Hizi ni stori za kwenye Biblia ambazo zimeniacha na maswali sana

Hizi ni stori za kwenye Biblia ambazo zimeniacha na maswali sana

Duh
Angalau kwa biblia ila Kuna kitabu hiko Kuna Aya hadi leo inanifikirisha sana na sielewi kwanini wafuasi wake wanakaza shingo kukiamini

Qu'ran 2:97
Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.

Nani ni adui wa Jibril? Jibu ni shetani
Kwanini shetani ateremshe Quran na tunaambiwa kuran ni tukufu?

Hili swali haitatakea nikapata jibu la kuridhika
!
 
Hapo kwa Ayubu, picha linaanza huyo Mungu wenu anamuona Shetani anamuuliza atokako(ni muweza wa yote huyo kumbuka), anamuuliza kama kamuona mtumishi wake Ayubu, like Seriously!? Ina maana hawa wawili sio maadui kama isemwavyo kama wapo.

Hapo bustanini, Mungu hakujua kama Eva angekula tunda na asimuumbe!? Na kwa nini walivyoshindwana na shetani kwa nini asingemuua?


Wacha niwasikilize kwanza Wachokonozi
 
Mimi ni mkristo na ninaamini Mungu yupo na anatenda. Ila kuna mambo ukisoma kwenye biblia lazima ujiulize maswali mengi sana yanayokosa majibu. Leo nitashea nanyi mambo ambayo naona kama yana ukakasi;

1. Kwenye Mwanzo 1:26 imeandikwa kuwa Mungu alisema tuumbe mtu kwa mfano wetu. Nimejiuliza ina maana uumbaji ulifanywa nae kwa kushirikiana na wengine? Hakuwa peke yake? Hao wengine kina nani?

2. Mwanzo 6 - 10 kuna stori maarufu ya Nuhu. Hii ni stori ina ukakasi zaidi. Nikiandika maswali yote niliyojiuliza uzi utakuwa mrefu. Ninashauri mkaisome ili tuifungulie uzi wake.

3. Kutoka 11:5-6 kuna maandiko yanayosema kuwa wazaliwa wa kwanza wote wa wamisri kwa upande wa binadamu hadi wanyama watauwawa na Mungu mwenyewe ili waisraeli wapewe ruhusa ya kwenda nchi ya ahadi. Kiukweli haya yalikuwa ni mauaji ya halaiki kwa wasio na hatia. Unaambiwa hadi mzaliwa wa kwanza wa mbuzi, kuku, ng'ombe, mbwa na farasi waliuwawa. Kwanini isingetumika njia nyingine hao waisraeli wakaondoka?

4. Kitabu kizima cha Joshua kimejaa stori za mauaji matupu. Ikumbukwe Joshua alichukua nafasi ya Musa kwenye kuwaingiza waisraeli nchi ya ahadi baada ya kifo cha Musa. Nchi waliyoahidiwa ilikuwa tayari ina wakazi wake ambao ilibidi wauwawe wote ili kuwapisha waisraeli. Hivi ilishindikana vipi kufanya kama alivyofanya Mama Samia kuwatoa wamasai Ngorongoro na kuwapeleka Msomera kwa amani kabisa bila kumwaga damu? Kama leo 2024 bado kuna maeneo duniani hayajakaliwa na binadamu ilikuwaje enzi za Joshua? Ukisoma kitabu cha Joshua utaona kila sehemu waliyopita walikuwa wakiua wenyeji watakaowakuta. Kulikuwa na sababu zipi za msingi za mauaji haya yote?

5. Ayubu 1:6-12 utaona stori ya shetani alipojiunga na wana wa Mungu kupita mbele ya Mungu kumwabudu hadi Mungu akashangaa imekuwaje shetani akawa eneo lile? Baada ya hapo Mungu na Shetani wakakubaliana kwenda kumjaribu Ayubu kwa sharti la kutogusa mwili wa ajabu (kumuua). Katika yale majaribu watoto wa Ayubu waliuwawa na shetani. Naweza kusema ni mauaji yaliyokuwa na approval toka juu. Ilikuwa kazi maalum. Je, sio kwamba wawili hawa hukutana na kukubaliana baadhi ya mambo? Sio kwamba kuna kazi za shetani zina kibali maalum?
1. Kama umesoma fasihi utaona kwamba maandiko matakatifu na lugha inayotumika kwenye uandishi wa sheria ni lugha tofauti na lugha inayotumika katika uandishi wa vitabu vya sayansi, jiografia, historia au hata kilimo. Maandishi yenye maudhui ya hekima/maana iliyozama huwasilishwa kwa kutumia 'figures of speech' (misemo iliyobeba maana nzito zaidi ya kilichoelezwa) na huhitaji kufasiliwa. Ndiyo maana misemo ya hekima hutumia methali au nahau katika uwasilishaji wake wa ujumbe kwa hadhira husika. Kwenye uandishi wa sheria utakutana na misemo kama: "Judges like Caesar's wife must be beyond reproach" au "Justice must not only be done, it must also seen to be done" au "The accessory does not lead, but follows its principal" au "Where two clauses in a will are repugnant one to the other, the last in order shall prevail" au "He who is first in time has the strongest claim in law" etc. Style hii ya uandishi huwezi kuikuta katika disciplines nyingine. Hali kadhalika Biblia imeandikwa kwa style yake ambayo huwezi kuikuta katika uandishi wa kawaida. "Tufanye mtu kwa mfano wetu" ni style ya uandishi inayoonyesha "ukuu wa Mungu" (majestic/royal language). Katika sheria Judge anakuwa addressed "His lordship/Your lordship" wakati katika ku'address' watu wengine hatutumii lugha ya namna hii. Au pia Rais anakuwa addressed "His/Her Presidency/Excellency" lakini Rais ya Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) au wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) au Dodoma hatutumii "His/Her Presidency/Excellency". Baadhi ya lugha kama Kifaransa rafiki au mtu unayelingana naye cheo au umri unamsalimia "Comment ca va" (sawa na kusema "hujambo")? (katika umoja). Kama unayemsalimia ni mkubwa kwa umri au cheo unamsalimia "Comment les vous" (sawa na kusema "hamjambo")? (katika wingi). Katika lugha ya Chichewa (Malawi) kumsalimia mtu unayelingana naye umri/cheo utasema "mulibwanji?" (sawa na kusema "hujambo"? (katika umoja). Lakini kama anakuzidi umri/cheo utamsalimia "alibwanji" (sawa na kumsema "hawajambo?" (katika wingi).

2. Simulizi la Nuhu pia lina style yake uwasilishaji. Kila character katika uandishi ana style yake ya uandishi, lakini katika yote ni simulizi linaloonyesha kwamba katika yote mwisho wa siku ni Mungu ndiye anayesimama kama mshindi - kwamba nguvu za asili zinaonyesha mwisho wa siku Mungu ndiye mshindi na katika ushindi huo maisha mapya huanza. Kama umesoma literature utakumbuka matumizi ya masimulizi ya 'tragedy' au mambo yanayotisha/kuogopesha lengo lake ni nini? Ni kujenga ujasiri/kuonyesha kwamba wale wanaoweza kustahimili matatizo au magumu ya maisha ndiyo huibuka washindi, wakati wanaokata tamaa wanashindwa hata kabla ya kuanza safari yao.

3. Biblia imeandikwa katika tamaduni mbalimbali ambazo baadhi zilitumia vita kama njia ya kufikia malengo yao (kuwashinda washindani) na funzo tunalolipata katika masimulizi kama haya ni kwamba kama sisi tunaona kwamba anayeshinda katika vita ndiye jemedali/mpampanaji, Mungu ni zaidi ya huyo jemedali/yeye ndiye mshindi wa washindi. Kama unakumbuka Yesu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake kwamba msimwogope "mtu anayeua mwili", bali yule anayeweza "kuua mwili na roho" - maana yake ni kwamba ukiwaona watawala dhalimu usiwaogope kwa sababu hawana uwezo wa kuangamiza roho yako, bali ukimwogopa Mungu ina maana utaendelea kuishi kwa sababu wale wengine hawawezi kuangamiza roho yako.

4. Ukisoma Biblia ni sawa na mtu anayejiangalia kwenye kioo. Ukijiangalia kwenye kioo utaona sura yako, pamoja na kitu chochote kilicho karibu nawe. Biblia ni Neno la Mungu, na imeandikwa katika muktadha wa jamii za waandishi au hadhira yao, yaani ni mambo gani pia yalikuwa katika maisha yao: kama yalikuwa ya furaha yataonyeshwa (kula na kunywa) na kama yalikuwa ya vurugu (mapigano/kulipiza kisasi) na hii ina maana kwamba hata katika jamii zetu tumezungukwa na mambo mengi ya furaha au huzuni ambayo ni sehemu ya yale tunayoyafanya au fanyiana sisi kwa sisi. Ujumbe wa waandishi usingefika kama wasingeandika mambo yaliyokuwa yakitokea katika maisha yao. Mfano, ukisoma 'Kitabu cha Amos' utakuta unyama uliokuwa ukifanywa 'mtu ananunuliwa kwa bei ya kanda mbili', 'baadhi ya watu walikuwa wakichunwa ngozi', hii ni kuonyesha jinsi jamii ilikuwa imekubuhu katika kutenda maovu dhidi ya watu wenzao kwa sababu ya uchu wa mali, lakini pamoja na hayo yote Amosi aliwaasa watu wake kumtegemea Mungu, kwamba hayo yote yatapita na mwisho wa siku Mungu ndiye atakuwa mshindi.

5. Katika Kitabu cha Ayubu, mwandishi anataka kuonyesha pia kwamba hata uteseke vipi kama ukiweka imani yako kwa Mungu (ukiwa na imani thabiti) hakuna atakayeweza kukuungamiza. Shetani kuwa pamoja na 'watoto wa Mungu' ni sawa na pale wanafunzi wake walipomwambia Yesu kuhusu watu wasio na imani na wakamwambia kwamba je angetaka wakaombe moto ushuke kutoka mbinguni uwaangamize? Lakini yeye akasema "hapana, iacheni ngano ikue pamoja na magugu" na siku ya kuvuna, mvunaji ndiye anayeweza kuona vizuri ipi na ngano bora na yapi ni makapi au magugu na ataweza kutenganisha vizuri. Katika maisha yetu pia tunaona mambo mengi yako sambamba na mabaya na wakati mwingine haya mabaya si kwa level ya uovu, lakini hata hivyo yote yanatufundisha kwamba ubaya au uovu hauwezi kuushinda wema. Na ndiyo maana waliomuua Yesu walidhani wamemwangamiza/wamemumaliza kabisa! Lakini alifufuka akiwa na nguvu/uwezo zaidi wa hata kuweza kupita kwenye mlango uliofungwa bila kufunguliwa - yaana ana mwili ambao haufungwi tena na laws of nature, uwezo ambao hao waliomuua hawana. Hivyo, soma Biblia kwa lengo la kupata ujumbe na siyo kukwama kwenye matukio. Mfano, 'mwezi ukiwa bado mchanga' kabla haujaonekana vizuri mtu akiwahi kukuonyesha kwa kidole "mwezi ule..." usibaki ukiangalia kidole chake, jaribu kufuatisha kidole kule anakokuelekeza ndiko utakapopata huo mwezi na siyo kwenye kidole chake. Hata matukio yaliyo kwenye Biblia yana lengo moja la kutuelekeza/yanatupa ujumbe fulani ambao inabidi tuutafakari na siyo kubaki kwenye hayo matukio, maana tukifanya hivyo hatutapata ujumbe uliokusudiwa.
 
Mimi ni mkristo na ninaamini Mungu yupo na anatenda. Ila kuna mambo ukisoma kwenye biblia lazima ujiulize maswali mengi sana yanayokosa majibu. Leo nitashea nanyi mambo ambayo naona kama yana ukakasi;

1. Kwenye Mwanzo 1:26 imeandikwa kuwa Mungu alisema tuumbe mtu kwa mfano wetu. Nimejiuliza ina maana uumbaji ulifanywa nae kwa kushirikiana na wengine? Hakuwa peke yake? Hao wengine kina nani?

2. Mwanzo 6 - 10 kuna stori maarufu ya Nuhu. Hii ni stori ina ukakasi zaidi. Nikiandika maswali yote niliyojiuliza uzi utakuwa mrefu. Ninashauri mkaisome ili tuifungulie uzi wake.

3. Kutoka 11:5-6 kuna maandiko yanayosema kuwa wazaliwa wa kwanza wote wa wamisri kwa upande wa binadamu hadi wanyama watauwawa na Mungu mwenyewe ili waisraeli wapewe ruhusa ya kwenda nchi ya ahadi. Kiukweli haya yalikuwa ni mauaji ya halaiki kwa wasio na hatia. Unaambiwa hadi mzaliwa wa kwanza wa mbuzi, kuku, ng'ombe, mbwa na farasi waliuwawa. Kwanini isingetumika njia nyingine hao waisraeli wakaondoka?

4. Kitabu kizima cha Joshua kimejaa stori za mauaji matupu. Ikumbukwe Joshua alichukua nafasi ya Musa kwenye kuwaingiza waisraeli nchi ya ahadi baada ya kifo cha Musa. Nchi waliyoahidiwa ilikuwa tayari ina wakazi wake ambao ilibidi wauwawe wote ili kuwapisha waisraeli. Hivi ilishindikana vipi kufanya kama alivyofanya Mama Samia kuwatoa wamasai Ngorongoro na kuwapeleka Msomera kwa amani kabisa bila kumwaga damu? Kama leo 2024 bado kuna maeneo duniani hayajakaliwa na binadamu ilikuwaje enzi za Joshua? Ukisoma kitabu cha Joshua utaona kila sehemu waliyopita walikuwa wakiua wenyeji watakaowakuta. Kulikuwa na sababu zipi za msingi za mauaji haya yote?

5. Ayubu 1:6-12 utaona stori ya shetani alipojiunga na wana wa Mungu kupita mbele ya Mungu kumwabudu hadi Mungu akashangaa imekuwaje shetani akawa eneo lile? Baada ya hapo Mungu na Shetani wakakubaliana kwenda kumjaribu Ayubu kwa sharti la kutogusa mwili wa ajabu (kumuua). Katika yale majaribu watoto wa Ayubu waliuwawa na shetani. Naweza kusema ni mauaji yaliyokuwa na approval toka juu. Ilikuwa kazi maalum. Je, sio kwamba wawili hawa hukutana na kukubaliana baadhi ya mambo? Sio kwamba kuna kazi za shetani zina kibali maalum?
1. Mungu katika nafsi tatu: Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu
2. Hakuna ukakasi wowote endapo utaisoma na kulielewa
3. Mzaliwa wa kwanza wa Kimisri alikuwa akitumika kama madhabahu ya mungu wa Kimisri. Kwa hiyo kilichofanyika katika hilo tukio ni kuziharibu madhabahu za Mungu ya Kimisri
4. Siyo kweli kwamba wote waliuawa. Kuna Wagibeoni. Wao walipotambua kuwa Mungu Muumbaji wa vyote Yupo upande wa Wana wa Israeli, walifanya nao agano la amani. Waliouawa ni wale waliokaidi kulitilia Neno la Mungu
5. Ayubu alifungua mwenyewe mlango wa majaribu kwa njia ya hofu (Ayubu 3:25). Vinginevyo , Shetani asingefua dafu kwake.
 
Kwanza umelidharau sana neno la Mungu kwa kuanzia
Unaita neno la Mungu stori yani MASTORI
Alafu unatarajia utapata ufunuo wake
 
Biblia ni kitabu cha kweli na MUNGU anayetajwa kwenye hicho kitabu ndiye MUNGU wa kweli.

Sijajua kuhusu Quran mana sijawahi hata kuishika, ila huwa nasikia baadhi ya aya zake zikitajwa na watu mbali mbali.

Watu wanaosema Biblia ni kitabu kilicho jaa janja - janja ni wale ambao hawajawahi hata kuombea watu wenye mapepo na yakatoka.

Mtu mwenye mapepo anaweza akakusemesha baadhi ya mambo yaliyoko kwenye Bible.
Alafu baadaye ukija kumuuliza huyo mtu kuhusu hayo mambo alokuwa anakusemesha atakuambia Mimi sijaongea na wewe kuhusu hayo mambo.
Hi imewahi kunikuta zaidi ya maramoja.

Mimi sio Pastor ila watu wengi huwa wananiamini na sijaandika ili kubishana na watu ila nimeandika mambo ambayo nimewahi kukutana nayo.
 
1. Kama umesoma fasihi utaona kwamba maandiko matakatifu na lugha inayotumika kwenye uandishi wa sheria ni lugha tofauti na lugha inayotumika katika uandishi wa vitabu vya sayansi, jiografia, historia au hata kilimo. Maandishi yenye maudhui ya hekima/maana iliyozama huwasilishwa kwa kutumia 'figures of speech' (misemo iliyobeba maana nzito zaidi ya kilichoelezwa) na huhitaji kufasiliwa. Ndiyo maana misemo ya hekima hutumia methali au nahau katika uwasilishaji wake wa ujumbe kwa hadhira husika. Kwenye uandishi wa sheria utakutana na misemo kama: "Judges like Caesar's wife must be beyond reproach" au "Justice must not only be done, it must also seen to be done" au "The accessory does not lead, but follows its principal" au "Where two clauses in a will are repugnant one to the other, the last in order shall prevail" au "He who is first in time has the strongest claim in law" etc. Style hii ya uandishi huwezi kuikuta katika disciplines nyingine. Hali kadhalika Biblia imeandikwa kwa style yake ambayo huwezi kuikuta katika uandishi wa kawaida. "Tufanye mtu kwa mfano wetu" ni style ya uandishi inayoonyesha "ukuu wa Mungu" (majestic/royal language). Katika sheria Judge anakuwa addressed "His lordship/Your lordship" wakati katika ku'address' watu wengine hatutumii lugha ya namna hii. Au pia Rais anakuwa addressed "His/Her Presidency/Excellency" lakini Rais ya Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) au wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) au Dodoma hatutumii "His/Her Presidency/Excellency". Baadhi ya lugha kama Kifaransa rafiki au mtu unayelingana naye cheo au umri unamsalimia "Comment ca va" (sawa na kusema "hujambo")? (katika umoja). Kama unayemsalimia ni mkubwa kwa umri au cheo unamsalimia "Comment les vous" (sawa na kusema "hamjambo")? (katika wingi). Katika lugha ya Chichewa (Malawi) kumsalimia mtu unayelingana naye umri/cheo utasema "mulibwanji?" (sawa na kusema "hujambo"? (katika umoja). Lakini kama anakuzidi umri/cheo utamsalimia "alibwanji" (sawa na kumsema "hawajambo?" (katika wingi).

2. Simulizi la Nuhu pia lina style yake uwasilishaji. Kila character katika uandishi ana style yake ya uandishi, lakini katika yote ni simulizi linaloonyesha kwamba katika yote mwisho wa siku ni Mungu ndiye anayesimama kama mshindi - kwamba nguvu za asili zinaonyesha mwisho wa siku Mungu ndiye mshindi na katika ushindi huo maisha mapya huanza. Kama umesoma literature utakumbuka matumizi ya masimulizi ya 'tragedy' au mambo yanayotisha/kuogopesha lengo lake ni nini? Ni kujenga ujasiri/kuonyesha kwamba wale wanaoweza kustahimili matatizo au magumu ya maisha ndiyo huibuka washindi, wakati wanaokata tamaa wanashindwa hata kabla ya kuanza safari yao.

3. Biblia imeandikwa katika tamaduni mbalimbali ambazo baadhi zilitumia vita kama njia ya kufikia malengo yao (kuwashinda washindani) na funzo tunalolipata katika masimulizi kama haya ni kwamba kama sisi tunaona kwamba anayeshinda katika vita ndiye jemedali/mpampanaji, Mungu ni zaidi ya huyo jemedali/yeye ndiye mshindi wa washindi. Kama unakumbuka Yesu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake kwamba msimwogope "mtu anayeua mwili", bali yule anayeweza "kuua mwili na roho" - maana yake ni kwamba ukiwaona watawala dhalimu usiwaogope kwa sababu hawana uwezo wa kuangamiza roho yako, bali ukimwogopa Mungu ina maana utaendelea kuishi kwa sababu wale wengine hawawezi kuangamiza roho yako.

4. Ukisoma Biblia ni sawa na mtu anayejiangalia kwenye kioo. Ukijiangalia kwenye kioo utaona sura yako, pamoja na kitu chochote kilicho karibu nawe. Biblia ni Neno la Mungu, na imeandikwa katika muktadha wa jamii za waandishi au hadhira yao, yaani ni mambo gani pia yalikuwa katika maisha yao: kama yalikuwa ya furaha yataonyeshwa (kula na kunywa) na kama yalikuwa ya vurugu (mapigano/kulipiza kisasi) na hii ina maana kwamba hata katika jamii zetu tumezungukwa na mambo mengi ya furaha au huzuni ambayo ni sehemu ya yale tunayoyafanya au fanyiana sisi kwa sisi. Ujumbe wa waandishi usingefika kama wasingeandika mambo yaliyokuwa yakitokea katika maisha yao. Mfano, ukisoma 'Kitabu cha Amos' utakuta unyama uliokuwa ukifanywa 'mtu ananunuliwa kwa bei ya kanda mbili', 'baadhi ya watu walikuwa wakichunwa ngozi', hii ni kuonyesha jinsi jamii ilikuwa imekubuhu katika kutenda maovu dhidi ya watu wenzao kwa sababu ya uchu wa mali, lakini pamoja na hayo yote Amosi aliwaasa watu wake kumtegemea Mungu, kwamba hayo yote yatapita na mwisho wa siku Mungu ndiye atakuwa mshindi.

5. Katika Kitabu cha Ayubu, mwandishi anataka kuonyesha pia kwamba hata uteseke vipi kama ukiweka imani yako kwa Mungu (ukiwa na imani thabiti) hakuna atakayeweza kukuungamiza. Shetani kuwa pamoja na 'watoto wa Mungu' ni sawa na pale wanafunzi wake walipomwambia Yesu kuhusu watu wasio na imani na wakamwambia kwamba je angetaka wakaombe moto ushuke kutoka mbinguni uwaangamize? Lakini yeye akasema "hapana, iacheni ngano ikue pamoja na magugu" na siku ya kuvuna, mvunaji ndiye anayeweza kuona vizuri ipi na ngano bora na yapi ni makapi au magugu na ataweza kutenganisha vizuri. Katika maisha yetu pia tunaona mambo mengi yako sambamba na mabaya na wakati mwingine haya mabaya si kwa level ya uovu, lakini hata hivyo yote yanatufundisha kwamba ubaya au uovu hauwezi kuushinda wema. Na ndiyo maana waliomuua Yesu walidhani wamemwangamiza/wamemumaliza kabisa! Lakini alifufuka akiwa na nguvu/uwezo zaidi wa hata kuweza kupita kwenye mlango uliofungwa bila kufunguliwa - yaana ana mwili ambao haufungwi tena na laws of nature, uwezo ambao hao waliomuua hawana. Hivyo, soma Biblia kwa lengo la kupata ujumbe na siyo kukwama kwenye matukio. Mfano, 'mwezi ukiwa bado mchanga' kabla haujaonekana vizuri mtu akiwahi kukuonyesha kwa kidole "mwezi ule..." usibaki ukiangalia kidole chake, jaribu kufuatisha kidole kule anakokuelekeza ndiko utakapopata huo mwezi na siyo kwenye kidole chake. Hata matukio yaliyo kwenye Biblia yana lengo moja la kutuelekeza/yanatupa ujumbe fulani ambao inabidi tuutafakari na siyo kubaki kwenye hayo matukio, maana tukifanya hivyo hatutapata ujumbe uliokusudiwa.
Pumba tupu
 
1. Mungu katika nafasi tatu: Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu
2. Hakuna ukakasi wowote endapo utaisoma na kulielewa
3. Mzaliwa wa kwanza wa Kimisri alikuwa akitumika kama madhabahu ya mungu wa Kimisri. Kwa hiyo kilichofanyika katika hilo tukio ni kuziharibu madhabahu za Mungu ya Kimisri
4. Siyo kweli kwamba wote waliuawa. Kuna Wagibeoni. Wao walipotambua kuwa Mungu Muumbaji wa vyote Yupo upande wa Wana wa Israeli, walifanya nao agano la amani. Waliouawa ni wale waliokaidi kulitilia Neno la Mungu
5. Ayubu alifungua mwenyewe mlango wa majaribu kwa njia ya hofu (Ayubu 3:25). Vinginevyo , Shetani asingefua dafu kwake.
Mtoto wako akiuwawa na ukaambiwa alikuwa madhabahu utakubali ni sahihi? Akija mtu hapo kwenu na kuwaondoa kinguvu kwamba katumwa na Mungu utakubali?
 
Mtoto wako akiuwawa na ukaambiwa alikuwa madhabahu utakubali ni sahihi? Akija mtu hapo kwenu na kuwaondoa kinguvu kwamba katumwa na Mungu utakubali?
Hakuna haja ya kuwauawa watu wenye mapepo kwa sasa kwa sababu Jina la Yesu Lipo. Unalikemea pepo linatoka na mtu anabaki huru.
 
Angalau kwa biblia ila Kuna kitabu hiko Kuna Aya hadi leo inanifikirisha sana na sielewi kwanini wafuasi wake wanakaza shingo kukiamini

Qu'ran 2:97
Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.

Nani ni adui wa Jibril? Jibu ni shetani
Kwanini shetani ateremshe Quran na tunaambiwa kuran ni tukufu?

Hili swali haitatakea nikapata jibu la kuridhika
Say, ˹O Prophet,˺ “Whoever is an enemy of Gabriel should know that he revealed this ˹Quran˺ to your heart by Allah’s Will, confirming what came before it—a guide and good news for the believers.”
 
Anayenisaidia kuelewa Mambo ya Kiroho ni Roho Mtakatifu....!

Yote yaliwezekana baada ya kuacha kuufanya Moyo wangu kuwa Mgumu, nilifungua Moyo wangu, nikajikuta naanza kuelewa Mambo ya Ulimwengu wa Roho...!

Maisha yetu yanaanzia kwenye Ulimwengu wa Roho, kila kinachotokea kwenye Ulimwengu wa Mwili, kilianzia kwenye Ulimwengu wa Roho..!

Ndo maana Biblia inasema Kwa Wenye Akili (Wanaotumia Akili za Kibinadamu) habari ya Mungu kwao ni Upumbavu...!
Na udhibitisho wa ukisemacho unao wewe tu!
 
Back
Top Bottom