PakiJinja
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 11,689
- 25,848
Ngoja tuone litakavyokuwaKwa hiyo unataka kusema remittance ya diaspora itaanza kupungua worldwide?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ngoja tuone litakavyokuwaKwa hiyo unataka kusema remittance ya diaspora itaanza kupungua worldwide?
Hakika kabisa! Kuliko hivi sasa tumebaki kujisifia watu ambao tayari walikwisha ukana uraia wa Tanzania kama Sunak Waziri Mkuu wa UK wa sasa ni Mtanzania, au huyu mwafrika ambaye amechaguliwa kuwa seneta huko Ujerumani ni Mtanzania kwa kuwa tu wazazi wake ni wa asili ya Tanzania au yule Mzanzibari mwandishi wa vitabu ambaye sasa ana uraia wa Uingereza.Jamaa nmemuelewa, uraia pacha usiwe kwa watu wa nje lakini uwe ni kwa ajili ya haya makundi mawili ya watanzania
1)Watoto walozaliwa na wazazi ambapo mzazi mmojawapo ni mtanzania
2)Watanzania ambao wapo nje (ughaibuni) waruhusiwe kuwa raia wa hizo nchi pamoja na kuwa bado watanzania.
Hio itazuia hofu iliopo kwamba mwekezaji wa nje ataomba uraia wa tz then aje abebe rasilimali za wazawa kwa sababu haki ya uraia pacha wanapewa wazawa tu.
Bongo zozo kwa hili ana point nzuri sana kiukweli.
Mbona masuala ya ushoga na ndoa za jinsia moja serikali ilinywea baada ya nchi za magharibi kuijia juu na kukanusha maneno Makonda?kwani nimesema ni mtanzania au aliwahi kuwa mtazania?
msisitizo wangu ni kwamba mtu asiye raia wa tz hawezi akasema jambo kisha serikali ikamsikiliza. Hata hao walioukana uraia kisha wanataka serikali iwasikilize, serikali haiwezi ikamsikiliza mtu asiye raia kuhusiana na masuala ya ndani ya nchi.
anzisha uzi kuhusiana na ushoga na usagaji, huu uzi unahusu masuala ya uraia pachaMbona masuala ya ushoga na ndoa za jinsia moja serikali ilinywea baada ya nchi za magharibi kuijia juu na kukanusha maneno Makonda?
Nimeisevu comment yako lakini usije tu kubadilisha ID.Hiyo hoja ikikubaliwa mniite mbwa, niko nyuma ya keyboard nimekaa.
Uhuru umewafaidisha tu elites na vizazi vyao. Hatutaki iwe hivyo kwa uraia pacha.Nyie ndio wale mliochelewesha uhuru eti tusipewe uhuru hadi wote tulielimike. Hopeless.
Umechanganyika na roho mbaya na uoga kwamba diaspora wameshaamka kutoka usingizi wa pono !!Ushamba wa viongozi ndio tatizo
Umemaliza !!CCM ni waoga wa kila kitu.
Hata kitoto kidogo kikiongea kitu, ambacho hawakipendi utaanza kuona nkimepelekewa mavifaru ya Jeshi.
Huu uoga wa CCM ndio unapeleka wanaogopa KILA KITU, KILA MTU na wana tahadhari muda wote.
Kinachokwamisha hili suala ni uoga tu.
Pesa unatuma hata mara kumi kwa siku hakuna mtu wa kutaka ujieleze labda kama ni pesa za magumashi.Na nchi kama US sasa hivi wanafuatilia sana transactions za watu wanaofanya kazi kule. Kutumatuma hela kiwango kikubwa au mara tatu ndani ya mwezi lazima account yako waiminye na kukutaka ujielezee.
Hapo ndiyo mtaona watu wanakubali yaishe kwa kuamua kutotuma hela kuliko habari za kuonywa onywa
Nitakuacha na ujuzi wako, wala sitakuita mbishi, bali nakuita mjuziPesa unatuma hata mara kumi kwa siku hakuna mtu wa kutaka ujieleze labda kama ni pesa za magumashi.
Madhara ni ardhi yote nzuri watachukua wageni na tunaweza kuja kutawaliwa na mamluki nusu mtz nusu muingereza, hatufungulii mlango mabeberuUraia pacha hauna madhara yoyote.
Sibadilishi ID aiseNimeisevu comment yako lakini usije tu kubadilisha ID.
Nchi kubwa na ndogo duniani ambazo zinajali mataifa yao na yanajali utaifa wao tena ni wazalendo kweri kweri wala hawaziibii Nchi zao na wameruhusu Uraia pacha !! Sisi tuna uzalendo gani wa kutufanya tuukatae Uraia pacha ??!! Eti tunalinda utaifa wetu !! Khaa !! Tumuulize CAG kama kweli hao watu ni wazalendo wenye kujali Utaifa wao 😅😅🙏Wanasiasa wanawaza kutawala tu, hawawezi kuikubari.
Nchi gani iliyochukuliwa Ardhi yake nzuri yenye Uraia pacha ? Taja japo moja !!Madhara ni ardhi yote nzuri watachukua wageni na tunaweza kuja kutawaliwa na mamluki nusu mtz nusu muingereza, hatufungulii mlango mabeberu
Mawazo dhaifu kabisa.Madhara ni ardhi yote nzuri watachukua wageni na tunaweza kuja kutawaliwa na mamluki nusu mtz nusu muingereza, hatufungulii mlango mabeberu
Siku hiyo CHADEMA tukishashika Dola nitakuja PM na Konyagi yangu.Sibadilishi ID aise