Huu haukuwa muda muafaka wa Rais Samia kutembelea Marekani: Amejiweka kwenye Shinikizo la kulazimishwa kuilaani Urusi

Tanzania ilikuwa na msimamo wakati wa Nyerere; baada ya hapo ni bendera fata upepo.
Inategemea suala linahusu nini, balozi wetu aliuweka wazi msimamo wetu na video ilikuwa inatembea mwezi ule ule vita ilipoanza kule Ukraine.
 
Halafu sijui huko atapokelewa na nani pale airport! Maana kiprotocol ni Rais hupokelewa na Rais! Je Rais Biden ataenda kumpokea? Kinyume Cha hapo ni fedheha Sana kwa Tanzania!
Kikwete aliwahi kwenda Australia akaishia kupokelewa na Mayor wa mji(huyo Ni diwani tu).
 
Msiwe mnaropoka mambo msiyoyajua. Wewe ni mwongo mkubwa.

Hivi unajua kuwa kutoka kwa Mandela gerezani ilikuwa ni baada ya Marekani kuuwekea vikwazo utawala wa makaburu? Marekani haikuwahi kutamka kuwa Mandela au kiongpzi yeyote wa ANC ni gaidi.

Urusi haikuwahi kuzisaidia nchi za Afrika kupata uhuru. Bali wapigania uhuru wa Afrika, walikuwa wakinunua silaha toka Urusi kwa sababu ya unafuu wa bei. Urusi mchango wake kwa Afrika, iwe wakati kupigania uhuru au baada ya uhuru, ni minimum. Nchi ambayo ilikuwa na msaada kwa Afrika katika kupugania uhuru ni Kyuba, siyo Urusi.

Kitu pekee ambacho Urusi ilikuwa ikikitoa kwa nchi za Afrika ni nafasi za masomo.
 
Udhalimu ni udhalimu tu ufanywe kwa mwafrika au kwa mzungu.Mrusi anaua watoto,wazee na hata kubaka raia wa ukraine kwa sababu ya MAAMUZI yao kutaka kujiunga na umoja wa ulaya .Kwani kuna kosa gani hapo?Mbona sisi tulijiunga na zanzibar na jumiaya ya Afrika mashariki?Kama ungekuwa unangalia aljazira france24 na cnn pengine ungewaombea waukraine Mungu awaepushe na hii kamanyola
 
Yaani usifanye mambo yako kisa mtu mmoja tu aliyeamua kumvamia mwingine kwa ajili ya ego yake?
Kwani kuilaani Urusi, kama inatenda unyama, kuna hasara gani? Ni nini huwa unakipata kutoka Urusi kinachokufanya upate hofu ya kusimama katika Ukweli?

Israel ilitujengea UDSM, ilituanzishia JKT, iligharamia sana mafunzo ya wanajeshi na wataalam wa kilimo, lakini walipowaua Wapalestina tuliwalaani vikali, na kuvunja mahusiano ya Kibalozi. Sasa Mrusi anayewaua wananchi wasio na hatia, kwa nini tusimlaani?
 
Labda waliona hadhi yake ni sawa ni diwani wa huko kwao πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†
😁😁😁😁 alifulululiza kwenda huko jamaa wakaona huyu tukifuata mambo ya protocol kila siku hatuwezi,atapokelewa na diwani tu.
 
Tatizo una uelewa mdogo.

Huwezi kuilaani US kwa vita ya Iraq, ilikuwa ni UN resolution. Nchi zaidi ya 50 zilishiriki kwenye vita ile. Ukitaka kulaani, ilaani UN Assembly ambayo na Tz ni mwanachama.
 
Futari ya burger, haa haa aiseee!
 
Usidhani ukiandika upuuzi kwa Kiingereza huwa unabadilika
 
Mimi nasuburi nione mwenyeji wake atakayempokea ni nani? Itakuwa fedheha Sana kwa Nchi yetu Kama hatapokelewa na Rais Biden!
Kwani lengo ni kupokelewa? Hivi Rais wa TZ, ni sawa na Rais wa US?
 
Yaani usifanye mambo yako kisa mtu mmoja tu aliyeamua kumvamia mwingine kwa ajili ya ego yake?
"...kwa ajili ya ego yake?"
Unaonyesha usivyoelewa haya mambo. Nilitaka kutumia neno 'mjinga', ambalo ni sahihi zaidi, lakini nimeona niwe mpole.
Watu kama nyinyi msioelewa kitu chochote katika siasa za dunia, halafu mnajiweka mbele mbele kuzungumzia msiyoyafahamu ni hatari sana kwa taifa letu.
 
Fikra za utegemezi hazitatuondolea kero za maendeleo. Swali la msingi tangu tumepata uhuru tumekuwa tukitegemea na kupewa misaada, je, imetuondolea umaskini?
Ngekosa hiyo misaada, hata hivyo vibarabara vya lami ungeviona? Bila misaada ya hawa watu, hali ingekuwa mbaya zaidi. Sababu kubwa ya umaskini wetu ni kichwani.
 
Anapokelewa na waziri wa mambo ya nje, huo ndio utamaduni wa Marekani, sio Samia tu, hata marais wengine

Waziri wa mambo ya nje wa U.S.A is busy na mambo ya UKRAINE; pengine atapokelewa na balozi wetu huko Marekani!!
 

Ukiona adui yako anakusifia UJUE una mapungufu!!! Wazungu hawawezi kumsifia mtu mwenye akili kuliko wao!!!
 
Wewe unajua ameenda kufanya nini?mbona mna midomo kama nyuchi za chura?
 
Inabidi kujiuliza kama safari ni State visit au safari ya aina nyingine (official visit, official working visit) n.k. Zote hizi zina itifaki yake. Kama ulivyoandika, mara nyingi safari hizi za wakuu wa nchi hupangwa kwa muda mrefu na agenda za mazungumzo zinakuwa zinajulikana na wahusika (japokuwa kuna kuchomekea issues, ila ni rahisi kupangua). Mtihani upo iwapo kunamkutano na waandishi wa habari maana hawa hawana simile.
Hivyo kabla watu hawajaanza kulalamika na kutoa hitimisho zao ni vyema kupata taarifa za ziada za safari husika.
 
Nakuelewa sana ndugu yangu. Yes wakati wa press conference kuna maswali ya kuchomekea kimkakati, ila naamini jibu lake ni simple tu, msimamo wa nchi. Kikubwa amani amani ya dunia.
 
...she will not be able to standup against the wishes of the American Government,which is infact Satans' right hand arm.
Umemaliza mkuu; na sifa kuu za shetani ni ulaghai na uuaji.

Hata hivyo mwisho wake hauko mbali. Ukiona hata watu wake wa karibu miaka yote kama saudia wanaanza kumgeuka, fahamu kuwa hali si shwari.
 
Kama tutapata mpunga Bora ailaani,ikumbukwe Tanzania ilikuwa inapata pesa nyingi sana tukiwa MCC..

Sisi wa Kigoma tulipata umeme via mcc,sisi wa Rukwa tulioata lami kutoka msaada wa MCC na miradi mingine kama hiyo..

Kama US wataturudisha kwenye MCC mama asichelewe kuilaani hiyo Russia maana haina msaada wowote wa maana kiuchumi kwa Tanzania..

Huyo Mpuuzi Putin na Russia ndio wanatuletea ushenzi wa kuvurugika kwa uchumi Duniani

Binafsi nitasimama upande wa Beberu daima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…