Waziri Mkuu Majaliwa: Wenye degree kasomeni ufundi VETA mjiajiri
Nadhani watatia mkopo wa kusoma VETA!!! Hivi wote waliomaliza VETA wameajiriwa/ wamejiajiri?
Na nani??, Veta inatakuwa kichaka cha serikali kujifichia kushindwa kutengeneza mazingira wezeshi kwa vijana kuajiriwa au kujiajiri!!.
 
Mbona ni kauli yenye kujenga, sema watu kutaka makubwa, na ni kwakuwa hiki ni kipindi cha uchaguzi basi kila kauli itajadiliwa... Simple kama unaoana umesoma na bado degree haijaweza kukutoa ulipo...

Piga kozi za veta kuna mawili aidha ujiajiri ama uajiriwe kwa level ya chini... Sababu huku level ya chini possibility ya kupata ajira ni kubwa kuliko level ya juu

We unahisi ukisoma kozi ya ufundi umeme, huwezi pata hata kazi ya kupiga wiring kwenye majengo?

au kozi ya kuchomelea, huwezi pata fursa ya kutengeneza mageti?
Mkuu elimu sio shida,shida ni elimu ulio nayo inakuletea ugali nyumbani?
Nakumbuka nchini Norway watu hujifunza carpentry welding,painting ili wakiamua kujenga nyumba wapunguze gharama za kuajili mafundi.

Mfano mwingine ni mtu kujifunza kutengeneza bidhaa kama sabuni n.k
Au kupata mafunzo ya kulea watoto wadogo hizo zote zitakuingizia kipato.

Degree itabaki kuwa degree.
 
Huyo eti waziri mkuu akijbu swali la suluhisho la ajira kwa vijana kwny taifa lake, ndo maana linapaka mapiko ili lionekane halina mvi za uzee, ili tuende veta na dgree au masters tunataka tuwaone watoto wa majaliwa, samia, pinda, tulia, nk wakiwa veta.
Ulichoandika mfano wake kwenu muwe hamna uwezo hata wa kupata mlo alafu unasema hautafanya kazi ya kubeba tofali hadi uone mtoto wa Waziri mkuu na Rais na wao wanabeba matofali ndo wewe utabeba.

Sasa unamkomoa nani?
 
Mbona mh. Majariwa yupo sahihi, sema hamtak kuambiwa ukwel.. Koz mambo mengne bdo mnalinganisha kisiasa..
~ mh. Kaona kabxa tatzo la ajira nchin na wasomi ni wengi wahtaj ajira. Wasomi wajiongeze kwa mambo mawili kupitia msemo wa wazir mkuu.
1.- waende VETA wapate ujuz waje wajiajiri wapate pa kujishkiza wakiwa wanasubir ajira za madgree.
2.- wajiajiri wastegemee kuajiriwa pekee, mitaan fursa ni nyingi.
 
Habari!

Elimu ya VETA tunaweza kuiita elimu ya kati. Wakufuzi wake ni wahitimu wa elimu za juu. Wapo pia wakufuzi wenye elimu ya kati, nawafahamu.

Bahati mbaya kauli ya Majaliwa haijawataja hao wenye degree anataka waenda VETA ni degree za fani gani, na je, nini hatma ya elimu yao ya degree.

Huko VETA wakasome kozi za mda gani? Kwa lengo gani? Nani atagharamia ada na mahitaji mengine na nini hatma ya elimu yao ya VETA ikiwa hatma ya degree zao haijapatikana?

Mh. Samia usiogope gharama ya kuvunja bunge kwa kumtimua huyo Mh. Majaliwa.
Majaliwa ni jirani yangu huko Lindi ila kwenye mambo ya kitaifa Mimi sina jirani. Timua kabisa ili kuwepo na funzo kwa viongozi wengine waache kuongea kwa misisimko.

NJE YA MADA

Kama kuna mtoto wa Kiongozi mteule wa Rais anasoma VETA mje mnipige ngumi 4 za puani niko hapa TAZARA Dar es salaam nawasubiri.

Achana na watoto wa vichochoroni, nazungumzia mtoto aliyekulia nyumba za bure za viongozi.
Acheni ujinga nyinyi mnaorukia kauli za viongozi pasipo kutafakari na mihemuko yenu. Mheshimiwa waziri Mkuu yuko sahihi.
mbona leo tunaona hao waliomALIZA DEGREE ZAO WANENDESHA BODA? mbona hilo hamjalilalamikia? hiyo leseni ya uendeshaji wa vyombo vya usafiri inapatikana wapi? kama sio VETA? mbona wanaenda kusoma VETA kupata Leseni? Au unadhani kupata degree ndo umemaliza maisha?
 
Acheni ujinga nyinyi mnaorukia kauli za viongozi pasipo kutafakari na mihemuko yenu. Mheshimiwa waziri Mkuu yuko sahihi.
mbona leo tunaona hao waliomALIZA DEGREE ZAO WANAENDESHA BODA? mbona hilo hamjalilalamikia? hiyo leseni ya uendeshaji wa vyombo vya usafiri inapatikana wapi? kama sio VETA? mbona wanaenda kusoma VETA kupata Leseni? Au unadhani kupata degree ndo umemaliza maisha? Pata Ujuzi mbalimbali ili uwe marketable kwa fursa pia nyingi nyingi,
 
Wewe umejiajiri au umeajiriwa?
Uwen umeajiriwa au la, kasome VETA acha Uvivu, Soma tafuta kazi zinazotokana na mafunzo ya veta utakuwa na fursa ya kutengeneza Fedha. Tatizo ni kukariri ukoloni wa Kuajiriwa
Naunga mkono kauli ya Mheshimiwa waziri mkuu, Mwezi Julai 2025 tukutane VETa, mimi naingia darasa la VETapamoja na kuwa na Masters.
 
Acheni ujinga nyinyi mnaorukia kauli za viongozi pasipo kutafakari na mihemuko yenu. Mheshimiwa waziri Mkuu yuko sahihi.
mbona leo tunaona hao waliomALIZA DEGREE ZAO WANAENDESHA BODA? mbona hilo hamjalilalamikia? hiyo leseni ya uendeshaji wa vyombo vya usafiri inapatikana wapi? kama sio VETA? mbona wanaenda kusoma VETA kupata Leseni? Au unadhani kupata degree ndo umemaliza maisha? Pata Ujuzi mbalimbali ili uwe marketable kwa fursa pia nyingi nyingi,
Mkuu kama unaona PM kaongea point basi utakuwa ni mtu uliyekata tamaa ya maisha kabisa. Vijana wa Tanzania wanahitaji sheria na sera bora zaidi kuweza kuwa na mifumo imara ya kuwasaidia kufanya shughuli zao. Kuendesha bodaboda sio jambo la kufurahia. Kauli ya PM inamfanya awe level moja na kina Msukuma au Babutale.
 
Ukimaliza degree unajisajili PSRS hapo huwezi tena kuajirika kwa astashahada au stashahada labda kwa mchina ukalipwe laki mbili na nusu.
Mfumo wa PSRS hauwezi kumuajiri mtu kwa low entry level huku profile yake iko juu. Au wewe utakubali ukimaliza elimu ya degree ya miaka 3 au 4 usijisajili PSRS badala yake usubiri umalize kozi ya miaka 2 au 3 ya VETA ndipo ujisajili kwa level ya chini?
Yaani umalize degree na uisahau kabisa
Kwaiyo mzee ukishakosa kazi serikalini ndo basi tena?
 
Kwanza kabisa kwa kunipa historia. Ninachopingana nacho ni uwongo wa Kasimu majaliwa kuhusi afya ya Magufuli. Kwani angesema anaitwa lakini ana hali nzuri au akakaa kimya kabisa kitu gani kingetokea.
Eti "Yuko timamu na anaendelea na majukumu yake" wakati mtu kashafariki
Sikuelezei tena. Kama hujaelewa.
 
Hivi degree ni kitu gani kwani mtu anamaliza na hajui chochote hadi aelekezwe tena.

Waziri Mkuu yuko sawa kama hawataki wakae nyumbani wazeeke na degree zao.
Wqziri Mkuu inawezekana kakosea kuwasilisha hoja, inawezekana hakuiwasikisha vizuri.

Lakini hoja hii si mpya. Rais Nyerere kaisema sana, mpaka kuna wakati aliiandika katika vitabu kama "Elimu ni Kazi". Watu wamesahau tu au hawakufuatilia.

Aung San Suu Kyi kashalisema hili Myanmar.

Jamii imeweka msisitizo sana kwenye elimu ya chuo kikuu na kudharau elimu ya ufundi, wakati elimu zote mbiki zinatakiwa kwenda pamoja.

Ila, viongozi nao wanasema maneno bila kuweka mikakati ya hayo maneno kutimia.

Mfano, kumwambia kijana ajifunze kushona nguo VETA wakati serikali inaruhusu uingizaji wa mitumba mingi ya bei nafuu bila hata regulation ni kum set huyu mwanafunzi wa VETA for failure.

Ona hapa Aung San Suu Kyi aliongelea suala hili.


"Daw Aung San Suu Kyi urged youth to “open their eyes and ears for more opportunities” and to develop the capacity to handle many other jobs.” The State Counsellor promoted vocational education, telling the public in Kalay that university education and vocational training are equally important, and that her government is doing its best to reduce unemployment."

Nyerere pia kaongea sana kuhusu Education for Self Reliance.
 
Habari!

Elimu ya VETA tunaweza kuiita elimu ya kati. Wakufuzi wake ni wahitimu wa elimu za juu. Wapo pia wakufuzi wenye elimu ya kati, nawafahamu.

Bahati mbaya kauli ya Majaliwa haijawataja hao wenye degree anataka waenda VETA ni degree za fani gani, na je, nini hatma ya elimu yao ya degree.

Huko VETA wakasome kozi za mda gani? Kwa lengo gani? Nani atagharamia ada na mahitaji mengine na nini hatma ya elimu yao ya VETA ikiwa hatma ya degree zao haijapatikana?

Mh. Samia usiogope gharama ya kuvunja bunge kwa kumtimua huyo Mh. Majaliwa.
Majaliwa ni jirani yangu huko Lindi ila kwenye mambo ya kitaifa Mimi sina jirani. Timua kabisa ili kuwepo na funzo kwa viongozi wengine waache kuongea kwa misisimko.

NJE YA MADA

Kama kuna mtoto wa Kiongozi mteule wa Rais anasoma VETA mje mnipige ngumi 4 za puani niko hapa TAZARA Dar es salaam nawasubiri.

Achana na watoto wa vichochoroni, nazungumzia mtoto aliyekulia nyumba za bure za viongozi.
Fahamu Kuna kitu kinaitwa retrain or upgrade skills to enhance your chances of either employment or self employment.
Enzi za serikali kuajiri na kuajiri imepitwa na wakati. Tumia elimu yako uliopata kufungua njia upate maisha.
Bado Tanzania Kuna Fursa za kujiengea maisha bila kukaa kulia Lia na kulaumu serikali.
 
He was right though simkubali huyu jamaa ni very low education personnel to hold such power
 
1741942227410.jpg
 
Habari!

Elimu ya VETA tunaweza kuiita elimu ya kati. Wakufuzi wake ni wahitimu wa elimu za juu. Wapo pia wakufuzi wenye elimu ya kati, nawafahamu.

Bahati mbaya kauli ya Majaliwa haijawataja hao wenye degree anataka waenda VETA ni degree za fani gani, na je, nini hatma ya elimu yao ya degree.

Huko VETA wakasome kozi za mda gani? Kwa lengo gani? Nani atagharamia ada na mahitaji mengine na nini hatma ya elimu yao ya VETA ikiwa hatma ya degree zao haijapatikana?

Mh. Samia usiogope gharama ya kuvunja bunge kwa kumtimua huyo Mh. Majaliwa.
Majaliwa ni jirani yangu huko Lindi ila kwenye mambo ya kitaifa Mimi sina jirani. Timua kabisa ili kuwepo na funzo kwa viongozi wengine waache kuongea kwa misisimko.

NJE YA MADA

Kama kuna mtoto wa Kiongozi mteule wa Rais anasoma VETA mje mnipige ngumi 4 za puani niko hapa TAZARA Dar es salaam nawasubiri.

Achana na watoto wa vichochoroni, nazungumzia mtoto aliyekulia nyumba za bure za viongozi.
Huu Uzi hauna mudaa wata ufutaa...Jana nilikutana na huu Uzi nikajikunja kuchangia baada ya muda ukafutwa.

Niliumia kupoteza muda kuandaa point zangu na click batan nikazinguka opppsss something went wrong..🏃🏃🏃
 
Back
Top Bottom