Hawa ni watu waliomdhihaki Mungu na kupatwa na shida

Hawa ni watu waliomdhihaki Mungu na kupatwa na shida

Wala tusiende Mbali Afande sele aliwahi kumdhihaki Mungu na bado tuko nae anadunda.
 
wewe jamaa ni mwongo mwongo sana Eti
Stephen Hawking alimkana huyo Mungu ndio akapata ugonjwa wa ajabu hivi hizi stori hua manazipata wapi?
Hebu Rudi kasome historia ya maisha ya huyo nguli ndio urudi hapa utupige Kamba zako!
Huwa wanazipata kwenye mahubiri ya shehe su mchungaji mtoa mapepo
 
Huwa wanazipata kwenye mahubiri ya shehe su mchungaji mtoa mapepo
Religion is Opium,
Yaani ukiwa mfuasi wa Dini lazima ukubali kua nyumbu,hivi Hawa watu wamefungwaje akili,mbona Mimi naona Kabisa Dini na Imani za Mungu,miungu,mashetani,
mapepo,mizimu,majini nk ni propaganda tu ila still Watu Bado wanaamini tu!
Daaaa Mimi nimeshindwa Hata Kwa kujilazimisha!
 
1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)
Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966. Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)
Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)
Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute" Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.

4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC
Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata Mungu hawezi kuizamisha" Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)
Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya "Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'. Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.

6.
Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa mtoto wake.
Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye boneti la gari". Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa. Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika.

7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)
Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia" Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)
Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simuhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu
hakuna kama Mungu.

Follow me on twiiter as LegalGentleman
Hapa kuna funzo kubwa sana, Nami nitaongezea kisa kimoja nilichopata kusimuliwa na watu ninaowaamini.
Miaka ya hapa kati (2010-2015) kanisa moja la Anglican tena ni kanisa kuu la diocese lilikuwa linafanya sherehe za kutimiza karne moja tangu kuanzishwa kwa diocese hiyo, moja kati ya diocese kongwe hapa Tanzania.
Basi Siku hiyo kulikuwa na maandamano ya waumini na viongozi wa kanisa kutoka mahali ambapo ndipo palikuwa na kanisa la kwanza kabisa la dayosisi hiyo mpaka lilipo kanisa kuu la sasa ambalo nalo ni la zamani sana.
Basi maandamano yalikatiza mitaa ya katikati ya mji wakiongozwa na kiongozi wa maandamano aliyebeba MSALABA mkubwa wa mbao.
Waandamanaji walipofika maeneo ya katikati ya mji akatokea bwana mmoja aliyekuwa mchukuzi maarufu wa maeneo hayo kwa jina maarufu CHENGO, basi yule bwana CHENGO alicheka kwa kejeli na kutoa maneno ya kuudhihaki msalaba, alizidi kutoa maneno machafu kwa Waandamanaji na juu ya ule MSALABA MTAKATIFU.
Baada ya maandamano kupita na kuisha katika maeneo yale yule bwana alipata ajali ambayo mpaka leo hakuna ajuaye BWANA CHENGO aligongwa na chombo gani. Hakuna gari iliyoonekana kwa macho ikimgonga lakini ndiyo hivyo yule bwana akapoteza uhai siku ileile tena muda mfupi baada ya kuunanga MSALABA MTAKATIFU

Tuweke akiba ya maneno
 
Umejuaje haya yote, wakati hujawahi kufa?Yote haya uliyoandika ni mambo ya kusimuliwa tu.

kuyaelewa haya inahitaji afya nzuri ya akili kuzitafuta fact
kwanza elewa binaadmu ni muunganiko wa vitu viwili Roho na mwili
soul + body = humanbeing
pia mahitaji na maisha ya binaadamu lazima yawe hivyo kimwili na kiroho ndio maana HAKUNA KUFA BALI KUNAKUHAMA THE DEPARTURE OF THE SOUL FROM BODY
 
kuyaelewa haya inahitaji afya nzuri ya akili kuzitafuta fact
kwanza elewa binaadmu ni muunganiko wa vitu viwili Roho na mwili
soul + body = humanbeing
pia mahitaji na maisha ya binaadamu lazima yawe hivyo kimwili na kiroho ndio maana HAKUNA KUFA BALI KUNAKUHAMA THE DEPARTURE OF THE SOUL FROM BODY
Unaposema inahitaji afya nzuri ya akili kuzitafuta fact una maana gani mkuu?

Na ni njia ipi unayotumia kupata facts ambayo inahitaji uwe na afya ya akili?
 
Unaposema inahitaji afya nzuri ya akili kuzitafuta fact una maana gani mkuu?

Na ni njia ipi unayotumia kupata facts ambayo inahitaji uwe na afya ya akili?

njia rahisi nikujiuliza tu ila unapojiuliza lazima uwe na akili timamu
yapo maswali kama 4 hivi na zaidi
1. Mimi ni nini ?
2 na kabla ya kuwepo hapa nilipo nilikua wapi?
3, hapa nilipo ni kwa hiyari yangu na kupenda kwangu au ni nguvu fulani ilionisukumia hapa.
4, nikitoka hapa nilipo nitakwenda wapi na kwenda kwangu itakua hiari yangu au ni nguvu fulani itakayo nisukuma huko
 
Nakupa list ya wachungaji na masheikh ambao hawakumdhihaki Mungu na walipata shida na kufariki

1. TB JOSHUA
2. MAMA LWAKATALE
3. STEPHEN AKNOLA
4. ISSA TURAY
5. WILSON BADEJO

Sheikh nooren mohammed hakumdhihaki Mungu lakini alikufa kwa ajali mbaya sana.

Sheikh Saeed bin nahynan huyu kafa siku nne zilizopita naye kwa ajali mbaya sana na hakumdhihaki Allah

Rashid bin Mohammed naye alikufa kwa shambulio la moyo na hakuwahi mdhihaki Mungu.

Na sio tu hao wapo wengi sana wamekufa na wengine wakipata shida pasipo hata kumdhihaki Mungu.

Kinachokufanya uone hao watu uliowataja kua wamepatwa na shida kutokana na wao kumdhihaki Mungu ni kipi? Nani asiyepata tabu hapa ulimwenguni?

Huyo Mungu wako historia ya dini inaonesha yeye ndio alikua muanzilishi wa kupata tabu baada ya vita yake na shetani ambapo shetani alizua utata huko juu mpaka akafanikisha kusepa na robo tatu ya malaika unafikiri tabu aliyoipata huyo Mungu ilikua ndogo?

Kwa hiyo nayeye tuseme alimdhihaki nani mpaka ikamfika hiyo tabu?

Utakuwa umshiba ukavimbiwa unaongea kwa kibri
 
Hapa kuna funzo kubwa sana, Nami nitaongezea kisa kimoja nilichopata kusimuliwa na watu ninaowaamini.
Miaka ya hapa kati (2010-2015) kanisa moja la Anglican tena ni kanisa kuu la diocese lilikuwa linafanya sherehe za kutimiza karne moja tangu kuanzishwa kwa diocese hiyo, moja kati ya diocese kongwe hapa Tanzania.
Basi Siku hiyo kulikuwa na maandamano ya waumini na viongozi wa kanisa kutoka mahali ambapo ndipo palikuwa na kanisa la kwanza kabisa la dayosisi hiyo mpaka lilipo kanisa kuu la sasa ambalo nalo ni la zamani sana.
Basi maandamano yalikatiza mitaa ya katikati ya mji wakiongozwa na kiongozi wa maandamano aliyebeba MSALABA mkubwa wa mbao.
Waandamanaji walipofika maeneo ya katikati ya mji akatokea bwana mmoja aliyekuwa mchukuzi maarufu wa maeneo hayo kwa jina maarufu CHENGO, basi yule bwana CHENGO alicheka kwa kejeli na kutoa maneno ya kuudhihaki msalaba, alizidi kutoa maneno machafu kwa Waandamanaji na juu ya ule MSALABA MTAKATIFU.
Baada ya maandamano kupita na kuisha katika maeneo yale yule bwana alipata ajali ambayo mpaka leo hakuna ajuaye BWANA CHENGO aligongwa na chombo gani. Hakuna gari iliyoonekana kwa macho ikimgonga lakini ndiyo hivyo yule bwana akapoteza uhai siku ileile tena muda mfupi baada ya kuunanga MSALABA MTAKATIFU

Tuweke akiba ya maneno
Nitwaminije ya kwamba Hii kweli na si chai,je tutajuaje kama wale Watu wa Dini walimfanyia tukio Ili ionekane eti aliukashifu msalaba na amepigwa tukio na huyo Mungu,
Kisa chako kina walakini kwanza Mimi najua mbinu za hao wanaojiita watu wa Dini kutengeneza matukio Ili kuwatisha na kuwahadaa watu na Hapo wakiita ni miujiza,
Kwangu Mimi hilo tukio naona ni coisendence ya kawaida tu au Kuna figisu alifanyiwa huyo bwana ila swala la kusema ni laana au sijui miujiza nooop!
 
Nitwaminije ya kwamba Hii kweli na si chai,je tutajuaje kama wale Watu wa Dini walimfanyia tukio Ili ionekane eti aliukashifu msalaba na amepigwa tukio na huyo Mungu,
Kisa chako kina walakini kwanza Mimi najua mbinu za hao wanaojiita watu wa Dini kutengeneza matukio Ili kuwatisha na kuwahadaa watu na Hapo wakiita ni miujiza,
Kwangu Mimi hilo tukio naona ni coisendence ya kawaida tu au Kuna figisu alifanyiwa huyo bwana ila swala la kusema ni laana au sijui miujiza nooop!
Kumbe unajua kuna laana na miujiza? Mimi sikuelezea hivyo
 
Kumbe huna hoja ya kuthibitisha hakuna Miungu.

Unafikiri hiyo akili ya kujua mantiki sijui nini kakupa nani? Kwanini mbuzi hawajui habari za mantiki?

Unakwepakwepa tu.

Utakuwa ulipitia magumu ndio maana unaona hakuna Mungu.
watu wasomuamini mungu hua na mtindio wa ubongo, mungu amekua jawabu la mambo mengi ambayo science wanayoitukuza imeshindwa, mfano; vipimo na matibabu ya kisayansi yanamwambia mtu hawezi kupata mtoto isipokua kwa kupandikiza bt ukija mbele za mungu utapata mtoto bila hata kupandikiza.
 
njia rahisi nikujiuliza tu ila unapojiuliza lazima uwe na akili timamu
yapo maswali kama 4 hivi na zaidi
1. Mimi ni nini ?
2 na kabla ya kuwepo hapa nilipo nilikua wapi?
3, hapa nilipo ni kwa hiyari yangu na kupenda kwangu au ni nguvu fulani ilionisukumia hapa.
4, nikitoka hapa nilipo nitakwenda wapi na kwenda kwangu itakua hiari yangu au ni nguvu fulani itakayo nisukuma huko
Ngoja nijibu maswali yako

1. Mimi ni mtu naye tambulika kwa majina matatu niliypewa na wazazi wangu

2. Kabla ya kuwepo, sikuwepo. Kuuliza mahali nilipokuwa wakati sipo ni contradiction

3. Hapa nipo kwasababu ya juhudi zangu za kjjiepusha na hatari zinazoweza kufanya nisiwepo, nipo hapa kwasababu cell zangu hazichachoka. Kwa hiyo hakuna nguvu yeyote inayonisukuma

4. Nikitoka hapa kwa namna gani? Kama una maanisha kufa, basi jibu ni simple, kilichokufa hakiwezi kufanya movements yeyote ya kwenda sehemu nyingine, labda kama unakusudia kuzikwa

Kwa hiyo hayo maswali ulivyokosa majibu ndio yalikusababisha mpaka ukaamini Mungu?
 
wewe jamaa ni mwongo mwongo sana Eti
Stephen Hawking alimkana huyo Mungu ndio akapata ugonjwa wa ajabu hivi hizi stori hua manazipata wapi?
Hebu Rudi kasome historia ya maisha ya huyo nguli ndio urudi hapa utupige Kamba zako!
Wewe ndio ukatafute historia yake ujifunze vizuri
 
Kumbe huna hoja ya kuthibitisha hakuna Miungu.

Unafikiri hiyo akili ya kujua mantiki sijui nini kakupa nani? Kwanini mbuzi hawajui habari za mantiki?

Unakwepakwepa tu.

Utakuwa ulipitia magumu ndio maana unaona hakuna Mungu.
Mimi nina hoja ya kuthibitisha Mungu hayupo

Kwasababu mimi ndio Mungu wa kweli na Mungu unayemdhania wewe sio wa kweli hayupo

Unabisha?

Kama unabisha thibitisha mimi sio Mungu wa kweli
 
Wala tusiende Mbali Afande sele aliwahi kumdhihaki Mungu na bado tuko nae anadunda.
Walisema ameomba radhi ila baada ya kusikia kuna njama za watu kumfata na mapanga usiku

So wangemkata na mapanga halafu wanegekuja na kauli kua ni laana ya Mungu
 
Back
Top Bottom