Habari za Kiuchunguzi kuhusu Maelfu ya Askari wa Rwanda waliouawa katika mapigano ya DRC

Habari za Kiuchunguzi kuhusu Maelfu ya Askari wa Rwanda waliouawa katika mapigano ya DRC

..Mobutu pamoja na mabaya yake yote hakumwaga damu ya Wacongo kwa kiwango ambacho Kagame, Museveni, na vibaraka wao, wamefanya.

..Wacongo waliopoteza maisha tangu 1998 Kagame, Museveni,na vibaraka wao, walipovamia DRC, ni wengi kupita kiasi, na inaleta ugumu mkubwa kuitetea Rwanda, au Uganda, katika madai yao dhidi ya DRC.
Sidhani kama upo sahihi kuhusiana na Hoja yako hii.

Dikteta Mobutu Sese Seko aliua Watu wengi Sana nchini Zaire, hili lipo wazi kabisa.
Enzi za Utawala wake nchini Zaire, kumkosoa Mobutu Sese Seko ilikuwa ni kujikatia tiketi ya kifo.
Wakosoaji wengi sana wa Utawala wa Kidikteta wa Mobutu Sese Seko walikuwa wanatekwa hadharani na Wanajeshi wa Vikosi kazi (Abduction Squads) kutoka kwa Kikosi Maalumu Cha Kumlinda Rais na kisha unapelekwa nyumbani kwa Rais Mobutu Sese Seko kijijini kwake Gbadolite ili ukateswe na kisha kuuawa. Ndege za Jeshi na Helicopter zilikuwa hazikauki angani kwa Safari za kuwasomba Mateka kutoka katika miji mbambali iliyopo kwenye nchi hiyo ya Zaire na kuwapeleka katika Kijiji Cha Gbadolite nyumbani kwa Mobutu Sese Seko.

Hadi leo hii Watu wengi wa Nchi hiyo hawataki kwenda kuishi katika Kijiji hicho Cha Gbadolite kwa Madai kwamba ni eneo lenye laana kubwa kutokana na damu nyingi sana za Watu kumwagika hapo chini ya Utawala wa Mobutu.
 
..

..maiti wamekuwa wengi mno, askari wa vyeo vya chini wanazikwa katika mass graves huko DRC.

..miili ya maofisa inayorudishwa Rwanda ina hali mbaya ya kutisha, familia zinalazimishwa kuzika bila kuonyeshwa wapendwa wao.

..Mzee Kagame amekiri "kiaina" katika moja ya hotuba zake alipogusia kwamba mchango wa askari waliopoteza maisha hautasahaulika.

..kupata taarifa nzima soma hapa chini.

Ufichaji wa taarifa za Kijeshi ni kote sio Rwanda pekee
 
Usalama wa Mashariki ya DRC, unahitaji Rwanda apigwe. Na hizi diplomatic solutions hazina maana kwenye mgogoro huo. Kinachotakiwa ni military intervention. Over
Military intervention ni suluhisho pekee ila huwezi kukurupuka inatakiwa mkae kikao kwanza , kikao ndo kiamue mtu achapwe ili kusiwe na lawama na uadui kati ya nchi na nchi, kichapo kikitolewa kisingizio ni kikao, nchi moja huwezi kupigana na nchi tano utachapika tu hata kama itachukua muda ila mwishowe utainua mikono.
 
Inakuaje M23 wanateka miji??

DRC is a failed state.

Utawala uliopo huko upo dhaifu Sana.
Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo pia lipo dhaifu Sana kupita kiasi.

Jeshi la DRC lipo uchi wa mnyama kwa Utawala wa Rwanda.
Kuna uasi wa chini chini usiokwisha ndani ya Jeshi la DRC.

Wanajeshi wengi sana wa DRC pia ni Wapiganaji wa Siri wa M23.

Viongozi wengi wa Serikali ya DRC pia ni Mawakala wa Siri wa Utawala wa Rwanda na Vikosi vya Waasi wa M23.

Try to imagine: General Kabarebe aliwahi kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF) wa nchi hiyo ya DRC, lakini baadaye Mwanajeshi huyo alihama nchi na kwenda kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF) wa nchi ya Rwanda.

Wewe uliwahi kuona wapi jambo la namna hii?
 
Military intervention ni suluhisho pekee ila huwezi kukurupuka inatakiwa mkae kikao kwanza , kikao ndo kiamue mtu achapwe ili kusiwe na lawama na uadui kati ya nchi na nchi, kichapo kikitolewa kisingizio ni kikao, nchi moja huwezi kupigana na nchi tano utachapika tu hata kama itachukua muda ila mwishowe utainua mikono.
kwa jinsi ulivoeleza mi naona ni bora kikao kikubaliane kuachana na M23 badala yake kigali ishushiwe kipondo na pk akimbie! Pale rwanda akakae makonda"
 
..

..maiti wamekuwa wengi mno, askari wa vyeo vya chini wanazikwa katika mass graves huko DRC.

..miili ya maofisa inayorudishwa Rwanda ina hali mbaya ya kutisha, familia zinalazimishwa kuzika bila kuonyeshwa wapendwa wao.

..Mzee Kagame amekiri "kiaina" katika moja ya hotuba zake alipogusia kwamba mchango wa askari waliopoteza maisha hautasahaulika.

..kupata taarifa nzima soma hapa chini.

Ahahah situmeambiwa Rwandwa ni Israel ya EA

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
..EAC ndio kichwa cha mwendawazimu kabisa.

..inawezekana vipi mwanachama mmoja akamvamia kijeshi mwanachama mwingine?

..au mwanachama mmoja akawa anafuga makundi ya waasi / magaidi dhidi ya mwanachama mwingine?

..kabla ya kuwa mwanachama wa EAC nchi husika ilipaswa kuwa na vigezo fulani ikiwemo utawala wa sheria, stability, etc
Mwl wangu Dr. Mohabe Nyirabu pale UDSM kwenye somo la Regional Integration alitoa vigezo mahususi ili kuwa member wa regional economic bloc lakini naona viongozi wa nchi leo wanajifanyia yao tu mpaka wakawaruhusu Rwanda, Somalia na DRC eti nao kuwa members😂😂
 
E
Afrika inataka kupewa kiti UN Baraza la Usalama ikiwa na kura yenye nguvu.
Ninapinga sana AU kupewa kiti hata cha kusikiliza, hawana kitu wanachoweza

Hawawezi mgogoro wa M23 wanataka kura ya kuamua ugomvi wa Russia, India, China , USA au Europe

Kosa lilikuwa ''rapid expansion'' ya EAC na kuwashirikisha Congo, Rwanda and Burundi.
Hawa wangekuwa nje ya EAC kungekuwa na mandate ya kuwaamuru lakini sasa ni ''miongoni'

M23 ni Rwanda wanaotaka kupanua eneo lao kwa ksingizio cha Congo.

Juzi kulikuwa na mjadala JF, Mh Zitto alialikwa kama mto mada.
Swali aliloulizwa mara 3 ni, M23 wanakosa haki gani ndani ya Congo kiasi cha kuchukua silaha.

Zitto Kabwe hakuweza kujibu alizunguka zunguka licha ya kwamba ndiye alisema M23 washirikishwe serikali ya Kinshasa.

Kwa hoja za Zitto Ruyagwa, kwa mtazamo wangu ipo siku Watu wa Kigoma wenye ''elements'' za huu mgogoro watabeba silaha wakitaka Serikali ya Tanzania iwashirikishe. Jambo la hatari sana

Suluhishio ni SADC-EAC kuwapa kipigo M23 kisha kutengeneza Buffer Zone katika mpaka wa Rwanda.
Au wawafurushe hadi Rwanda ndani kabisa ili Rwanda wapate joto la vita
Exactly, well said brother!
 
DRC is a failed state.

Utawala uliopo huko upo dhaifu Sana.
Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo pia lipo dhaifu Sana kupita kiasi.

Jeshi la DRC lipo uchi wa mnyama kwa Utawala wa Rwanda.
Kuna uasi wa chini chini usiokwisha ndani ya Jeshi la DRC.

Wanajeshi wengi sana wa DRC pia ni Wapiganaji wa Siri wa M23.

Viongozi wengi wa Serikali ya DRC pia ni Mawakala wa Siri wa Utawala wa Rwanda na Vikosi vya Waasi wa M23.

Try to imagine: General Kabarebe aliwahi kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF) wa nchi hiyo ya DRC, lakini baadaye Mwanajeshi huyo alihama nchi na kwenda kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF) wa nchi ya Rwanda.

Wewe uliwahi kuona wapi jambo la namna hii?
Hii ya barebe ni kweli?

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
 
DRC is a failed state.

Utawala uliopo huko upo dhaifu Sana.
Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo pia lipo dhaifu Sana kupita kiasi.

Jeshi la DRC lipo uchi wa mnyama kwa Utawala wa Rwanda.
Kuna uasi wa chini chini usiokwisha ndani ya Jeshi la DRC.

Wanajeshi wengi sana wa DRC pia ni Wapiganaji wa Siri wa M23.

Viongozi wengi wa Serikali ya DRC pia ni Mawakala wa Siri wa Utawala wa Rwanda na Vikosi vya Waasi wa M23.

Try to imagine: General Kabarebe aliwahi kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF) wa nchi hiyo ya DRC, lakini baadaye Mwanajeshi huyo alihama nchi na kwenda kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF) wa nchi ya Rwanda.

Wewe uliwahi kuona wapi jambo la namna hii?
I strongly agree with 100% kwamba DRC is a failed state. Central and Local Government administrative setup ya DRC ni ya hovyo sana, nafikili ni kutokana na aina ya utawala aliotumia mkoloni wake. Kila kitu kiko Kinshasa huko periferal wanajiongoza wenyewe, hakuna cha viongozi, sheria wala taratibu za ki-utawala kule.

Prof. Wamba Dia Wamba akiwa UDSM miaka hiyo pale Nkrumah Hall aliwai kusema kwamba jinsi administrative setup ya DRC ilivyokaa haiwezi kuja kuachana na uvamizi au vita. Jeshi la DRC haliko imara kabisa na wananchi hawataki kuingia kwenye jeshi!

Huyo Joseph Kabarele kutoka Rwanda alikuwa ni CDF wa DRC kutokana na makubaliano na Desire Kabila kwamba akifanikiwa kumuondoa kwa msaada wa Rwanda basi u-CDF na I-Waziri wa Ulinzi atawaachia wanajeshi kutoka Rwanda. Once again, DRC is a failed state!!!
 
1. Suala hili la Mgogoro wa huko DRC (Zaire) ni Complex sana. Lina historia ndefu Sana.

Isipokuwa kuna Ukweli mchungu Sana kwamba Watu/Raia wengi wa DRC wa kutoka kwenye maeneo hayo ya pembezoni mwa nchi hiyo ikiwamo na Majimbo ya Kivu na Katanga huwa wanahesabika Kama Raia wa Daraja Pili au raia wa Daraja la mwisho kabisa kwenye nchi hiyo. Hii ni kutokana na Mfumo au Sera ya Siasa mbaya sana za Kuwagawa Watu ili Watawala wa nchi hiyo ya DRC waweze kutawala kiurahisi. Kuna tatizo la Siasa za Ubaguzi kwa Watu wa maeneo hayo ya Mashariki mwa nchi hiyo ya DRC na kuwapendelea zaidi Watu wengine wa kutoka katika maeneo mengine ya nchi hiyo. Watu wengi wa Mashariki mwa DRC kwa kiasi kikubwa Sana wanahesabika Kama siyo WaCongoman, hiki ndio chanzo kikubwa Sana Cha kuwepo kwa huo Mgogoro usiokoma, ukiachana na vyanzo vingine kama vile kuwepo kwa rasilimali nyingi sana za madini ya vito, udhaifu wa Jeshi la DRC, Udhaifu wa Utawala wa nchi hiyo ya DRC, n.k..

2. Siyo rahisi hata kidogo kulipiga na kulifurusha Jeshi la M23 kwa sababu nyingi sana. Mathalani, Watu/Wananchi wengi Sana waishio kwenye maeneo hayo ya Kivu wanawaunga mkono Wapinzani wa Utawala wa nchi hiyo ya DRC, M23 wanaungwa mkono na Wananchi. Aidha, Utawala wa nchi hiyo ya DRC ni dhaifu Sana kupita kiasi. Bad enough, hata Jeshi la nchi hiyo nalo pia ni dhaifu Sana, na pia kuna Mawakala wengi Sana wa M23 ndani ya Serikali na ndani ya Jeshi la Serikali ya DRC. Kuna vitendo vingi Sana vya Uasi wa chini chini ndani ya Jeshi la Serikali ya DRC.

3. Kwa bahati mbaya sana, hata hapa nchini Tanzania, Watu wengi wa kutoka katika mikoa ya pembezoni mwa nchi kama vile Mkoa wa Kigoma, pia wamekuwa wakichukuliwa kama ni 'Wakimbizi.' Tatizo hili lipo sana katika nchi hii, Mimi binafsi nimewahi kushuhudia mara nyingi sana mambo ya namna hii. Kuna ' bad sentiment' miongoni mwa Watu kuwaona Watu wa kutoka Kigoma kuwa ni Wakimbizi kutoka katika nchi za jirani, tatizo hili lipo katika Jamii zetu za Tanzania.
Well done
 
Upande wa magharibi lazima tuwe waangalifu, ya M23 yanaweza kutusumbua siku zijazo.
Usidhani M23 wataishia DRC, wakimalizana na DRC watahamia Tanzania!

Hii ni expansion ya Himaya!
Hofu yangu ni kwamba hivi watawala wa hii nchi wanaona kama sisi tunavyoona?

Wana hofu kama sisi tuliyonayo juu ya hili suala na usalama wa nchi yetu kwa ujumla?

Mbona kama wapo wapo tu kama hawajui wanalolifanya?
 
Hii ya barebe ni kweli?

Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app

Ni kweli ndiyo.

Tatizo Watu wengi sana humu mtandaoni wamekuwa wakifanya uchambuzi juu ya masuala haya ya Vita ya huko DRC (Zaire) bila ya kufanya utafiti wa kina kabisa kuhusiana na historia nzima ya Mgogoro huo. Watu wengi hawana taarifa za kutosha kuhusu suala hili. Lakini kama wangelikuwa wanafanya utafiti wao kwa kina kabisa, basi naamini ufumbuzi wa kudumu juu ya Vita hiyo tayari ungekuwa umepatikana.
 
..

..maiti wamekuwa wengi mno, askari wa vyeo vya chini wanazikwa katika mass graves huko DRC.

..miili ya maofisa inayorudishwa Rwanda ina hali mbaya ya kutisha, familia zinalazimishwa kuzika bila kuonyeshwa wapendwa wao.

..Mzee Kagame amekiri "kiaina" katika moja ya hotuba zake alipogusia kwamba mchango wa askari waliopoteza maisha hautasahaulika.

..kupata taarifa nzima soma hapa chini.

Kale kazee kauwaji sana. Kenyewe na watoto wake wako state house watoto wa wakulima ndio wanapelekwa front line.
 
Kwanini Tanzania tunajihusisha sana na hizi mambo, eti ooh kikao cha usuluhishi kifanyike Tanzania why? Mm ningeshauri tujifanye kama hatujui kinachoendelea kisha tulinde mpaka wetu kwa nguvu, tuajiri walimu bora kwenye mashule yetu. Tupandishe mishahara ya walimu wetu, tujenge maabara za kisasa kwenye mashule yetu tuongeze bajeti ya elimu.

Elimu ndiyo itatutoa siyo hizo mambo za bunduki bunduki
 
Back
Top Bottom