Yamenifika shingoni sijui la kufanya mimi

Ahsante mkuu nimeupokea ushauri wako
 
Ulisoma chuo gani wewe?
 
I’m

upo sahihi jana kuna mtu alimieleza mama yake alimtelekeza kwa bibi yake bila sababu na yupo hai
Akaona haitoshi akamtumia na majini
Yaani ulimwengu huuu
Wazazi wengine sio kama wazazi
Acha tu mpaka unaanza kufikilia au kuna kitu kinawaendesha sio wao
 
Ahsante Nimekuelewa mkuu
 
😁sawa mkuu nimekuelewa
 
Sio mimi ila hili jina nimelitoa kwa huyo folk unayemzungumzia ndo maana nikajiita Folk Part II baada ya kuona aliyoyapitia namimi nayapitia kama kuumwa nayeye ikampelekea had kutokupendwa tena
 
Ahsante sana mkuu ubarikiwe kwa ushauri wako
 
Kabla sijakushauri,nataka ujue tupo tuliowahi kuyaishi hayo,tukiwa na mama wa kambo na baba asiyejali na m'binafsi,mshirikina sana na anayetaka utajiri wa kafara ya mtoto wa kwanza kuzaliwa [wakiume].
Suluhisho lilikuwa ni kujitenga naye kwa maisha yote,bila kuonana hata kuwasiliana[hiyo ni pamoja na jamii yake yote {pamoja na kuwa tupo mkoa mmoja}na kumwachi kila kitu kisicho hamishika.
USHAURI;
Kwa umri wako huhitaji usimamizi wa baba., Kwa usalama wako,ondoka hapo uende asikokujua,badilisha simu[usiwasiliane na yeyote wa kwenu kwa muda ,ishi maisha yako.
Hata siku moja,usijione mnyonge hata kuwaza kujidhuru kwasababu za ujinga wa mtu [ni upumbavu], chukua hatua mapema na usiage kwa yeyote.
 
Ahsante ndugu ubarikiwe umenena vizuri kinachoniumiza niyeye kutokufurahia ninavyovifanya yan anakunja sana mkuu
Huyo hataki uwe karibu yake ila we hujamsoma, inawezekana anafanya hivyo ili ujiongeze.

Mzee wangu wakati fulani alikuwa anajenga chumba cha nje kwa ajili ya watoto wa kiume ila ilipofikia muda namalizia chuo alikibadili matumizi akafugia 😂(kwa sasa nimemuelewa). Hapendi kabisa maswala ya kukaa nyumbani muda mrefu na kutokomeza ilo akafanya hivyo. Kwahyo kuna mambo mengine bila kukua vya kutosha ni ngumu sana kuyaelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…