Huyu Wenje mbona anazidi kumuharibia Mbowe, kama amechangia 250M Mkutano Mkuu wa Taifa nani amechangia mikutano mikuu 64,000 ya misingi nchi nzima?

Huyu Wenje mbona anazidi kumuharibia Mbowe, kama amechangia 250M Mkutano Mkuu wa Taifa nani amechangia mikutano mikuu 64,000 ya misingi nchi nzima?

View attachment 3189332
Kamanda Wenje mbona unazidi kumuanika na kumuharibia kabisa kamanda Mbowe,

Umesema CHADEMA hatuna pesa ni kweli hatuna lakini kwanini hatuna pesa?Jibu wahisani hawamwamini tena Mbowe.

Naomba unijubu maswali haya,

1. Je, mikutano mikuu yote ya misingi zaidi ya 64,274 nchi nzima ni Mbowe katoa pesa zake?

2. Je, mikutano mikuu yote ya matawi zaidi 16,602 ni Mbowe ametoa pesa zake?

3. Je, mikutano mikuu yote ya kata zaidi ya 3,956 ni Mbowe katoa Pesa zake?

4. Je, mikutano mikuu ya majimbo yote 264 katoa pesa Mbowe?

5. Je, mikutano mikuu ya Mikoa yote 31 ni Mbowe katoa Pesa zake?

6. Je, mikutano mikuu yote 10 ya Kanda za Chama ni Mbowe katoa Pesa zake?

7. Sasa Wenje, kama hawa wanachama waliogharamia mikutano mikuu yao yote tangu misingi mpaka Kanda wanashindwaje kujigharamia kwenye mkutano Mkuu wao huu maalum mmoja tu wa Taifa?

Mwisho, Mkutano Mkuu wa mwaka 2019 Mbowe aliichangia kiasi gani mbona hujasema??!!

Mbowe kwanini hakuchangia 2019 achangie 2024?!!

Hii TZS250M ni rushwa toka CCM


Hakuna namna Mbowe ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA lazima apishe akili mpya za kutafuta pesa sio kuchangisha wajumbe wa Kamati Kuu kwani hilo sio jukumu la mjumbe wa Kamati Kuu.


Huyu ni mchumba wa abdul
 
Kuagizwa kutafuta pesa kutoka wapi kwa kificho kama sio kufungua mlango wa pesa za Abdul na Mama yake kuingia ndani ya chama...?

Miaka yote taratibu na mipango ya kutafuta pesa za kuendesha au kugharamia shughuli fulani ndani ya CHADEMA mfano kampeni, uchaguzi nk hufanyika kwa uwazi (transparently) kwa njia ya harambee, michango nk na kila mtu kusema kwa uwazi. Leo imekuwaje mambo yafanyike gizani...?

Hiki ndicho ambacho wanachama na wapenzi wa CHADEMA wanakishitukia. Tunatafuta ushahidi wa rushwa wakati kila kitu Kiko wazi...?

Hawa waliopewa kazi ya kutafuta pesa kwa njia ya kificho, wanatumia njia gani kizipata ambazo wakiziweka wazi tutakubaliana nao..?

Hivi wewe, kwa mfano, umwambie mtu kama Hezekiah Wenje akatafute TZS 30,000,000; atazipataje kwa kufikiria tu....

By the way, si unajua kuwa yeye (Wenje) ni kiongozi mkuu wa Kanda ya Ziwa Victoria?
..?

Ana influence na uwezo kuamusha hamasa au siyo...?

Je, unadhani kwa influence yake hiyo ana uweza ku - influence wanachama, wapenzi na mashabiki wa CHADEMA ktk Kanda yake kuchangia pesa hiyo (30M) tu ili kugharamia shughuli za chama kwenye Kanda yake...? Anaweza...????

Acheni ujinga wa kujaribu kudanganya watu wazima wenye akili timamu
Mbona Lissu amekuwa akichangiwa na mpaka naxCCM au hujui hata hela za kununua gari na za matibabu alichangiwa je ilikuwa rushwa?

Maamuzi ya kanati kuu unayaita maamuzi ya gizani inaonyesha huna uwezo wa kudadavua mambo ni ushabiki tu. Hivi baraza la mawaziri kwa mfano wakiamua au kujadili jambo huwa huku nje wananchi wanajua kilichozungumzwa. Basi nini maana ya vikao kama kila kinachozungumzwa katika kikao kiwe wazi kwa umma wote.

Hata Marekani wamemaliza uchaguzi majuzi mbona vyama vimechangiwa na matajiri? CCM wakitaka kufanya mkutano wao mkuu huea wanachangiwa na wafanyabiashara kwani hawana wanachama na vitegauchumi kibao.

Hujui namna ofisi zinavyoendeshwa shughuli ziinavyopangwa ambazo zinaweza kuwa katika horizon ya miaka 1, 5 au hata zaidi mfano dira ya taifa miaka 25.

Rudi jifunze namna ofisi zinavyoendeshwa. Wenzako sisi tumezeekea humo tukipanga kuanzia strategic plans, programme , projects,, budgets, action plans na kuchambua maandiko mbalimbali na kushauri .
 
Moja ya kosa kubwa analofanya Mbowe ni kumweka mbele mtu mjinga jinga kama Wenje, Wenje ni muongo muongo asiye na kumbukumbu nzuri kuwa marehemu chacha wangwe alimtuhumu Mbowe kuchukua pesa za chama anajimilikisha kisha huchukua hiyo hiyo pesa na kujidai kukopesha chama kienyeji pasipo na mpangilio wala Takwimu, Hutakatisha pesa alizoiba kwenye cha kuwa kujidai ameikopesha chadema, Mbowe siyo Tajiri ni mtu wa kawaida anapata wapi pesa za kukopesha chama au kuhudumia chama?mbowe ni mwizi wa pesa za chama ikiwemo pesa zote za misaada toka kwa wahisani, na sasa anatumia hiyo pesa kugawa kwa Wajumbe wamsaidie kununua uenyekiti kwa njia haramu za kuiba kura na uchakachuaji
 
7. Sasa Wenje, kama hawa wanachama waliogharamia mikutano mikuu yao yote tangu misingi mpaka Kanda wanashindwaje kujigharamia kwenye mkutano Mkuu wao huu maalum mmoja tu wa Taifa?
  • Uchaguzi wa tawi unagharamiwa na wadau wa tawi
  • ULchaguzi wa wilaya unagharamiwa na wadau wa wilaya
  • Uchaguzi wa mkoa unagharamiwa na wadau wa mkoa
  • Uchaguzi wa kanda unagharamiwa na wadau wa kanda
  • Uchaguzi wa taifa unagharamiwa na wadau wa taifa

 
Dalali Wenje ndiyo anazidi kuyatimba akiamini anamsaidia Sultan Mbowe
 
Lissu kapewa mwongozo wa kuchangia wastani wa tsh 30 million kwaajili ya mkutano mkuu.Mpaka leo hajatoa hata ndururu.

Wajumbe wote wa Kamati Kuu wamepewa wajibu wa kukusanya fedha za mkutano mkuu.

Lissu kama mgombea nafasi ya Mwenyekiti alitakiwa kuchangia chama.

Kwa lugha rahisi Mbowe katoa fedha za kulipa wajumbe ambao wengine watampigia Lissu kura.

Lissu kazi yake ni kupiga domo huko Club house ambao hata kuchangia 1 million hawawezi.
 
Lisu aliomba msaada wa kupata pesa za kutengeneza gari baada ya mbowe kumzungusha sana kila akiomba pesa Mbowe anamzungusha kwani Account ya chama anayo mbowe mwenyewe ndiyo mhasibu idara ya pesa za chama ni Mbowe peke yake hata katibu mkuu wa chama Mnyika hana mamlaka na pesa za chama akitaka pesa huomba kwa mbowe na hata akipewa hapewi kwa mda atapewa kwa mbinde sana tena pungufu, Mbowe ni mwizi wa pesa za chama kwani hakuna anayejua kwenye A/C kuna shilling ngapi akiba ya chama zaidi ya mbowe binafsi, chadema ni Duka na saccos ya mbowe binafsi
 
Chacha Wangwe alimwambia aonyeshe wapi na wapi alikikopesha chama na kwa kufuata utaribu upi!

Na hicho kiasi anachokidai aonyeshe matumizi mchanganuo wake pamoja na risiti halali!

Mbowe anakuja tu anasema nimekikopesha chama!

Ajabu marehemu Wenje kufuatilia anaona gharama alizozitoza Mbowe anatoza kwa viwango vya mtalii anavyotozwa.

Na hata pesa alizozitumia kununulia baadhi ya vitendea kazi kwa ajili ya Chama ambavyo Mbowe anasema alitumia pesa yake kuikopesha ofisi, amejibinafsishia na kuwa vya kwake binafsi na si vya chama.

Huyu Mbowe tulichelewa kumjua!
Mbowe maji ya shingo...
 
Chadema ni Duka na saccos za mbowe binafsi sasa Dalali Wenje kaamua kumteketeza Mbowe pasipo kujua kuwa anamdhoofisha Mbowe, yeye anaongea hovyo akizani anamchafua Lisu kumbe anamchafua Mbowe zaidi
 
Siasa ni pesa hata pale USA Trump katumia hela kibao,na wanakuambia kama hauna hela utaishia kuimba rushwa rushwa na kumlaumu shetwani.Bila pesa vyama haviendi,mdio maana JK Nyerere aliamzisha miradi ya vyama
 
Rudi kasikilize clip vizuri.
Usiwe mjuaji wakati hata uwezo wa kuelewa huna.

Mbowe sio kamati kuu, kamati kuu imeamua namna ya kupata fedha za mkutano, huyo Lissu wako ni mjumbe wa kanati kuu .

Kutokana na deficit kila mjumbe amepangiwa kuasi cha kutafuta na kuleta Lissu wako amepangiwa sh milioni 30 na hajatoa hata shilingi. Sasa ulitaka mkutano mkuu usifanyike?

Ulivyo huna akili eti unasema wajumbe wanaweza kujisafirisha yaani huelewi taasisi inavyofanya kazi. Kila jambo huamuliwa na mwenye mandate kwa namna inavyofaa. Isitoshe kama mjumbe akiamua kujigharamia katika mkutano huo na akakataa kuchukua posho ya kujikimu kwani analazimishwa kuchukua?

Hiyo mikutano mikuu ya tawi hadi wilaya haihitaji posho kwa sababu mjumbe anaweza kwenda kuhudhuria mkutano na kurejea nyumbani siku hiyo hiyo bila kulazimika kulala.

Posho ya kukikimu hulipwa pale mjumbe anapolaka nje ya nyumbani kwake hivyo kwa chama chenu mkutano wa ngazi ya mkoa kwa baadhi ya wajumbe wabaotoka wilaya za mbali wanalazimika kulipwa posho za kujikimu.

Hizo posho watakazolipwa wajumbe wa mkutano mkuu wamo pia wale watajaompigia kura Lissu.

Kila ngazi ya chama ina mamlaka ya kufanya maamuzi juu ya jambo lililo mbele yake kwa kufuata taratibu zao walizojiwekea sio kufuata porojo za kila mpumbavu mtandaoni anawaza nini.

Kujua kubonyeza key board haimaanishi kichwani pia akili za kudadavua mambo zimo.
Huyu alitaka Wajumbe wa Mkutano Mkuu wakalale Benjamin Mkapa Stadium.

Wanasheria wanaomuunga mkono Lissu wameshindwa hata kumchangia 50,000 wamebaki kupiga domo tu.
 
Pesa za mbowe kaiba kwenye A/C ya chama ni pesa za chadema, Lisu achangishe vipi wakati anajua Mbowe kaiba pesa za chama na anazitumia kugawa kwa wale wabunge 19 haramu na chawa wake waje kumsaidia kuiba kura na uchakachuaji
 
Siasa ni pesa hata pale USA Trump katumia hela kibao,na wanakuambia kama hauna hela utaishia kuimba rushwa rushwa na kumlaumu shetwani.Bila pesa vyama haviendi,mdio maana JK Nyerere aliamzisha miradi ya vyama
Vyama vingine pesa huwa ya wote lakini chadema pesa huwa ya mbowe peke yake na kula na chawa wake kikundi cha propaganda uzushi fitna uchakachuaji na mambo yote ya hovyo
 
Mbowe alizoea chaguzi zote anapita bila kupingwa, safari hii kaona cha moto, pesa zote alizokwapua kwenye chama zitaliwa na chawa wake mpaka akome
 
Kwa hiyo kazi ya kiongozi ni kupiga domo kama Tundu Lissu?
Domo lipi Lisu kapiga? Kama Domo Mbowe anapiga na sasa wenje anapiga Domo la kuwavua nguo nyie chawa mbowe na boss wenu mwizi wa pesa za chama
 
Kwa hiyo kazi ya kiongozi ni kupiga domo kama Tundu Lissu?
Mafisadi muda wenu umewadia kutuliza wenge.
Mbowe kila akichangia anaandika ni mkopo ruzuku ikija analipwa, hajawahi ku hangia bure kwani hulipwa hadi riba
 
Hicho unachoita mpango kazi sio kuwa ninakifahamu bali maisha yangu yote ya kazi kuandaa mpango kazi ni sehemu ya kazi yangu kwa hiyo ninafahamu kuliko wewe unayekariri. Mpango kazi unaendana na bajeti na kila ngazi ya uongozi ina majukumu yake na bajet yake na mpango kazi wake.
Kama unaelewa, ulikuwa unaleta chokochoko za nini sasa...?

Sasa niambie, kwenye kipengere cha "kugharamia mkutano mkuu wa uchaguzi mwaka 2024" bajeti yenu inasema source ya funding ya mkutano huo itatoka wapi? Wajumbe wa kamati kuu kutoa pesa zao toka kwenye mfuko yao? Huo unadhani ni utaratibu mzuri? Is it sustainable?
Katika ngazi ya tawi, jimbo, wilaya pesa inayihitajika siyo kubwa kwa sababu hakuna mjumbe anayelipwa pesa ya malazi; mjumbe anakuja na kurudi nyumbani kwake.
Kwa hiyo fedha ktk ngazi hizi hahitajiki? Is this what you mean....?
Pili uongozi wa ngazi hizo ni jukumu lake kugharimia uendeshaji wa ofisi kwa ngazi hiyo hata kama sehemu ya bajeti yake inatoka hq.
Hapo ☝🏻☝🏻☝🏻 juu umesemaje kwani?

Si umesema hazihitajiki pesa kwa kuwa wajumbe kama kuna shughuli au kikao makao makuu ya jimbo au wilaya au mkoa au kanda basi watakuja na kurudi kulala makwao?

Sina hakika hata kama unajua unacho argue hapa Ndugu RMC a.k.a bwana mipango a.k.a Mr Planning Officer...

Well: Chukua mfano kanda ya Victoria anayoingoza huyo dalali wenu wa rushwa za Abdul Mr Wenje...

Kanda hii ina mikoa mitatu: Mwanza, Geita na Kagera. Kwa hiyo kama kuna kikao cha kanda huko Mwanza cha siku mbili wajumbe wa Bukoba, Ngara, Chato, Biharamulo watakuja Mwanza kwenye kikao na "watakuwa wanarudi kwenda kulala makwao, au siyo..?

Sikiliza bwana RMC, HQ inatakiwa kubakiwa na 20% tu ya mapato ya chama and the rest (80%) lazima kishuke chini ambako ndiko kwenye watu na wanachama na shughuli za chama zilipo...

Huu ujinga wa kusema HQ ina shughuli nyingi muache. Maana hakuna cha shughuli nyingi wala nini bali ni pesa kulipa madeni hewa ya kutengeneza kama haya mnayosema "wajumbe wa kati kuu wamekubaliana huyu atafute milioni 20, yule 30, yule 50 nk na eti mwenyeki Freeman Mbowe eti 250M...

Hizi pesa zinatolewa na ma CCM kama rushwa kwenu, baadaye mnazidai kulipwa kama madeni yenu. Kama mnafikiri haijulikani, mnajidanganya...
Suala la kuchangia si la lazima kwa mwanachama kwa sababu kwanza linategemea uwezo wa mwanachama na inategemea anavyoguswa.
Umesikiliza interview ya Hezekiah Wenje Wasafi TV & radio leo....?

Unageuka na kudanganya tena..?
Hiyo idadi ya wanachama inaweza kuwa sio sahihi na ilikuzwa makusudi au hata kama ni sahihi ni historical sio updated. Mtu anaqeza xkuwa mwanachama wa chama fulani kisha kuacha kimya kimya.
Idadi gani ya wanachama? Nani kaitaja hiyo idadi..?

All in all, CHADEMA ina wanachama, wapenzi na mashabiki mamilioni Tanganyika na duniani kote. Chama hakiwezi kukosa pesa hata bilioni kadhaa kama tuna uongozi thabiti, credible na unaoaminika...

Chama kipo kwenye ukata hata kuwa vulnerable kwa fedha za rushwa za Abdul na mama Abdul wa CCM kwa sababu wanachama hawauamini uongozi huu tena chini ya Freeman Mbowe na kwa hiyo hawawezi kutoa pesa zao kuliwa na kikundi kidogo cha huyu bwana....!


Busara ya kawaida kama kamati kuu nzima imepotoka kama Lissu na nyie mnaomshabikia blindly mnavyoamini basi ufumbuzi ni kujitenga na kuanzisha chama chenu ili sasa kiyafanye hayo yaliyo sahihi. Hao mnaodai wananchi watawafuata huko mtakakoenda.
Kama kamati kuu imepotoka, suluhu sio kukimbia wala kuanzisha chama bali ni kukubali kuwa liko tatizo na ni vyema litatuliwe kwa haraka..

Na tatizo liko very clear. Ni tatizo la leadership chini ya uenyekiti wa Freeman Mbowe...

Tundu Lissu hatakimbia wala sisi wafuasi wake. Tutapambana na tutarekebishana humohumo ndani hata kama ikibidi kwa kutumia ngumi na mijeledi..

Lazima chama kirudi kwa wanachama. The time is now...!!

9
Hairatokea kamati kuu ikae kujadili jambo kwa kufuata maoni ya mtandaoni tena ya watu wenye poor reasoning.
Mjinga wewe. Na hata hizi fikra ni za kijinga pia...

Mitandao ni njia ya mawasiliano...

Kinachosemwa mitandaoni ndicho hicho kilicho kwenye field...

Kutokufanyia kazi mawazo hayo ni ujinga wa upumbavu wa viongozi tu...!!
 
Marehemu???

Nilikuwa naangalia interview yake aliyofanya Wasafi.

Sema nilichogundua waandishi wa pale uwezo wao ni wa wastani sana katika kuhoji watu maswali.

Kuna maswali ambayo wameyauliza kirahisi na mengine hawajayauliza kabisa.

Ndio maana kwangu kuna waandishi watatu tu kwenye hiyo field ya maswali ambao wanafanya poa.
Wenje kanunua kipindi kile ikabidi waende sambamba na ujinga wa wenje
 
Back
Top Bottom