[emoji777]Mlikataa matokeo ya Urais
[emoji777]Mlimkataa Rais na kusema hamumtambui;
[emoji777]Mlikataa kushiriki kuapishwa kwake;
[emoji777]Mlikataa kumsikiliza Bungeni na mkatoka nje (mwenzenu Zitto aka Kigogo alishafanya maridhiano maana siku hii alibaki Bungeni);
[emoji777]Mlimuita Rais anayewaletea wananchi maendeleo kuwa ni Dikteta;
[emoji777]Mkapanga Maandamano (UKUTA) kuvuruga amani ya nchi;
[emoji777]Mkazunguka Dunia nzima kumshtaki na kujaribu kuidanganya dunia, mkashangaa wazungu hao hao wanaleta misaada na wanakuja kuwekeza;
[emoji777]Mnamzushia tuhuma mbalimbali za kijinga;
[emoji777]Mkafurahia hujuma za ndege kukamatwa;
[emoji777]Mkasusia baadhi ya chaguzi ndogo;
[emoji777]Mkasusia uchaguzi wa Serikali za Mitaa;
[emoji777]Mkatangaza kutowatambua viongozi wa Serikali za Mitaa;
*Katika yote bado Mzee Baba kama hawaoni vile:*
[emoji457]Ameimarisha uchumi wa nchi kwa kuongeza mapato ya Serikali na nidhamu ya matumizi;
[emoji457]Anajenga barabara na madaraja yakiwemo maflyover;
[emoji457]Anatoa elimu bure kwa bilioni 23 kila mwezi;
[emoji457]Anajenga vituo vya afya 480 na hospitali za wilaya 90 na za Kanda 8;
[emoji457]Amenunua ndege 11 mpya "cash."
[emoji457]Anajenga reli ya kisasa SGR kwa trilioni 7 cash;
[emoji457]Anajenga mradi wa umeme Rufiji Trilioni 6.5 cash;
[emoji457]Ametoa Bilioni 153 kuunda meli mpya na kukarabati zingine 3 na cherezo kimoja;
[emoji457]Anajenga daraja la Kigongo Busisi kwa bilioni 700 cash;
[emoji457]Ametoa fedha kwa wakati za mikopo ya elimu ya juu zaidi ya bilioni 450 na hakuna tena maandamano vyuoni;
[emoji457]Anasambaza umeme vijijini kwa kasi zaidi, afikisha vijiji 9,000 na kufikia 2021 vijiji vyote 12k nchini vitakuwa na umeme.
[emoji457]Anajenga mabweni ya wanafunzi, majengo ya vyuo, madarasa n.k
[emoji457]Anajenga Daraja la Wami, kakamilisha daraja la kihistoria la Sibiti na sasa ameanza kupanua Barabara Dar kwenda Kibaha kwa njia nane;
[emoji457]Mkoa wa Kigoma uliochoka sasa unaunganishwa na Tabora na Katavi na Kagera kwa barabara za lami;
[emoji457]Anainda meli mpya Ziwa Tanganyikabna kuikarabati MV Liemba;
[emoji457]Amewalipa wakulima wa korosho bei nzuri baada ya kutaka kunyonywa na makabaila weusi na weuoe, ametumia Bilioni 700;
[emoji457]Heshima imerudi mjini na hata Krismas hii tunaheshimiana hapa mjini;
[emoji457]Nimetua Moshi juzi tu, katugusa sisi wa Machame, karejesha treni safi baada ya kukarabati reli;
[emoji457]Kahamasisha viwanda na tunaviona vinajengwa na watu wanapata ajira;
[emoji457]Madini mnajua, wale wa kujimwambafy Acacia wako chali, wamebaki wanaumeeee Barrick na sisi mezani tunagawana chetu kwa haki;
[emoji457]Mirerani shamba la Bibi la Tanzanite kaigeuza kuwa hub ambapo mapato yanepanda kutoka Milioni 70 hadi Bilioni 2.5;
[emoji457]Mapato sekta ya madini kwa ujumla yameongezeka kutoka Bilioni 191 hadi Bilioni 320 na mwaka huu wataalamu wanasema yatavuka Bilioni 400;
[emoji457]Anatoa mshahara kwa watumishi wa umma haizidi tarehe 23 ya mwezi bila kukosa.
[emoji457]Kaongeza mshahara kwa watumishi kwa njia ya annual increament kwa watumishi zaidi ya laki 3 na kapandisha madaraja watumishi zaidi ya laki 5 ikiwa ni baada ya kusimamia tangu mwaka 2013;
[emoji457]Kashusha kodi kwenye mishahara kutoka asilimia 14 mpaka 9;
[emoji457]Kaweka rekodi ya makusanyo ya mwezi kufikia trilioni 1.7, haijawahi kutokea tangu nchi hii iwepo na kabla haijakuwepo;
[emoji457]Katimiza ahadi ya miaka 40 ya nchi kuhamia Dodoma na kila aliyehamia kalipwa haki zake hakuna madeni;
[emoji457]Kajenga mji mpya wa Serikali Dodoma na anaendelea kujenga;
[emoji457]Kawabana mafisadi sawa sawa na kaanzisha mahakama maalum;
[emoji457]Kakamilisha ujenzi wa megawati 240 umeme wa gesi Kinyerezi II na anakamilisha Kinyerezi I extension megawati nyingine 185;
*Niendelee????......... inatoshaaaaa!!!*
Kama haya na mengineyo yamefanyika bila MARIDHIANO mi naona nyie endeleeni kususa tu, sisi tuendelee kutekeleza.