Wanabodi,
Naomba kuanza na angalizo!
Simple Mind Discuss People
Ordinary Mind Discuss Events
Great Minds Discuss Ideas。
Hili ni moja ya mabandiko yangu ya kiutu uzima,ya ku discuss ideas, hakuna kutaja majina,wala ku discuss watu!。
Naomba wachangiaji tujadili hoja tuu ya msingi bila kutaja jina la mtu yoyote,na ikitokea ukajisikia kuwashwa washwa kutaja majina,wewe ujijue bado ni mtoto,bandiko hili sii saizi yako,nakuomba jipitie zako kimya kimya,nenda kwenye mabandiko ya saizi yako!,na nimuombe mode,turudishe ile nidhamu ya jf ya zamani, ukiona mtu yoyote kataja jina lolote kwenye bandiko hili,futilia mbali hiyo post,tuanze kurudisha ile jf ya enzi zile,watu wanakata issues hivyo kutenganisha mambo kikubwa na mambo ya watoto。
Hili ni bandiko la swali,huu ni mwaka wa uchaguzi,kuna vitu tumekuwa tunaviomba vifanyike kabla ya uchaguzi wa mwaka huu wa 2025, mpaka sasa tumeingia mwaka wa uchaguzi,badhi ya vitu hivyo,vimefanyika,baadhi vimefanyika but not the right way,na vingine havijafanyika kabisa ikiwemo the most important,mabadiliko madogo ya katiba。
Kwenye hli la katiba,minimum reforms, limepelekea mimi kujiuliza,hivi Inawezekana ni kiburi na jeuri ya serikali kuwa hatufanyi,inawezekana ni kiburi na jeuri ya wasaidizi wake sheria,hawajamwambia ukweli wa the legal status ya katiba yetu na sheria yetu ya uchaguzi,au ameambiwa na ajua ila ameamua atafanya kwa muda wake, ila mkilizimisha ndio sifanyi,kwani nisipo fanya, mtanifanya nini?。
Na kwavile na kiukweli kabisa katiba yetu ya JMT,inamruhusu kufanya jambo lolote,au kutofanya jambo lolote na asiwe amefanya kosa lolote kwasababu,katiba yetu imemruhusu,anaruhusiwa kushauriwa tuu na yeyote,lakini kwenye kufikia maamuzi,atafikia maamuzi yeye mwenyewe kama yeye,halazimiki kufuata ushauri wa yeyote,na maamuzi yake hayahojiwi na mamlaka yoyote!。
Na hata ikitokea akafanya maamuzi yoyote kwa makosa ya kisheria,kikanuni na kiutaratibu,tumempa kinga ya kutokushitakiwa popote,unless kama makosa hayo ni makosa ya ukiukwaji na uvunjaji wa katiba ya JMT,then anashitakiwa kwa mujibu wa Ibara ya 56A ya katiba。
Je ni mara ngapi viongozi wetu wamekiuka katiba,wamekanyaga katiba,wamevuja katiba bila kufanywa chochote?!。
Tena imefikia mpaka kiwango cha Mahakama Kuu ya Tanzania,imetoa uamuzi na imetamka wazi jambo fulani ni kinyume na katiba,lakini bado viongozi wetu wanalitenda!,wanakanyaga katiba,wanavunja katiba,wanakiuka katiba na hawafanywi lolote!itakuwa haya ya kusema tuu humu, kuandika magazetini na kwenye mitandao, itasaidia?.
Au inawezekana ni kweli kabisa yuko real very busy sana,na hapati kabisa muda wa kutusoma?,kututazama na kutusikiliza,awategemea zaidi wasaidizi wake tuu!,wamsomee,wamtazamie na kumsikilizishia,na hao wasaidizi wake nao ikatokea na wao pia wako too busy sana,hawajapata kabisa
nafasi ya kumwambia ukweli wa ubatili wa katiba yetu na ubatili wa hii sheria yetu mpya ya uchaguzi aliyoisaini mwaka jana ambayo ndio tunakwenda kuifanyia uchaguzi wa mwaka huu, kuwa ni sheria batili inayokwenda kinyume cha katiba ya JMT?.
Kuna vitu vya ajabu ajabu vya kisheria vinavyofanyika nchini mwetu, ukiwa ni mwanasheria, ni vigumu sana kuvielewa, kama hili la ubatili wa katiba na ubatili wa sheria yetu ya uchaguzi!.
Mahakama Kuu ya Tanzania, imetoa uamuzi kuhusu ubatili wa sheria ya uchaguzi, tukaamua kutunga sheria mpya ya uchaguzi, wanasheria nguli, wabobezi na wabebovu wakatungaje muswada wenye ubatili ule ule?!.
Tuliposhirikishwa kwenye hatua zote tatu, kwenye kukusanya maoni ya wadau, kuna watu tulisema,
Kabla ya muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, tukaitwa kutoa maoni, tukasema
Na baada ya muswada kusomwa kwa mara ya kwanza, tukaitwa kutoa maoni Bungeni Dodoma, tukasema
Sheria ilipokuja kutoka, ina ubatili ule ule mtu unajiuliza Bunge chini ya mwalimu nguli mbobezi na mbobevu wa
sheria. linatungaje sheria batili kinyume na katiba?!. Halafu bila aibu, anapelekewa kusaini!.
Kwenye hili la ubatili wa katiba na ubatili wa sheria, nimesisitiza mtu asiye
mwanasheria hawezi kuujua
ubatili wa katiba au ubatili wa sheria, bila kuelezwa na wanasheria!, hivyo inawezekana mpaka ninapoandika hapa, mwenyewe wala hajui tuna katiba batilifu, wala hajui ametungiwa sheria batili, na yeye kuisaini bila kujua ni batili!.
Hivyo kumlaumu mtu kama huyu ni kumuonea bure tuu,kumbe masikini wa watu yeye wala hajui?!。
Kwa vile huu ndio mwaka wa uchaguzi,something must be done kuhusu hii sheria mpya ya uchaguzi,ni sheria batili kwasababu ina vifungu fulani batili,viko kinyume cha katiba ya JMT,ya mwaka 1977
Mahakama Kuu iliisha utangaza ubatili huo ni kinyume na katiba!。
Serikali ikauchukua ubatili huo,ukauchomekea kiubatili ndani ya katiba yetu,ili sasa ule ubatili wa sheria ya uchaguzi,uliotangazwa na Mahakama Kuu,kuwa ni batili,sasa umehalalishwa kwasababu ubatili huo sasa umechomekewa ndani ya katiba yetu!.
Mahakama Kuu ikakomaa kuwa sheria hiyo ni batili,na uchomekeaji wa vifungu hivyo batili ndani ya katiba yetu, nao umefanyika kiubatili!.
Mahakama ya Rufani,ikakiri ubatili huo,ila kwa vile sasa ubatili huo,umechomekewa ndani ya katiba yetu,upo ndani ya katiba, hata kama uchomekeaji huo umefanywa kiubatili, lakini upo!, na aliyechomekea ubatili huo ni Bunge letu tukufu!,kwa kuliheshimu Bunge, Mahakama ya Rufaa, ikaamua,Mahakama haiwezi kuliingilia Bunge katika jukumu lake la kutunga sheria,hivyo mpira huo wa ubatili wa katiba na ubatili wa sheria, ukarudishwa mezani kwa Bunge,liuondoe!。 Bunge likatia mpira kwapani na kula kobisi mpaka leo hii ninapoandika hapa!,ubatili huo bado upo ndani ya katiba yetu!,tumetunga sheria mpya ya uchaguzi yenye ubatili ule ule sasa tunajiandaa kufanya uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa katiba batilifu na sheria batili!。Je tufanye nini?.
A Way Forward
Ikitokea this time akaliona bandiko hili na kuvisikia vilio hivi, naendelea kusisitiza kuna kufanya, jambo zuri, doing the right thing, amefanya makubwa mazuri mengi!, na tumemoongeza sana!.
Ila.kwenye dunia ya sasa ya utandawazi na usasa, doing the right thing, is not enough, one has to do the right thing, at the right time and do it right!. Kuna vitu amevifanya ni right thing lakini havijafanyika the right way!
Nashauri
- Muda uliopo unatosha,kufanya minimum reforms za katiba kwa hati ya dharura,kuucholopoa huo ubatili uliochomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu na kuifanya iwe ni katiba safi na halali。
- Sheria mpya ya Uchaguzi,is the right thing done on a wrong way!, sheria hii ifumuliwe,vile vifungu batili viondolewe,kila Mtanzania awe huru kupiga kura kumchagua kiongozi anayemtaka kwa mujibu wa ibara ya 5。Kwa sasa Mtanzania hayuko huru kumchagua kiongozi anayemtaka,analazimishwa lazima amchague kiongozi aliyeletewa na chama cha siasa!.
- Ibara ya 21 yakatiba irekebishwe kila mtu aruhusiwe kugombea uongozi,kwa sasa Mtanzania haruhuhusiwi kugombea uongozi,analazimishwa kwanza ni lazima ajiunge na chama cha siasa,hicho chama ndio kimdhamini,ndipo aruhusiwe kugombea uongozi wa umma, matokeo yake tunawakosa watu wazuri, watu makini kutuwakilisha huku tukijaza mazagazaga na matutusa kule kwenye vyombo vyetu vya uwakilishi,matutusa na mazagazaga mengine kazi yao ni kugonga tuu meza kupiga makofi na kusema ndiooo!,nawengine haswa wale wa vitu maalum,wako pale kwa kazi maalum!,tungekuwa na watu makini mule wa kutosha,yale madudu ya ajabu ajabu yaliyopitishwa mule yasinge pita kwa mserereko kivile!。
- Watanzania walitaka Tume Huru na Shirikishi ya Uchaguzi,na sio kuibadili tuu jina kutoka Tume ya Uchaguzi NEC,kuwa Tume Huru ya Uchaguzi INEC,lakini tume ni ile ile,watu ni wale wale!. Tume Huru ya Uchaguzi is the right thing,tuirekebishe,isukwe upya na iwe shirikishi!。
- Creation of level playing field kwenye the game of politics。
Watanzania tunatakiwa tutafakari kwa pamoja,tufanye nini ili kupata haki zetu za msingi za kidemokrasia na uchaguzi wa 2025 ukawa uchaguzi huru na wa haki?
Paskali