Dini zimechangia kudumaza ufahamu wa mwafrika

yani umekiri kabisa kua ni vitabu viwili tu ambavyo umeviona machoni. halafu hapo hapo tena unarukia hitimisho kua hakijawahi tokea kitabu cha mfanano wa model ya uandishi kama huo

tukueleweje?
usikaze fuvu
 
mkuu nilidhani utaweka hoja badala yake umeweka hisia mbele kuliko upeo wako wa kufikili.
 
Ujumbe sio lazima uandikwe.
Kusoma na kuyaelewa maneno basi ndo ujumbe umeshafika.
hayo maneno ya kusomwa yataonekana vipi bila kuandikwa?

au unatumia telepathic communication?
 
hayo maneno ya kusomwa yataonekana vipi bila kuandikwa?

au unatumia telepathic communication?
Huwa muda wa mipasho nimenyimwa.

Kwa heri ndugu.

A lot of things to do.
 
watu wenyewe walioleta hz dini waliwatesa na kuwapiga mijeredi mababu zetu ili kuwalazmisha wazikubali hzo dini. sasa unajiuliza hv kama kweli znahubiri upendo wa kweli je kwa nn wawapige mijered wenzety? yaan mambo ya dini yana story nyng sana ambazo huwa sizielewi!
 
Wewe ni nani jf wa kuniambia mimi nirekebishe mada yangu?

Una mamlaka yoyote kuniambia hivyo?
Unadhani kwanini mods wameipitisha?
Anamamlaka ya kukuambia urekebishe kama upeo wako wa uelewa ni mdogo kuliko yeye.
 
Duuu! Kweli kwa mawazo haya shida za duniani Zitatuwasha na mbinguni hatutafika. Hivi mnavyo sema dini imemdumaza mwafrika. Je mmesha jiuliza mchango wa dini hizikatika jamii ?. Je dini ya asili ya mwafrika Inamchango gani kwenye jamii. Binafsi siungi mkono hata kidogo kwa sababu dini za nje zinamchango mkw bwa mf.zimeleta elimu, na inavunja ukabila hata utaifa, inashirikiana na serikali kupunguza uharibifu. Leo hii nikikutana na mukristo au muislam mwenye Iman kiasi najua kiwango flani naweza kuwa salaam kwakuwa ana mafundisho sahihi yenye kumpendaza mungu. Sasa hii African culture ni dhaana ambayo kiukweli tulichochola zaana mpaka leo umeonyesha mapungufu makubwa mauwaji ya albino, ndugu kukosana, kwanza ni dini sizo taka maarifa utaskia flani kamloga mtoto wa flani. Kutokuwa na umoja utaskia wayakyusa wa Mila zao, wahehe zao, wachaga zao Sasa hapa kweli kunamaendeleo kweli. Isikitisha Sana kuona hata hao wapiga lamli wanamtambua mungu ndio maana ni waoga Sana hata katika swala kifo kwa kuwa wanakujua waendako




Hitimisho mtoa maada ni Bora kuwa wajinga wakosefu wa maarifa kuliko kuwa na wenye maarifa na wasio na iman sahihi Kama wewe maana kwa huu uzi wako ni Bora tu ungekuwa ni mjinga usiyejua lolote hata kuposti huumu jamii forum. Ila siku laumu sana sana humu duniani ni uwanja wa kampeni mgombea ni mungu na shetani. kwahiyo hata hi post yako inawakilisha mgombea wako
 
Mawazo ya mkoloni bado yanaishi kichwani kwako. Jielimishe kuhusu dini za waafrika. Utapata mengi mazuri positive kuliko negativity uliofundishwa na dini za wakoloni. Wakoloni wangekua wana nia nzuri na dini. Wasingeweka rangi kwenye dini. Maana kuanzia malaika.....etc wote ni wazungu. Amka my african brother. Waafrika tulikua tunamjua mungu wa kweli na kuabudu hata kabla ya wazungu. Usidharau kila kitu cha muafrika. Unadharau kwa sababu historia nzuri ya muafrika umefichiwa toka utotoni.
 
Bilashaka wewe utakuwa ni wakala wa Shetani..

Kwaiyo katika kufikilia kwako kote, ndiyo ukaona dini ndiyo tatizo kubwa katika maendeleo ya afrika.

Nchi nyingi duniani zimepokea dini hizo kama zilivyopokelewa afrika lakini zina maendeleo makubwa sana. Mfano, Brazil, Turkey, n.k

Tatizo haliwezi kuwa dini, kuna mambo makubwa muhimu mawili ya kuangalia hapa kama;
- Mfumo wa elimu ( Quality people )
- Mfumo wa Utawala ( Quality leadership )

Uwezi kuwa na taifa bora kama hauna watu bora na viongozi bora !!
 
Wanakosea kuamini katika Dini badala yake wanapaswa kuamini katika Mungu
 
Hawa wazungu sijui walifanikiwaje kwenye hili mbona kule China & India walitawaliwa na wazungu lakini bado walibaki na dini zao
Ishu sio kubaki na cha kwako au kuiga cha mwingine.Ishu ni hicho kitu kina manufaa gani yanayojipambanua wazi wazi!
 
1. Ni vizuri tukajenga hoja kwa ushahidi (with cogent justification). Kwa vile umesema hapa Afrika kuna dini kubwa mbili - Uislamu na Ukristo - na kwa vile mimi ni Mkatoliki (Mkiristo), nimeamua nitoea mifano ya baadhi ya waumini wa Kikristo (bofya hapa List of Christians in science and technology - Wikipedia) waliaomini uwepo wa Mungu kupitia imani yao ya kuwa Wakristo, waliweza kugundua mambo mbalimbali ambayo sayansi na teknolojia tunazotumia zimetokana nayo au baadhi ya hayo mambo.
2. Kwa msingi huu siwezi kuamini kwamba kama hawa watu waliweza kuamini na kugundua mambo waliyogundua, kwa nini sisi katika kuamini katika hiyo dini yao kutufanye kudumaze ufahamu wetu kama kichwa chako cha habari kinavyoeleza?
3. Kutokana na hili, siwezi kuamini kwamba kuamini katika dini ndiko kunakodumaza ufahamu wa Mwafrika na hujatoa ushahidi wowote wa kimaandishi jinsi dini inavyodumaza ufahamu wa Mwafrika isipokuwa umetumia hoja 'zoazoa' (blanket/wholesale conclusion) bila kuangalia mtiririko wa 'premises' zako.
 
Tukaambiwa Mungu amejigawa sehemu tatu, tukaitikia "ndio mzungu " Mungu ameandaa moto wa kuchoma watu wake! Ndio mzungu! Hakuna aliyehoji .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…