mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,227
- 6,670
Sipo kusapoti utegemez!! Napinga pale mtu anakuja na kualaum viongoz kwenda nje na kuomba msaada, kwasaab huu ni utegemez umewekewa mizizi tang enzi za mwalimu. Kama Taifa kwa watawala hawana dira ya Taifa kutuondoa taratibu kweny huu utegemez, so huez laumu wa sasa kwann aende nje kuomba msaada! Hata kipind cha Mwendazake staili ile ya kupiga vita wazungu haikupaswa. Ilitakiwa aweke misingi kimya kimya ya kuja kuondoa utegemez lkn haitakua haraka na rahisi tu, utawala tang enzi ulipaswa uweke misingi ya muda mref ya kujikwamua na utegemez.
Nakubaliana nawe kuwa UTEGEMEZI ni hulka ya viongozi wengi wa nchi maskini. Ni utegemezi ambao umeasisiwa na Wakoloni na unaendelezwa katika ukoloni mamboleo, kwa Sera za Biashara Huria na Utandawazi.
Sikubaliani na wewe kuhusu alichofanya Mwendazake kuwa ilitakiwa aweke misingi kimya kimya ya kuja kuondoa utegemezi. Miradi ya kimkakati na ujenzi wa miundombinu ya usafiri wa ardhini, maji na angani, aliyosimamia ni nguzo kuu ya kuchochea ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa. Kwa mfano barabara bora na imara zinamwezesha mkulima, mvuvi, mwenye kiwanda na mfanya biashara kusafirisha mazao/bidhaa kwa haraka na gharama nafuu. Pia kuwepo kwa barabara bora na imara kunapanua soko la mazao/bidhaa. HUO NDIO MSINGI WA KUJITEGEMEA