Benki ya Dunia yasitisha kufadhili mradi wa REGROW. Mradi huo unahusishwa na ukiukaji wa Haki za Binadamu nchini Tanzania

Benki ya Dunia yasitisha kufadhili mradi wa REGROW. Mradi huo unahusishwa na ukiukaji wa Haki za Binadamu nchini Tanzania

Kwa mujibu wa taarifa iliyonukuliwa na gazeti la the Guardian inaelwza kwamba Benki ya Dunia WB Imezuia kuendelea kutoa ufadhili wa Mradi wa Regrow kufuatia madai ya ukiukwaji wa Haki za binadamu.
Hawa pia walikataa JNHPP… lakini hawana shida na Israel kuua wapalestina
 
Kule maandamano yakiongozwa na maafande huku wananchi wanafukuzwa mbugani kule misaada inaondoshwa kwa kuwahujumu wananchi.

Ahahahaa, pesa inatafutwa kwa njia zote!.
 
Ni aibu kwa serikali taasisi za nje kuonesha kujali maisha ya wananchi wako wakati nyie wenyewe mnajali wanyama kuliko binadamu.
 
madudu na dhuluma ya awamu ya 4 hayo, walifukuza watu ruaha kama vile wafanyavyo sasa hivi kupora ardhi ya Watanzania huko Ngorongoro, WB ilikuwa under pressure kufadhili dhuluma na uporaji …
 
madudu na dhuluma ya awamu ya 4 hayo, walifukuza watu ruaha kama vile wafanyavyo sasa hivi kupora ardhi ya Watanzania huko Ngorongoro, WB ilikuwa under pressure kufadhili dhuluma na uporaji …
Hakuna anaefukuzwa Ngorongo vinginevyo hii statement ya CAG isingesema haya 👇
Screenshot_20240418-180813.jpg
 
Benki ya Dunia imesitisha ufadhili wa mradi mkubwa wa utalii nchini Tanzania kwa madai kuwa umesababisha mateso miongoni mwa maelfu ya wanakijiji kama ilivyokuwa katika kuwahamisha jamii ya maasai kutoka Ngorongoro.
Hii ni baada ya kundi moja la kutetea haki nchini Marekani kwa muda mrefu kumtaka mkopeshaji huyo wa kimataifa kuchukua hatua hiyo.

Benki ya Dunia imechukua hatua ya kusitisha mradi huo wa dola milioni 150, ambao unalenga kuboresha usimamizi wa maliasili na utalii katika vijijini vya kusini mwa Tanzania.

Katika taarifa iliyotolewa leo Jumanne, Taasisi ya Oakland iliyokuwa ikiendesha kampeni hiyo imedai kwamba "kushindwa kuchukua hatua za haraka kulisababisha madhara makubwa kwa jamii."

Angalau dola milioni 100 zilikuwa tayari zimetolewa kwa mradi huo, ambao ulianza mwaka 2017 na hatua ya kusimamishwa kwake imeanza rasmi Aprili 18.

Taasisi ya Oakland, shirika la kutetea haki za binadamu lenye makao yake mjini California ambalo linaangazia jamii zilizotengwa, kwa miaka mingi imekuwa ikitoa wito kwa Benki ya Dunia kusitisha ufadhili wa mradi unaojulikanao kwa kifupi REGROW, kwa kwa madai ya ukiukwaji mkubwa wa haki miongoni mwa wenyeji katika eneo hilo.

Kundi hilo katika ripoti iliyotolewa mwezi Novemba liliishutumu Benki ya Dunia kwa kushindwa kuziwajibisha mamlaka za Tanzania kwa kile ilichokiita "mauaji ya watu wengi na unyanyasaji wa kijinsia" wakati wa upanuzi wa Mbuga ya Wanyama ya Ruaha.

Ripoti hiyo ilisema mbinu za serikali ya Tanzania kulazimisha jamii kuondoka ili kuongeza utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, kama lengo la mradi wa REGROW, "zilisababishwa moja kwa moja na ufadhili wa Benki ya Dunia."

Benki ya Dunia ilisema wakati huo kwamba "haivumilii vurugu katika miradi inayoifadhili," na iliunda jopo la wakaguzi kupitia malalamiko yanayohusiana na mradi huo ili "kuamua kama maswala yaliyoibuliwa ni halali."

Katika mawasiliano ya hivi majuzi kati ya Benki ya Dunia na Taasisi ya Oakland yaliyoonekana na shirika la habari la The Associated Press, mkopeshaji huyo alithibitisha kusimamishwa kwa malipo zaidi kwa mradi wa REGROW "hadi kuwe na uhakika kwamba mradi unazingatia viwango vya kijamii na kimazingira."

Anuradha Mittal, mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Oakland, alisema uamuzi wa Benki ya Dunia kusitisha ufadhili ni ushindi kwa jamii zilizotengwa katika taifa hilo la Afrika Mashariki. Mital ameongeza kuwa uamuzi huo unatuma ujumbe mzito kwa serikali ya Tanzania kwamba kuna matokeo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki unaofanyika kote nchini humo wakati ikiendeleza biashara ya utalii. Hata hivyo, mamlaka ya Tanzania haikutoa maoni kuhusiana na taarifa hii.
 
Benki ya Dunia imesitisha ufadhili wa mradi mkubwa wa utalii nchini Tanzania kwa madai kuwa umesababisha mateso miongoni mwa maelfu ya wanakijiji kama ilivyokuwa katika kuwahamisha jamii ya maasai kutoka Ngorongoro.
Hii ni baada ya kundi moja la kutetea haki nchini Marekani kwa muda mrefu kumtaka mkopeshaji huyo wa kimataifa kuchukua hatua hiyo.

Benki ya Dunia imechukua hatua ya kusitisha mradi huo wa dola milioni 150, ambao unalenga kuboresha usimamizi wa maliasili na utalii katika vijijini vya kusini mwa Tanzania.

Katika taarifa iliyotolewa leo Jumanne, Taasisi ya Oakland iliyokuwa ikiendesha kampeni hiyo imedai kwamba "kushindwa kuchukua hatua za haraka kulisababisha madhara makubwa kwa jamii."

Angalau dola milioni 100 zilikuwa tayari zimetolewa kwa mradi huo, ambao ulianza mwaka 2017 na hatua ya kusimamishwa kwake imeanza rasmi Aprili 18.

Taasisi ya Oakland, shirika la kutetea haki za binadamu lenye makao yake mjini California ambalo linaangazia jamii zilizotengwa, kwa miaka mingi imekuwa ikitoa wito kwa Benki ya Dunia kusitisha ufadhili wa mradi unaojulikanao kwa kifupi REGROW, kwa kwa madai ya ukiukwaji mkubwa wa haki miongoni mwa wenyeji katika eneo hilo.

Kundi hilo katika ripoti iliyotolewa mwezi Novemba liliishutumu Benki ya Dunia kwa kushindwa kuziwajibisha mamlaka za Tanzania kwa kile ilichokiita "mauaji ya watu wengi na unyanyasaji wa kijinsia" wakati wa upanuzi wa Mbuga ya Wanyama ya Ruaha.

Ripoti hiyo ilisema mbinu za serikali ya Tanzania kulazimisha jamii kuondoka ili kuongeza utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, kama lengo la mradi wa REGROW, "zilisababishwa moja kwa moja na ufadhili wa Benki ya Dunia."

Benki ya Dunia ilisema wakati huo kwamba "haivumilii vurugu katika miradi inayoifadhili," na iliunda jopo la wakaguzi kupitia malalamiko yanayohusiana na mradi huo ili "kuamua kama maswala yaliyoibuliwa ni halali."

Katika mawasiliano ya hivi majuzi kati ya Benki ya Dunia na Taasisi ya Oakland yaliyoonekana na shirika la habari la The Associated Press, mkopeshaji huyo alithibitisha kusimamishwa kwa malipo zaidi kwa mradi wa REGROW "hadi kuwe na uhakika kwamba mradi unazingatia viwango vya kijamii na kimazingira."

Anuradha Mittal, mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Oakland, alisema uamuzi wa Benki ya Dunia kusitisha ufadhili ni ushindi kwa jamii zilizotengwa katika taifa hilo la Afrika Mashariki. Mital ameongeza kuwa uamuzi huo unatuma ujumbe mzito kwa serikali ya Tanzania kwamba kuna matokeo kwa ukiukwaji mkubwa wa haki unaofanyika kote nchini humo wakati ikiendeleza biashara ya utalii. Hata hivyo, mamlaka ya Tanzania haikutoa maoni kuhusiana na taarifa hii.
$150m ni hela ndogo sana kwa serikali; hata mimi nanaweza kuzitoa kiziba pengo hilo. Muhusika anitafute nimpe checki
 
$150m ni hela ndogo sana kwa serikali; hata mimi nanaweza kuzitoa kiziba pengo hilo. Muhusika anitafute nimpe checki
Hiyo ni Bilioni 400 sawa na kujenga rami zaidi ya kilometa 300 sio hela ndogo!
 
Wamewaone TU,,mbona hukonhakuna shida kabisa,,Mbona wakati wajiwe alikataa fedha za elimu za masharti ya ushoga
 
Back
Top Bottom