Wizara ya Fedha inamsaidia sana Rais Samia kutekeleza miradi ya maendeleo

Wizara ya Fedha inamsaidia sana Rais Samia kutekeleza miradi ya maendeleo

Nchi inaenda vizuri sana. Mungu ni mwema. Ukizunguka huko mikoani (nje ya Majiji) utaona jinsi ambavyo halmashauri na maeneo yote ya kiutendaji yanavyofanya kazi za miradi kwa bidii na bila malalamiko.

Kwa wasiofahamu, Serikali imemwaga fedha nyingi kwenye halmshauri zote nchi nzima. Huko ndipo walipo wananchi wengi wanaofikiwa na huduma za kijamii kama za afya, elimu, maji, umeme, miundombinu na kadhalika. Tusishtuke tukiona picha za mashule, mahospitali, mabomba ya maji na mengine.

Kipekee naipongeza Wizara ya Fedha na watendaji wake wote kwa ujumla. Ubunifu, uchapakazi na weledi wao umeisaidia nchi kunufaika na miradi ya kimaendeleo inayoendelea kufanyiwa kazi huko 'site'. Ule msisitizo wa 50% pesa ya bajeti zinazopelekwa kwenye wizara zote zitumike kwenye maendeleo imesaidia mno. Na usimamizi umekuwa mkali kuhakikisha pesa haipotei na matumizi yake yanaonekana.

Kama mtu ni mfuatiliaji wa mambo, bila shaka atakubaliana nami kuwa hivi sasa pesa imemwagwa kweli kweli. Sijui ndio ile inaitwa injection au induction. Nina uhakika matokeo yake yataonekana tu kwani hata vyuma vilivyokaza vimeanza kulegea.

Nimpongeze pia Dkt. Mwigulu Nchemba (almaarufu Zakayo), kiongozi aliyeamua rasmi kutumia taaluma yake kuisaidia nchi na kupunguza siasa za majukwaani. Ukifuatilia mwenendo wake unamuona kabisa ni mtu anayejitahidi kubadilika sana. Nilipenda ukaribu na ushirikiano wake na Odo Ummy Mwalimu alipokuwa TAMISEMI. Hata ule ushuhuda wa Rais Samia kuwa alipigiwa simu usiku kuhusu masuala ya kifedha sio wa kuuchukulia poa. Ilionesha dhamira yake ya dhati kwa maslahi ya nchi.

Mawaziri, watendaji na viongozi wengine nao wanafanya kazi nzuri katika maeneo yao. Kuanzia kwa kiongozi ninayemkubali Prof. Mbarawa, Odo Ummy, Mchengerwa, Bashe, Mulamula, Ndumbaro, Nape (promising) n.k.

Jambo moja tu linalotakiwa kuwekwa vizuri ni suala la demokrasia. Tena iwe demokrasia ya kweli. Vyama vya upinzani na viongozi wao wapewe nafasi ya kuichalenji serikali bila hofu ya kukamatwa au kushitakiwa kwa makosa ya kisiasa. Hilo tu!

Tuiombee nchi yetu. Tuwaombee viongozi wetu.
Katika masnitch wakubwa wa Samia huyu jamaa ni konki


Aendelee kumfuga na kumrutubisha hadi siku ambayo itakuwa too late
 
Hahahahaha.......sema ulikuwa umekusudia kudanganya.

Hakuna uongo wowote hapo. Unajua unaweza ukaandika kitu kingine na kichwani ukawa umesoma kitu kingine. Hata urudie vipi unasoma kilichopo kichwani. Sijui hiyo hali inaitwaje 😀
 
Katika masnitch wakubwa wa Samia huyu jamaa ni konki


Aendelee kumfuga na kumrutubisha hadi siku ambayo itakuwa too late
Si kweli, angekuwa snitch basi asingemsaidia kuperform. Bahati mbaya sana Watanzania tuna tabia ya kujiaminisha mambo.
 
Si kweli, angekuwa snitch basi asingemsaidia kuperform. Bahati mbaya sana Watanzania tuna tabia ya kujiaminisha mambo.
Tuanze kwenye TOZO la kijizi.

Unadhani raia wanafurahia huu wizi?

Endeleeni kukopa mkimuaminisha Hangaya kuwa no worries.
 
Kwanza ndio Kazi hasa kutoa fedha za miradi kwa wakati.

Walioko ofisini na wanaotekeleza miradi na watoa huduma ni mashahidi kwa namna ambavyo flow ya pesa inatoka kwa wakati..

Hongera SSH maana miaka mingine utekelezaji wa bajeti ulikuwa chini ya asilimia 70%.
 
Well said, lakini hapo anaposhauri ziliwe kwa staha sijapasikia au ni maoni na tafsiri yako binafsi? Wapo walioona kama ni onyo lililotolewa kwa lugha ya upole.

Kuhusu fedha kutafunwa na kupelekea miradi hiyo kukwama, tayari wizara imeshatoa agizo kwa wakaguzi wa ndani kukagua na kutoa ripoti ndani ya mwezi mmoja ili kujua pesa zimetumikaje, wapi miradi imekwama, nani hakuwajibika na kama zimeliwa nani amekula ili hatua zichukuliwe. Tusubiri maamuzi baada ya ripoti.

NB: Nimekuwekea video hapo chini ujiridhishe. Hakuna namna kiongozi wa taifa atahalalisha rushwa na ufisadi hadharani. Wewe inakuingia akilini?
Kwa historia ya chama cha CCM ya kulitafuna Taifa hili kupitia ufisadi inaniingia akilini Samia kuhamasisha ufisadi kwenye Serikali yake.Kama enzi za ufisadi wa Escrow na Richmond viongozi wa CCM walipakia hela kwenye viroba na kwenye Sandarusi, kwa nini nishangae leo Samia kuhamasisha ufisadi katika serikali yake?

Samia alikuwa anahamasisha ufisadi kwa sababu kwa maneno yake alikuwa anawaambia mawaziri kuwa siyo kweli kwamba hawapati kitu kwenye maeneo yao na aliwasisitiza kuwa tatizo wanakula hadi kuvimbiwa kitu ambacho kinakwamisha miradi.Ndipo akawashauri kuwa wajipimie badala ya kula kwa ulafi kitu ambacho kinakwamisha miradi ya maendeleo.
 
Tuanze kwenye TOZO la kijizi.

Unadhani raia wanafurahia huu wizi?

Endeleeni kukopa mkimuaminisha Hangaya kuwa no worries.

Pengine unaishi maeneo ya mjini au upo kwenye comfortable life so unaweza usielewe hizi unazoita tozo za kijizi zinavyosaidia huko site. Na hakuna nchi duniani isiyokopa, msijiaminishe na kuaminisha umma kuwa kukopa ni jambo baya, hatutafika.

La muhimu tupigie kelele uwajibikaji na ndicho kinachofanywa na wenye nia ya dhati serikalini kwa sasa, japo msafara wa mamba na kenge huwa hawakosekani.
 
Kwanza ndio Kazi hasa kutoa fedha za miradi kwa wakati.

Walioko ofisini na wanaotekeleza miradi na watoa huduma ni mashahidi kwa namna ambavyo flow ya pesa inatoka kwa wakati..

Hongera SSH maana miaka mingine utekelezaji wa bajeti ulikuwa chini ya asilimia 70%.

Moja ya jambo kubwa analofanya Rais ni flow ya pesa kwenda kwenye mashina huko chini na zinawafikia walengwa haswa. Mfumo wa forced account umesaidia sana pesa kutumika kwa malengo kusudiwa.

Kuna watu wamezoea kupigizana kelele mitandaoni na kupinga pinga, hawaelewi uhalisia wa mambo, tuwaelimishe.
 
Kwa historia ya chama cha CCM ya kulitafuna Taifa hili kupitia ufisadi inaniingia akilini Samia kuhamasisha ufisadi kwenye Serikali yake.Kama enzi za ufisadi wa Escrow na Richmond viongozi wa CCM walipakia hela kwenye viroba na kwenye Sandarusi, kwa nini nishangae leo Samia kuhamasisha ufisadi katika serikali yake?

Samia alikuwa anahamasisha ufisadi kwa sababu kwa maneno yake alikuwa anawaambia mawaziri kuwa siyo kweli kwamba hawapati kitu kwenye maeneo yao na aliwasisitiza kuwa tatizo wanakula hadi kuvimbiwa kitu ambacho kinakwamisha miradi.Ndipo akawashauri kuwa wajipimie badala ya kula kwa ulafi kitu ambacho kinakwamisha miradi ya maendeleo.
Sawa mkuu. Inaonekana kwako hii ni imani. Ngumu mno kukuelewesha tofauti na unavyoamini. At least nimejaribu!
 
Ukipewa maelezo unaita mapambio. Hoja yako nzuri inaharibiwa na mihemko. Una ushauri wowote? Andika hapa, huwezi kujua nani anasoma na huenda maoni/ushauri wako ukafanyiwa kazi.

Ni hatua zipi zinaweza kuchukuliwa na bei zikashuka?
Nyie ndio mnaoajiriwa na kukomba mishahara minono bila kuwa na weledi halafu unataka uje JF tuwapeni maarifa ya jinsi ya kumshauri Hangaya na mkifanikiwa hamsemi mlitumia akili za nani Mpaka mkafanikiwa!! You have to acknowledge kuwa BULESI ndio aliwapa hilo suluhisho!! Uzalendo una mwisho watu hawali uzalendo!!! Tonny Blair mnamlipa lakini wazalendo mnataka wawafanyie kazi bure!!!
Ngoja nikumegee kidogot basi. Wafanyabiashara na other middlemen wanaweza kuwa chanzo cha mfumuko wa bei whenever ARTIFICIAL shortages are created when they hoard commodities, hivyo serikali kwa kuthibiti hoarding of different commodities hakutakuwa na upungufu wa bidhaa sokoni na bei zake itabidi kushuka kwasababu there will be an increase in the supply of commodities to consumers!! Hopefully umeelewa.
 
Nyie ndio mnaoajiriwa na kukomba mishahara minono bila kuwa na weledi halafu unataka uje JF tuwapeni maarifa ya jinsi ya kumshauri Hangaya na mkifanikiwa hamsemi mlitumia akili za nani Mpaka mkafanikiwa!! You have to acknowledge kuwa BULESI ndio aliwapa hilo suluhisho!! Uzalendo una mwisho watu hawali uzalendo!!! Tonny Blair mnamlipa lakini wazalendo mnataka wawafanyie kazi bure!!!

Hii inaashiria kuwa huna mawazo mbadala zaidi ya kuponda, kusiliba na kuongea vibaya. Jikague mkuu!
 
Ila kwenye jambo la kukatika katika umeme naona hawamuungi mkono kabisa mama
 
Pengine unaishi maeneo ya mjini au upo kwenye comfortable life so unaweza usielewe hizi unazoita tozo za kijizi zinavyosaidia huko site. Na hakuna nchi duniani isiyokopa, msijiaminishe na kuaminisha umma kuwa kukopa ni jambo baya, hatutafika.

La muhimu tupigie kelele uwajibikaji na ndicho kinachofanywa na wenye nia ya dhati serikalini kwa sasa, japo msafara wa mamba na kenge huwa hawakosekani.
Hakika bongo nyoso kwelikweli.

Yaani unaniibia na unanieleza faida ya kuibiwa na kunifanya sina akili hata kidogo.

Skiza.
Unapokuja jukwaani kutetea ujinga mnaoufanya huko, jifunze kuwa huku kuna wataalam wa kila aina. Uongozi siyo incentive ya kuongeza kipaji bali ni dhamana hivyo usijifanye una akili kutuzidi.

Mnaposhindqa kusimamia fedha za umma na mnafikia kukwapua hata kidogo cha wananchi huku mkihakikisha mnaminya mianya muhimu ya kupata fedha msidhani hao wananchi ni wajinga

Tunachokijua ni kwamba mnampa ushauri mbaya Rais wetu ili tumchukie hivyo kurahisisha agenda zenu za kipuuzi.

Kama mnataka kuonesha uzalendo punguzeni mishahara yenu na marupurupu kwa asilimia 50% kisha mje kukwapua zetu.

Masnitch wahed
 
Back
Top Bottom