mjumbe wa bwana
JF-Expert Member
- Sep 19, 2016
- 5,252
- 6,118
Hapa ili tujue ukweli ni kuwahoji makampuni ya kupandisha watalii mliman na yale ya kuwatembeza porini
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ukiitaka kujua Ie billion 100 italeta unafuu kiadi gani kwenye bei ya mafuta kwa waTanzania ambao tuko million 60 ni simple.: 100b/60m=1,667.Kama wanavyosema watu kwamba ujinga ni mtaji mkubwa sana wa Wanasiasa hasa wa Africa na zaidi Tanzania. Ukizingatia kwamba ujinga bado ni tatizo kubwa sana kwa Tanzania, wanasiasa wanachofanya ni ku'capitalize' kwenye ujinga wa Watanzania.
Mtu akishakujua wewe ni mjinga maana yake hata akiamua kukudanganya bado atafanikiwa kwa sababu wewe ni mjinga. Ujinga ni hali ya kutokujua jambo fulani, ila ukishajua unakua sio mjinga tena kwenye hilo jambo. Tatizo la Tanzania watu wengi ni wajinga karibu kwenye kila kitu hata vile vitu vya msingi ambavyo unatarajia kua mtu lazima awe anavijua kwa Tanzania bado ni tatizo.
Ujinga uliopo sasa ni wa takwimu, serikali na wanasiasa kupika takwimu ili kutetea filamu ya royal tour. Juzi nimemsikia kiongozi mmoja akisema Watalii Tanzania wamejaa hadi mwezi wa 9, yaani hoteli za Tanzania zimejaa kwa miezi 3 ijayo ziko full booked kutokana na mafanikio ya Royal Tour.
Kuna kiongozi mwingine leo kaenda mbali zaidi akasema Tanzania kwa sasa inaongoza kwa kua na watalii wengi Afrika nzima kutokana na Royal Tour.
Kwa wasiofahamu, Kabla ya Covid, Nchi iliyokua inaongoza kwa idadi ya Watalii Afrika ilikua ni South Afrika ambayo ilikua inapokea watalii milioni 16 kwa mwaka ikifuatiwa na Tunisia milioni 12 kwa mwaka. Ila baada ya Covid, South Afrika mwaka jana imepata watalii 9.5m huku ikizidiwa na Tunisia iliyopata watalii 10m. Tanzania kwa miaka yote imekua ikiambulia watalii kati ya milioni moja hadi milioni 1.8 kwa mwaka.
Turudi kwenye hoja yangu ya uongo ulipo. Kama watanzania wangekua wanajua facts chache tu ambazo ziko wazi wala wasingehangaika na maneno ya wanasiasa.
Ili ujue kama Watalii wanaongezeka Tanzania ama lah angalia thamani ya shilingi dhidi ya Dollar ya Marekani kwa kipindi cha miezi 5 iliyopita hadi leo hii June 2022.
Thamani ya shilingi imezidi kuporomoka siku hadi siku kutokana na kwamba hakuna vyanzo vya kuingiza Dollar nchini. Kwa Tanzania vyanzo pekee vya kuingiza pesa za kigeni ni utalii na mauzo ya mazao ghafi kama Korosho, Kahawa ama Pamba.
Ukiangalia takwimu za Shilingi dhidi ya Dollar, shilingi ilipanda mwezi Septemba mwaka jana hadi December kutokana na mauzo ya Korosho, msimu wa korosho ulipoisha tu Dollar imekua ikipanda kwa fujo na labda itashuka tena kuanzia Septemba mwaka huu.
Iwapo kungekua na inflow kubwa hivyo ya watalii kama inavyosemwa na wanasiasa, inflow ya Dollar ingeonyesha matokeo yake kwenye thamani ya shilingi dhidi ya Dollar. Kwa tunaojua soko la Dollar shilingi tunajua ni maneno tu ya wanasiasa maana dollar haipo kabisa sokoni.
Watanzania wengi wangekua wanajua hata hizi naked facts wanasiasa wasingekua wanathubutu kusema uongo ila kwa kua wanajua watanzania wengi ni wajinga, watasema wanachotaka kusema.
Ahsante sana.
Kwamba rais anacheza movie!!!Rais unaanzaje kuigiza?
Ujue mie mwenzenu mpaka Leo bado sielewi elewi.(pole jamani nje ya mada )
Dah we jamaaKama hizi taarifa ni kweli basi aibu nimeona mimi.
Msoga Jazz band-walamba asali leo tupo hapa Royal Tour BarRoyal tour ni mchongo wa msoga gang. Ni upigaji wa kawaida sana.
Tupo kwenye hii tasnia ya utalii hakuna, order mpya ni zile booking za mwaka jana, sio Kwa ajili ya rolaytour, kama kuna kampuni imepata mafuliko ya watalii Kwa ajili ya rolaytour itoe ushuhuda.Hapa ili tujue ukweli ni kuwahoji makampuni ya kupandisha watalii mliman na yale ya kuwatembeza porini
Kila mtu mwenye mawazo tofauti na nyinyi mnambatiza kuwa ni HATER!! Acheni upumbavu huo watu wote hatuwezi kuwa tunafikiri sawa sawa.!Haters hawaamini basi wamebaki kujaribu kuharibu kila kitu cha mama......kila dakika ni kujaribu, bila mafanikio, kurusha thread ya kuipondea Royal tour lakini wapi!!!!
Mi nawaangalia na kujisemea, HIIIIIIIIIIÌÌIIIIIIIIII
Utaitwa sukuma gang!
Uzuri ni kwamba hii awamu ina machawa kutoka pande zote 2. Kuna yale machawa kutoka ccm na yale ya kutoka chadema
Hapa tunajadili mustakabari wa watanzania wanaofanya shughuli za utalii sio siasa maana Sisi wengine tuko independent na ndiyo sio machawa wa watuMmehama kwenye katiba mpya mmekuja royal tour?
Upo sahihi, royal tour haijatimiza hata nusu mwaka toka itoke, hivyo ni vigumu kusema imeleta tija.Tupo kwenye hii tasnia ya utalii hakuna, order mpya ni zile booking za mwaka jana, sio Kwa ajili ya rolaytour, kama kuna kampuni imepata mafuliko ya watalii Kwa ajili ya rolaytour itoe ushuhuda.
Mkuu kinachoendelea si unakisia kama sio kukiona? Maana wafuta viatu wanasema rolaytour ishaanza kuleta wageni, ilo ndilo ninalopinga Mimi sio vinginevyo na ñdiyo maana nikasema kama kuna kampuni yoyote iliyopata mafuliko ya wageni kinyume na booking za kawaida itupe ushuhuda. Tufauti wanavyotuaminisha akina mwijaku kama impact ya rolaytour imeanza kuonekana .Upo sahihi, royal tour haijatimiza hata nusu mwaka toka itoke, hivyo ni vigumu kusema imeleta tija.
Kwa hiyo Tanzania imepigwa na watanzania wenyewe? 😂Ningeona Ana Akili sana , awe sponsor kwenye movies zinazojulikana kama Fast & Furios , Avengers kwa hiyo hela , wamtengenezee scene yenye vivutio vya Tanzania katikati ya stori ya movie
Au angefanya Digital Marketing, nchi ya Marekani Ni namba moja katika matumizi ya intaneti , So kila anayeingia mtandaoni anakutana na matangazo ya Utalii Tanzania.
hivi kuna Mtanzania anaamini huo uongo wa viongozi ?Kama wanavyosema watu kwamba ujinga ni mtaji mkubwa sana wa Wanasiasa hasa wa Africa na zaidi Tanzania. Ukizingatia kwamba ujinga bado ni tatizo kubwa sana kwa Tanzania, wanasiasa wanachofanya ni ku'capitalize' kwenye ujinga wa Watanzania.
Mtu akishakujua wewe ni mjinga maana yake hata akiamua kukudanganya bado atafanikiwa kwa sababu wewe ni mjinga. Ujinga ni hali ya kutokujua jambo fulani, ila ukishajua unakua sio mjinga tena kwenye hilo jambo. Tatizo la Tanzania watu wengi ni wajinga karibu kwenye kila kitu hata vile vitu vya msingi ambavyo unatarajia kua mtu lazima awe anavijua kwa Tanzania bado ni tatizo.
Ujinga uliopo sasa ni wa takwimu, serikali na wanasiasa kupika takwimu ili kutetea filamu ya royal tour. Juzi nimemsikia kiongozi mmoja akisema Watalii Tanzania wamejaa hadi mwezi wa 9, yaani hoteli za Tanzania zimejaa kwa miezi 3 ijayo ziko full booked kutokana na mafanikio ya Royal Tour.
Kuna kiongozi mwingine leo kaenda mbali zaidi akasema Tanzania kwa sasa inaongoza kwa kua na watalii wengi Afrika nzima kutokana na Royal Tour.
Kwa wasiofahamu, Kabla ya Covid, Nchi iliyokua inaongoza kwa idadi ya Watalii Afrika ilikua ni South Afrika ambayo ilikua inapokea watalii milioni 16 kwa mwaka ikifuatiwa na Tunisia milioni 12 kwa mwaka. Ila baada ya Covid, South Afrika mwaka jana imepata watalii 9.5m huku ikizidiwa na Tunisia iliyopata watalii 10m. Tanzania kwa miaka yote imekua ikiambulia watalii kati ya milioni moja hadi milioni 1.8 kwa mwaka.
Turudi kwenye hoja yangu ya uongo ulipo. Kama watanzania wangekua wanajua facts chache tu ambazo ziko wazi wala wasingehangaika na maneno ya wanasiasa.
Ili ujue kama Watalii wanaongezeka Tanzania ama lah angalia thamani ya shilingi dhidi ya Dollar ya Marekani kwa kipindi cha miezi 5 iliyopita hadi leo hii June 2022.
Thamani ya shilingi imezidi kuporomoka siku hadi siku kutokana na kwamba hakuna vyanzo vya kuingiza Dollar nchini. Kwa Tanzania vyanzo pekee vya kuingiza pesa za kigeni ni utalii na mauzo ya mazao ghafi kama Korosho, Kahawa ama Pamba.
Ukiangalia takwimu za Shilingi dhidi ya Dollar, shilingi ilipanda mwezi Septemba mwaka jana hadi December kutokana na mauzo ya Korosho, msimu wa korosho ulipoisha tu Dollar imekua ikipanda kwa fujo na labda itashuka tena kuanzia Septemba mwaka huu.
Iwapo kungekua na inflow kubwa hivyo ya watalii kama inavyosemwa na wanasiasa, inflow ya Dollar ingeonyesha matokeo yake kwenye thamani ya shilingi dhidi ya Dollar. Kwa tunaojua soko la Dollar shilingi tunajua ni maneno tu ya wanasiasa maana dollar haipo kabisa sokoni.
Watanzania wengi wangekua wanajua hata hizi naked facts wanasiasa wasingekua wanathubutu kusema uongo ila kwa kua wanajua watanzania wengi ni wajinga, watasema wanachotaka kusema.
Ahsante sana.
Huyo ni mleviKila mtu mwenye mawazo tofauti na nyinyi mnambatiza kuwa ni HATER!! Acheni upumbavu huo watu wote hatuwezi kuwa tunafikiri sawa sawa.!
Hao ni waleviMkuu kinachoendelea si unakisia kama sio kukiona? Maana wafuta viatu wanasema rolaytour ishaanza kuleta wageni, ilo ndilo ninalopinga Mimi sio vinginevyo na ñdiyo maana nikasema kama kuna kampuni yoyote iliyopata mafuliko ya wageni kinyume na booking za kawaida itupe ushuhuda. Tufauti wanavyotuaminisha akina mwijaku kama impact ya rolaytour imeanza kuonekana .