Hii ndio mikoa ambayo Rais Samia amewekeza nguvu kubwa kuiletea maendeleo

Nyie kama wakazi wa eneo husika mmechukua hatua gani? Au mkipeww tishet na kofia mnasahau everything?
 
Mkoa wa Mwanza maendeleo gani aliyofanya mama Samia? Mfano miundombinu ya barabara ni mibovu kupindukia hasa ndani ya Wilaya ya Nyamagana
Wewe umezaliwa na kukulia vijijini huko, so mambo yanayofanyika mjini katu hauwezi kuyaona. Utaishia kupinga na kulalamikia usichokijua.
 
Hili nalo neno,huko nasikia kuna mijengo inaporomoshwa kama mvua ya mawe.
Kumbe unasikia tu.. mimi nilifikiri ulikwenda kushuhudia kwa macho yako ili kujiridhisha kuwa unachosikia ni cha kweli au majungu na porojo kutoka kwa wanasiasa uchwara.

Uwe makini na kila unachokisia. Maana hata 2008 ulisikia kuwa Lowasa ni fisadi, alaf 2015 ukaja kusikia kuwa Lowasa sio fisadi. Kibaya waliosema fisadi 2008 ndio hao hao waliosema sio fisadi 2015.
 
Tatizo hela zinatoka Tanganyika kuendeleza nchi jirani ya Zanzibar.
Umeshaandika mwenyew kuwa kila kitu unasikia tu. Hebu weka ushahidi wa hiki ulichoandika hapa.
 
Sasa niende kufanya nini nchi jirani,tena siku hizi wanatutaka tuende na passport.
 
Sasa niende kufanya nini nchi jirani,tena siku hizi wanatutaka tuende na passport.
Mbona mtanganyika anatawala kule bila passport?

Wambie wewe ni mpwa wa raisi wao kutokea Mkuranga.
 
Nyie kama wakazi wa eneo husika mmechukua hatua gani? Au mkipeww tishet na kofia mnasahau everything?
Huenda wakichagua wapinzania pia hawaoni mabadiliko.

Mbowe ameshakuwa mbunge kwa takriban miaka 15, lakini ameshindwa hata kuwachimbia kisima cha kuwashukuru wapiga kura wake waliomchagua miaka yote 15 aliyochaguliwa. Alikuwa anakula bata Dar, alaf ikibaki miezi michache ya uchaguzi ndo anajifanya kwenda kufanya mkutano wa hadhara ili kuwahadaa wamchague tena. Hali hiyo wananchi waliichoka na kupelekea kuzomewa na kurushiwa mawe na wapiga kura wake.

Lisu kakaa bungeni miaka 15, Zito miaka 15 na wengine wengi, lakin hakuna cha maana walichofanya kwenye majimbo yao.
 
Hahaha umejaribu sana ku spin lakin bado natudi pale pale. Eneo husika walishajaribu kuchagua upinzani? ( masuala ya mbowe na lissu kupanda na kushuka hayanihusu, siwazungumzii wao)
 
Hahaha umejaribu sana ku spin lakin bado natudi pale pale. Eneo husika walishajaribu kuchagua upinzani? ( masuala ya mbowe na lissu kupanda na kushuka hayanihusu, siwazungumzii wao)
Ikiwa walijaribu walishindwa kuona matokeo chanya kwa waliojaribu. Inakuaje na wao waendelee kupoteza muda kujaribu.

Cha muhimu ni kuchagua mtu sahihi bila kujali chama. Anaeleta kofia kama haeleweka mnachukua na hamumchagui. Ila kama anaeleweka mnamchagua.
 
Raisi Samia hawezi kushinda Mkoa wowote bila ya kuiba Kura.
 
Karibu tamasha la kizimkazi kusini UNGUJA ufurahie huduma za tigo zantel na mtandao wa 5G tigo zantel imeitika kizimkazi nawe itika 18_25 agost hahaπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„
 
Huwa unatoa wapi hivi VICHEKESHO??πŸ€”πŸ€”πŸ˜…
 
Miradi ya maendeleo katika hiyo mikoa siyo zawadi, wala hisani, ni pesa zetu zinazotokana na kodi, na mikopo ambayo inalipiwa na Kodi zetu.

Kwahiyo wanainchi wataunga mkono chama kutokana na sera.
 
Weka tume huru ya uchaguzi, uone.

Weka Policcm pembeni, ndo utajua kama Kuna upinzani au hamna upinzani 😎😎
 
Karibu tamasha la kizimkazi kusini UNGUJA ufurahie huduma za tigo zantel na mtandao wa 5G tigo zantel imeitika kizimkazi nawe itika 18_25 agost hahaπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„πŸ˜„
1) Kwenye kuchagua viongozi wa chama cha upinzani taifa.. Ni lazima mwenyekiti, makamu, katibu mkuu na viongozi wengine waandamizi watokee kaskazini.

2) Kwenye kuchagua sehemu ya kufanya maandamano ambayo yatasababisha vurugu, biashara za watu kufungwa, watu kupigwa, kujeruhiwa na wengine kupata ulemavu wa kudumu basi ni lazima iwe Mbeya au Songwe.

Yani mpaka leo 2024 watu wa Songwe na Mbeya wameshindwa kujua tu kama wanatumiwa na wanasiasa wa kaskazini kwa faida zao na familia zao. Haitotokea kuona maandamano ya aina hii yanapangwa kutokea Moshi hata siku 1. Sababu watu wa Moshi wanajitambua, hakuna atakaekuwa tayari kufunga biashara yake eti aende akaandamanishwe na Mbowe.
 
Huu ndiyo mkoa pendwa
Ni lini Mbowe ata andaa maandamano Moshi? Au anahofia hayatopata watu? Maana hakuna mtu wa Moshi atakaekuwa tayari kufunga duka lake eti akaandamanishwe na Mbowe ambae walimpa ubunge miaka 15, akawa anaishi zake Dar bila kuwasaidia chochote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…