Pre GE2025 CCM wamchangia Lissu Milioni 5 atengeneze gari lake. Lissu azipokea
Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Wanajaribu kuwahadaa mabeberu ili mali binafsi za viongozi wa ccm zisikamatwe na marekani kwa ushenzi walioufanya kina Sugu juzi. Wanataka ionekane yale ni makosa ya polisi na wao ccm hawahusiki hivyo wasionekane wabaya kumbe ndio mashetani wenyewe.
 
Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema siasa si uadui hivyo ni vyema kushikana mkono panapobidi kwani wanasiasa wote wanaijenga Tanzania.
Yeye kama Nchimbi anaweza kuamini hivyo, lakini hawezi kuisemea CCM kama chama juu ya jambo hilo. Imekwisha onekana mifano mingi iliyo kinyume na hayo anayo yaamini Nchmbi.

Atoe mchango wake yeye kama Nchimbi. Vinginevyo ni hadaa tu za kawaida zilizo zoeleka.
Hata 'Chura Kiziwi', kuna wakati alikwenda kupapasa mto wa kulalia wa Tundu Lissu hospitalnii
 
1000031257.jpg
 
Lissu rudisha hizo hela, wanajikosha tu baada ya kuwatendea ukatili.
Lissu anaangalia tumbo lake na mustakabali wa familia yake. Wewe ni nani mpaka umwambie arudishe?

Kama 2015 alikula za fisadi papa na kushirikiana na mwenyekiti wake kutaka kumpeleka huyo waliesema fisadi papa ikulu. Sasa ndo atakataa hizi ambazo waliotoa hawakuwepo kwenye ile list yao ya mafisadi papa?

Anyway anaweza kujifanya anaikataa ili kuwafumba macho wajinga. Lakini wenye akili tumeshamjua toka 2015 kuwa na yeye ni miongoni mwa wapigania matumbo yao kupitia siasa uchwara za Tanzania.

I don't trust any politician iwe wa serikali, CCM or upinzani. Wote ni wale wale, tofauti ni vyama, vyeo na uongozi.
 
Huyu Awadhi Ni katili Sana TUNAOMBA tumchukulie Hatua katuaibisha Sisi Chama na serikali,,aliyofanya hakutumwa ule ulikuwa utashi wake.ccm hoyeee
 
vxr hiyo hela hata matairi haitoshi, hivi bungeni kuna biashara gani inayolipa hivyo hadi mtu atembelee VXR?
 
Kwa upande wake, Dkt Emmanuel Nchimbi amesema siasa si uadui hivyo ni vyema kushikana mkono pale panapobidi kwani wanasiasa wote wanaijenga Tanzania.
Hii taarifa ni tofauti na ile kwenye mada nyingine kuhusu CCM kummchangia Lissu.

Hawa wanaochanga hapa, hata kama ni wanachama wa CCM, lakini hii ni hiari binafsi ya watu hao kuchanga au kutochanga.

Hii pesa iliyo changwa hapa siyo ya CCM.
 
Ila kiukweli mambo kama haya nduo yalipaswa kumtaja rais ametoa, na sio chama. Ccm kina mambo mengi sana ya kufanya zaidi ya kutoa michango isiyo na tija kwa taifa
 
Alikataa ile hongo ya Abdul sasa Msigwa kamtumia Nchimbi.
Kuna issue Ccm wana itega kwa Lissu. Soon ita kuwa wazi. Usishangae Lissu akaenda kupokelea huo mchango Lumumba
Na Lissu akisha pokea tu, utasikia kejeli chungu nzima humu. Hawa watu ni majuha sana.
 
Mimi CCM lakini Chadema hawajamtendea haki Lissu

Lissu ni makamu mwenyekiti taifa kweli Chadema wanashindwa kumnunulia gari makamu mwenyekiti taifa la kutembelea? Kwa pesa za Ruzuku ambazo hakuna ambaye angehoji Lisu kununuliwa gari na chama kama makamu mwenyekiti taifa kuwa mojawapo ya kitendea kazi chake ni kuwa na gari na dereva vyote vikigharimiwa na Chama

Chadema pesa mnapeleka wapi hadi makamu mwenyekiti taifa anabidi kugeuka omba omba kama kule karibu na kwao eneo la suka mahela ambapo unakuta kijiji kile watu wamejipanga barabara kuu waki duka mahela yaani wakiomba hela kwa kila gari inayopita

Lisu naye kageuka kuwa mkazi wa kijiji cha Suka Mahela

Au ana nyumba pale kijiji kile cha suka mahela? Au ni mzaliwa wa kile kijiji?
Wasafiri njia kuu ya Dodoma hadi singida hicho kijiji cha Suka mahela lazima mtakuwa mnakijua

Nembo yake ni kukuta omba omba wengi barabarani wakiomba pesa

Na kibao kipo kinachoonyesha kuwa hapa sasa unaingia Suka Mahela
 
Back
Top Bottom