Hii akiba ya fedha za kigeni dola Bilioni 6,253 aliyosema Rais Samia kiboko, deni la Taifa lingekuwa hela ya peremende

Hii akiba ya fedha za kigeni dola Bilioni 6,253 aliyosema Rais Samia kiboko, deni la Taifa lingekuwa hela ya peremende

Mwandishi atakuwa Francophone. Wafaransa ndio wanatumia koma kwenye nukta. Yaani kwa Kifaransa bilioni 6,253 = bilioni 6.253. Lakini kusema ukweli Ikulu yetu ni jumba bovu. Nyaraka za Ikulu km vile press release za uteuzi zimejaa typos!!
Leo ndio umeona Mkuu unakuta font tu sio uniform, Tangazo zima ni bold. Personally naona Rais Hana muda wa kuwahakiki wasaidizi wake yeye anapokea tu
 
Nilidhani sijasikia vyema ikabidi nimfuate kule tube kusikiliza Tena nikajirithisha kuwa masikio yangu ni mazima!
Huenda ni kweli BoT wanazo hizo dollar bilioni elfu sita. Basi walipe deni lote la taifa ili nchi isidaiwe Tena. Au mnasemaje ndugu zangu?
Kama hicho kiwango alichotaja hakipo basi huu ni mkwaju au bakora nyingine Tena tumechapwa nayo wananchi!
Hivi inawezekana kufanya editing kwenye hotuba iliyokwisha ruka hewani?
Nimshauri bi mkubwa kuwa, kabla ya kuisogelea mimbari yoyote asome alichokabidhiwa kwanza ajiridhishe vinginevyo Kuna siku atawekewa barua ya posa ya bintiye naye atatusomea Kama hotuba! Bi mkubwa ajiri waandishi na wanahabari wazalendo na watiifu kwako achana na hao waandishi michongo unaoletewa watakuangushia gari bovu!
Halafu inatosha kwa miezi saba...
 
Hizo sio hela za umma tu ni pamoja na za sector bijafsi.

Stock ya dola ina maana wakichukua dola zote za serikali, na zile zinazomilikiwa na watu binafsi kwenye bank na bureau ndio unapata akiba ya fedha za kigeni. Kusema serikali ikazilipie deni sio sahihi maana sio hela zake

Sasa mkuu, kama haiwezi kuzilipia deni inawezaje kuzifanyia matumizi ya kununulia chakula?
 
Mh Rais kwenye hotuba yake hapo jana kwa wananchi amesema kuwa nchi yetu hadi leo ina akiba ya pesa za kigeni zaidi ya dola billion elfu sita miambili hamsini na tatu (Dola billion 6253).

Ukiangalia hiki kiasi kwa kukifanyia mahesabu utagundua Tanzania ina ukwasi mkubwa sana na tena tunaweza kuihudumia hata Marekani kibajeti na kwa hakika tunapaswa kulipa madeni yote hapo kesho kama kweli hichi kiasi cha pesa kipo chote na kweli kama alivyosema Mh Rais!

Mh Rais hizo hela ulizotaja hata USA awezi kuwanazo kwa haraka!

Ni kweli Mh Rais tuna dola trillion 6+ kama akiba?

Hakika kama ni kweli basi Marekani +China +Japani tunawakaribisha waje kukopa kwetu!

Ni kweli tuna akiba ya dolla billion 6253?
 
Nadhani kwny B ilipaswa kusomeka M

Wewe pengine ndio unakosea maana Rais anasoma hotuba hatoi kichwani kabisa sasa watu hadi wanaandika ni wazi wanajua ukweli na Rais lazima alipitia hotuba kabla ya kusoma! Pengine hicho kiasi kipo kweli hivyo tulipe kabisa madeni!
 
Back
Top Bottom