Je, kuna faida gani ya kuwa na mikutano ya vyama vya siasa baada ya uchaguzi?

Hii nchi inawapuuzi wengi sana,ndo maana haiwezi kuendelea,...swali kwako mikutano inazuia vip chama kilichopo kufanya maendeleo
 
Hii nchi inawapuuzi wengi sana,ndo maana haiwezi kuendelea,...swali kwako mikutano inazuia vip chama kilichopo kufanya maendeleo
hapo upuuzi uko wapi ?
 
Ccm wamejaa hofu baada ya mikutano kuruhusiwa na hali itakuwa tete zaidi kwa baadhi ya wabunge baada ya mkutano wa Furahisha
 
"Mzoea vya kunyonga vya kuchinja haviwezi"jambo moja unalotakiwa kujua KATIBA ni sheria mama jambo lililokubalika ndani ya katiba hakuna wa kubatilisha na ukiona kiongozi anabatilisha yaliyomo, jua kuwa hayo ni matumizi mabaya ya madaraka.Ili kubatilisha jambo ndani ya katiba unapelekwa mswaada bungeni kufanya marekekebisho ya katiba na si kwa mihemuko kama yako.
 
Lengo la Mikutano ya Vyama vya Siasa ni:-1.Kuikumbusha Serikali pale inapojisahau katika ahadi ilizotoa wakati wa kampeni.2.Kujenga vyama na mifumo imara.3.Kuimarisha mshikamano na Umoja kwenye Vyama vyao.4.Kurekebisha kasoro kubwa na ndogo ambazo zinakiathiri chama husika.5.Kujua dira,maendeleo na mapungufu ya chama.
 
Lengo la Vyama vya siasa siyo kusubiria uchaguzi tu,bali ni kuwa na sera mbadala ambayo kwa namna moja au nyingine itawasaidia Wananchi wa nchi husika kuelewa matatizo yao na kujipanga kisawa sawa ili kuikabili Serikali iwapo imeshindwa kuwahudumia wananchi na pia kufanya Serikali isilale kama Serikali ya Magufuri ilivyokuwa imelala.
 
umeeleweka
 
Katika Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977:-
1.Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.(Ibara ya 1)
2.Jamhuri ya Muungano ni nchi ya KIDEMOKRASIA na ya KIJAMAA,isiyokuwa na dini,yenye kufuata MFUMO WA VYAMA VINGI VYA SIASA(Ibara 3(1)
3.Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayoofuata Misingi ya Demokrasia na Haki ya Kijamii,na kwa hiyo:-
(a)Wananchi ndio msingi wa mamlaka yote,na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii
(b)Lengo kuu la Serikali litakuwa ni USTAWI WA WANANCHI
(c)Serikali itawajibika kwa Wananchi
(d)Wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.(Ibara 8(1)(a-d)
4.Lengo la Katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au wa chochote kati ya vyombo vyake na udugu na amani kutokana na kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea,ambayo inasisitiza utekelezaji wa Misingi ya Kijamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika Jamhuri ya Muungano.Kwa hiyo ,Mamlaka ya Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza Sera na Shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha:-
(a)Kwamba Utu na Haki nyinginezo zote za Binadamu zinaheshimiwa na kuthaminiwa
(b)Kwamba Sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa
(c)Kwamba Shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba UTAJIRI WA TAIFA unaendelezwa,unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya Wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia kumnyonya mtu mwingine
(d)Kwamba Maendeleo ya uchumi wa Taifa yanakuzwa na kupangwa kwa ulinganifu na kwa pamoja
(e)Kwamba Kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi,na KAZI maana yake ni shughuli yoyote ya halali inayompatia mtu Riziki yake
(f)Kwamba Heshima ya Binadamu inahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata Kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu Haki za Binadamu
(g)Kwamba Serikali na vyombo vyake vyote vya umma vinatoa nafasi zilizo sawa kwa Raia wote,wake kwa waume,bila ya kujali rangi,kabila,dini au hali ya mtu
(h)Kwamba Aina zote za Dhuluma,Vitisho,Ubaguzi,Rushwa,Uonevu au Upendeleo zinaondolewa nchini
(i)Kwamba Matumizi ya Utajiri wa Taifa yanatilia mkazo maendeleo ya Wananchi na hasa zaidi yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha Umaskini,Ujinga na Maradhi
(l)Kwamba Shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia zinazoweza kusababisha Ulimbikizaji wa Mali au Njia kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi
(k)Kwamba Nchi inatawaliwa kwa kufuata MISINGI YA DEMOKRASIA NA UJAMAA.(Ibara 9(a)-(k)










0
 
Reactions: RNA
Kunq haja ya kuweka muda wa kuruhu mikutano
 
tumepata faida gani leo ?
 
Ukitafuta faida huwezi kuipata Ila ni Ajira za watu na matumizi mabaya ya pesa na Muda Wa watu
 
Hizi ndio itikadi za Bwana enu na genge lake LA kuamini akishinda basi yeye afanye anachotaka Sasa juu Yao Kuna muumba keshaamua ugomvi ule.
Kwa bahati mbaya kawaacha nyie msiojitambua, mwenyezi kamuumba binadamu na masikio mawili ili asikie kushoto na kulia. Mkutano ni fursa ya kusikia Yale nyie msiotaka kuyasikia. Wananchi wanayohaki ya kusikia na wasiochaguliwa kwa hila zenu. Nyie mnaamini vitu sie tuna taka maendeleo ya watu.
 

Labda ili swali ligeulizwa kwa watunzi wa katiba na tunajua research zilifanywa kabla ya hivyo vipengere kuwekwa je wewe umefanya research au unabishana na researchers? Just curious bruh.
 
Ukitafuta faida huwezi kuipata Ila ni Ajira za watu na matumizi mabaya ya pesa na Muda Wa watu
Kukiwa na mikutano ya siasa Machinga wanauza sana,mama ntilie wanapata faida sababu watu wanahitaji kula,Wenye baa na mahoteli wanaingiza pesa kibao,boda boda na daladala pamoja na bajaji siku hiyo wanapata faida kweli,wenye masheli au vituo vya mafuta siku hiyo wanauza kweli kweli na kufanya mzunguko wa pesa mtaani kuwa mwingi.
 
Inabidi katiba ibadilishwe ili huu upuuzi wako uweze kutekelezeka kisheria.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…