanalalamika ajira lakini hakuna ambae amekufa njaa means watu wanajishughulisha kwamba veta ndo only option serikali imewaza it's okay Kuna almost wahitimu wa 135k wote waende veta wakasome then walimu 150k na wao waende veta wakasome ts oky sera ya nchi kuhusu huko veta inasemaje ? Kwamba wote tukiend hakutokua na saturation mmemlz wote 1m inakuaje ishu sera zinasemaje kuhusu wahitimu wew huwez kumsomesha mtu kwa mkopo ad now unamdai zaid ya 20m af humjengei mazingira ili pesa Yako urudi unamwambia aende veta et ajiajir as the only yu have
 
Haya mambo ni magumu sana, ngoja nisitie neno dhidi ya graduates ambao ni jobless
 
Yeye Kassim Majaliwa alipomaliza certificate ya ualimu ni kwa nini hakwenda veta ili awe fundi seremala?
Kwani mkuu PM amelazimisha wote waende VETA au ametoa wito kulingana na uhitaji wa mtu husika? PM ametoa hamasa, wengine mnafata mkumbo kwa wapotoshaji
 
Sijaona baya ambalo Majaliwa ameongea! Binafsi nilienda UCC kusoma Diploma in Web Dev baada ya kumaliza Masters, na sijui miaka ya sasa lakini wakati ule UCC ilikuwa ni VETA tu iliyochangamka!
 
Lakini kwani amesema kitu gani kibaya au kwani amesema uongo kwamba Hakuna uwezo wa kuwaajiri wahitimu wote wenye madigirii ??!

Sasa kama Serikali haina uwezo wa kuwaajiri wote waliohitimu kuna Ubaya gani mtu kutoa ushauri unaofaa ili watu waweze kujikimu kimaisha. ???!

Mimi naona ni bora yule anayesema kweli kuliko yule atakaye kuwa anatoa ahadi zisizo tekelezeka miaka nenda miaka rudi !

Mtu akisha ambiwa ukweli kwamba hichi kitu hakiwezekani ni lazima awe na Plan B yake afanye nini ili maisha yaendelee ! It’s just as simple as that 😳 !
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu !
 
M
Shida ni kuwa hata hao wa VETA watakuwa wengi sana, kama hakuna viwqnda twaitegemea China tatizo litaendelea kuwepo
Mtu akihitimu kile alichosomea aenda akakifanye mwenyewe kwa kushirikiana na wengine kuanzisha kiwanda au Kazi zozote zile !

Haya mambo ya kusubiri kuajiriwa ndio yanayoleta shida !
Na tukumbuke maisha yenyewe ni mafupi tu muDunia !
Waswahili Wanasemaga Chelewa Chelewa utakuta mwana si wako 😳 !
 
Ninamheshimu sana Waziri mkuu ila katika hili ninampinga 100%. Badala ya kuongea huo utumbo angeshauri serikali iachane na matumizi yasiyo ya lazima ili pesa ziende zikasaidie vijana. Kuna vijana wenye biashara ndogo ndogo za kiubunifu ambapo wangewezeshwa mitaji wangekuza biashara zao na kuajiri wenzao. Kuna haja gani ya kununua VX LC300 mpya na kuachana na V8 za zamani? Mtu kasoma udaktari miaka mitano halafu arudi VETA kusomea cherehani? PM tutake radhi.
 
Nani alikukataza usiwwe na akiki za kwenda shule? Mbona una wivu kwa walisoma. Kwa nini uliogopa umande na unawaonea wivu wasime kama ilivyokuwa kipindi cha jpm kwamba bora tukose wote
Hapa nilipo nina degree na sina ajira na naona mheshimiwa waziri yupo sahihi
 
Achana na huyu Nandagala One

Jamaa analitaka jimbo la Ruangwa; shida yake kabla ya kuanza kutoa hongo kwa wajumbe; anahofia wajumbe wenyewe wana loyalty kwa Majaliwa ndio msingi wa mada zake.

Swala la elimu, sasa huyu Prof Mkenda mwenyewe wakati anazindua mkakati wake alipewa kim dmo cha kuacha porojo na kutoa hotuba.

Maana yake hiyo sera yenyewe hata kwenye baraza la mawaziri aikujadiliwa.

Sasa kama unajua lolote kuhusu strategy za nchi, maswala ya usalama wa taifa uwezi kuwa na sera isiyo-oana na dira ya taifa.

Ni hivi japo PM karopoka kutokana na mazingira husika, ila deep down nchi aina civil service imara.

Story ni ndefu, ila kwa kifupi nchi aina usalama wa taifa imara ndio msingi wa upuuzi.

Usalama wa taifa ni mchezo wa watu wenye akili, at senior level ni watu wenye uwezo wa long term strategic planning.

Ni hivi kazi ya kuongoza nchi sio rahisi.

Hatuko hapo kwa bahati mbaya, ila uwezo wetu mdogo wa kupanga mipango na watu tunaowapa nafasi.

Shida yetu ni uwezo.
Ni upuuzi wa hali ya juu kushindwa kujenga hoja ,kila hoja inayohusu PM, kuhusisha na uchaguzi na jimbo, hivi mimi ndo nilomtuma aropoke???

Kama huna hoja kaa kimyaa, binafsi Sina political ambitions hata chembe, acha kumletea taharuki.

Kwa anayetaka jimbo la Ruangwa ni jepesi mno kuliko watu wanavyodhani, kila muhula ushindi ni WA magumashi kwa wapinzani, ndani ya chama na nje ya chama!!

Nakuambia Ruangwa ni Jimbo jepesi mno kwa mtu anayehitaji, hasa kupitia upinzani!!!
 
Back
Top Bottom