Jamaa yangu ananitesa kisa alinitafutia kazi, ni haki?

Mbaya zaid wanafanya kazi sehemu moja, ningekuwa mm yaani ningeanza kutembea na bible kila niengapo, jamaa angejitenga na mm bila kupenda, maana kama tunakuwa kwenye usafir labda kanipa lift mm ni mapambio kwa kwenda mbele.
Kabla gari haijaondoka unamwambia tusali. Hamjakaa sawa unamsimulia kisa cha Absalomu mwana wa Daudi🤣Yeye mwenyewe ataanza kukukimbia
 
Acha hiyo kazi aliyokutafutia, tafuta kazi nyingine wewe mwenyewe.


Ukihisi huwezi basi jua jamaa anastahili kujimwambafy
 
Tafuta kazi nyingine. Ni rahisi kupata kazi ukiwa na kazi
 
Inategemea mshahara wako ukoje kama unaweza mpe laki mbili halafu achana naye. Akiendelea kukwambia mtoke mwambie toka na mkeo!
 
Mimi nadhani hujui kula na kipofu,kuna jamaa yangu ana mshahara mkubwa tu na tena anaweza nizidi mshahar mara nne au tano,ni mambo mengi nimemsaidia kabla hajapata hiyo kazi,na yeye husema hivo,amenisaidia kutafutia ajira kwa ndugu zangu zaidi ya sita na wanapiga kazi,mizinga kwa ndugu zangu haishi na hata kwangu.


Sioni shida wala kunungunika kwani yeye si ndugu wala mzazi wangu kwa wema alotenda kwangu,huwa namsaidia awapo na shida


Nakushauri kuwa vumiliia,msaidie uwapo na nafasi na kama huna nwambie,usioneshe jeuri kwake ,maisha hayana mbabe
 

Temana nae
Mungu husaidia watu kupitia watu yeye sio Mungu kwahiyo asiwe na mamlaka makubwa kila siku ya Mungu hata yeye kuna mahala alisaidiwa
 
Acha kunywa pombe. Kumbuka ulikotoka mwambie rafiki yako umeamua kuacha pombe Anza kuhudhuria ibada mara kwa mara. Especially ukienda usabato kule utakuepo salama kwasababu hakuna ukiritimba wa michango mingi. Ukiendelea hivyo hivyo utakuepo mtumwa wake wa rafik yako
 
Hii kali sasa daah [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
ndo hvo ss unafanyeje kujitenga na mtu kama huyo, akiniomba hela nafungua bible namsomea kuhusu fungu la kumi na malimbuko, nampa ufafanuzi kwamba tunatakiwa kuwasaidia wenye uhitaji na sio ambao hawana, namwambia wewe una kazi kwa hyo unatakiwa kusaidia na sio kusaidiwa, namtaka tuende kwenye kituo cha watoto yatima kutoa msaada mshahara ukitoka, hajakaa sawa namwambia hata pombe, soda, juice etc anatakiwa kuacha awe anakunywa maji tu, mbona ataniona kama nimechanganyikiwa na atanikimbia mwenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…