Hii imekaaje jamani? Mzee mdee na mabinti zake 18 kutetewa na mawakili wa serikali?
au ni kweli kwamba haya matapeli 19 ni NDAGU ya kuvuta pesa za wafadhili hazwa zile euro milion 900 kwamba ionekane kuna upinzani bungeni uko active baada ya wizi mkubwa wa kizembe uliofanyika 2020?
Msaada tafadhali Mr Mayala au njaa kwa lugha ya kisukuma
Pascal Mayalla
Mwanasheria Mkuu wa Serikali,alisha leta Mawakili wanne wakiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Gabriel Mallata.
Baada ya Kuona Chadema imetia timu Mahakamani bila wao Kutegemea.
Wamekuja Mawakili wa Serikali Wanne tena wakiongozwa na Ayoub Sanga
Wapo 8 + Wa Mdee 3 =11
Kituko cha Kwanza
Mawakili wa Mdee na Wanasheria Serikali wa Serikali Katika Maombi yao.
Ombi la Kwanza Wanaomba Mahakama Iweke zuio "Court Injunction"Wasivuliwe Ubunge na Bunge.
Kabla ya ombi hili halija sikilizwa Leo asubuhi Spika Tulia Kashasema wataendelea na Ubunge
Jopo la Mawakili wa Serikali na Mawakili wa Mdee kwa Pamoja
Wanaomba Kwanza Mahakama itoe zuio la Mdee na Mwenzake Waendelee Kuwa wabunge mpaka pale ambapo Kesi ya msingi Kesi itakapoisha.
Baada Wasilisho lao,Mahakama italazimika Kusikiliza Ombi hilo Kwanza kutoka pande zote
Amesimama wakili Peter Kibatala
anachambua kwanza Viapo vyao ambavyo vimesainiwa na Mawakili wao na Wateja (Wakina Mdee)
1.Viapo havionyeshi waapaji (Wakina Mdee) Wameapa wapi.
2.Waapaji hawajataja Dini zao katika Viapo vyote
Kibatala anaendeleaaaaaa
Wakili Kibatala anaendelea kusema
Ombi lao la kubaki na ubunge alijaelekezwa kwa yoyote kati ya wadaiwa (Mdee na wenzake)
Katika maombi yao hawasemi kama wanataka kuendelea kuwa wanachama wa Chadema ila wanataka kuendelea na ubunge tuh