Hii akiba ya fedha za kigeni dola Bilioni 6,253 aliyosema Rais Samia kiboko, deni la Taifa lingekuwa hela ya peremende

Hii akiba ya fedha za kigeni dola Bilioni 6,253 aliyosema Rais Samia kiboko, deni la Taifa lingekuwa hela ya peremende

Mh Rais kwenye hotuba yake hapo jana kwa wananchi amesema kuwa nchi yetu hadi leo ina akiba ya pesa za kigeni zaidi ya dola billion elfu sita miambili hamsini na tatu (Dola billion 6253)

Ukiangalia hiki kiasi kwa kukifanyia mahesabu utagundua Tanzania ina ukwasi mkubwa sana na tena tunaweza kuihudumia hata Marekani kibajeti na kwa hakika tunapaswa kulipa madeni yote hapo kesho kama kweli hichi kiasi cha pesa kipo chote na kweli kama alivyosema Mh Rais!

Mh Rais hizo hela ulizotaja hata USA awezi kuwanazo kwa haraka!

Ni kweli Mh Rais tuna dola trillion 6+ kama akiba?

Hakika kama ni kweli basi Marekani +China +Japani tunawakaribisha waje kukopa kwetu!

Ni kweli tuna akiba ya dolla billion 6253?
Kwenye ile speech yake (full text) hebu c&p text inayosema hivyo kama ilivyo.
 
Leo Rais Samia wakati akitoa hotuba ya kufunga mwaka 2021 ameitaja akiba ya fedha za kigeni dola za kimarekani bilioni 6,253. Nikajua labda lafudhi ya kizanzibari imenichanganya au kosa la usomaji.

Kumbe ndivyo alivyoandikiwa kwenye hotuba yake, najiuliza mchakato wote wa maandalizi ya hotuba na kwenye mikono iliyopita wameshindwa kung'amua tofauti kubwa hivi ya fedha.

Hizi hela ni zaidi ya trilioni 14,000 za kitanzania, yaani lile deni la trilioni 70 wanalogombania na Ndugai ingekuwa hela ya peremende na sio mboga.

View attachment 2064430
Ni sahihi kwani dola bil 6250 unajua ni shilingi ngapi? Si ni til.14 na huo ndio ukweli..

Acha ujinga mtoa mada ,forex reserves haitumiki kulipa madeni bali kuagiza bidhaa za nje na ku stabilize currency.Tatizo lenu ni mbumbumbu wa uchumi..

Ni mara kadhaa kama huwa mnasoma na kusikiliza bajeti utasikia lugha hiyo ya milioni 3467 nk nk ..

Mpende kujifunza sio kujaza ujinga vichwani
 
Akili za Watawala zimewekezwa kukimbizana na wapinzani tu, basi.
 
Jana tu nilisema aache kusoma hotuba ,,Taifa linaserereka kama gari bovu
 
Kwa hakika kuna watendaji mizigo huko serikalini; ugomvi mkubwa unaoendelea nchini hivi sasa tena baina ya mihimili ya kiutawala ni deni la taifa; Rais vs Speaker.

How comes wanakosa umakini kwenye jambo nyeti kama hili la akiba ya fedha za kigeni kwenye speech muhimu kwa wakati muhimu na msomaji muhimu hivi? Tunadanganywa mangapi kwa uzembe kama huu?
 
Hizo sio hela za umma tu ni pamoja na za sector bijafsi.

Stock ya dola ina maana wakichukua dola zote za serikali, na zile zinazomilikiwa na watu binafsi kwenye bank na bureau ndio unapata akiba ya fedha za kigeni. Kusema serikali ikazilipie deni sio sahihi maana sio hela zake
Naona umeamua kumlisha maneno mama samia.
 
Mwandishi atakuwa Francophone. Wafaransa ndio wanatumia koma kwenye nukta. Yaani kwa Kifaransa bilioni 6,253 = bilioni 6.253. Lakini kusema ukweli Ikulu yetu ni jumba bovu. Nyaraka za Ikulu km vile press release za uteuzi zimejaa typos!!
Speech imeandikwa kwa Kiswahili wala sio kwa Kifaransa. Speech ya juu kabisa katika nchi ni speech ya Rais; haitakiwi kuwa na makandokando ya aina yoyote!

Inatakiwa inyooke kama rula in all aspects; in short ni final. Haitakiwi aje sijui nani baadaye kurekebisha speech ya Rais ikishaenda hewani. Baada ya hapo ni wananchi kutoa maoni yao tu.
 
Back
Top Bottom