CAG aongea na waandishi wa habari - Aprili 8, 2021

CAG aongea na waandishi wa habari - Aprili 8, 2021

CAG Kicheere anaongea na waandishi wa habari muda huu.

Updates;
========

CAG: NILIBAINI WAKALA NNE ZA SERIKALI ZILIKUWA ZINADAIWA BILIONI 783.39

TANROADS ilikuwa na deni kubwa lenye thamani ya bilioni 770.1 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka hazina, wakala wa majengo bilioni 1, RUWASA bilioni 12 na TARURA milioni 125

-Ni madeni ya wakandarasi, watoa huduma na washauri katika hizo taasisi nne

CAG: MIRADI INAYOTEKELEZWA INA TOZO YA RIBA YA BILIONI 14.9

Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) amesema miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ina riba ya bilioni 14.9 kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi kinyume na masharti ya mikataba

-CAG amesema malipo hayo hayana tija kwani yangeweza kuepukika kwani baadhi ya pesa ni za wafadhili ambazo zipo lakini mlolongo mrefu wa malipo kwa serikali unakwamisha

MALIASILI NA UTALII

CAG: Nilifanya ukaguzi maalum wizara ya maliasili na utalii, nilibaini bilioni 6.8 zililipwa kutoka kwenye mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii bila idhini ya afisa masuuli kinyume na kanuni ya fedha. Pamoja na haya nilibaini matumizi ya jumla ya bilioni 16 yalifanyika bila kuwa na hati za malipo pia yalibainika matumizi ya bilioni 11 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi na milioni 89 zilizotumiwa na makumbusho ya Taifa kwa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.

Kwa maoni yangu mkurugenzi wa utalii na mhasibu waliokuwa wanahusika walitumia vibaya fedha za tozo ya utalii jumla ya Tshs Bilioni 34

CAG: BODI YA WAKURUGENZI YA ATCL HAINA MJUMBE MWENYE UZOEFU NA MASUALA YA ANGA

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema hayo na pia kuongeza kuwa Shirika linadaiwa hivyo inakuwa changamoto kuruka kwenye baadhi ya maeneo

Pia Viwanja vya Ndege vimetajwa kuwa na changamoto
Kazi Kweli kweli
 
CAG Kicheere anaongea na waandishi wa habari muda huu.

Updates;
========

CAG: NILIBAINI WAKALA NNE ZA SERIKALI ZILIKUWA ZINADAIWA BILIONI 783.39

TANROADS ilikuwa na deni kubwa lenye thamani ya bilioni 770.1 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka hazina, wakala wa majengo bilioni 1, RUWASA bilioni 12 na TARURA milioni 125

-Ni madeni ya wakandarasi, watoa huduma na washauri katika hizo taasisi nne

CAG: MIRADI INAYOTEKELEZWA INA TOZO YA RIBA YA BILIONI 14.9

Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) amesema miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ina riba ya bilioni 14.9 kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi kinyume na masharti ya mikataba

-CAG amesema malipo hayo hayana tija kwani yangeweza kuepukika kwani baadhi ya pesa ni za wafadhili ambazo zipo lakini mlolongo mrefu wa malipo kwa serikali unakwamisha

MALIASILI NA UTALII

CAG: Nilifanya ukaguzi maalum wizara ya maliasili na utalii, nilibaini bilioni 6.8 zililipwa kutoka kwenye mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii bila idhini ya afisa masuuli kinyume na kanuni ya fedha. Pamoja na haya nilibaini matumizi ya jumla ya bilioni 16 yalifanyika bila kuwa na hati za malipo pia yalibainika matumizi ya bilioni 11 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi na milioni 89 zilizotumiwa na makumbusho ya Taifa kwa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.

Kwa maoni yangu mkurugenzi wa utalii na mhasibu waliokuwa wanahusika walitumia vibaya fedha za tozo ya utalii jumla ya Tshs Bilioni 34

CAG: BODI YA WAKURUGENZI YA ATCL HAINA MJUMBE MWENYE UZOEFU NA MASUALA YA ANGA

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema hayo na pia kuongeza kuwa Shirika linadaiwa hivyo inakuwa changamoto kuruka kwenye baadhi ya maeneo

Pia Viwanja vya Ndege vimetajwa kuwa na changamoto
Bila shaka yule Dr wetu aliyekua waziri kwenye utalii anahusika vilivyo kwenye hayo
 
Utabadilisha sana id lakini kitu cha " mdigo" kitakuning'inia milele huko ikweta.

Sawasawa all rounder!

Kuhusu kuibadili hii ID hasa kutoka kuiita All - Rounder na kuanza kutumia Jina hili la Generalist ( ambayo yote yana maana moja ) wala sijaficha na nilishawah Kuwaambia ( Kuwataarifu ) Watu ( Members ) hapa hivyo sioni kwanini hili ( hilo ) linawateseni mno.

Hizo ID's zingine za Mabasha zenu wala hazinihusu na nashangaa mwenye hiyo ID ya GENTAMYCINE kutwa mnatajataja huku mkiinasibisha na Mimi utadhani mlimbebea Mimba zake sasa mmejifungua na mnataka Huduma ( Matunzo ) Wapuuzi wakubwa nyie.
 
Mkuu kuna vitu huwezi kuficha..vinakutambulisha..moja ni hilo la kujibu kwa hovyo..ulianza kwa jina la dawa,ukaja sijui mzunguko na sasa hili.

Kwahiyo nawe una hamu ujibiwe hovyo?
 
Report umeilewa vizuri au unakurupuka tu.
Sasa nimeelewa kwanini hakutaka vyombo vya habari vifunguliwe.
Kumbe Dr Abbas anahusika kwenye huu uratibu wa matumizi yasiyo na utaratibu.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
CAG Kicheere anaongea na waandishi wa habari muda huu.

Updates;
========

CAG: NILIBAINI WAKALA NNE ZA SERIKALI ZILIKUWA ZINADAIWA BILIONI 783.39

TANROADS ilikuwa na deni kubwa lenye thamani ya bilioni 770.1 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka hazina, wakala wa majengo bilioni 1, RUWASA bilioni 12 na TARURA milioni 125

-Ni madeni ya wakandarasi, watoa huduma na washauri katika hizo taasisi nne

CAG: MIRADI INAYOTEKELEZWA INA TOZO YA RIBA YA BILIONI 14.9

Mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali(CAG) amesema miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini ina riba ya bilioni 14.9 kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi kinyume na masharti ya mikataba

-CAG amesema malipo hayo hayana tija kwani yangeweza kuepukika kwani baadhi ya pesa ni za wafadhili ambazo zipo lakini mlolongo mrefu wa malipo kwa serikali unakwamisha

MALIASILI NA UTALII

CAG: Nilifanya ukaguzi maalum wizara ya maliasili na utalii, nilibaini bilioni 6.8 zililipwa kutoka kwenye mfuko wa tozo ya maendeleo ya utalii bila idhini ya afisa masuuli kinyume na kanuni ya fedha. Pamoja na haya nilibaini matumizi ya jumla ya bilioni 16 yalifanyika bila kuwa na hati za malipo pia yalibainika matumizi ya bilioni 11 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi na milioni 89 zilizotumiwa na makumbusho ya Taifa kwa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.

Kwa maoni yangu mkurugenzi wa utalii na mhasibu waliokuwa wanahusika walitumia vibaya fedha za tozo ya utalii jumla ya Tshs Bilioni 34

CAG: BODI YA WAKURUGENZI YA ATCL HAINA MJUMBE MWENYE UZOEFU NA MASUALA YA ANGA

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali amesema hayo na pia kuongeza kuwa Shirika linadaiwa hivyo inakuwa changamoto kuruka kwenye baadhi ya maeneo

Pia Viwanja vya Ndege vimetajwa kuwa na changamoto
"Chadema" wametuharibia sana hii nchi.
 
WASIJE WAJANJA WAKATUMIA MWANYA KUMUHADAA MAMA,MAANA HIVI VIINI MACHO KODI ILIKUWA INAKUSANYWA TILIONI 2 NA POIN KWA MWEZI IWEJE KUWE NA MADENI
 
Kiufupi nimesikitika sana wezi na ubadhirifu wa fedha kila mahali. Mara matumizi mabaya, hundi ziko wazi, kinyume na mkataba au hamna mkataba, mara nyaraka hamna hadi nyingine nje ya bajeti.
Tuna safari ndefu ila sijui tunaekea wapi.
 
Zingine watakuwa wamekula waungamkono juhudi....maana Kuna Kipindi biashara ilishamiri kweli kweli....kwa madudu haya....ili kujilinda angebadili Katiba ili aendeleee kuficha uovu....ndio maana aliaanza na bunge la kijani tupu.
 
Kiufupi nimesikitika sana wezi na ubadhirifu wa fedha kila mahali. Mara matumizi mabaya, hundi ziko wazi, kinyume na mkataba au hamna mkataba, mara nyaraka hamna hadi nyingine nje ya bajeti.
Tuna safari ndefu ila sijui tunaekea wapi.
Dada angu yule hayati ndo katufikisha hapa, Tuzidishe maombi tu Mwenyezi Mungu azidi kutuepusha na haya madudu zaidi na zaidi..
 
Zingine watakuwa wamekula waungamkono juhudi....maana Kuna Kipindi biashara ilishamiri kweli kweli....kwa madudu haya....ili kujilinda angebadili Katiba ili aendeleee kuficha uovu....ndio maana aliaanza na bunge la kijani tupu.
Zingine watakuwa wamekula waungamkono juhudi....maana Kuna Kipindi biashara ilishamiri kweli kweli....kwa madudu haya....ili kujilinda angebadili Katiba ili aendeleee kuficha uovu....ndio maana aliaanza na bunge la kijani tupu.
Na zile show za fiesta huwezi kuniambia wasanii kama kina diamond walikuwa wanapiga show mshahara ubwabwa na soda.
 
Kumbe ndio maana waliamua kupeleka Bungeni wabunge wa Chama kimoja tu.

Huyu Mama Rais ni mpango wa Mungu. Alipewa hii riport na CAG kwenye kitabu cha peke yake, Mama karuhusu madudu yote yaje yasemwe
 
UHURU ni kitu kitamu sana jamani. Ona toka CAG aambiwe aseme, anagonga nondo tu, page kwa page! Mamaeeeehi
 
Back
Top Bottom