Binafsi nakereheka mno na hii mbinu waliyojiwekea ya kuijadili ripoti ndani ya kamati ya pac ambayo nayo haitakuwa na tija Bali muendelezo wa business as usual!
Nashauri wabunge wanaojitambua na wenye angalau kachembe ka uzalendo kalikobakia wapeleke hoja mahsusi bungeni ya kuomba bunge liishinikize serikali ipeleke mswada wa Sheria bungeni wa kumpa mamlaka ya kisheria ya kushitaki na kuendesha kesi kwa wake wanaokutwa na makosa ya matumizi mabaya ya fedha za umma.
Tunayo mahakama ya uhujumu uchumi hivyo sioni sababu ya takukuru kupewa uwezo wa kushitaki na kumnyima cag uwezo huo. Wote wapewe uwezo sawa wa kushitaki na kuendesha kesi za uhujumu uchumi na ufisadi. Najua walafi watatumia nguvu kubwa lakini serikali izibe masikio na kufunga macho kumwezesha cag kushitaki moja kwa moja ili nchi ipone.
 

Mnufaika numero wanu! Unadhani zile bajaji na vijimtungi vya gas alivyogawa jimboni kwake alivipata kwa mshahara wake? Think thrice wewe Jamaal
 
Ameshaona hamna mwenye akili hata nukta mule ndani.
Auuu sijui lakini ila wanawake bado sana kuongoza.
Mama kala dodo tunamuomba angalau aturudishie kokwa.
 
Mkuu, amini usiamini, kutokana na hali halisi ya mapato yatokanayo na makusanyo ya TRA kwa kweli fedha ni nyingi sana kwa maendeleo ya Nchi. Aidha na ukizingatia huu ufujaji, wizi na matumizi mabaya na ya anasa ndani ya Nchi, basi bila shaka yeyote Chama chochote cha upinzani kikipata baraka ya kuunda Serikali na ikaisimamia ipasavyo na kuweka wazi vipaumbele vyake na kufuata taratibu na sheria kwa mujibu wa Sheria za Nchi hakika kitafanya maajabu na hapo ndipo watu watajitambua na kujijutia.
 
Ukitazama kwa jicho la mwewe utagundua jinsi gani rais samia yuko na maadui lukuki bungeni kuliko hata mitaani. Yani mwigulu anafanya ubadhirifu makusudi kisha anamsakizia Raisi kwamba anajua huo ujinga wake. Leo Rais Samia anawataka wezi washughulikiwe mapema ili isimuondolee sura ya amiri jeshi anatokea mtu amekonda makwapa kama kona za kinanda na mataya kama kufuli za magodown ya dangote anamrudisha nyuma na kumchafua mama kwa wananchi wake alioapa kuwatumikia kwa kuzuia mjadala. Hii sio sawa
 
Ameshaona hamna mwenye akili hata nukta mule ndani.
Auuu sijui lakini ila wanawake bado sana kuongoza.
Mama kala dodo tunamuomba angalau aturudishie kokwa.
Mimi Nina imani kubwa sana na spika, kama kweli amekataza kuna sababu ya umuhimu
 
Haya mambo si yanafanywa kwa ratiba kisheria? Sasa ilipelekwa bungeni kufanya nini?
 
Ile hoja ya Luhaga Mpina ya kuwataja viongozi ambao walitakiwa wawe jela, iliwavuruga sana,

Wameacha upepo upite kwanza, halafu ikifika mwezi wa tisa watu watakuwa wameshasahau,

Hili ndio limepita hivyo, tusubiri ripoti nyingine mwakani,

Sent from my Infinix X658E using JamiiForums mobile app
 
spika anataka waibe pesa zingine ili ripoti ijayo pia isijadiliwe wezi walioko serikalini walindwe na wabunge, si ndio kazi waliyopewa kuifanya. Wanatutia hasira sana, alafu wakija Makanisani na Misikitini kusali huwa wanaweka mikono nyuma tuwaone ni wastaarabu kumbe ndio majizi makubwa ya mali za nchi...hovyo sana haya madude
 
Mkuu koryo1952 , kiukweli uelewa wa baadhi yetu ni mgogoro, Spika hajapiga marufuku taarifa ya CAG kujadiliwa Bungeni bali amesema mjadala rasmi kuijadili ni kikao cha November, ila mbunge yuko huru kutoa maoni yake yoyote kuhusu ripoti ya CAG ila asiiulize serikali kutoa majibu yoyote.

Amesema wameisogeza ili kutoa nafasi kwa wahusika kupewa haki ya kusikikizwa na kamati husika kisha ndipo Bunge litajadili na kutoa Azimio la Bunge kupelekwa serikalini kwa utekelezaji.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…