Waziri Prof. Mkenda dhambi hii ya udahili vyuoni isisubiri tamko la Rais Samia

Waziri Prof. Mkenda dhambi hii ya udahili vyuoni isisubiri tamko la Rais Samia

"like dissolve like" shule za serikali
Umeitumia mahala ambapo sipo hii kanuni. Hata shule za private ni za serikali pia. Diania ya leo serikali haiwezi ikafanya kila kitu ndiyo maana kuna PPP policy.

Private zinaisaidia serikali pahala ambapo haiwezi. Kwahiyo ustake kuhalalisha ubaguzi wa kivipato.
 
Mtoto ambae hakusoma shule za serikali hawezi kuwa kiongozi mzalendo

Watoto waliotoka ktk familia zenye uwezo ndiyo wazalendo na, huongoza mabadikiko ya kweli.

Mwalimu Julius Nyerere mtoto wa chifu, Fidel Castro mtoto wa mkulima mkubwa 'bepari' listi ni ndefu
 
Umenena kweli kabisa serikali ifanye mageuzi hapa wanafunzi waangaliwe toka mwanzo wa shule za serikali wapewe kipaumbele bila kuangalia ufaulu wa matokeo.

Hali ni mbaya vijana wanateseka sana vyuo vikuu hela ya kula na malazi ndo inaongezwa Kwenye ada ya watoto wa maskini hasa wakipata udahili kwenye vyuo binafsi..hufanya waishi kwa taabu sana
Halafu tunalalamika ndoa hazidumu siku hizi, wakati mama kaanza kudanga toka akiwa anasoma na baba naye kashazoea kulelewa asukume maisha mbele..!! Hali ni mbaya sana kwa kweli sijui tunaelekea wapi...???
 
Binafsi nimeona kwa macho mtoto aliyesoma shule ya serikali ya kata na kupata division 1 points 7 masomo ya sayansi (PCB) lakini amekosa udahiri chuo Cha serikali.
A level alipata ufaulu upi?
 
Umeitumia mahala ambapo sipo hii kanuni. Hata shule za private ni za serikali pia. Diania ya leo serikali haiwezi ikafanya kila kitu ndiyo maana kuna PPP policy.

Private zinaisaidia serikali pahala ambapo haiwezi. Kwahiyo ustake kuhalalisha ubaguzi wa kivipato.
Weeee!!! nimeitumia kwa kumaanisha kabisa. Vyuo vikuu vya serikali ni vyombo vya serikali vinavyotakiwa kutafsiri kwa vitendo sera ya elimu nchini. Mnyororo wa thamani wa elimu unaanzia chekechea hadi vyuo vikuu vya serikali kwa slogan ya "garbage in garbage out". Ona vyuo vyetu vya serikali havitaki kunasibishwa na dhaifu wa products za shule zao za serikali, hivyo wanatafuta malighafi nje ya serikali,. Hata huko nchi za Magharibi shule na vyuo vya serikali sio vizuri sana kulinganisha na baadhi ya vyuo binafsi.
 
Mtoto wa masikini lazima apambane asome kweli kweli ili apate scholarship maana hii scholarship haijamlenga tajiri au masikini imemlenga mtoto wa mtanzania yeyote atakae faulu vizuri masomo ya sayansi
Watu wenye akili nyingi kama Nyerere alifahamu kuwa elimu ni silaha sawa na silaha nyingine za mass distraction. Ilimfanya achukue uamuzi mgumu sana kama wa kutaifisha shule binafsi na kumsomesha bure kila mtu ili kutengeneza umoja huu unaouona Leo. Watu kama nyinyi wenye mawazo kama haya ni magugu kwenye ustawi wa taifa, mmevaa miwani ya Mbao.

Kama utachunguza Sana Ile hofu ya Mwl Nyerere iliyomfanya azitaifishe zile shule zipo hadi Leo. Leo hii watu wenye uwezo wa kumsomesha mwanawe shule binafsi ni wale wenye ajira, na wafanyabiashara wakubwa na wakati. Ukiziangalia ajira zetu maofisini Zina harufu Fulani.
 
Kuna watoto wengi wapo Muhimbili, UDSM, Mzumbe, UDOM ambao wamesoma St Kayumba!
Suala ni kufaulu tu
Nilikupa thanks, lakini kwa maandishi nasema foolish! Muhimbili imejaa rushwa, nepotism, ukabila, na umwanga mshenzi tu! Kwa ufupi, watoto wa maskini kwa sasa hawataweza tena kusoma medicine.

Hilo jambo aliloandika mleta thrd liangaliwe na watu wenye akili siyo kila mwenye akaunti ya JF. Waziri na rais Samia wote wanajichanganya. Karibuni Waziri alisema kuna Samia Scholarships kwa wanafunzi wa sayansi je, anajua wanafaulu sayansi wanatoka shule gani? Ni aibu kufikia uwaziri lakini huna analytical brain zaidi ya ukorofi tu!

Hakuna mwanafunzi wa shule ya kata ya form 1-4 na 5-6 anayeweza kupata sholarship kama hiyo. Ni uzembe mkubwa kwa waziri anayejiita profesa kusihia kutaja ufauklu kama kigezo pekee cha haki ya kusoma.
 
Hii sio siasa kaka bali ni kufa na kupona, watanzania hali zao ni mbaya sana kiuchumi, ndio maana CCM ikaja na sera ya elimu bure. Huyu aliyesoma bure Sasa vyuo vyao vinakwenda kukaliwa na watoto ambao hawakupenda kusomeshwa bure na serikali kwakuwa Wanazo pesa. Ni heri hawa wa private waendelee na mkondo wao wa private ili wale watoto wa maskini waendelee ku enjoy elimu nafuu vyuoni. Serikali lazima ijieleze ni kwa vipi mtoto aliyesoma bure shule za awali ghafla awe na uwezo wa kusoma chuo Cha 7m kwa mwaka? Are we realistic? Are we mad?
Kwani hao watoto siyo watanzania? Why wabaguliwe? Msilete siasa kwenye mambo serious, kama ni kutoa elimu bora boresheni elimu kwakutumia kodi za raia na msisingizie watanzania ambao wana haki sawa awe ni tajiri au masikini...Mkose njia bora za kuleta maendeleo kwakukosa innovation na hiyo incapabilities zenu mzi project kwa watanzania? Kama mmeshindwa una resign from where you are and leave those who are capable to do apropriate things...
 
Watu mnaanza kutumia mabavu kuficha incapabilities zenu, watanzania kwanini wawe maskini? With all these resources watu mnawaita masikini, why? Ni wewe unayeshindwa ku translate hizi resources za watanzania kwa kukosa ubunifu na sera bora kuongeza welfare ya raia then you come forward crying like a baby eti watanzania masikini...Masikini ni wewe mwenye mawazo mafupi yasiyoweza kuongeza tija kwenye maisha ya watanzania na kwakua mtu hajui jinsi ya ku create wealth then anataka kila mtu awe victim wa circumstances anayo i create yeye kwakung'ang'ania ku ongoza hata pale asipokuwa na uwezo....hii nchi si mali ya mtu au kundi la watu, kila raia anahaki ya kusoma sehemu anayoiona inafaa ilimradi anakizi vigezo. Umasikini si criteria ya mtu kusoma au kutokusoma, mmelazimisha haya na sasa mambo yameparaganyika you come up with funny proposals za kibaguzi na kunyanyasa raia wasio na hatia.
 
kaka mtoto anaesoma chuo binafsi kozi ya miaka 5 atahitaji mko wa sh. 10m x 5 = 50,000 tution fee na stationary tu wakati yule anaesoma shule ya serikali atahitaji mkopo wa shi 3m x 5 = 15,000 tu. Wote hawa wanakwenda kuhudumia watanzania baada ya masomo yao.
Badala ya kuhoji kwanini mtoto wa masikini aliyesoma shule ya serikali asifaulu kama yule wa shule binafsi huku chini lakini the pattern inageuka elimu ya juu, you come with allegations badala ya facts?

I think you need to stop being naive like this, sorry unani provoke na uandishi wako kwakua unaonekana kupenda kuleta simple answers kwenye serious na critical issues
 
Mkuu ni bahati mbaya kwamba hiki unachokisema hakipo na hakitakaa kiwepo, siku kikiwepo basi tutakuwa tumefikia pabaya zaidi. Admission za vyuo hazitolewi kama hisani bali kwa merits. Ni bahati mbaya pia kwamba kuwachukua waliofeli kisa wametoka shule za kayumba sio kuwasaidia. Wengi hawa utakuwa unawapeleka kwenye moto bila sababu. Usisahau disco ni jambo la kawaida kwenye hivi vyuo unavyotaka viwape waliofeli nafasi. Ni vema vikaendelea kupokea watu wenye uwezo na kwa hapa hakuna kipimo kingine zaidi ya ufaulu wa mitihani yao ya form four na six.
Ahsante kwa mchango wenye tija kwa taifa letu...
 
Kwani hao watoto siyo watanzania? Why wabaguliwe? Msilete siasa kwenye mambo serious, kama ni kutoa elimu bora boresheni elimu kwakutumia kodi za raia na msisingizie watanzania ambao wana haki sawa awe ni tajiri au masikini...Mkose njia bora za kuleta maendeleo kwakukosa innovation na hiyo incapabilities zenu mzi project kwa watanzania? Kama mmeshindwa una resign from where you are and leave those who are capable to do apropriate things...
Hao watoto walijibagua wao wenyewe na wazazi/walezi wao, waliziita shule zote za serikali na zile za kata kuwa ni za kishenzi na kuibeza serikali kwenye mipango yake ya kumsogezea karibu shule kwa kuzijenga kila kata na kuondoa ada. Wazazi hawa wakazipuuza shule na jitihada hizi za serikali na kupeleka watoto wao shule za ghrama kubwa. Nia yao ni uvu sana hawa watu kwani walikuwa wanawakatisha tamaa watoto wa masikini wanaosoma hizi shule za serikali zisizokuwa na mabweni, usafiri, mabweni, chakula shuleni wala madawati. Kinachowashangaza walalahoi ni kuona hawa watoto waliozinyanyapaa shule za serikali wanakwenda kuvikimbilia vyuo vya bei nafuu vya serikali na kuwasukumia watoto maskini kule vyuo binafsi kwenye ada kubwa kwa kisingizio cha ufaulu, nonsense!!!

Kila msiba una mwenyewe, msiba wa watoto waliosoma shule za kata (st. Kayumba) mwenyewe ni vyuo vikuu vya serikali. Watoto hawa wavijaze vyuo hivi vya serikali kwanza kabla ya watoto wengine kupata nafasi huko. Serikali (TCU) wametoa ufafanuzi ni mtoto yupi amefaulu na yupi amefeli, mtoto yupi anaweza kusoma kozi gani na yupi hawezi. Vyuo vya serikali havina hiari kwenye jambo hili la kisera. Vyuo binafsi ndio viwe na hiari ya kuchagua cut-off points zao.
 
Watu mnaanza kutumia mabavu kuficha incapabilities zenu, watanzania kwanini wawe maskini? With all these resources watu mnawaita masikini, why? Ni wewe unayeshindwa ku translate hizi resources za watanzania kwa kukosa ubunifu na sera bora kuongeza welfare ya raia then you come forward crying like a baby eti watanzania masikini...Masikini ni wewe mwenye mawazo mafupi yasiyoweza kuongeza tija kwenye maisha ya watanzania na kwakua mtu hajui jinsi ya ku create wealth then anataka kila mtu awe victim wa circumstances anayo i create yeye kwakung'ang'ania ku ongoza hata pale asipokuwa na uwezo....hii nchi si mali ya mtu au kundi la watu, kila raia anahaki ya kusoma sehemu anayoiona inafaa ilimradi anakizi vigezo. Umasikini si criteria ya mtu kusoma au kutokusoma, mmelazimisha haya na sasa mambo yameparaganyika you come up with funny proposals za kibaguzi na kunyanyasa raia wasio na hatia.
Huna unachokifahamu wewe, Mwl. Nyerere alitusomesha bure sisi wote kwa dhana kwamba wako maskini ambao wasingeweza kumudu kusoma na kusomesha. Serikali yetu ya sasa imefuta ada kuanzia chekechea hadil A level kwa sababu hizohizo kubwa hata yule mwenye ajira ujira anaoupata ni mdogo sana, ajira hakuna, masoko ya mazao hakuna, watu wetu bado wanalima kwa kijembe cha mkono na kutegemea mvua, wafugaji wanachunga hawafugi, machinga na wafanyabiashara hawalipi kodi ndio maana wanadhani kuwa wanapata faida, watu wetu wananunua magari makuukuu, wanavaa nguo za mitumba, hawakopesheki na wale wanaokopesheka riba ni kubwa sana.

kama unadhani wewe unazofedha tafadhali mpeleke mwanao vyuo binafsi ndani na nje ya nchi badala ya kubadilisha gia angani na kurudi vyuo vya serikali kuzibia wale wasio na kitu kabisa.
 
Badala ya kuhoji kwanini mtoto wa masikini aliyesoma shule ya serikali asifaulu kama yule wa shule binafsi huku chini lakini the pattern inageuka elimu ya juu, you come with allegations badala ya facts?

I think you need to stop being naive like this, sorry unani provoke na uandishi wako kwakua unaonekana kupenda kuleta simple answers kwenye serious na critical issues
What you say may be true, but you do not need to conduct any study in order to know why government schools are weaker in academic performances. Priorities, bad policies, low economic, poor planning, unfair world trade transactions, and climate change are among of the basic cause of this. It is a managerial rather than a research issue.

Ninachosema mimi kwenye uzi huu ni kwambaaa, wakati huu ambao wewe na wenzio mnatafuta kwanini watoto kwenye shule za kata hawapati division I ya point 3 na 4 kama wenzao wa shule za private, hivi vyuo vya serikali viendelee kudahiri watoto wengi kutoka shule za serikali, na vyuo vikuu binafsi na mashirika ya dini viendelee kupokea kwa wingi watoto kutoka shule binafsi. Hii itawapunguzia kadhia ya kukusanya ada zao vyuoni, maana mtoto aliyesoma shule ya kata kwenda kusoma chuo binafsi kama KMC, St. Joseph, Kampala International University, Kairuki, Aga Khan au St. John's ni shida tupu.
 
Hao watoto walijibagua wao wenyewe na wazazi/walezi wao, waliziita shule zote za serikali na zile za kata kuwa ni za kishenzi na kuibeza serikali kwenye mipango yake ya kumsogezea karibu shule kwa kuzijenga kila kata na kuondoa ada. Wazazi hawa wakazipuuza shule na jitihada hizi za serikali na kupeleka watoto wao shule za ghrama kubwa. Nia yao ni uvu sana hawa watu kwani walikuwa wanawakatisha tamaa watoto wa masikini wanaosoma hizi shule za serikali zisizokuwa na mabweni, usafiri, mabweni, chakula shuleni wala madawati. Kinachowashangaza walalahoi ni kuona hawa watoto waliozinyanyapaa shule za serikali wanakwenda kuvikimbilia vyuo vya bei nafuu vya serikali na kuwasukumia watoto maskini kule vyuo binafsi kwenye ada kubwa kwa kisingizio cha ufaulu, nonsense!!!

Kila msiba una mwenyewe, msiba wa watoto waliosoma shule za kata (st. Kayumba) mwenyewe ni vyuo vikuu vya serikali. Watoto hawa wavijaze vyuo hivi vya serikali kwanza kabla ya watoto wengine kupata nafasi huko. Serikali (TCU) wametoa ufafanuzi ni mtoto yupi amefaulu na yupi amefeli, mtoto yupi anaweza kusoma kozi gani na yupi hawezi. Vyuo vya serikali havina hiari kwenye jambo hili la kisera. Vyuo binafsi ndio viwe na hiari ya kuchagua cut-off points zao.
Ebu jaribu kosoma tena kisha kama unathamini utu wako rudi ndani ya moyo wako na kujiuliza haya uliyoyaandika yanamaana ya kuleta suluhu au kujitetea ili hoja yako ishinde kishabiki?

Kama ni mmoja miongoni mwa watu wenye influence kwenye maamuzi basi inabidi nikubali tu Mungu ndiye awezaye kusaidia watanzania, acha nirudi kwake kwa maombi kuliko kuendeleza mjadala huu na mtu mwenye mtizamo kama wako...Kimtazamo mimi nikiwa kusini wewe utakuwa kaskazini....Sioni tunapokutana kihoja.
 
Elimu ndio chombo pekee kinachoweza kuwakutanisha mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini katika ofisi moja na mgahawa mmoja. Takwimu zinaonyesha kuwa shule binafsi za msingi na sekondari nchini ni ghali kuliko za serikali lakini ndizo zenye mazingira mazuri ya kujifunzia na kutoa ufaulu mkubwa kwa wanafunzi wengi.

Na vyuo vikuu vya Serikali ni nafuu kusoma lakini ndivyo vyenye mazingira mazuri na miundombinu ya kufundishia na watoto kupata taaluma ya uhakika. Mpaka hapo hatubishani na hakuna ubishi.

Dhambi inakujaje wakati wa udahiri wa wanafunzi?
1. Vyuo vya serikali vinatoza ada ndogo sana lakini vinadahiri wanafunzi wenye ufaulu mkubwa sana(e.g Muhimbili University), bila shaka wengi wa wanafunzi wenye sifa hizi wengi wao ni wale wanaotoka kwenye shule za binafsi za sekondari kama FEZA, kanosa, etc.

Wazazi wa watoto hawa wengi wao ni wale wenye uchumi wa juu na wakati nchini ambao wanafahamu kuwa vyuo vya serikali vina walimu bora na miundombinu mizuri ya elimu, hivyo pamoja na kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha wa kuendelea kuwasomesha watoto vyuo binafsi nchini na nje ya ya nchi lakini hawawapeleki watoto wao kwenye vyuo binafsi nchini kwakuwa wanavijua kuwa hata walimu wao ni wazee waliochoka na vijana wasiokuwa na uwezo mkubwa wa kufundisha.

2. Vyuo vya binafsi havina miundombinu mizuri ya kufundishia (walimu, madarasa, practice, library, office, ect) lakini vinatoza ada kubwa sana ili kumudu kulipa mishahara ya watumishi, majengo, na tozo mbalimbali za serikali. Pamoja na ughali wa vyuo hivi lakini Watoto wa maskini waliosoma shule za serikali wanajikuta wakisukumiwa kwenye aina hii ya vyuo baada ya kukosa nafasi kwenye vyuo vya serikali vyenye ada ambayo wazazi wangeimudu kulipa japo pia kwa tabu.

Kadhia hii inasababisha mambo mabaya sana kwa watoto na wazazi wao zikiwemo za wazazi kuuza kila kitu yaani kila kitu cha familia ili kumudu ada ya mtoto mmoja kwenye chuo binafsi, watoto kukosa mitihani na kuacha shule kwa kukosa ada, wanafunzi kujiingiza kufanya vitendo vibaya vya kuuza mili na madawa au kufanya biashara na wizi ili kusaidia wazazi wao kujaza kile kinachokosekana kwenye gharama za vyuo binafsi.

3. Fedha ya serikali (loans board) inapotea bure kwa watoto hawa kwenye vyuo binafsi. Yaani mtoto anaacha chuo katikati kwa kukosa kulipa kiasi cha ada kujalizia kile cha mkopo alichopewa na loans board. Watoto hawa wanateseka sana vyuoni kwasababu wanalazima kutumia ile meals and accommodations wanayopewa kwa kulipia ada zao. Mtoto akiacha masomo maana yake hata kiasi alichokopeshwa na loans board kimepotea pia.

4. Scholarships na mikopo vinaangalia ufaulu wa mtoto bila kuangalia mtoto kasoma shule gani. Hii inamaanisha kuwa wenye nacho wataongezewa pia hapa. Yaani watoto wa wenye nacho ndio waliosoma shule za private na wengi ndio wenye ufaulu mkubwa kuweza kuwa na sifa za kupata scholarships na mikopo.

5. Mtoto wa Maskini hatakutana na mtoto wa tajiri ofisi moja kama trend itakuwa hiihii.


Hapa ni ama;
Shule za Serikali pia ziongezewe ubora katika kutoa elimu, vyuo vya private vipewe ruzuku na serikali ili ada yao pia iwe himilivu au vyuo vya serikali vihudumie zaidi shule za serikali.

Mifumo ya Serikali lazima isomane, haiwezekani vyuo vya serikali na shule za serikali hiyohiyo havisomani, yaani shule za serikali zinazalisha watoto wasiotakiwa na vyuo vya serikali.
Huna hoja. Ufaulu hautegemei kama upo private au serikalini. Hilo ndilo Prof. Ndalichako alikosea. Acha wapimwe kwa ufaulu
 
Ebu jaribu kosoma tena kisha kama unathamini utu wako rudi ndani ya moyo wako na kujiuliza haya uliyoyaandika yanamaana ya kuleta suluhu au kujitetea ili hoja yako ishinde kishabiki?

Kama ni mmoja miongoni mwa watu wenye influence kwenye maamuzi basi inabidi nikubali tu Mungu ndiye awezaye kusaidia watanzania, acha nirudi kwake kwa maombi kuliko kuendeleza mjadala huu na mtu mwenye mtizamo kama wako...Kimtazamo mimi nikiwa kusini wewe utakuwa kaskazini....Sioni tunapokutana kihoja.
Daaaaah! umeongea kwa hisia kali sana, lakini ukweli lazima tuuseme hata kama unauma. Serikali imefanya jambo zuri kuruhusu kuweko kwa shule na vyuo binafsi nchini, kabla ya mwaka 1998 hakukuwa na vyuo vikuu binafsi nchini, watu wote tulisoma kwenye vyuo vichache vya serikali kwa kusaidiwa na kigezo kimoja tu cha ufaulu wetu, hivyo watoto wengi walikosa nafasi ya kusoma. Leo hii shule za serikali na binafsi zimeongezeka inversely proportional na kuongezeka kwa vyuo vikuu nchini. Hali kama hii inahitaji sera na utaratibu maalumu ili kulifanya taifa lisiinamie upande mmoja, kwakuwa sasa hivi kigezo cha kusoma chuo kikuu sio ufaulu wa mtoto kama zamani, bali nguvu za kiuchumi za familia. shule za serikali zina changamoto nyingi mno, hivyo ili mtoto apate ufaulu mkubwa wa kumuwezesha chuo cha bei nafuu cha serikali lazima akasome shule za private. Fikiria itakuwaje kama shule nzuri za watu binafsi zitaongezeka sana kiasi kwamba wanafunzi wao wote wanapata division I points 3, 4 na 5 hii itamaanisha kuwa watoto wa masikini watakaosoma shule za serikali (zenye changamoto nyingi) hawatapata nafasi ya kusoma vyuo. Maana watoto kutoka shule za private watakuwa na uwezo wa kuvijaza vyuo vya serikali kwa kutumia ufaulu wao mkubwa na kuvijaza vile vya private kwakutumia nguvu zao za kiuchumi za wazazi wao (double deaths na double wins). Watoto wa maskini watapigwa nje ndani, bara na pwani, huku na kule na hivi na vile (onlookers)

vyuo binafsi vinatoa elimu ya chuo kikuu kwa gharama kubwa sana ukilinganisha na vyuo vya serikali. Unachosema wewe unataka iwe "survival of the fittest", yaani
 
Huna hoja. Ufaulu hautegemei kama upo private au serikalini. Hilo ndilo Prof. Ndalichako alikosea. Acha wapimwe kwa ufaulu
Uwanja wa kuwapima lazima uwe sawa kwa watoto wote. Shule za serikali hazina maabara halafu scholarships ni kwa watoto waliofaulu masomo ya sayansi. Hapa ni kumaanisha kuwa automatically scholarships hizi ni kwa watoto waliosoma private kwenye maabara safi za sayansi na walimu Bora.
 
Nilikupa thanks, lakini kwa maandishi nasema foolish! Muhimbili imejaa rushwa, nepotism, ukabila, na umwanga mshenzi tu! Kwa ufupi, watoto wa maskini kwa sasa hawataweza tena kusoma medicine.

Hilo jambo aliloandika mleta thrd liangaliwe na watu wenye akili siyo kila mwenye akaunti ya JF. Waziri na rais Samia wote wanajichanganya. Karibuni Waziri alisema kuna Samia Scholarships kwa wanafunzi wa sayansi je, anajua wanafaulu sayansi wanatoka shule gani? Ni aibu kufikia uwaziri lakini huna analytical brain zaidi ya ukorofi tu!

Hakuna mwanafunzi wa shule ya kata ya form 1-4 na 5-6 anayeweza kupata sholarship kama hiyo. Ni uzembe mkubwa kwa waziri anayejiita profesa kusihia kutaja ufauklu kama kigezo pekee cha haki ya kusoma.
Wasomi wetu wanathamini mtu mwenye uwezo wa kukumbuka na siyo kufikiri
Ndiyo maana wao pia hawana huo uwezo wa kufikiri.
 
Back
Top Bottom