Wizara ya Fedha inamsaidia sana Rais Samia kutekeleza miradi ya maendeleo

Wizara ya Fedha inamsaidia sana Rais Samia kutekeleza miradi ya maendeleo

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,072
Nchi inaenda vizuri sana. Mungu ni mwema. Ukizunguka huko mikoani (nje ya Majiji) utaona jinsi ambavyo halmashauri na maeneo yote ya kiutendaji yanavyofanya kazi za miradi kwa bidii na bila malalamiko.

Kwa wasiofahamu, Serikali imemwaga fedha nyingi kwenye halmshauri zote nchi nzima. Huko ndipo walipo wananchi wengi wanaofikiwa na huduma za kijamii kama za afya, elimu, maji, umeme, miundombinu na kadhalika. Tusishtuke tukiona picha za mashule, mahospitali, mabomba ya maji na mengine.

Kipekee naipongeza Wizara ya Fedha na watendaji wake wote kwa ujumla. Ubunifu, uchapakazi na weledi wao umeisaidia nchi kunufaika na miradi ya kimaendeleo inayoendelea kufanyiwa kazi huko 'site'. Ule msisitizo wa 50% pesa ya bajeti zinazopelekwa kwenye wizara zote zitumike kwenye maendeleo imesaidia mno. Na usimamizi umekuwa mkali kuhakikisha pesa haipotei na matumizi yake yanaonekana.

Kama mtu ni mfuatiliaji wa mambo, bila shaka atakubaliana nami kuwa hivi sasa pesa imemwagwa kweli kweli. Sijui ndio ile inaitwa injection au induction. Nina uhakika matokeo yake yataonekana tu kwani hata vyuma vilivyokaza vimeanza kulegea.

Nimpongeze pia Dkt. Mwigulu Nchemba (almaarufu Zakayo), kiongozi aliyeamua rasmi kutumia taaluma yake kuisaidia nchi na kupunguza siasa za majukwaani. Ukifuatilia mwenendo wake unamuona kabisa ni mtu anayejitahidi kubadilika sana. Nilipenda ukaribu na ushirikiano wake na Odo Ummy Mwalimu alipokuwa TAMISEMI. Hata ule ushuhuda wa Rais Samia kuwa alipigiwa simu usiku kuhusu masuala ya kifedha sio wa kuuchukulia poa. Ilionesha dhamira yake ya dhati kwa maslahi ya nchi.

Mawaziri, watendaji na viongozi wengine nao wanafanya kazi nzuri katika maeneo yao. Kuanzia kwa kiongozi ninayemkubali Prof. Mbarawa, Odo Ummy, Mchengerwa, Bashe, Mulamula, Ndumbaro, Nape (promising) n.k.

Jambo moja tu linalotakiwa kuwekwa vizuri ni suala la demokrasia. Tena iwe demokrasia ya kweli. Vyama vya upinzani na viongozi wao wapewe nafasi ya kuichalenji serikali bila hofu ya kukamatwa au kushitakiwa kwa makosa ya kisiasa. Hilo tu!

Tuiombee nchi yetu. Tuwaombee viongozi wetu.
 
Nchi inaenda vizuri sana. Mungu ni mwema. Ukizunguka huko mikoani (nje ya Majiji) utaona jinsi ambavyo halmashauri na maeneo yote ya kiutendaji yanavyofanya kazi za miradi kwa bidii na bila malalamiko.

Kwa wasiofahamu, Serikali imemwaga fedha nyingi kwenye halmshauri zote nchi nzima. Huko ndipo walipo wananchi wengi wanaofikiwa na huduma za kijamii kama za afya, elimu, maji, umeme, miundombinu na kadhalika. Tusishtuke tukiona picha za mashule, mahospitali, mabomba ya maji na mengine.

Kipekee naipongeza Wizara ya Fedha na watendaji wake wote kwa ujumla. Ubunifu, uchapakazi na weledi wao umeisaidia nchi kunufaika na miradi ya kimaendeleo inayoendelea kufanyiwa kazi huko 'site'. Ule msisitizo wa 50% pesa ya bajeti zinazopelekwa kwenye wizara zote zitumike kwenye maendeleo imesaidia mno. Na usimamizi umekuwa mkali kuhakikisha pesa haipotei na matumizi yake yanaonekana.

Kama mtu ni mfuatiliaji wa mambo, bila shaka atakubaliana nami kuwa hivi sasa pesa imemwagwa kweli kweli. Sijui ndio ile inaitwa injection au induction. Nina uhakika matokeo yake yataonekana tu kwani hata vyuma vilivyokaza vimeanza kulegea.

Nimpongeze pia Dkt. Mwigulu Nchemba (almaarufu Zakayo), kiongozi aliyeamua rasmi kutumia taaluma yake kuisaidia nchi na kupunguza siasa za majukwaani. Ukifuatilia mwenendo wake unamuona kabisa ni mtu anayejitahidi kubadilika sana. Nilipenda ukaribu na ushirikiano wake na Odo Ummy Mwalimu alipokuwa TAMISEMI. Hata ule ushuhuda wa Rais Samia kuwa alipigiwa simu usiku kuhusu masuala ya kifedha sio wa kuuchukulia poa. Ilionesha dhamira yake ya dhati kwa maslahi ya nchi.

Mawaziri, watendaji na viongozi wengine nao wanafanya kazi nzuri katika maeneo yao. Kuanzia kwa kiongozi ninayemkubali Prof. Mbarawa, Odo Ummy, Mchengerwa, Bashe, Mulamula, Ndumbaro, Nape (promising) n.k.

Jambo moja tu linalotakiwa kuwekwa vizuri ni suala la demokrasia. Tena iwe demokrasia ya kweli. Vyama vya upinzani na viongozi wao wapewe nafasi ya kuichalenji serikali bila hofu ya kukamatwa au kushitakiwa kwa makosa ya kisiasa. Hilo tu!

Tuiombee nchi yetu. Tuwaombee viongozi wetu.
Na suala la umeme unalizungumziaje?
 
Na suala la umeme unalizungumziaje?

Wizara ya Nishati ilishatolea ufafanuzi suala la umeme. Kuna marekebisho yanaendelea kwenye gridi ya taifa kwa mujibu wa taarifa ya Tanesco. Uchakavu wa miundombinu pia ni suala linaloshughulikiwa. Mahitaji na idadi ya watu imeongozeka hivyo hili lilitarajiwa.

Kwa upande mwingine chanya, umeme umeendelea kusambazwa vijijini kote na mpaka sasa Tanzania inaongoza kwa kufikisha umeme sehemu kubwa ya nchi kuliko nchi yoyote Afrika Mashariki.
 
Mfumuko wa bei huyo Mwigulu anaelewa athari zake kwa ustawi wa wananchi! Acheni uchachawa wenu !! Wananchi wote wa mijini na vijijini wote wanalia!!

Mfumuko wa bei unatokana na sababu nyingi, ikiwemo hili janga za uviko/omicron na mabadiliko ya bei ya mafuta. Ni kweli athari yake ni kubwa lakini bado hatujafikia kwenye hali mbaya. Tuwe wakweli. Tutarajie bei ya mafuta iwe stable kwa kipindi kirefu ili bei za bidhaa na huduma ziwe nafuu.
 
Mfumuko wa bei unatokana na sababu nyingi, ikiwemo hili janga za uviko/omicron na mabadiliko ya bei ya mafuta. Ni kweli athari yake ni kubwa lakini bado hatujafikia kwenye hali mbaya. Tuwe wakweli. Tutarajie bei ya mafuta iwe stable kwa kipindi kirefu ili bei za bidhaa na huduma ziwe nafuu.
Endelea kuimba mapambio chawa wewe!
 
Sawa mkuu. Hoja yako ni ipi?
Kuwa unaimba mapambio!! Wewe na waziri wako hamumsaidizi Samia kuhusu inflation!! Hiyo bei ya mafuta kupanda wenzenu wanajua jinsi ya kuhedge ili upand ski wa bei ya mafuta duniani usiathiri uchumi wao!!
Nyie viazi mnakaa na kuimba mapambio ya Samia tu huku mkimdanganya Hangaya wa watu!
 
Kuwa unaimba mapambio!! Wewe na waziri wako hamumsaidizi Samia kuhusu inflation!! Hiyo bei ya mafuta kupanda wenzenu wanajua jinsi ya kuhedge ili upand ski wa bei ya mafuta duniani usiathiri uchumi wao!!
Nyie viazi mnakaa na kuimba mapambio ya Samia tu huku mkimdanganya Hangaya wa watu!

Wewe ndio una hoja inayojadilika japo huna adabu. Yule mwingine aliishia kuandika kashfa tu, hoja hana.

Jitihada za kudhibiti mfumuko wa bei zinaendelea na soon or later utaanza kuona inflation rate ikishuka. Taarifa zinatolewa kila siku, ni kufuatilia tu.
 
Hapo Samia anahamasisha ufisadi katika serikali yake.

Si kweli. Hakuna Rais anayeweza kuhalalisha ufisadi. Fuatilia context ya hiyo hotuba achana na hizi short clips. Wewe ni mwerevu, jiongeze, usije kujikuta unashiriki kwenye ajenda na propaganda za watu bila kujua.
 
Wewe ndio una hoja inayojadilika japo huna adabu. Yule mwingine aliishia kuandika kashfa tu, hoja hana.

Jitihada za kudhibiti mfumuko wa bei zinaendelea na soon or later utaanza kuona inflation rate ikishuka. Taarifa zinatolewa kila siku, ni kufuatilia tu.
Tunataka matokeo sio mapambio!!Tunataka kuona bei ya vifaa vya ujenzi na vyakula zinazoeleweka na sio hizi za leo. Kuna hatua za ndani mnaweza kuchukua na bei zikashuka kwani sio sababu zote za inflation ni externally induced!!
 
Si kweli. Hakuna Rais anayeweza kuhalalisha ufisadi. Fuatilia context ya hiyo hotuba achana na hizi short clips. Wewe ni mwerevu, jiongeze, usije kujikuta unashiriki kwenye ajenda na propaganda za watu bila kujua.
Samia kwenye hii hotuba yake anahamasisha ufisadi katika serikali yake.

Ukiangali hii video ndefu ambayo haijakatwa,Samia anasimulia jinsi miradi haikamiliki kutokana na fedha za miradi kuliwa.

Anatolea mifano ya miradi ya Meli,barabara na Bandari jinsi ambavyo fedha zake zinatafunwa hadi miradi hiyo kukwama(compromised).Kitendo hicho anakiita kuwa ni kula hadi kuvimbiwa na ndipo anashauri kuwa fedha hizo za miradi ziliwe kwa staha ili miradi isikwame na kitendo hicho anakiita kuwa ni kujipimia.
 
Tunataka matokeo sio mapambio!!Tunataka kuona bei ya vifaa vya ujenzi na vyakula zinaeleweka na sio hizi za leo. Kuna hatua za ndani mnaweza kuchukua na bei zikashuka kwani sio sababu zote za inflation ni externally induced!!

Ukipewa maelezo unaita mapambio. Hoja yako nzuri inaharibiwa na mihemko. Una ushauri wowote? Andika hapa, huwezi kujua nani anasoma na huenda maoni/ushauri wako ukafanyiwa kazi.

Ni hatua zipi zinaweza kuchukuliwa na bei zikashuka?
 
Samia kwenye hii hotuba yake anahamasisha ufisadi katika serikali yake.

Ukiangali hii video ndefu ambayo haijakatwa,Samia anasimulia jinsi miradi haikamiliki kutokana na fedha za miradi kuliwa.

Anatolea mifano ya miradi ya Meli,barabara na Bandari jinsi ambavyo fedha zake zinatafunwa hadi miradi hiyo kukwama(compromised).Kitendo hicho anakiita kuwa ni kula hadi kuvimbiwa na ndipo anashauri kuwa fedha hizo za miradi ziliwe kwa staha ili miradi isikwame na kitendo hicho anakiita kuwa ni kujipimia.
View attachment 2090707

Well said, lakini hapo anaposhauri ziliwe kwa staha sijapasikia au ni maoni na tafsiri yako binafsi? Wapo walioona kama ni onyo lililotolewa kwa lugha ya upole.

Kuhusu fedha kutafunwa na kupelekea miradi hiyo kukwama, tayari wizara imeshatoa agizo kwa wakaguzi wa ndani kukagua na kutoa ripoti ndani ya mwezi mmoja ili kujua pesa zimetumikaje, wapi miradi imekwama, nani hakuwajibika na kama zimeliwa nani amekula ili hatua zichukuliwe. Tusubiri maamuzi baada ya ripoti.

NB: Nimekuwekea video hapo chini ujiridhishe. Hakuna namna kiongozi wa taifa atahalalisha rushwa na ufisadi hadharani. Wewe inakuingia akilini?
 

Attachments

  • CUE IN 1 - DKT. MWIGULU LAMECK NCHEMBA, WAZIRI WA FEDHA.mp4
    43.6 MB
Wizara ya Nishati ilishatolea ufafanuzi suala la umeme. Kuna marekebisho yanaendelea kwenye mkongo wa taifa kwa mujibu wa taarifa ya Tanesco. Uchakavu wa miundombinu pia ni suala linaloshughulikiwa. Mahitaji na idadi ya watu imeongozeka hivyo hili lilitarajiwa.

Kwa upande mwingine chanya, umeme umeendelea kusambazwa vijijini kote na mpaka sasa Tanzania inaongoza kwa kufikisha umeme sehemu kubwa ya nchi kuliko nchi yoyote Afrika Mashariki.
Mkongo wa Taifa siku hizi unagenerate umeme?!😡😡
 
Back
Top Bottom