Jeshi la Polisi: Bado tunamsubiri Tundu Lissu na dereva wake ili kufanya uchunguzi

 
Duh!

Kwa hiyo victims ndio mashahidi wakuu, endapo wangevuta na uchunguzi nao ungejifia hapo...
 
Kuhusu malipo si aliwah kutuambia kwamba serikali ya Samia imemlipa fedha zake zote
 
Mengine unaachana nayo tu ilimradi uzima upo
Ni kwa maslahi ya Taifa kwa kufikia mwisho wa hili, ambalo ni tukio la kutisha zaidi kuwahi kutokea kwenye Makao Makuu ya Nchi yetu.

Kushambuliwa kwa Mbunge wa JMT akiwa Bungeni sio jambo dogo,ni jambo lililotia dosari Nchi yetu ya amani na upendo.

Lazima tupate closure kwenye hili, hata kama waliotenda watakuwa wamezikwa pembeni ya Ziwa.
 
Jeshi la polisi limesema bado linaendelea kumsubiria mwanasiasa huyo na dereva wake ili wawakamate na kuwahoji namna tukio lilivyotokea
Kadiri siku zinavyokwenda ndivyo ninavyozidi kupata ufahamu namna hawa Wapinzania wanavyoshughulikiwa ili wadhalimu waendelee kuwatafuna jasho la Watanzania.

Inashindikana nini kwa jeshi la Polisi kuomba kupata maelezo ya mhanga wa tukio kutoka Ubeligiji bila kuathiri usalama wake? Interpol inaweza kutumika kuomba jeshi la polisi Ubeligiji wakaweka mazingira ya mahojiano baina ya Lisu na Polisi Tz kupitia hata njia za kidijitali au akatumwa afisa upelelezi kule akachukua maelezo kiaha akarudi nayo ili kazi iendelee.

Nilishaanza kuamini uhusika wa mamlaka kwenye hii kadhia. Afrika isiwaue thinktanks wake. Isiue wapinzani wake bali iweke mazingira ya kupambanisha fikra kwa maendeleo ya Afrika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…