Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Taifa wa CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji ajiunga na CCM

Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu Taifa wa CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji ajiunga na CCM

Hawa Sasa wanaenda sababisha vita huko wanakoenda. Kuna watu wamekuwa wazalendo ndani ya chama chao, wanakuja mamluki na kubeba nyadhifa mbalimbali ilhali wao wanaendelea kubakia na uvuvuzela wao.
 
CHADEMA haiwezi kuzuia watu kununuliwa ama kujiuza , hii si kazi yetu , bali unachotakiwa kufahamu ni kwamba kabla KANU ya Kenya haijafa na kuzikwa , ilifanya kama inavyofanya CCM, ilinunua kila imtakaye akiwemo Raila Odinga aliyepewa Ukatibu Mkuu.
Sawa lakini KANU wote wamerudi madarakani kwa mwavuli wa Jubilee. Hadi majuzi Moi alikuwa anatoa ushauri Nchi iendeshwe vipi. Sasa sielewi kama tunahitaji chama tofauti awa wanasiasa tofauti.
 
hp4510,
Ndio maana nimekushangaa uliposema eti wabunge wengi walipatikana kwa ajili ya uwepo wa Lowassa. Kama watu wanachagua mgombea wa cdm kisa hawaipendi CCM na kinyume chake, iweje useme hao wa CHADEMA wameletwa na Lowassa. Ndio nikataka unidhibitishie alifungua matawi mangapi.
 
Simba ikishuka daraja, wale mashabiki au wapenzi wa Simba hawawezi kuhamia kuanza kuipenda ama kuishabikia Yanga. Wengi watahamia timU nyingine lakini sio Yanga.

Wapenzi, wamachama na mashabiki wa CHADEMA ni wale wasiofurahishwa CCM kwa Mambo yake yote, kwa matendo yake yote, kwa hila zake zote.
 
Kwani Sheria Ya Vyama Vya Siasa
Vipoanzishwa 1992 Inasema Nini?
Inataka Ccm Ibaki Yenyewe Ama Na Vyama Vingine
 
Bora nikae kimya maana nilishapigwa ban wamenirudisha leo kisa niliandika kuhusu wale wanyama akivuka mmoja wengine wanafuata.

Ila CDM wamevuna walichopanda na mwisho wao naanza kuona shimo moja na NCCR au CUF.
 
njaa haina 'baunsa'
Kabisa

Kuna dogo mwingine anaitwa Ahmed Ally pale CDM zao la mzee wa MABADILIKO.

Na siku ukisikia Tundu ndio utazimia kabisa.

Unaitwa huu mchezo hautaki hasira.
 
Kuhama chama ni haki ya msingi ya kila mtu kikatiba, ndiyo maana Tundu Lissu alihama kutoka NCCR Mageuzi na kwenda Chadema, Zitto alihama kutoka Chadema na kwenda ACT, Sumaye na Lowasa walihama kutoka CCM na kwenda Chadema na baadaye wamerudi tena CCM, Nyarandu alihama CCM na kwenda Chadema, Maalimu Seif alihama CCM na kwenda CUF na baadaye ACT.

Huo ndio ukomavu wa demokrasia, unaamua uwe chama gani kwa ridhaa yako. Mtu anapohama chama hutakiwi kumkejeri na kumtukana ni haki yake kikatiba na hiyo ndiyo demokrsia tunayoitaka kila siku na kuihubiri.
Mkuu, pigia mstari nipaone nilipomkejeli mtu.

Mi mwenyewe nakubali mtu kutafuta maslahi sehemu anayeona panamfaa, siasa ni kama ajira zingine.
 
Kwani Sheria Ya Vyama Vya Siasa
Vipoanzishwa 1992 Inasema Nini?
Inataka Ccm Ibaki Yenyewe Ama Na Vyama Vingine
Ibaki na Vyama vingine,.
Lakini zipo kauli zinasema zinataka kuua upinzani,na kua kwenyewe ni kuzuia mikutano ya wapinzani kujitangaza,kununua viongozi wa upinzani na kubambikia kesi wapinzani .
 
Hawa Sasa wanaenda sababisha vita huko wanakoenda. Kuna watu wamekuwa wazalendo ndani ya chama chao, wanakuja mamluki na kubeba nyadhifa mbalimbali ilhali wao wanaendelea kubakia na uvuvuzela wao.
Kwa kukusaidia japo sina upande wa kivyama, ni kwamba ikitokea CCM ikashinda nafasi ya uraisi kwa mara nyingine basi watu wengi waliopo na waliokuja kuunga juhudi hawataweza kulala na njaa, nikimaanisha kuna nafasi nyingi sana za uteuzi unaomtegemea raisi na wengineo waliopo kwenye mfumo, hivyo kila mmoja anaweza akapata nafasi na bado zikabaki. fikiria nafasi za uteuzi alizonazo raisi then fikiri ni nani atakosa.
 
Back
Top Bottom