CHADEMA yajiondoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Waziri Jafo awashangaa kususia uchaguzi

CHADEMA yajiondoa kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Waziri Jafo awashangaa kususia uchaguzi

Kuna uzi niliuna jana hapa jukwaani kwamba polepole angeongea na vyombo vya habari.

Kuna chochote cha maana kasema?
 
Natoa pongezi kwa CHADEMA kujitoa maana kushiriki ktk kitu kinacho nasibishwa na uchaguzi ni kuwadanganya wananchi na jumuiya ya kimataifa kuwa kuna kitu kinachoitwa uchaguzi huru na wa haki nchini Tanzania chini ya utawala huu wa awamu ya tano.

Kujitoa kwa chama hiki makini cha upinzani kitapelekea Tanzania kuzidi kumulikwa kwa kurunzi ya watetezi wa demojrasia nchini na kimataifa inayopima kama kweli demokrasia ya vyama vingi ipo au la Tanzania.

Hatua hii ni Mbinyo mmojawapo kwa utawala huu kutambua kuwa haiwezi kuwaburuza wananchi kwenda ktk sanduku la kura kisa kuwapatia nguvu batili utawala wa awamu ya tano kujitangaza imewekwa mamlakani kidemokrasia wakati siyo kweli.

Turejee Kesi ya makada wa CCM kusimamia chaguzi
10 May 2019
Mahakama Kuu nchini Tanzania kanda ya Dar es Salaam imesema sheria ya uchaguzi inayowapa uhalali wakurugenzi kuwa wasimamizi wa uchaguzi ni batili, na hivyo imetamka kuvifuta vipengele viwili katika sheria hiyo.

Source: DW Kiswahili
 
Ambacho wamesahau ni kuwa vyama vingine hasa ACT vinaona hii ni fursa kwao kujiimalisha na kuja kuwa chama kikuu cha upinzani

Vita ya mbowe na zito hapa zito ndio atakuwa mshindi japo ni snitch
Hiyo Ndio demokrasia

Kama hujajipanga unajiandaa kwa wakati mwingine

TLP itatoa ushindani sasa
 
Kumbe ndio maana hata kujiandikisha hawakutoa hamasa...
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ametangaza chama chake kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019 kwa madai wakishiriki wanahalalisha ubatili

Maamuzi hayo yanakuja ikiwa ni baada ya Wabunge wa CHADEMA kukutana leo alasiri Novemba 7, 2019 katika Kikao cha Kamati Kuu ya dharura ya chama kilichofanyika mkoani Dodoma

Jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema alisema Kamati hiyo itakutana leo kutoa msimamo wao wa mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Pia soma
Tulishajua kuwa hawana uwezo wakushinda Si waliwahamasisha pia wanachama wao kupitia mitandao ya kijamii wasijiandikishe? Sasa walianza je kushiriki?
 
Naona hapa kinachoenda kutokea ni mabaki ya CCM kwenda kwenye vyama vingine na kugombea huko.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ametangaza chama chake kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 24, 2019 kwa madai wakishiriki wanahalalisha ubatili

Maamuzi hayo yanakuja ikiwa ni baada ya Wabunge wa CHADEMA kukutana leo alasiri Novemba 7, 2019 katika Kikao cha Kamati Kuu ya dharura ya chama kilichofanyika mkoani Dodoma

Jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema alisema Kamati hiyo itakutana leo kutoa msimamo wao wa mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Pia soma
Na huu ndio mwisho wa CHADEMA Tz
 
Sasa vyama vingine ACT, NCCR nk vitangaze kujitoa ili hata upinzani CCM B kama CUF, TLP na UDP vikiungana na mume wao CCM hata wakiendelea shauri yao.
Chadema imefanya vizuri kusubiri hadi hatua hii ili ushahidi wa uzandiki wao uwe wazi
Nyama vingine sio mali ya mtu binafsi!
 
Back
Top Bottom