FT: Simba 0-3 Raja Casablanca | CAF Champions League | Estadio Benjamin Mkapa | 18.02.2023
No, kama Vipers alikufa kwake, Simba leo kafa kwake, mwenye faida hapa labda ni Horoya kama atawakazia waarabu nyumbani kwake apate hata suluhu..

Lakini ikitokea Horoya akapoteza pointi kwa Vipers, then Simba ashinde zote mbili za Vipers, bado nafasi ipo, sema hawa jamaa ndio wataongoza kundi kwa pointi nyingi sana.
Hesabu za vidole hizi, huyo Vipers kumfunga kwake Sio rahisi
 
Sasa kama nyumbani tu unakubali kufungwa 3 bila! Ukienda kwao si unaenda kupigwa 🤚

Ndiyo hii timu ilikuwa inawakejeli Vipers, ambao wametoa sare na mbabe mwingine Horoya!!

Kwa hali hii sitashangaa wakishika mkia kwenye kundi lao.
Kushika mkia kawaida ata chura kashashiriki makund confederation zote kaambulia kushika mkia tu
 
Sasa hivi mashabiki wa Simba walivyo jikusanya maongezi yao utazani mamotivation speaker wa kilimo cha matikiti "heka moja mil 5,ukilima heka 20 hukosi mil 100 " watajua hawajui siku wa kingia shambani.

Eti Vipers wanampiga nje ndani,Horoya hatoki kwa mkapa ,Morocco wanaenda kutafuta droo ........ halafu serious kabisa ngojea wakiingia uwanjani ndipo watajua kuwa hawajui.
 
I am not surprised na Matokeo.

Nilishawahi kuandika hapa kuwa tuwape nafasi makocha wa ndani, tuwaamini na tuwajengee uwezo ...... they can make impossible possible.

Hata waarabu makocha wao wengi ni wazawa.

Kocha mzawa ananafasi kubwa ya kujua uwezo sahihi wa wachezaji na kujua namna ya kufanya setting kuliko hawa ngozi nyeupe wanaotulia hela tu.

Mpira ni investment. Wenzetu waarabu wanalijua hilo.

Sisi hapa kwetu usajili ni papatu papatu usio na tija na hata tukisajili tunasajili watu wasio serious. Hii ya leo ni Aibu kama sio Msala.

Tatizo linaanzia kwa kocha , lack of skills ya kufanya setting. Lack of contingency plan for game change kipindi cha pili; that means hata kipindi cha kwanza hakujua ametoa boko wapi na hakukielewa.

Kumfunga SIMBA leo ilikuwa ni sawa na kutoa unywele kwenye maziwa. Tai anatabia ya kumnyanyua mnyama juu kisha anaenda kumla kunako. Huko kunako ni Morocco!


Goli tatu mbele ya mashabiki elf 60!

Nashauri Timu irudi kwa Mgunda, kwakweli hizi rangi nyeupe huwa hawajuagi chemistry ya wachezaji wetu wa Ndani.

Game kama hii Boko Haram anaanzaje? Sakho was supposed to play only 25 na atolewe.

The kocha Robatinyo is good for nothing, and arudi kwao immediately !

The Kama tunategemea kupata matokeo na wachezaji kama Sako, Boko Haram, etc etc ..tutaendelea kuwaona waarabu wakitutia vidole kila siku.


The Game kama hizi ni no show off game ; wachezaji wa Raja wanacheza technically na cautiously na kila hatua yao inamadhara.

Haya Simba ataenda kuliwa vyema huko Morocco.

Poleni wanasimba huu wa leo ni msiba Wenye aibu; makosa makubwa yanaanzia kwenye setting ya Kocha na kujua the right vocabulary in the right place : game change plan pia ikafeli.

Msijali, kesho wana Yanga Wananchi tunafuta huu MSIBA wa kipuuzi.
Wachezaji ni zero hakuna
 
Back
Top Bottom