Hivi inakuwaje mzazi anakua tegemezi Kwa mtoto ambaye amejitafuta Kwa jasho lake bila kumrithisha hata mbuzi mmoja

Hivi inakuwaje mzazi anakua tegemezi Kwa mtoto ambaye amejitafuta Kwa jasho lake bila kumrithisha hata mbuzi mmoja

Naam! Naweza kuwa kubwa jinga lakini ukweli utabaki kuwa UKWELI kwamba genetically (Biologically) wewe ni matokeo ya "kitendo" baina ya baba na mama yako. Hao wawili wasingejichanga nusu baba + nusu mama; wewe usingelikuwepo leo hapa duniani na kutoa maneno ya kifedhuli hivi. Mbona unakufuru kana kwamba ungeweza kujileta duniani i.e. kuwa Hai, Kujiumba na kujizaa mwenyewe? Kumbuka wapo wenye hekima waliowahi kusema Wazazi wako ndo Mungu wako wa hapa duniani -wakikubariki utabarikiwa na wakikulaani utalaanika. Hujawahi kusikia hilo? Tafakari heshima wanayostahili wazazi wako. Usijitutumue na kujiona mjanja hata kidogo mbele ya wazazi wako hata kama wamekuwa na mapungufu mengi kiasi gani.
Mkuu, wewe unaleta huruma za kidini, vitisho na psychological games. Mzazi anayetelekeza mtoto hapaswi kuonewa huruma hata kidogo..
 
Kwaiyo mama yako ulimtafutia wewe baba yako na pale kitandani kipindi cha tendo zile spem ni zako eti, huo ndio mchango kwa mzazi wako muheshimu
 
Mkuu, acha kumtisha mwenzako kwa imani vya hovyo. Mzazi wa hovyo ni lazima atukanwe. Hatulei maradhi sisi..
Dah! Vijana wa cku hizi! Kama kwa mtizamo wako umemwona mzazi wako ni wa hovyo; Labda nikushauri tu kwamba Uwe mnyenyekevu (ujishushe)mbele yake halafu Ongea naye kwa Heshima na Adabu huku ukimweleza hicho unachoona wewe kwamba ndicho kinamfanya aonekane ni wa hovyo na kama inawezekana umwombe ajaribu kurekebisha. Tena ningekushauri usiongee naye wewe uso kwa uso bali uongee naye kwa kupitia rafiki yake au baba/mama yako kama yupo. Epuka kabisa kwa gharama yoyote ile kumtukana mzazi wako. Usifanye kabisa kitendo hicho bro. Nakuomba tafadhali. Gharama yake ni kubwa mno.
 
Kwaiyo mama yako ulimtafutia wewe baba yako na pale kitandani kipindi cha tendo zile spem ni zako eti, huo ndio mchango kwa mzazi wako muheshimu
Kwanini anatelekeza mtoto baada ya kumzaa?? Kwanini anabagua watoto?? Anampa huyu, anamnyima yule??
 
Dah! Vijana wa cku hizi! Kama kwa mtizamo wako umemwona mzazi wako ni wa hovyo; Labda nikushauri tu kwamba Uwe mnyenyekevu (ujishushe)mbele yake halafu Ongea naye kwa Heshima na Adabu huku ukimweleza hicho unachoona wewe kwamba ndicho kinamfanya aonekane ni wa hovyo na kama inawezekana umwombe ajaribu kurekebisha. Tena ningekushauri usiongee naye wewe uso kwa uso bali uongee naye kwa kupitia rafiki yake au baba/mama yako kama yupo. Epuka kabisa kwa gharama yoyote ile kumtukana mzazi wako. Usifanye kabisa kitendo hicho bro. Nakuomba tafadhali. Gharama yake ni kubwa mno.
Acha kunitisha mkuu. Mimi George wa mwaka 2015 na yule wa mwaka 2024 ni watu wawili tofauti kabisa.

Mzazi ana watoto 7. Anauza nyumba kisha anawabagua kwenye mgao. Watoto 4 anawapa, alafu 3 hawapi.

Huyo mzazi pesa imemuisha alafu unataka mimi nimsaidie??..
 
Hapana. Alikuleta kwa Upendo. Unaonaje kama ilipotungwa mimba yako mama yako na baba yako wangelikubaliana kwenda kuiflash? Wamekuwa wavumilivu kwako kukulea/kukutunza kama kitu chenye thamani kubwa hadi leo hii umekuwa mtu mzima halafu unawageukia na kuwatupia madongo vile?
Mkuu, kui flash mimba au kumleta mtoto duniani kisha ateseke kwa kumtelekeza, bora nini??..
 
Mkuu, wewe unaleta huruma za kidini, vitisho na psychological games. Mzazi anayetelekeza mtoto hapaswi kuonewa huruma hata kidogo..
Sijaleta mambo ya huruma za kidini wala vitisho. Mbona mzazi anayetelekeza mtoto bado anayo huruma? Si angeweza kumnyongelea mbali huyo mtoto au kumtupa chooni? Lakini huyo mzazi anako-kachembe ka huruma ndo mana kaona ni kheri nimwache hapa (mahali fulani) watapita watu hapa kumsaidia. Kumbuka Wazazi wengine huwatelekeza watoto huku wazazi hao wenyewe wanalia.
 
Huwa nashangaa unakuta mzazi anakua tegemezi Kwa kijana ambae amejitafuta Kwa jasho na damu amejipata mzazi anakua analandalanda kumnyonya huyu kijana Kwa lengo kwamba amemzaa kwani huyu mzazi yeye alizaa Ili amfanye mtoto punda yaani kiasi kwamba mtoto asipomsaidia mzazi anatangaza kutoa laana wakati na yeye alikua kijana kwahiyo anampa mzigo huyu mtoto baada ya kupambania familia yake anaanza kulea mzazi asiejielewa aisee mtu mweusi akili hana kabisa huu ni udiktekta mambo leo Kwa watoto ukweli usemwe nyie wazee msipende Ganda la ndizi
Acha uzwazwa. Bila mzasi mtoto angekuwapo na hivyo alivyo? Alaaniwe anayewateiekeza wazazi akijiona kajitengeza. Hata hivyo kama mzazi alikutelekeza si vibaya kumtelekeza.
 
Sijaleta mambo ya huruma za kidini wala vitisho. Mbona mzazi anayetelekeza mtoto bado anayo huruma? Si angeweza kumnyongelea mbali huyo mtoto au kumtupa chooni? Lakini huyo mzazi anako-kachembe ka huruma ndo mana kaona ni kheri nimwache hapa (mahali fulani) watapita watu hapa kumsaidia. Kumbuka Wazazi wengine huwatelekeza watoto huku wazazi hao wenyewe wanalia.
Mkuu, kumyongelea mbali, kumtupa chooni, kui flash mimba au kumleta mtoto duniani kisha ateseke kwa kumtelekeza, bora nini??..
 
Nimeiona, sijui unapitia nini? Ila najua unaumia sana kila ukifikiria kumuhusu. Kwa nacho amini mimi:-

Mathayo 6:12 Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.

Ila jifunze kusamehe itakusaidia sio lazima uwe na bond nzuri na mzazi wako. Ndiyo maana nimesema samehe na kusahau. Wenda itaondoa mzigo moyoni mwako ingawa sio lazima.
 
Mkuu, kui flash mimba au kumleta mtoto duniani kisha ateseke kwa kumtelekeza, bora nini??..
Bora mlete mtoto duniani halafu wewe ondoka kwa kifo au kwa kumtoroka mtoto wako i.e. kumtelekeza. Nakuhakikishia 100% atatunzwa, atalelewa na hatopungukiwa chochote hadi awe mtu mzima na kustawi kuliko wewe uliyemtelekeza. Mifano ipo ni mingi tu. Kuflash mimba ni Uuaji sawa kama yalivyo mauaji mengine. Ni ukatili uliokithiri mno kwani mtoto-mimba hawezi kujitetea kwa namna yoyote ile.
 
Mkuu, kumyongelea mbali, kumtupa chooni, kui flash mimba au kumleta mtoto duniani kisha ateseke kwa kumtelekeza, bora nini??..
Hili nimelieleza hapo #178.
Kwa nyongeza tu naomba nikuulize: Kwani ni lazima Mtoto akitelekezwa ateseke? Hebu fafanua anateseka kivipi.
 
Back
Top Bottom