Freeman Mbowe: Rais leta maridhiano ya Kitaifa, sisi CHADEMA tuko tayari

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amemtaka Rais Magufuli kuleta maridhiano ya kitaifa na kwamba yeye na chama chake wamenyoosha mkono wa mapatano.

Ifuatayo ni Hotuba Fupi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini Tanzania Freeman Aikael Mbowe mbele ya Watanzania katika kuadhimisha miaka 58 ya Uhuru:

Mheshimiwa Rais,
Waheshimiwa viongozi wote mlioko mahali hapa,
Waheshimiwa watanzania wenzangu!

Nimekuja kushiriki sherehe za miaka 58 ya Uhuru kama uthibitisho wa ulazima wa kuwepo maridhiano, kuwepo upendo, na kuwepo mshikamano katika Taifa letu.

Nawapongeza sana Watanzania kwa siku hii ya leo na ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu demokrasia. Tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano.

Na Mheshimiwa Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia. Basi Mheshimiwa Rais tumia nafasi hiyo ukaliweke Taifa katika hali ya utengamano.

Nakushukuri sana. Asante sana.
_____________
Hotuba fupi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na KUB, Mh *Freeman Mbowe* katika sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, zilizofanyika Jijini Mwanza leo 9 Disemba 2019
 
Iddi Amin alipokubaliana na watekaji wandege ya air France 1976, ilitumika njia ya majadiliano ya kumlghai ili ajione anaweza kumbe makanda wa IDF walikuwa kwenye rehearsal kwaajili ya kufanya uokozi.

Asomaye na afahamu.
 
Kikwete aliwaita sana lakini hwapi ,wapinzani wa bongo ni pasua kichwa

Wapinzania watafungwa kwa ishu ya akwilina mambo ya kuomba maridhiano sio time yake


USSR
 
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amemtaka Rais Magufuli kuleta maridhiano ya kitaifa na kwamba yeye na chama chake wamenyoosha mkono wa mapatano
Lini chadema walimtambua Magufuli Kama Raisi? Kuapishwa walisusa kuwa hawamtambui,bungeni alipoenda Kama Raisi walitoka kumkataa.

Watoe kwanza tamko la kumtambua Magufuli Kama Raisi.

Wanataka maridhiano na Magufuli Kama Nani kwao ?
 
Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kuwa Mbowe ameenda Mwanza kibwege bwege. Na sio yeye tu, yaani Heche, Mnyika, Sugu, Lema, Boniface waende Mwanza bila kuwa na jambo la maana? Sidhani
Dawa imewaingia na imekaa kunako

Mapinduzi ya kimaendeleo yaliyofanyika ndani ya miaka minne hii utakuwa mjinga kama ukaendelea kupinga

VIVA Magufuli
 
Maridhiano ni lazima na muhimu. Chama changu cha CCM, kikigomea usuluhisho, tutapata pigo kubwa kisiasa na tutakosa sifa.

Inajulikana kuwa CDM wanahitaji kujikosha na makosa yao ya kisiasa, wanahitaji wakati wa kupumua na kujitafakari.

Wapewe hiyo nafasi ni haki yao, upinzani madhubuti na wenye muelekeo ni tija kwa chama tawala.
 
Maridhiano ni lazima na muhimu. Chama changu cha CCM, kikigomea usuluhisho, tutapata pigo kubwa kisiasa na tutakosa sifa.

Inajulikana kuwa CDM wanahitaji kujikosha na makosa yao ya kisiasa, wanahitaji wakati wa kupumua na kujitafakari.

Wapewe hiyo nafasi ni haki yao, upinzani madhubuti na wenye muelekeo ni tija kwa chama tawala.
Una mawazo mazuri lakini hao watu unawajua kweli Vichwa vyao
 
Unaenda kumpigia magoti mtu aliyemtandika risasi 38 nduguyo utadhani anaua CHATU na kama haitoshi akaendelea kumshughulikia vivyo hivyo huku akiwa hoi kitandani.

CHADEMA hakuna kitu
Acha ujinga wa kuropoka Uzushi wewe
 
Back
Top Bottom