JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

Ili tujue ukweli ni vema tusikilize upande wa pili.

Kuna stori moja ya jeshini ningeweka ila basi tu, kuna wakati watu huonewa sana kwa kisingizio cha nidhamu ya kijeshi
Jambo la muhimu ni msingi wa haki yenyewe. JKT huwa wak straight tangu siku ya kwanza kwamba hawatoi Ajira ila watu huwa wanaenda kucheza kama kamali tu.

Labda kama kuna haki tofauti wanadai.
 
Siwafundishi kazi, bali naamini taalamu yenu inawataka mfanye hivyo na si kuishia kupata taarifa za upande mmoja tu kwa maana ya maelezo ya viongozi wa Jeshi na serikali tu bila kuwahoji Vijana waliofukuzwa.

Wateendeni haki hawa vijana ili umma uweze kuwahukumu kwa haki maana teyari wameshaitwa waasi(sifa mbaya sana katika Jamii na kila watakokwenda).

Mazingira ya kufukuzwa hawa vijana, kwa mtazamo wangu, hayana tofauti na mazingira ya wale vijana waliofukuzwa UDOM na hayati Magufuli mwaka 2017.

Yangu ni hayo tu.
Mkuu jkt toka lini kukawa na ajira? Kule huwa ni kujitolea mkuu .
Afadhali serekali ingeongeza nguvu , vijana wawe wanaenda veta kupata ujuzi kuliko huko kwenye upuuzi Wa jkt , kule Hua ni kwenda kupoteza muda Tuu,
Alafu Kazi Ya jeshi Hua ni kufuata amri tu Ya viongozi ukikaidi unakua ni uhain na unatimuliwa
 
Jambo la muhimu ni msingi wa haki yenyewe. JKT huwa wak straight tangu siku ya kwanza kwamba hawatoi Ajira ila watu huwa wanaenda kucheza kama kamali tu.

Labda kama kuna haki tofauti wanadai.
Kuna fitna kule usione watu wako na uniforms ukadhani wamepata kirahisi.

Walikuwa 2400 sasa wamepunguzwa 800+ inawezekana jeshi limefanya analysis limegundua halitaweza kuchukua wote 2400 sasa linawatoa kwenye reli kijanja.
Hii nchi usiichukulie poa vimemo kila kona mkuu
 
Hata tafsiri ya askari kuasi nadhani ipitiwe upya.
Askari wanaonewa sana kuanzia kwenye maslahi, maisha yao ya kiutumishi n.k
Lakini wahusika mara zote wanawambia wakihoji watashtakiwa kwa kuasi, hili neno limekuwa ni kichaka cha kunyanyasa watu huko majeshini, watu wanahamishwa kwa fitna, wanapigwa adhabu za chuki lakini hawawezi kuhoji wala kuuliza kwa kisingizio hiki cha kuasi jeshi.

Kuna watu wanadhulumiwa mpaka posho zao zilizowekwa kisheria lakin sentensi ya kuasi jeshi inahalalisha dhuluma hiyo.
CDF ni mzazi kaa na hao watoto hebu wasikilize neno kwa neno, CDF hata ww una watoto, una wajukuu n.k
Wakati mwingine wafuasi wako wanaweza kukupa maneno ya ukakasi ukajua ndio sura halisi ya jambo lakin mengine unaweza usiambiwe.
Ukitaka haki saaana au ukihitaji kutumia akili yako, usiwe mwanajeshi.

Hutaweza
 
Mnarudia wewe na nani..

Wewe hapo jkt ndio nani.

Jf bwana kila mtu ni boss wa idara ya serikali

Ewe boss wa jkt tukuulize basi, kwamba hao wengine waliopata ajira kupitia jkt na wengine wako katika majesh mbalimbali na idara mbalimbali za serikali walipataje hizo ajira
kabla ya kupewa mkataba JKT mnaambiwa kabisa..JKT haitoi AJIRA bali inatoa mafunzo ya uzalendo na kujiajiri..Wewe unaamua kukubali afu usipoajiriwa unalalamika
 
“Tunasikitika kufuta mikataba ya vijana 854 wa JKT kutokana na kufanya vitendo vya uasi.”Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania - Jenerali Venance Mabey
----------



Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jen. Venance Mabeyo amesema wamefuta mikataba ya Vijana 854 wa JKT ambao ni miongoni mwa walioahidiwa kupewa ajira kwa kujenga Ikulu, Chamwino na hii ni kutokana na Vijana hao kufanya uasi kwa kugoma na kuandamana kwenda Ikulu.

Mytake ; Gharama kubwa zilizotumika kuwaandaa hao vijana ili kuja kulitumikia taifa zinarejesChwa vipi?

Orodha na majina ya hao waasi iko wapi ili watanzania wawe makini nao
 
Suala hili likifumuliwa tutaona mengi.
 
Kugoma ni UASI na hiyo kitu ni hatari..emu fikiria Mtu wa namna iyo unamuajiri Awe askari kamili...uyu anaweza kumsikiliza mkubwa wake?..
.na adhabu za kufanya mgomo jeshini kwa askari kamili iwe kukataa amri kutoka kwa mkuu wako adhabu yake uwa ni kufukuzwa jeshini, kufungwa na inategemea wapi umegoma muda mwingine adhabu huwa ni KIFO
 
Mwendazake aliwadanganya watoto wa wenzake huku akiwafanyisha Kazi kama ma cheapest labour kwenye ujenzi kwa ujira wa wali maharage kwa ahadi ya ajira.This is too bad.
 
Kugoma ni UASI na hiyo kitu ni hatari..emu fikiria Mtu wa namna iyo unamuajiri Awe askari kamili...uyu anaweza kumsikiliza mkubwa wake?..
.na adhabu za kufanya mgomo jeshini kwa askari kamili iwe kukataa amri kutoka kwa mkuu wako adhabu yake uwa ni kufukuzwa jeshini, kufungwa na inategemea wapi umegoma muda mwingine adhabu huwa ni KIFO
Uliwahi kuajiriwa jeshini?
Kama hukuwahi nyamaza tu
Kuna watu wanaonewa na wakubwa wao mpaka mtu anakosa uvumilivu anakoki silaha jeshi lisikie kwa watu, kama upo huko basi uko position ya juu huonewi ndio maana uko comfortable
 
Kugoma ni UASI na hiyo kitu ni hatari..emu fikiria Mtu wa namna iyo unamuajiri Awe askari kamili...uyu anaweza kumsikiliza mkubwa wake?..
.na adhabu za kufanya mgomo jeshini kwa askari kamili iwe kukataa amri kutoka kwa mkuu wako adhabu yake uwa ni kufukuzwa jeshini, kufungwa na inategemea wapi umegoma muda mwingine adhabu huwa ni KIFO
Lakini hao sio wanajeshi awajaajiriwa.
 
Uliwahi kuajiriwa jeshini?
Kama hukuwahi nyamaza tu
Kuna watu wanaonewa na wakubwa wao mpaka mtu anakosa uvumilivu anakoki silaha jeshi lisikie kwa watu, kama upo huko basi uko position ya juu huonewi ndio maana uko comfortable
Kiapo kinasemaje bro?
Utatekeleza yale yote utakayopewa na mkubwa wako..kama unaonewa nenda kashitaki kuna sehem za kupeleka malalamiko..hiyo ndo maana ya UTII, UAMINIFU NA UHODARI
We toka uzaliwe ushawahi sikia wapi askari anagoma?
 
Back
Top Bottom