Freeman Mbowe: Rais leta maridhiano ya Kitaifa, sisi CHADEMA tuko tayari
Unataka jambo gani la maana kuliko ujumbe walioutoa?
Rushwa labda?
Wamenunuliwa?
Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kuwa Mbowe ameenda Mwanza kibwege bwege. Na sio yeye tu, yaani Heche, Mnyika, Sugu, Lema, Boniface waende Mwanza bila kuwa na jambo la maana? Sidhani
 
Kwa mkakati huu Kamati kuu Chadema imeona mbali sana. Hii ni dalili kesi ya Kisutu imewakalia vibaya, wameenda kutafuta nafasi ya kufikiriwa😅😅😅
 
Wachawi hawataisha nchi hii, ukiwafunga sio kuua upinzabi, upinzani unaanzia ccm watu wamefunga midomo tu ili siku ziende.
Uwe unaomba mkeo apitie post kabla hujaipost
Kikwete aliwaita sana lakini hwapi ,wapinzani wa bongo ni pasua kichwa

Wapinzania watafungwa kwa ishu ya akwilina mambo ya kuomba maridhiano sio time yake


USSR
 
Hivi kweli baada ya miaka 4 ya Magufuli bado Mbowe anamatumaini ya kuwa na maridhiano ya kitaifa?.

Baada ya yote yaliyotokea kwenye uchaguzi 2015 na serikali za mitaa 2019 Mbowe unaomba maridhiano!!! Hivi haya maridhiano ya kitaifa yatafanya uchaguzi wa serikali za mitaa kurudiwa?

Nasubiri kauli ya Mh. TLS baada ya kamati kuu ya Chadema kuhudhuria sherehe za maridhiano na alichokiomba Mbowe kwa Rais!

Wabunge wa chadema na wanachama wao wasubiri matusi, kejeli na vijembe kutoka kwa wabunge wa CCM kuwa walipandishwa ndege na kula ubwabwa siku ya Uhuru.

Hii nchi ilipofika inahitaji kulazimishwa sio kufanya maridhio!!
 
Hata wapumbavu na wajinga huzeeka, hii ni kauli ya Madebe lakini leo nimeiamini
Lini chadema walimtambua Magufuli Kama Raisi? Kuapishwa walisusa kuwa hawamtambui,bungeni alipoenda Kama Raisi walitoka kumkataa.

Watoe kwanaza tamko la kumtambua Magufuli Kama Raisi.

Wanataka maridhiano na Magufuli Kama Nani kwao ?
 
Kuna watu wanahoji, kwanini Kamati Kuu Chadema imeamua kuhudhuria sherehe za Uhuru leo baada ya kususia kwa miaka kadhaa.

Kuna fununu zinasikika zikifanywa na viongozi wa dini na wazee wastaafu kuhakikisha maridhiano yanapatikana baina ya serikali na vyama vya upinzani hasa Chadema, kama ni kweli basi hatuna budi kuipongeza serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli na kamati kuu ya Chadema kwa uamuzi wake huo. Najua Chadema italaumiwa na wengi hasa wahafidhina wasiopenda mabadiliko, lkn kama imeamua kwa misingi ya kujenga umoja wa kitaifa basi tuipe ushirikiano kwa manufaa ya nchi.

Inawezekana ni udhaifu fulani Chadema imeonyesha, lkn kwa jicho jingine inawezekana pia ni ukomavu wa kisiasa na ni mwanzo mzuri kwa umoja wa kitaifa. Kwanini tuumizane kwa kugombea fito.

Nchi jirani ya Kenya kwa kipindi kirefu kumekuwa na mvutano baina ya Serikali ikiongozwa na Mhe. Uhuru Kenyata dhidi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani Raila Odinga. Lakini baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 tumeona juhudi kubwa za wazi za upatanishi zikiongozwa na rais Uhuru mwenyewe, kwa kiasi fulani zimeanza kuzaa matunda na nchi inasonga, ila kwa kufanya hivyo Uhuru amempoteza marafiki wake wengi akiwepo rafiki wake wa karibu Ruto.

Wasiopenda Maridhiano watabeza, wasiotaka amani hawatapenda tukio hili lifanikiwe.

Maendeleo hayana chama.
 
Lini chadema walimtambua Magufuli Kama Raisi? Kuapishwa walisusa kuwa hawamtambui,bungeni alipoenda Kama Raisi walitoka kumkataa.

Watoe kwanaza tamko la kumtambua Magufuli Kama Raisi.

Wanataka maridhiano na Magufuli Kama Nani kwao ?
Kunywa maji upumzike haya mambo ya kikubwa huyawezi
 
Back
Top Bottom