Aibu kubwa! Msomi unakosaje kazi ya kufanya nchi hii yenye kila aina ya rasilimali?

Aibu kubwa! Msomi unakosaje kazi ya kufanya nchi hii yenye kila aina ya rasilimali?

Nakubaliana na wewe hapa kuna tatizo. Lkn usikubali kudhalilika kwa kukaa kwa mtu (hata kama Ni nduguyo) kwasabb tu unaziogopa changamoto.
Vipi wewe umeshamfukuza shemeji yako au ndio unamlia timing🧐
 
Nimekuuliza gharama za kukuza Miche ya parachichi na michikichi mpaka muda kuanza kuvua
Miaka 3 tu. Wakati unasubiria unakuwa unapiga ishu za kilimo kama karanga na mihogo ambayo haihitaji chochote.

Jamani ingieni kwenye kilimo
 
Kama kilimo kingekuwa kinalipa,basi mikoa ya Kanda ya ziwa,nyanda za juu kusini ingeongoza kwa kipato kimkoa na mchango kwenye pato la Taifa,lakini unajua mkoa unaoongoza?ni Dar es salaam,mkoa ambao hauna shughuri kubwa za kilimo lakini unachangia asilimia 80 ya pato la Taifa!!
Kwa kila shilingi 100 inayoingizwa kwenye mfuko wa Taifa,asilimia 80 inatoka Dar!!hiyo mikoa inayolima ipo wapi??
Hoja zako kwamba vijana wakiomaliza vyuo waende mikoani,wakamate ardhi(ambayo ipo bwelele)walime,zimekaa kinadhalia tu na ni story za kwenye makaratasi hazina uhusiano na Hari halisi iliyopo kwenye mazingira yao.
Huwezi kutoka hapa ukaenda Katavi,ukachukua ardhi,ukaanza kulima mahindi,ukavuna!na ukapiga pesa ndeefu!?
Mfuko wa mbolea unauzwa 100000Tsh,gunia la mahindi linauzwa 20000Tsh!

Mwamba kumbuka kuna kilimo cha kujikimu na kilimo cha biashara. Huku kanda ya ziwa kilimo ni cha kujikimu, ziada ndio tunauza.

Lau tungefanya kilimo cha biashara, maarifa ambayo hatunayo kama wenzetu wa Nyanda za juu kusaini, mjadala huu ungekuwa na afya.

Mfano WA kilimo cha biashara ni kilimo cha maua huko Kaskazini, kilimo cha chai na Pareto huko kusini.
 
Miaka 3 tu. Wakati unasubiria unakuwa unapiga ishu za kilimo kama karanga na mihogo ambayo haihitaji chochote.

Jamani ingieni kwenye kilimo
Ungejazia na pcha , jins Miche yako ilivyokua, shamba lnavyopendeza tupate motsha zaid..
 
Miaka 3 tu. Wakati unasubiria unakuwa unapiga ishu za kilimo kama karanga na mihogo ambayo haihitaji chochote.

Jamani ingieni kwenye kilimo
Hapa ishu inayogomba ni mtaji ku sustain hicho kilimo mpaka uanze kupambana na changamoto za soko
 
Kwa hiyo unataka kusema hakuna haja ya kuwa na elimu?
Kwani umachinga na bodaboda vinahitaji ujinga mkuu? Kazi ya elimu ni kupambana na changamoto za mazingira yako.

Nchi zetu za Afrika hazina mazingira yanayomfanya msomi aishi mtaani kwa elimu yake. Watu hawasomi vitabu, watu hawahitaji msaada wa kisheria, hawahitaji ushauri wa kisaikolojia, hawahitaji ushauri wa kuanzisha na kuendeleza biashara, hawahitaji ramani kujenga nyumba, hawahitaji ushauri wa kiafya na kitabibu. Haya yangefanyika wasomi wangekuwa lulu.
 
Mleta hoja nakuunga na kukupinga pia!

Unalima mbegu zipo?
Soko la uhakika unalo? Au nitafute?
Usafiri kwenye hayo maeneo yapo? Au tunatumia punda?
Mambo ya kodi, ushuru leseni unayajua kuwa yapo?

Kilimo ni pesa tena hiyo aridhi bila mbolea na madawa utapoteza kazi bure!
Ukikuta sehemu aridhi bwelele ipo ujue changamoto ni usafri! Au na barabara nitengeneze mimi?

kwa vijana wasomi,

Wajaribu kuunganisha nguvu, mawazo na ubunifu ili kutatua changamoto endapo watafanya kazi kwa umoja ni rahisi sana kukopesheka( vijana wamemaliza chuo hawana mitaji), hata kama ni kilimo watapunguza gharama ya pesa na muda wakiwa katika vikundi.
hapa chanagamoto kubwa huwa ni UBINAFSI.

wengi wao kila mmoja anataka apambane kivyake! hapo kutoboa ni ngumu.. kuweni na umoja kama ule mnafanya (Group discussion)huko vyuoni.

NJIA YA MAFANIKIO INA GHARAMA YAKE NI ZAIDI YA KUKAA MJINI AU KIJIJINI.
 
Usisahau kuwa Kilimo cha biashara kinaitaji mtaji pia. Na sio kwamba hatuba hio akili ya kuwekeza kwenye Kilimo ila changamoto zinakuja kwenye mtaji wa kuanzia
 
Nakubaliana na wewe hapa kuna tatizo. Lkn usikubali kudhalilika kwa kukaa kwa mtu (hata kama Ni nduguyo) kwasabb tu unaziogopa changamoto.
Co kuzalilika ni uhalica umelima kwa changamoto nyingi umevuna unauza kwa shida chini ya gharama za uzalishaji
Leta hoja sio unarukaruka kwenye key board
Mi naruka mbona we umekaa au hiyo ndio hoja bac sawa nimeiona hoja yako nitaifanyia kazi
 
Mbona na wewehutumii nafac yako kuwapa hao vijana matumaini halic ili ucwe kama cc
Bora umenisaidia. Watanzania wanataka kusikia mialiko kwamba waje hoteli fulani nyota tano Kuna mafunzo ya ujasiriamali.

Vyote ni upuuzi tu.
1. Nani aliwafundisha bodaboda nchi nzima kuingia kwenye hiyo biashara?
2. Nani aliwafundisha wapiga debe nchi nzima?
3. Nani aliwafundisha mama ntilie nchi nzima?
4. Nani aliwafundisha machinga nchi nzima?
5. Nani aliwafundisha wakulima nchi nzima?

Kama mafunzo yangekuwa na maana Basi wahitimu wa SUA wangekuwa ndiyo wakulima wenye mafanikio makubwa nchi hii. Maana wanasomea kilimo miaka 4, lkn wakimaliza wanafua boksa za shemeji zao.

Mafanikio yako ndani mwa mtu. Ukiyasukuma yanatoka nje, ukiyaacha ndani unakufa nayo.
 
Usisahau kuwa Kilimo cha biashara kinaitaji mtaji pia. Na sio kwamba hatuba hio akili ya kuwekeza kwenye Kilimo ila changamoto zinakuja kwenye mtaji wa kuanzia
Anza kidogo kidogo mkuu. Tumia watu wanaokulisha na kukuvisha wakati huna kazi wakupe mtaji kidogo utoboe kupitia kilimo
 
Anza kidogo kidogo mkuu. Tumia watu wanaokulisha na kukuvisha wakati huna kazi wakupe mtaji kidogo utoboe kupitia kilimo
Sio kila anaekulisha na kukuvisha anataka ufanikiwe au anauwezo wa kukusapoti
 
Issue sio ardhi issue unacholima utauza wapi au utegemee dalali sokoni

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
Unajua nashangaa sana hiyo nchi. Hivi kweli Waziri wa biashara Professor mzima ameshindwa kuweka mfumo mzuri wa kuuza mazao sokoni hata akawaachia madalali jamaa wasio na Elimu ya biashara hata darasa moja? Kuna mambo yanafanyika Tanzania ni vichekesho lakini pia highly counterproductive kwa uchumi na maendeleo. Hao madalali ni kama wameshindikana halafu kila pembe ya nchi.
 
Unajua nashangaa sana hiyo nchi. Hivi kweli Waziri wa biashara Professor mzima ameshindwa kuweka mfumo mzuri wa kuuza mazao sokoni hata akawaachia madalali jamaa wasio na Elimu ya biashara hata darasa moja? Kuna mambo yanafanyika Tanzania ni vichekesho lakini pia highly counterproductive wa uchumi na maendeleo. Hao madalali ni kama wameshindikana halafu kila pembe ya nchi.
Waziri wa biashara nchi hii huwa Hana kazi yoyote. Hakuna kabisa zaidi ya kupiga picha na kurekwbisha tai shingoni.
 
Ukute na wewe umeajiriwa na mshahara haufiki milion mbili njaa Kali una wananga wenzako hapo
Siwanangi, nawaamsha wasikae sebuleni kwa dada zao miaka 3 ama zaidi wakisubiria ajira ambazo hazipo na hazitakuwepo.

Wajiajiri kwenye kilimo.
 
Back
Top Bottom