Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Mbarawa azungumza kuhusu uwekezaji wa Bandari

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Mbarawa azungumza kuhusu uwekezaji wa Bandari

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 

Attachments

  • IMG_1068.MP4
    2.1 MB
  • 3DBA2C45-A50D-4319-8254-A3C1AB24F6F3.jpeg
    3DBA2C45-A50D-4319-8254-A3C1AB24F6F3.jpeg
    32 KB · Views: 1
  • 629E7CA7-9216-4246-AE4C-C6C0AB2EC6CA.jpeg
    629E7CA7-9216-4246-AE4C-C6C0AB2EC6CA.jpeg
    140.9 KB · Views: 1
  • 268E9966-3CC4-477F-9F14-7971DA4881BC.jpeg
    268E9966-3CC4-477F-9F14-7971DA4881BC.jpeg
    37.4 KB · Views: 1
  • 7F1A625B-1DA9-4C8B-A9B0-003C9FF749E0.jpeg
    7F1A625B-1DA9-4C8B-A9B0-003C9FF749E0.jpeg
    148.7 KB · Views: 1
  • 9A97A0EE-0405-410D-AB36-1D01351D3153.jpeg
    9A97A0EE-0405-410D-AB36-1D01351D3153.jpeg
    115.9 KB · Views: 1
  • 2B6F888E-2D50-4163-B694-1D9AD1B00FEE.jpeg
    2B6F888E-2D50-4163-B694-1D9AD1B00FEE.jpeg
    58 KB · Views: 2
  • 96AC4F70-B2B1-4483-B6EB-59C4C23120B2.jpeg
    96AC4F70-B2B1-4483-B6EB-59C4C23120B2.jpeg
    55.5 KB · Views: 1
  • 9FD5F3E9-2F97-426B-8B18-EA4727B5A1A7.jpeg
    9FD5F3E9-2F97-426B-8B18-EA4727B5A1A7.jpeg
    57 KB · Views: 1
  • 5F9C7745-B184-4CEF-B236-059905C9BB48.jpeg
    5F9C7745-B184-4CEF-B236-059905C9BB48.jpeg
    57.3 KB · Views: 1
  • 9E2FE5EF-DF92-462B-860C-7F69309901D1.jpeg
    9E2FE5EF-DF92-462B-860C-7F69309901D1.jpeg
    62 KB · Views: 1
  • 66B200BE-D450-44A5-B79C-BCC191D22E79.jpeg
    66B200BE-D450-44A5-B79C-BCC191D22E79.jpeg
    9.9 KB · Views: 1
  • 15A80DBA-904A-4724-8218-84B6ABCE6004.jpeg
    15A80DBA-904A-4724-8218-84B6ABCE6004.jpeg
    115 KB · Views: 1
  • FEDD7557-CC0F-4249-BEDB-4090AF55C406.jpeg
    FEDD7557-CC0F-4249-BEDB-4090AF55C406.jpeg
    55.3 KB · Views: 3
  • A684B876-BDAB-4823-BE27-2C985FDF8C82.jpeg
    A684B876-BDAB-4823-BE27-2C985FDF8C82.jpeg
    150.5 KB · Views: 2
  • FAE4437F-EE0B-48B8-A44D-D97387AC1004.jpeg
    FAE4437F-EE0B-48B8-A44D-D97387AC1004.jpeg
    131.1 KB · Views: 1
  • 002A75F3-6A7E-4FA1-9266-E2CC6D26613C.jpeg
    002A75F3-6A7E-4FA1-9266-E2CC6D26613C.jpeg
    75.7 KB · Views: 1
  • F4A9A5BF-A2B6-43BD-8834-35658C235242.jpeg
    F4A9A5BF-A2B6-43BD-8834-35658C235242.jpeg
    55.1 KB · Views: 1
  • IMG_1261.MP4
    632.6 KB


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa anazungumza na Waandishi wa Habari, Jijini Dar es Salaam muda huu kuhusu uwekezaji wa Bandari.

Mbarawa:
Pamoja na Serikali kuendeleza juhudi za maboresho ya Bandari zetu, bado ufanisi katika utoaji huduma wa Bandari haujafikia viwango vinavyotakiwa kimataifa.

Hali ya ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam na nyingine nyingi zinazoendeshwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania upo chini sana, udhaifu huo unaonekana katika utendaji wa kila siku wa Bandari zetu pamoja na ukusanyaji wa mapato

Bandari ya Dar imeendelea kuwa nyuma dhidi ya Bandari shindani katika Kanda, mfano wastani wa meli kusubiri nangani ni siku 5 sawa na Saa 120 ikilinganishwa na siku 1 na saa 6 kwa bandari ya Mombasa.

Meli kutumia muda mrefu kupakia shehena kantini kwa wastani wa siku tano wakati kimataifa ni siku moja inayokubalika kimataifa.

Ufanisi mdogo wa Bandari ya Dar es Salaam umetokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kukosekana mifumo ya kisasia ya TEHAMA, kutokuwepo kwa maeneo ya kutosha ndani na nje ya Bandari ya kuhifadhia shehena za mizigo pamoja na maegesho ya kutosha ya kuegeshea meli.

Changamoto nyingine ni kukosekana kwa mitambo ya kutosha na ya kisasa inayobadilika mara kwa mara kutokana na teknolojia na hivyo kuwa na gharama kubwa.

Athari za kutokuwa na ufanisi katika Bandari ya Dar es Salaam ni meli kusubiri muda mrefu nangani, mfano gharama ya meli kusubiri nangani kwa siku moja ni takribani Dola 25,000 (Tsh. Milioni 58).

Meli kutumia wastani wa siku tano kupakia na kupakua shehena ukilinganisha na siku 1 inayokubalika kimataifa.

Meli kubwa kutokuja katika Bandari ya Dar es Salaam kutokana na kuchukua muda mrefu kuhudumiwa, hivyo kusababisha bandari yetu kuwa inayolishwa na Bandari nyingine.

Uwezo mdogo wa Bandari ya Dar unaikosesha Nchi mapato makubwa ambayo yangeweza kusaidia katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa Nchini.

Ili kutoendelea na hali hiyo, Serikali iliingia makubaliano 2000 Serikali ya Awamu ya Tatu iliingia mkataba wa upangaji na uendeshaji na Kampuni ya TICTS, mkataba ambao ulidumu kwa miaka 22 na kuipa haki za kipekee TICTS kuendesha shughuli za gati namba 8 hadi 11 za Bandari ya Dar es Salaam huku maeneo mengine yakihudumiwa na TPA.

Desemba 2022, Serikali ya Awamu ya 6 baada ya kuona mkataba hauendani na maslahi mapana ya Nchi yetu iliamua kusitisha mkataba huo.

Serikali kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania ilipokea mapendekezo ya wawekezaji mbalimbali Duniani, lengo kuu likiwa ni kufungua masoko ya kimkakati katika kufungua eneo la bidhaa na usafirishaji ndani ya Nchi na maeneo yanayotuzunguka.

Baada ya uchambuzi wa kina Serikali ilianzisha majadiliano na Kampuni ya DP World kwa sababu zifuatazo:

Uwezo mkubwa wa uendeshaji wa shughuli za Bandari Afrika, Asia, Ulaya, Marekani ya Kaskazini na Kusini na Australia.

DP World ina uwezo na kuchagiza mnyororo mzima wa usafirishaji kutoka maeneo ambapo bidhaa zinatoka hadi kwa walaji wa bidhaa.

DP World inamiliki zaidi ya meli 400 za mizigo, ina uzoefu wa uendeshaji wa Bandari 6 Afrika na zaidi ya Bandari 30 Duniani kote.

Wawekezaji wengine waliowasilisha mapendekezo yao hayakukidhi sifa kwa mwekezaji ambaye alihitajika.

Mkurugenzi TCCA: Hakuna ardhi ya Tanzania ambayo itauzwa
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini, Hamza Johari amewatoa hofu Watanzania kuhusu tarifa za kuwa nchi imeuzwa kutokana na mkataba wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai akisema kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote.

Kauli hiyo ameitoa leo Julai 14, 2023 alipokuwa akizungumza katika mkutano na wahariri jijini Dar es Salaam huku akiwataka watu kutoingiza siasa kwenye masuala yahusuyo uchumi wa nchi na kusisitiza kuwa mkataba huo ni mzuri.

Huo uwekezaji na uendeshaji tuna uweza mkishindwa sana kodisheni management toka nchi zingine. Kwa miaka sema 5 . Na kuhusu vifaa mnaweza kununua hata Kwa mkopo au karadha.
Tehema nayo inaweza kununuliwa au kuwakodisha watu wengine.
Mwisho tupate plan ya upanuzi WA bandari yetu toka kampuni tofauti ili tuweze kumiliki wenyewe na kufanya wenyewe siku zijazo.
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Maswali mazuri
 
 
ITV watakata matangazo ikifika saa Saba Ili kupisha taarifa ya Habari ya Saa Saba
 
Kitenge ni form 4 total failure
FYI: Waandishi wa Habari wengi sana hapa Tz hawana shule ya kutosha kichwani, yaani walio wengi elimu yao ni ya kuunga unga. Wapo wachache sana ambao kimsingi wapo fit kielimu na pia wako competent kwenye taaluma na kazi ya uandishi wa habari, pia wako serious na kazi zao za hanari. Kitu cha kusikitisha zaidi ni kwamba, hata hao waandihi wa habari ambao mnawafahamu kwamba ni watu maarufu hapa nchini, nao uki hunguza kwa umakini sana utaona pia elimu zao ni za kuungaunga, ukanjanja, na wengine wapo katika taasisi za vyombo vy habari maarufu hapa nchini. Very sad indeed!
 
Mkuu mtumisji wa Serikali siku zote anatetea ugali wake na WA bosi wake na Wala siyo akili zake
Binafsi kwenye Hili Hamza kajitahidi sana kueleza kitaalamu kwa asilikia kubwa sijasema asilimia 100

Ila yuko vizuri ukimsikiliza Hamza mtu kama mimi Mkristo nasali kwa Mwamposya sipendi uongo wala unafiki nikipewa taarifa sahihi binafsi naona kabisa Hamza alifanya kazi yake vizuri mno akiwa na dhamiri njema mno kwa maslahi ya nchi kwa asilimia kubwa

Mimi.nimemuelewa hiyo nafasi ya kiofisi aliyonayo kama mkurugenzi wa Anga ni ndogo mno ukilinganisha na uwezo wa akili yake anastahili kuwa na na nafasi kubwa zaidi
 
Back
Top Bottom