Hatimaye ndoa yangu imevunjika

Hatimaye ndoa yangu imevunjika

Asalaam,

Ndoa yangu ilikua nzuri saana kwasababu tulianza tukiwa vijana wadogo maskini, kutokana na hivyo tuli inspire vijana wengi na ndoa nyingi kusimamia.

Tuka barikiwa watoto wazuri. Mungu alitubariki na unafuu wa maisha wa kupata tunachokita kwa level ya maisha ya kawaida. Basi ghafla maisha yakabadilika nikaanza kupitia magumu kiuchumi hata jero mtihani kupata.

Balaa lilianza hapo kudharaulika, kununiwa, Visa vya kila aina mpaka hatimaye Mimi ndiye nikawa "mama wa nyumbani" na yeye akawa anarudi nyumbani ka guest house ni kulala tuu bila kujali hata watoto wanna hali gani.

Biashara nimemfungulia mwenyewe, na hata kodi nimekua nikimsaidia kulipa. Pamoja sasa Sina shughuli maalumu lakini Mungu ananisaidia kumudu kutimiza mahitaji muhimu ya familia yangu.

Sasa amepata mwanaume mwingine na amenidhibitishia na nilipohitaji aende kwao akapumzika akaniambia hawezi atabaki Dar aendeleze maisha yake kwakua anashida saana ya hela. Kumbe nia yake ni kuendelea kuishi na huyu mwanaume.

Leo nimedhibitisha. Ndoa yangu haitakuwepo tena baada ya kukamilisha taratibu za kisheria.

Roho inauma kwakua sikutegemea kama wanangu wataishi na mzazi mmoja.

Wanaume tutafute hela, ndo thamani yetu!

#Mwanamkemkwelinimamayakotuu

Pole sana mkuu wanawake hawa jipe moyo mungu nyuma yako
 
Cha kujifunza kipo,
Mwanamke wa kwanza ndio mke, hawa wengine ni sarakasi tu kama yale ya mzee MENGI
Halad wanamsingizia mke wa kwanza wa mengi wakati watu tunamjua kwa kiasi chake yule mama na tabia mbaya za marehem mumewe. Yaan baba amehangaika na mbususu yule poooh
 
Na wengi walivyo wajinga, basi ex akikusimulia changamoto alizopitia basi unajiona mwamba au cuteeee; kumbe mwenzio anatafuta tu pa kutolea genye zake tu au ana shida zake anakuingiza king umsaidie. Kama msamaha angekuja kukuomba while everything was still ok with him/her; sio msamaha fake kisa ameona ametingwa. Watu wajifunze ku-move on; ukiachwa achika
Mahusiano na maex asilimia kubwa huwa ni unafiki tu.

Hamna real intimate relationship from hearts
 
Na wengi walivyo wajinga, basi ex akikusimulia changamoto alizopitia basi unajiona mwamba au cuteeee; kumbe mwenzio anatafuta tu pa kutolea genye zake tu au ana shida zake anakuingiza king umsaidie. Kama msamaha angekuja kukuomba while everything was still ok with him/her; sio msamaha fake kisa ameona ametingwa. Watu wajifunze ku-move on; ukiachwa achika
[emoji23][emoji23][emoji23]

UMIOENDWA PENDEKA

UKIACHWA ACHIKA...

yaan kuna watu walaghai kwelikweli[emoji23][emoji23]
Waongooo... si bora ninywe zangu chimpumu
 
Na mchepuko wa mkewe lazima tu azingue kwa maana katembea na mke wake lengo likiwa ni kumkomesha tu kumtia adabu wala sio mapenzi.

Kwaiyo nnaimani mwanamke yatamshinda na atarudi,
Ila somo jamaa atakua keshapata na akili itamkaa.
Hahaha ndio ndio. Muda ytasema
 
Kabisa,
Awamu nzima ya mwendazake jamaa anachepuka tu uko.

Hivi sijui akifka uko mbinguni atamjibu nini kiongozi wa malaika (JOKE[emoji2])
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Dah, mitano ya kwanza kwa mwenda zake anakiwashaaaa tu[emoji23][emoji23] mauno paka chongo na kibamia chake
 
Mkuu mimi sikupi pole bali nakupa moyo wa kuweza kujizatiti..
Kakutenda baada hali kuwa mbaya..
Atatendwa na yeye na kuja kwako kuomba msamaha...
Singo maza wana mitihani sana japo sio wote lkn wengi ndio walipo pitia visa kama chako..
 
Shida watu huleta mada ku paint vibaya partner's wao badala wasemd ukweli wapewe ushauri uliotukuka wao hujifanya malaika
Na huwaga mara nyingi siyo msaada. Hauwezi kuponaaa asilani. Ushauri unaokuacha katika comforting zone haujawahi kuwa mzuri
 
Nashukuru saana kwa ushauri hata hivyo Mungu mwema maana nilikua napitia mateso saana kwa huyu mwanamke Mungu ameniweka huru.

Kuhusu mke mwingine hapana wanangu ni wadogo saana
Wana umri gani kwani utakiwi kukurupuka kuoa lakini kuoa muda utafika
 
Magum mno,
Wee acha tu hivi vifua vyetu vinahifadhi mengi mno.

Mengine siwez kuweka humu hadharani,

Mi niliumia mno,
Sema kwa sababu nilijingundua ndio msababishi wa sarakasi zote zile za ukaidi na kushupaza shingo kwa kigezo cha niko tayar kua na mwaamke yeyote nnaemtaka kwa gharama yoyote.

Aisee liliponikuta nilikua mpole na mdogo kama piritoni nikafyata mkia maisha yakaendelea.

Namsifu sana mama watoto wangu kwa uvumilivu wake.

Ukilinganisha mizani mimi ndio nilimuumiza zaidi maana nilikua TOO MUCH.

Yaani kuna vitu nilikua naweza nikamfanyia afu baadae pemben nafs ikanisuta kwanini nilimfanyie vile, Sema tu ulikua ujeuri na kiburi.

Kwa sasa nimejifunza, na tunaenda vizur mno.

She is the best lover of my life.

Mungu akupe maisha marefu mno Mke wangu, japokua hauko jf wala hujui jf ni kitu gani.
Hahahaha kwahiyo bado hujapata mchepuko mwingine? Maana uliapa hutaacha
 
Na huwaga mara nyingi siyo msaada. Hauwezi kuponaaa asilani. Ushauri unaokuacha katika comforting zone haujawahi kuwa mzuri
Wengi hutaka lawama apewe partner na yeye aonewe huruma. Sindano huuma lakini Dr lazima akuchome ili upone
 
Kwa uzoefu nilionao, wanandoa wanapoacha kila mmoja wao hutoa lawama kali dhidi ya mwenzake. Hakunaga anayekubali makosa na kusema wazi kuwa yeye ndiye mkosaji.

Wewe umetuambia madhaifu ya aliyekuwa Mkeo. Ingependeza zaidi kama tungemsikia na Mkeo naye atueleze madhaifu yako ili tupime kwa haki.

By the way nakupa pole kwa kuvunjikiwa kwa ndoa yako. Ushauri wangu kwako ni huu :

"Kabla ya kutoa lawama kwa Mkeo, hebu kaa chini na ujitafakari wewe mwenyewe. Mimi naamini kilicho muondoa Mkeo kwako siyo "pesa" pekee. Lazima kuna mengi sana nyuma ya pazia".
 
Ange weza kuniua huyu maana hawara anadai ananijua kindaki ndaki wakati binafsi simjui
Tatizo la mwanamke akikolea penzini Ni anakolea kweli kweli,anaubwaga moyo ,akili na mwili kwa mtu aliempenda, ndio maana u unakuta sio tu kukuumiza kwa kuchepuka hata kutoa Siri zako zote kwa mpenzi wake mpya ....

Sisi kwetu Wazazi wetu walifariki tukiwa bado hatujatimiza miaka 18,ukoo ukamteua mama yetu mdogo kuwa msimamizi wa mirathi,mamdogo akadanganywa na hawara yake mwenye familia yake(mume wa mtu)

Aisee jinsi mamdogo alivyotubadilikia hakuna alieamini,jamaa alimshawishi watutapeli fedha zote na jamaa alikuwa anatujua a-z kuhusu sisi na ukoo kwa ujumla,Sasa hv fedha zimekwisha na sisi tunasonga japo kwa mwendo wa kinyonga , mamdogo amebaki na aibu,kila kukicha simu za vizinga
 
Back
Top Bottom