Freeman Mbowe: Rais leta maridhiano ya Kitaifa, sisi CHADEMA tuko tayari
Huwez kutofautisha kati kumbukizi ya kitaifa na matukio mengine. Mapambano ni process na yanabadilika kulingana na muda. Usiwe static otherwise tueleze mafanikio ya kususiana na kununiana kusikitika tu
 
Unaenda kumpigia magoti mtu aliyemtandika risasi 38 nduguyo utadhani anaua CHATU na kama haitoshi akaendelea kumshughulikia vivyo hivyo huku akiwa hoi kitandani.

CHADEMA hakuna kitu

Toa ushahidi wacha porojo, juzi kuna mtu kaandika mboe muuaji watu mkamwambia alete ushahidi sasa wewe unao ushahidi au ni porojo zako?
 
Nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kuwa Mbowe ameenda Mwanza kibwege bwege. Na sio yeye tu, yaani Heche, Mnyika, Sugu, Lema, Boniface waende Mwanza bila kuwa na jambo la maana? Sidhani
Fununu zilizopo ni kuwa mishale ya saa kumi jioni watakuwa na kikao Cha maridhiano kitakachoshirikisha cdm's crew, baadhi ya maaskofu, mawaziri wakuu wastaafu na aliyepo, Marais wastaafu na mkulu mwenyewe hapo ikulu ndogo jijini mwanza. Sio kikao Cha kitoto!
 
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amemtaka Rais Magufuli kuleta maridhiano ya kitaifa na kwamba yeye na chama chake wamenyoosha mkono wa mapatano

Ifuatayo ni Hotuba Fupi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini Tanzania Freeman Aikael Mbowe mbele ya Watanzania katika kuadhimisha miaka 58 ya Uhuru:

Mheshimiwa Rais,
Waheshimiwa viongozi wote mlioko mahali hapa,
Waheshimiwa watanzania wenzangu!

Nimekuja kushiriki sherehe za miaka 58 ya Uhuru kama uthibitisho wa ulazima wa kuwepo maridhiano, kuwepo upendo, na kuwepo mshikamano katika Taifa letu.

Nawapongeza sana watanzania kwa siku hii ya leo na ninamuomba Mwenyezi Mungu siku ya leo ikafungue milango tuweze kuishi kama Taifa linalopendana, tuvumiliane, tukosoane, turuhusu demokrasia. Tukajenge Taifa lenye upendo na mshikamano.

Na Mheshimiwa Rais una nafasi ya kipekee kuweka historia ya maridhiano katika Taifa kwani kuna wengine wanalalamika, wengine wanaumia. Basi Mheshimiwa Rais tumia nafasi hiyo ukaliweke Taifa katika hali ya utengamano.

Nakushukuri sana. Asante sana.
_____________
Hotuba fupi ya Mwenyekiti wa CHADEMA na KUB, Mh *Freeman Mbowe* katika sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru wa Tanganyika, zilizofanyika Jijini Mwanza leo 9 Disemba 2019
Kwanini Mbowe analazimisha ionekane kuna ugomvi
 
Mh Mbowe kaonyesha ukomavu mkubwa ktk Siasa. Siasa sio uadui, sio majigambo wala kiburi mbele ya Kiongozi wa Nchi na Wazalendo wa kweli kwa nchi yao bali ni kutumia angalau sekunde chache kuhakikisha kuwa ujumbe umefika panapostahili. Sasa basi ni jukumu la Kiongozi Mkuu wa Nchi kuyapokea na kiyafanyia kazi au kuyapuuzia. Nchi ni ya Watz wote ni si mali ya viongozi kama unavyowaza wewe. HONGERA SANA MH MBOWE kwa kuwa Kiongozi wa Mfano ktk Siasa za Kidemokrasia.
 
Viongozi wengi wa chadema wameshaambiwa na wanasheria wao kuwa kifungo kipo njiani ndio maana wanajipendekeza ili wapate huruma


USSR
 
Ebu tueleze wew ungekua Mbowe utafanyeje. Je aunde kikundi cha uasi mşituni. Mambo sio marais km unavyofikiria.
Uasi misituni Tz tulizika rasmi siku kama ya leo 1961 hivyo hatuwezi kuongelea tena uasi wa msituni. Hata hivyo tuliambiwa uvumilivu unakikomo baada ya uchaguzi tutaambiwa mwelekeo na hatua za kuchukua. Kwahiyo hayo maridhiano yanayoombwa sehemu isiyoombea ndiyo mwisho wa uvumilivu??
Hata hivyo nimependa comment ya Mambo sio rahisi kama ninavyofikiri!!
 
Kuna watu wanahoji, kwanini Kamati Kuu Chadema imeamua kuhudhuria sherehe za Uhuru leo baada ya kususia kwa miaka kadhaa.

Kuna fununu zinasikika zikifanywa na viongozi wa dini na wazee wastaafu kuhakikisha maridhiano yanapatikana baina ya serikali na vyama vya upinzani hasa Chadema, kama ni kweli basi hatuna budi kuipongeza serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli na kamati kuu ya Chadema kwa uamuzi wake huo. Najua Chadema italaumiwa na wengi hasa wahafidhina wasiopenda mabadiliko, lkn kama imeamua kwa misingi ya kujenga umoja wa kitaifa basi tuipe ushirikiano kwa manufaa ya nchi.

Inawezekana ni udhaifu fulani Chadema imeonyesha, lkn kwa jicho jingine inawezekana pia ni ukomavu wa kisiasa na ni mwanzo mzuri kwa umoja wa kitaifa. Kwanini tuumizane kwa kugombea fito.

Nchi jirani ya Kenya kwa kipindi kirefu kumekuwa na mvutano baina ya Serikali ikiongozwa na Mhe. Uhuru Kenyata dhidi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani Raila Odinga. Lakini baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 tumeona juhudi kubwa za wazi za upatanishi zikiongozwa na rais Uhuru mwenyewe, kwa kiasi fulani zimeanza kuzaa matunda na nchi inasonga, ila kwa kufanya hivyo Uhuru amempoteza marafiki wake wengi akiwepo rafiki wake wa karibu Ruto.

Wasiopenda Maridhiano watabeza, wasiotaka amani hawatapenda tukio hili lifanikiwe.

Maendeleo hayana chama.

Hamna maridhiano wala nini ni udhaifu tu, nampongeza Zito na chama chake kutokuhudhuria hiyo hafla na hao wahuni wanaobaka demokrasia yetu. Kwahili cdm wamechemsha.
 
Viongozi wengi wa chadema wameshaambiwa na wanasheria wao kuwa kifungo kipo njiani ndio maana wanajipendekeza ili wapate huruma


USSR
Ok. kama ndivyo hivyo kuna ubaya gani.
 
Hata hujielewi,soma barua ya msajili wa vyama vya siasa ikialika viongozi wa vyama utambue kuwa viongozi hao wamejigharamia gharama zote ikiwemo nauli.
Unadhihirisha ulivyo mjinga na unatumika kama ndomu tu
 
Unadhani Lissu hajui kuwa wenzie wako Mwanza? Aliyekudanganya hivyo Nani? Karata ya Leo ya CDM imehit vibaya, matusi na kejeli za baba Jesca mbele ya watu makini hakuna. Sijasikia Kitwanga kakaa na mwanamke white au Mongela kaiba mke wa mtu. Nilichosikia "Wenyeviti wa Vyama njooni hapa, MBOWE njoo basi". Taifa linahtaji mawazo ya watu wote wakiwemo punguani pia, hivyo hata haya mawazo ya kima cha chini tumekusikia.
 
Kuna watu wanahoji, kwanini Kamati Kuu Chadema imeamua kuhudhuria sherehe za Uhuru leo baada ya kususia kwa miaka kadhaa.

Kuna fununu zinasikika zikifanywa na viongozi wa dini na wazee wastaafu kuhakikisha maridhiano yanapatikana baina ya serikali na vyama vya upinzani hasa Chadema, kama ni kweli basi hatuna budi kuipongeza serikali inayoongozwa na Rais John Magufuli na kamati kuu ya Chadema kwa uamuzi wake huo. Najua Chadema italaumiwa na wengi hasa wahafidhina wasiopenda mabadiliko, lkn kama imeamua kwa misingi ya kujenga umoja wa kitaifa basi tuipe ushirikiano kwa manufaa ya nchi.

Inawezekana ni udhaifu fulani Chadema imeonyesha, lkn kwa jicho jingine inawezekana pia ni ukomavu wa kisiasa na ni mwanzo mzuri kwa umoja wa kitaifa. Kwanini tuumizane kwa kugombea fito.

Nchi jirani ya Kenya kwa kipindi kirefu kumekuwa na mvutano baina ya Serikali ikiongozwa na Mhe. Uhuru Kenyata dhidi ya Kiongozi Mkuu wa Upinzani Raila Odinga. Lakini baada ya uchaguzi mkuu wa 2017 tumeona juhudi kubwa za wazi za upatanishi zikiongozwa na rais Uhuru mwenyewe, kwa kiasi fulani zimeanza kuzaa matunda na nchi inasonga, ila kwa kufanya hivyo Uhuru amempoteza marafiki wake wengi akiwepo rafiki wake wa karibu Ruto.

Wasiopenda Maridhiano watabeza, wasiotaka amani hawatapenda tukio hili lifanikiwe.

Maendeleo hayana chama.
CHADEMA ni nini? Kwani nayo ni serikali ndani ya serikali? Hicho chama cha watu kadhaa ndo kinajipa hadhi ya kutaka maridhiano na serikali?
The logic is simple, when the enemy is too elephant, simply join and show your weaknesses.
 
Hamna maridhiano wala nini ni udhaifu tu, nampongeza Zito na chama chake kutokuhudhuria hiyo hafla na hao wahuni wanaobaka demokrasia yetu. Kwahili cdm wamechemsha.
Siku ya kuapishwa rais Magufuli Chadema walisusa Zitto alihudhuria na akampongeza, leo Zitto kasusa Chadema wamehudhuria, ndiyo siasa zilivyo.
 
Hivi kweli baada ya miaka 4 ya Magufuli bado Mbowe anamatumaini ya kuwa na maridhiano ya kitaifa?.

Baada ya yote yaliyotokea kwenye uchaguzi 2015 na serikali za mitaa 2019 Mbowe unaomba maridhiano!!! Hivi haya maridhiano ya kitaifa yatafanya uchaguzi wa serikali za mitaa kurudiwa?

Nasubiri kauli ya Mh. TLS baada ya kamati kuu ya Chadema kuhudhuria sherehe za maridhiano na alichokiomba Mbowe kwa rais!

Wabunge wa chadema na wanachama wao wasubiri matusi, kejeli na vijembe kutoka kwa wabunge wa CCM kuwa walipandishwa ndege na kula ubwabwa siku ya Uhuru.

Hii nchi ilipofika inahitaji kulazimishwa sio kufanya maridhio!!
Hii inanikumbusha walivyokaribishwa na Kikwete ikulu, wakapewa chai, baadaye wakahakikishiwa maoni yao juu ya katiba mpya yanafanyiwa kazi. Baadaye wakaonekana walikwenda kunywa chai tu!

Mbowe anajikuta anaishiwa wafuasi, siipokuwa kabila lake. Wote aliodhania ni wasaliti wa CCM, sasa wanarudi CCM. Hana jipya! Yabidi yeye mwenyewe ahamie CCM tu!
 
Hakika namsifu sana mh Mbowe kwa kuona mbele maana hayo mabadiliko siyo lazima tuyashuhudie sisi leo hii
Mbowe anaiona jela kibri kimeisha na sasa anatafuta pa kutokea

USSR
 
Uasi misituni Tz tulizika rasmi siku kama ya leo 1961 hivyo hatuwezi kuongelea tena uasi wa msituni. Hata hivyo tuliambiwa uvumilivu unakikomo baada ya uchaguzi tutaambiwa mwelekeo na hatua za kuchukua. Kwahiyo hayo maridhiano yanayoombwa sehemu isiyoombea ndiyo mwisho wa uvumilivu??
Hata hivyo nimependa comment ya Mambo sio rahisi kama ninavyofikiri!!
Ebu vaa viatu vya Mbowe. Wafuasi wa upinzan wanataka mabádiliko yaletwe na viongoz huku wao wamejifungia ndani. Mara ngapi Mbowe amehamasisha civil disobidience bara support ya wafuasi wa mabádiliko?Badala ya kulalamikiána Mbowe ungekuja na option. Mange Kimambi alipata support gán otherwise wew utakua vuvuzerá la Lumumba unafitinisha
 
Back
Top Bottom