Waziri Prof. Mkenda dhambi hii ya udahili vyuoni isisubiri tamko la Rais Samia

Waziri Prof. Mkenda dhambi hii ya udahili vyuoni isisubiri tamko la Rais Samia

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Elimu ndio chombo pekee kinachoweza kuwakutanisha mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini katika ofisi moja na mgahawa mmoja. Takwimu zinaonyesha kuwa shule binafsi za msingi na sekondari nchini ni ghali kuliko za serikali lakini ndizo zenye mazingira mazuri ya kujifunzia na kutoa ufaulu mkubwa kwa wanafunzi wengi.

Na vyuo vikuu vya Serikali ni nafuu kusoma lakini ndivyo vyenye mazingira mazuri na miundombinu ya kufundishia na watoto kupata taaluma ya uhakika. Mpaka hapo hatubishani na hakuna ubishi.

Dhambi inakujaje wakati wa udahiri wa wanafunzi?
1. Vyuo vya serikali vinatoza ada ndogo sana lakini vinadahiri wanafunzi wenye ufaulu mkubwa sana(e.g Muhimbili University), bila shaka wengi wa wanafunzi wenye sifa hizi wengi wao ni wale wanaotoka kwenye shule za binafsi za sekondari kama FEZA, kanosa, etc.

Wazazi wa watoto hawa wengi wao ni wale wenye uchumi wa juu na wakati nchini ambao wanafahamu kuwa vyuo vya serikali vina walimu bora na miundombinu mizuri ya elimu, hivyo pamoja na kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha wa kuendelea kuwasomesha watoto vyuo binafsi nchini na nje ya ya nchi lakini hawawapeleki watoto wao kwenye vyuo binafsi nchini kwakuwa wanavijua kuwa hata walimu wao ni wazee waliochoka na vijana wasiokuwa na uwezo mkubwa wa kufundisha.

2. Vyuo vya binafsi havina miundombinu mizuri ya kufundishia (walimu, madarasa, practice, library, office, ect) lakini vinatoza ada kubwa sana ili kumudu kulipa mishahara ya watumishi, majengo, na tozo mbalimbali za serikali. Pamoja na ughali wa vyuo hivi lakini Watoto wa maskini waliosoma shule za serikali wanajikuta wakisukumiwa kwenye aina hii ya vyuo baada ya kukosa nafasi kwenye vyuo vya serikali vyenye ada ambayo wazazi wangeimudu kulipa japo pia kwa tabu.

Kadhia hii inasababisha mambo mabaya sana kwa watoto na wazazi wao zikiwemo za wazazi kuuza kila kitu yaani kila kitu cha familia ili kumudu ada ya mtoto mmoja kwenye chuo binafsi, watoto kukosa mitihani na kuacha shule kwa kukosa ada, wanafunzi kujiingiza kufanya vitendo vibaya vya kuuza mili na madawa au kufanya biashara na wizi ili kusaidia wazazi wao kujaza kile kinachokosekana kwenye gharama za vyuo binafsi.

3. Fedha ya serikali (loans board) inapotea bure kwa watoto hawa kwenye vyuo binafsi. Yaani mtoto anaacha chuo katikati kwa kukosa kulipa kiasi cha ada kujalizia kile cha mkopo alichopewa na loans board. Watoto hawa wanateseka sana vyuoni kwasababu wanalazima kutumia ile meals and accommodations wanayopewa kwa kulipia ada zao. Mtoto akiacha masomo maana yake hata kiasi alichokopeshwa na loans board kimepotea pia.

4. Scholarships na mikopo vinaangalia ufaulu wa mtoto bila kuangalia mtoto kasoma shule gani. Hii inamaanisha kuwa wenye nacho wataongezewa pia hapa. Yaani watoto wa wenye nacho ndio waliosoma shule za private na wengi ndio wenye ufaulu mkubwa kuweza kuwa na sifa za kupata scholarships na mikopo.

5. Mtoto wa Maskini hatakutana na mtoto wa tajiri ofisi moja kama trend itakuwa hiihii.


Hapa ni ama;
Shule za Serikali pia ziongezewe ubora katika kutoa elimu, vyuo vya private vipewe ruzuku na serikali ili ada yao pia iwe himilivu au vyuo vya serikali vihudumie zaidi shule za serikali.

Mifumo ya Serikali lazima isomane, haiwezekani vyuo vya serikali na shule za serikali hiyohiyo havisomani, yaani shule za serikali zinazalisha watoto wasiotakiwa na vyuo vya serikali.
 
Udahili wa chuo kigezo ni kimoja tu, ufaulu wa mwanafunzi. Hizo nyingine za sijui kipato cha mzazi ni siasa!

Jambo la muhimu ni bodi ya mikopo itoe mikopo kwa wote wanao omba. Mtu mzima anaomba mkopo maana yake anauhitaji, waaache ujinga wao.
 
Umenena kweli kabisa serikali ifanye mageuzi hapa wanafunzi waangaliwe toka mwanzo wa shule za serikali wapewe kipaumbele bila kuangalia ufaulu wa matokeo.

Hali ni mbaya vijana wanateseka sana vyuo vikuu hela ya kula na malazi ndo inaongezwa Kwenye ada ya watoto wa maskini hasa wakipata udahili kwenye vyuo binafsi..hufanya waishi kwa taabu sana
 
Udahili wa chuo kigezo ni kimoja tu, ufaulu wa mwanafunzi. Hizo nyingine za sijui kipato cha mzazi ni siasa!

Jambo la muhimu ni bodi ya mikopo itoe mikopo kwa wote wanao omba. Mtu mzima anaomba mkopo maana yake anauhitaji, waaache ujinga wao.
Mikopo inatolewa kwa kutumia vigezo vya vyuo vya serikali. Ada chuo cha serikali ni 1.5m kwa mwaka lakini vyuo vya private ada inafika hadi 7.0 m, maana yake hata wanafunzi wote watapewa mikopo 1.5m yule anaesoma chuo binafsi atatakiwa atafute 5.5m zaidi. Unataka kusema kuwa shule za sekondari za serikali hazihitaji watoto wenye ufaulu mkubwa kutoka shule za msingi? Kutoka shule ya msingi kwanini hawakwenda shule za serikali, kwanini vyuo vikuu wanakwenda vyuo vya serikali? Yaani wao wanatafuta nafuu na ubora all the time kwa kutumia nguvu zao za kifedha.
 
Kuna watoto wengi wapo Muhimbili, UDSM, Mzumbe, UDOM ambao wamesoma St Kayumba!
Sula ni kufaulu tu
lete takwimu zao, wangapi wametoka shule za aina ipi. Kama wapo huko basi ni baada ya wenye ufaulu mkubwa saaana kuwa wacheche kuliko nafasi walizokuwa nazo
 
Udahili wa chuo kigezo ni kimoja tu, ufaulu wa mwanafunzi. Hizo nyingine za sijui kipato cha mzazi ni siasa!

Jambo la muhimu ni bodi ya mikopo itoe mikopo kwa wote wanao omba. Mtu mzima anaomba mkopo maana yake anauhitaji, waaache ujinga wao.
Kaka ni kweli, lakini mifumo yote ya serikali ni lazima isomane, vyuo vya serikali haiwezekani visisomane na shule za serikali, Hii ina maana kwamba zile 600 Samia scholarships kwa watoto watakaosoma kozi za sayansi zitakwenda kuwanufaisha watoto wa vigogo na kuwaacha watoto wa wakulima na wavuvi nchini.
 
Kuna watoto wengi wapo Muhimbili, UDSM, Mzumbe, UDOM ambao wamesoma St Kayumba!
Sula ni kufaulu tu
Binafsi nimeona kwa macho mtoto aliyesoma shule ya serikali ya kata na kupata division 1 points 7 masomo ya sayansi (PCB) lakini amekosa udahiri chuo Cha serikali.
 
Jambo la muhimu ni kuifuta loan board ili serikali itumie utaratibu wa awali ambapo ilikuwa inatoa ufadhili kwa wanafunzi waliokuwa wakidahiliwa kwenye vyuo vya umma kupitia wizara ya elimu. Endapo loan board itaendelea kuwepo basi ihusike zaidi na vyuo vya binafsi. Pia mazingira ya utoaji wa elimu ya msingi na sekondari kwa shule za serikali yaendelee kuboreshwa. Hii italeta ushindani sawa kati ya watoto wa matajiri na watoto wa wanyonge kwenye kupambania nafasi za udahili katika vyuo vya umma ambako watakuwa wanapata ufadhili (grants) ambazo zinatokana na kodi za wananchi.​
 
Jambo la muhimu ni kuifuta loan board ili serikali itumie utaratibu wa awali ambapo ilikuwa inatoa ufadhili kwa wanafunzi waliokuwa wakidahiliwa kwenye vyuo vya umma kupitia wizara ya elimu. Endapo loan board itaendelea kuwepo basi ihusike zaidi na vyuo vya binafsi. Pia mazingira ya utoaji wa elimu ya msingi na sekondari kwa shule za serikali yaendelee kuboreshwa. Hii italeta ushindani sawa kati ya watoto wa matajiri na watoto wa wanyonge kwenye kupambania nafasi za udahili katika vyuo vya umma ambako watakuwa wanapata ufadhili (grants) ambazo zinatokana na kodi za wananchi.​
Kweli kabisa, maana haina maana yoyote kwa serikali kutoa elimu bure shule za msingi na sekondari halafu ghafla mtoto huyohuyo anasukumiwa chuo binafsi akalipie sh. 6.5m kwa mwaka, na yule mtoto aliyekuwa anasoma shule za msingi na sekondari binafsi kwa sh. 5-10m kwa mwaka ghafla anajikuta yuko kwenye chuo kikuu cha serikali cha 1.5m kwa mwaka, kisa eti ana ufaulu mkubwa. Huu ni upuuzi sawa na upuuzi mwingine tu mitaani.

Maprofessor wetu jamaniiii msaidieni Rais kuhuhudumia wananchi wake. Kwanini vyuo vya serikali visihangaike kwanza na watoto hawa wa elimu bure walioko kwenye Ilani ya chama?

Vyuo vikuu vinaihujumu serikali. Hebu nenda pale MUHAS ukaone imedahiri watoto wenye ufaulu gani na ni watoto wa akina nani waliosoma shule gani. Tuanzie hapo kwanza.
 
Elimu ndio chombo pekee kinachoweza kuwakutanisha mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini katika ofisi moja na mgahawa mmoja. Takwimu zinaonyesha kuwa shule binafsi za msingi na sekondari nchini ni ghali kuliko za serikali lakini ndizo zenye mazingira mazuri ya kujifunzia na kutoa ufaulu mkubwa kwa wanafunzi wengi.
Mtoto wa masikini lazima apambane asome kweli kweli ili apate scholarship maana hii scholarship haijamlenga tajiri au masikini imemlenga mtoto wa mtanzania yeyote atakae faulu vizuri masomo ya sayansi
 
Kweli kabisa, maana haina maana yoyote kwa serikali kutoa elimu bure shule za msingi na sekondari halafu ghafla mtoto huyohuyo anasukumiwa chuo binafsi akalipie sh. 6.5m kwa mwaka, na yule mtoto aliyekuwa anasoma shule za msingi na sekondari binafsi kwa sh. 5-10m kwa mwaka ghafla anajikuta yuko kwenye chuo kikuu cha serikali cha 1.5m kwa mwaka, kisa eti ana ufaulu mkubwa. Huu ni upuuzi sawa na upuuzi mwingine tu mitaani. Maprofessor wetu jamaniiii msaidieni Rais kuhuhudumia wananchi wake. Kwanini vyuo vya serikali visihangaike kwanza na watoto hawa wa elimu bure walioko kwenye Ilani ya chama? Vyuo vikuu vinaihujumu serikali. Hebu nenda pale MUHAS ukaone imedahiri watoto wenye ufaulu gani na ni watoto wa akina nani waliosoma shule gani. Tuanzie hapo kwanza.
Hakuna kitu kama icho kwaiyo ukienda kwenye vyuo vya serikali wanaosoma wengi ni watoto waliotoka private? hapana kabisa nina mdogo wangu amesoma muhimbili na ametoka shule ya kawaida kabisa kikubwa watoto wajitahidi wafaulu alafu wakinyimwa iyo nafasi ya kusoma tuanzie hapo
 
Jambo la muhimu ni kuifuta loan board ili serikali itumie utaratibu wa awali ambapo ilikuwa inatoa ufadhili kwa wanafunzi waliokuwa wakidahiliwa kwenye vyuo vya umma kupitia wizara ya elimu. Endapo loan board itaendelea kuwepo basi ihusike zaidi na vyuo vya binafsi. Pia mazingira ya utoaji wa elimu ya msingi na sekondari kwa shule za serikali yaendelee kuboreshwa. Hii italeta ushindani sawa kati ya watoto wa matajiri na watoto wa wanyonge kwenye kupambania nafasi za udahili katika vyuo vya umma ambako watakuwa wanapata ufadhili (grants) ambazo zinatokana na kodi za wananchi.​
Sekta ya elimu imeboleshwa sana ndio maana ata umeona katika matokeo ya mwaka huu shule za serikali zimeongoza
 
Udahili wa chuo kigezo ni kimoja tu, ufaulu wa mwanafunzi. Hizo nyingine za sijui kipato cha mzazi ni siasa!

Jambo la muhimu ni bodi ya mikopo itoe mikopo kwa wote wanao omba. Mtu mzima anaomba mkopo maana yake anauhitaji, waaache ujinga wao.
Umenena vyema kupata nafasi ya chuo ni ufaulu mzuri basi hakuna cha mtoto wa tajiri au masikini issue ni kufaulu
 
Elimu ndio chombo pekee kinachoweza kuwakutanisha mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini katika ofisi moja na mgahawa mmoja. Takwimu zinaonyesha kuwa shule binafsi za msingi na sekondari nchini ni ghali kuliko za serikali lakini ndizo zenye mazingira mazuri ya kujifunzia na kutoa ufaulu mkubwa kwa wanafunzi wengi.
Kaka uzi wako umeingiliwa na wtu wenye IQ ndogo mnoo.. naomba uwavumilie tu.. yaan hawajaelewa kabisa mantik yako
 
Kama unataka udaktari na ma afya piga one kali ya 5 kurudi 3.

Kama unataka chuo cha serikali mwambie mwanao agonge one au two! Udsm, udom, mzumbe, aru, tia, ifm na cbe zinawangoja!

Kama utalamba three utafungua uzi mwng sana
 
Kaka uzi wako umeingiliwa na wtu wenye IQ ndogo mnoo.. naomba uwavumilie tu.. yaan hawajaelewa kabisa mantik yako
Nahamu kuwa hata kufikiri na kutafakari kwa kina kunahitaji kuwa na akili maalumu. Kila mtu anayo akili lakini wenye akili timamu sio kila mtu.

Chuo kikuu cha serikali kunyanyapaa wanafunzi wanaotoka shule za serilali kwa kisingizio cha aina yoyote haikubaliki.

Mimi nina ushahidi kuwa watoto wanaotoka shule za msingi na serikali serikali zenye msongamano mkubwa wa wanafunzi, walimu wachache, maabara chache na miundombinu hafifu sana kama atafika chuo kikuu na ufaulu wa division III, II au 1 ya mwisho kabisa anafanya vizuri sana kuliko mwanafunzi aliyepata alama A zote kutoka shule za private.

Wanafunzi kutoka private schools wengi wao wanakuwa na faida ya kuongea lugha ya kiingereza vizuri lakini uwezo wao kufikiria ni mdogo sana. Naomba mtu ufanye utafiti wake kwenye hili.
 
Kumbe wale waliosoma shule za FEZA, KEMEBOS, BABRO na wale wa kupelekwa na school bus nao wanaishia vyuo hivi hivi vya hapa nchini kama st Kayumba? Nilojua safari yao ni Oxford, Yale, Havard n.k
 
Kama unataka udaktari na ma afya piga one kali ya 5 kurudi 3.

Kama unataka chuo cha serikali mwambie mwanao agonge one au two! Udsm, udom, mzumbe, aru, tia, ifm na cbe zinawangoja!

Kama utalamba three utafungua uzi mwng sana
shule za private zinakaririsha maswali, zinaiba mitihani, zinaonyesha mitihani, wako wachache darasani, nk huko ni rahisi kuwapata watoto wenye ufaulu wa hivyo, je, shule za umma hazitaki watoto kutoka shule za umma? ni watoto wangapi kutoka shule za umma wana ufaulu wa point 3, 4 na 5? bogus
 
Back
Top Bottom