Uchaguzi 2020 Chato: Yaliyojiri Mapokezi ya mgombea Urais wa JMT kupitia CHADEMA, Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Chato: Yaliyojiri Mapokezi ya mgombea Urais wa JMT kupitia CHADEMA, Tundu Lissu

Nimezungumzia ukaguzi...sijui umejibu nini .
Halafu inashangaza kumbe alikuwa anaponda kitu ambacho hata hajakiona kwa macho..mambo ya kishamba sana kuwahi kutokea.
Chato inajengwa iwe kama Ulaya Wasukuma wangapi wa hapo wamefika Ulaya wakapenda na kutamani kuiga? Kuona kwa macho ndo Habari ya mjini!
 
Mgombea wa Urais anayetarajiwa kupata ushindi mkubwa Tundu Lissu leo ataitetemesha Chato na viunga vyake katika kampeni zake zilizoivuta Dunia.

Taarifa kutoka ndani ya Team yake ya Kampeni kabla ya kuhutubia mkutano wa Hadhara atautembelea Uwanja wa ndege wa Chato uliozua gumzo nchini kote kutokana na Ujenzi wake.

Tundu Lissu amepata uungwaji mkono mkubwa kutoka Makundi yote ya Jamii hususan Wafanyakazi ambao wanalaani kupitishwa kwa sheria Haramu ya kupora Mafao yao. CCM na serikali yake walipitisha sheria ya kuzuia Mafao ya Wafanyakazi hata Kama ameacha kazi akiwa na miaka 30 haruhusiwi kupewa haki yake ya mafao mpaka afikishe miaka 60.Sheria hii Haramu imelaaniwa na kila mfanyakazi na Tundu Lissu ameapa kuifutilia mbali Mara tu baada ya kuapishwa.

Ingawa Chato ni nyumbani kwa mgombea Urais wa CCM Lakini kwa muda mrefu CHADEMA imekuwa na uungwaji mkono mkubwa na inao wafuasi wa kutosha.Mmoja wa makamanda mashuhuri wanaotokea Chato ni mwanamama Husna Amri ambaye anajulikana nchi nzima kwa ujasiri wake.

Tunatarajia kuwaletea kila kitakachojiri katika mapokezi na Mkutano wa Kampeni hapa Chato.
Naomba katika ziara hiyo aende hadi nyumbani pale kijijini kabisa kwa Mzee. Awatembelee na ndugu zake wawili watatu waone kwamba zile risasi za ndugu yao hazikufua dafu mbele ya Mungu aliye hai.
 
Mpumbavu huangalia upana wa nyayo zake, mwenyehekima hupanga mirathi ya wana wajukuu zake.

Lisu yuko juu mno ya upeo wenu unaoishia kwenye wali maharage, khanga na kofia!.
Yupo juu ya upeo wenu wanachadema...nadhani mnamuona msomi na mwenye akili kuliko wote miomgoni mwenu. October 28 itathibitisha...
 
Kuna watu sijawahi ona, uwanja wa Chato uwanja wa Chato, hivi Chato ni wananchi wa wapi? Wao hawana haki ya kuwa na uwanja? Mbona mnakuwa wapumbavu kiasi hiki?

Mnatukana kila siku Chato utafikiri wao hawatakiwi kuwa na uwanja. Kwa taarifa yenu wananchi wa Chato si wajinga, muulizeni mgombea wenu alichokipata Buselesele na Katoro hadi akasitisha kwenda Chato, haya yote ni siasa mbovu isiyo na staha, hata kama unachallenge tumia lugha rafiki, don't be so biased to that extent, watu wa Chato amewatukana sana, Buselesele na Katoro yalikuwa maeneo ya upinzani lakini kutokana na dharau za Lissu matokeo yake CHADEMA leo inazomewa, Lissu asingezomewa Buselesele kwa namna ile, Awe na akiba ya maneno kwani anaowatukana wanasikia .

Inashangaza sana unatukana halafu bado eti unaenda kuwaomba kura,,,,, unatukana barabara kujengwa huku unazitumia, unatukana ndege huku unazipanda huo ni U CHICHIDODO.

Hopeless kabisa , let's stay tuned leo.
Aliyekwambia shida kubwa ya wananchi Wa Chato ni uwanja wa ndege nani? Uwanja wa ndege anauhitaji zaidi Magufuli mwenye uwezo wa kupanda ndege bure, wakazi wa Chato wanahtaji maji safi, huduma bora za afya, usafiri wenye gharama rafiki nk. Sasa hii Gbadolite International Airport inawasaidia nini watu wasio na uwezo hata wa Milo 3 ya uhakika kwa siku?
Umewahi kusikia Lissu akichallenge ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Chato?
Yaani mwanao hana viatu vya kuvaa kwenda shule, ghafla unamnunulia baiskeli ya kuchezea?
 
Chato nzima Imesimama wana Chato wameamua kuthibitisha kuwa Nabii hakubaliki kwenye nchi yake.

Watu wamekesha Barabarani kumsubiri Liasu wafanyakazi wameahidi kutoenda kazini, wafanyabiashara hawafungui Maduka ,Hakika saa ya ukombozi ni sasa.
majungu
 
Chato inajengwa iwe kama Ulaya Wasukuma wangapi wa hapo wamefika Ulaya wakapenda na kutamani kuiga? Kuona kwa macho ndo Habari ya mjini!
Haya aende akajionee..
Nikukumbushe tu kuwa uwanja wa ndege wa chato si kwaajili ya wanachato pekee. Labda ulitaka watalii wafikej vipi mbuga ya Burigi? Ndege sio kwa kila mtu..tunaopanda mabasi ya kuungaunga tutaendelea kuwepo. Wenye uwezo wa kupanda ndege watapanda.
Geita ni mkoa mkubwa kibiashara lazima maendeleo yapelekwe
 
Hii hesabu feki. Tanzania ni kubwa sana, hakukuwa na sababu ya Lissu kurudi kanda ya ziwa mara ya tatu. Anapoteza muda wake na resources, wasukuma hawezi kuacha kumpa kura mtu wao.
Mmeanza ukabila eti? Kwa hiyo na sisi huku Singida tuchague mwana Singida mwenzetu?
 
Na kule manyara pia
Yuko busy na kanda ya ziwa! Watamshangaza tarehe 28 Oct!! Hahaaaa!! Hawajui wazee wa kanda ya ziwa! Akamuulize Mzee Lowasa! Hii ni mara ya tatu anarudi kanda ya ziwa! Muulizeni amesahau nini? Hajiamini?? Hahaahaaa!!
Queen Esther
 
Yuko busy na kanda ya ziwa! Watamshangaza tarehe 28 Oct!! Hahaaaa!! Hawajui wazee wa kanda ya ziwa! Akamuulize Mzee Lowasa! Hii ni mara ya tatu anarudi kanda ya ziwa! Muulizeni amesahau nini? Hajiamini?? Hahaahaaa!!
Queen Esther
Hiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
JamiiForums409068559_680x455.jpg
 
Back
Top Bottom