Baba mkwe Shahidi wa Yehova kakataa mahari ya pesa, anataka apelekewe magovi matano ya watu wazima

Baba mkwe Shahidi wa Yehova kakataa mahari ya pesa, anataka apelekewe magovi matano ya watu wazima

Beba hiyo barua peleka polisi ili waitwe wakuonyesho wapi wanapopatia(ga) hicho walichokuagiza maana haiwezekani wakurupuke hiyo ni desturi yao. Wasipoonyesha waulize wewe ungepata wapi? Hakuna ndoa hapo wachafulie halafu binti akijileta atundikwe mimba msubiri msikie watasemaje tena

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
Naogopa hata kuunganisha nao ukoo. Yaani yule mzee awe mzazi mwenza wetu???
Inafikirisha sana aisee
 
Hapo tayari wameshatangaza vita. Kijana akutane na binti wapate mtoto maisha yaendelee. Wazee wanakuwa wadwanzi kama nini.
 
Umefanya kosa kubwa sana kuwachafua mashahidi wa Yehova na uchafu/uongo uliouandika hapa kwenye hii forum.

Laiti ungejua ukubwa wa kosa ulilolifanya ungeomba moderators waufute uzi huu. Story yako haina ukweli wowote ule. Hakuna shahidi wa Yehova yeyote ambae anaweza kufanya hicho ulichosema.

Mimi nimesharipoti huu uzi ufutwe kwa sababu umelenga kuwachafua mashahidi wa Yehova, hauna maana yoyote nyingine zaidi ya hiyo.
 
Ukiusikia usemi wa watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa basi sasa ndio amini kuwa usemi huo upo na unafanya kazi.

Jumapili iliyopita nilimsindikiza mpwa wangu ( mtoto wa dada yangu yangu) kwenda kujitambulisha na kupangiwa mahari huko kijijini kwa binti (Bibi harusi mtarajiwa)

Kwa kweli mapokezi yalikuwa baridi sana, na tukadhania huenda tungeitiwa wezi. Binti alifichwa na hatukuwa na mwenyeji hata mmoja.

Wenyeji walitupokea, wakatukaribisha chini ya mti na kutuacha kwa zaidi ya masaa manner, huku wao wakiwa ndani wakiendelea na kikao chao.

Baada ya masaa manne kupita hatimaye wakaja tulipo na kuanza kutuuliza maswali ya kebehi sana kuhusu imani yetu.

Wakatuambia wao ni Mashahidi wa Yehova, kwanini tumeenda kumposa binti yao tusitafute binti wa dhehebu letu?

Tukajibu kuwa sisi wote ni Wakristo, lakini hawakuridhishwa na jibu hilo. Dhihaka na kebehi zikaendelea.

Hatukupewa chakula wala maji hadi tunaondoka, tulaambiwa majibu yetu yatafuata kwa barua.

Leo jioni mshenga katuletea barua yenye jibu la ombi letu. Tunatakiwa kupeleka magovi matano ya wanaume watu wazima.

Isome mwenyewe hiyo barua.

Wito wangu kwenu wazazi, kama hamtaki binti yenu aolewe na mtu msiye mtaka, muwe wawazi, sio mnaleta mambo ya ajabu ajabu.

View attachment 2350522
Tukutane tar 18 sep mwaka gani huo? 2020
 
Umefanya kosa kubwa sana kuwachafua mashahidi wa Yehova na uchafu/uongo uliouandika hapa kwenye hii forum.

Laiti ungejua ukubwa wa kosa ulilolifanya ungeomba moderators waufute uzi huu. Story yako haina ukweli wowote ule. Hakuna shahidi wa Yehova yeyote ambae anaweza kufanya hicho ulichosema.

Mimi nimesharipoti huu uzi ufutwe kwa sababu umelenga kuwachafua mashahidi wa Yehova, hauna maana yoyote nyingine zaidi ya hiyo.
Inawezekana ni kweli na nibwa imani hiyo lkn huo ni msimamo hauusiani na dini. Ila kwa vile dini hyo ni watata... Mshenga akaunganisha matukio
 
Tukutane tar 18 sep mwaka gani huo? 2020
Ukisoma tarehe ya juu, mwanzo wa barua ni mwaka 2022. Huo mwaka wa ndani ya barua nadhani ni makosa tu ya kiuandishi, hasa ukizingatia umri wa mwandishi ni mtu mzima sana.
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Kiufupi,
Ni Familia ya kichawi hiyo mkuu,
Ushauri wangu: usioe Hapo,utajuta
Hilo ndio azimio letu. Hata bwana mdogo tume mshauri aachane na huyo binti, kwani hata wakisema wazae bila ndoa, atakuwa anauunganisha ukoo na watu wa ajabu.
 
Umefanya kosa kubwa sana kuwachafua mashahidi wa Yehova na uchafu/uongo uliouandika hapa kwenye hii forum.

Laiti ungejua ukubwa wa kosa ulilolifanya ungeomba moderators waufute uzi huu. Story yako haina ukweli wowote ule. Hakuna shahidi wa Yehova yeyote ambae anaweza kufanya hicho ulichosema.

Mimi nimesharipoti huu uzi ufutwe kwa sababu umelenga kuwachafua mashahidi wa Yehova, hauna maana yoyote nyingine zaidi ya hiyo.
Kuandika Baba Mkwe Shahidi wa Yehova sio kosa. Wala sijasema Mashahidi wa Yehova hawapokei mahari nyingine isipokuwa magovi.

Nimemuongelea mtu mmoja na mawazo yake.

Sasa kama wewe ni Shahidi wa Yehiva unayehisi umeumizwa hisia zako kwa uzi wangu huu, nenda katangulie mahakamani ili uipate haki yako
 
Back
Top Bottom