JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

JKT yasitisha Mikataba ya Vijana 854 waliofanya Uasi

Kwa yoyote aliyepita jeshini anafahamu kuwa kosa la KUGOMA AU KUANDAMANA jeshini ni KOSA KUBWA. Ni UASI. Na kila siku tunawaambia kwamba mafunzo ya JKT ni ya kujitolea na sio sehemu ya ajira. Na kwa taarifa yenu vijana waliotumikia jkt na kurudi mtaani baada ya kumaliza muda wao ni wengi zaidi ya hao na wanaendelea na maisha mengine. Watumie skills za jkt kujiajiri na kuzalisha mali. Jeshini ni amri,subra,ukakamavu,uzalendo na uvumilivu
 
Ukisikia baadae watu wamejinyonga ndo hapo .....mtu AME hustle zile SIX WEEK afu anafutwa. Mungu awape moyo wa ujasir
Miaka 3 mkuu sio 6 weeks

Aisee ktk ujinga wanafanya service man ni huu yaani woote uwa wanawaza kuingia Jwtz tu ssa watachukua wangapi wataacha wangapi ata polisi,maliasili wakienda kambini kufanya usaili mijitu inakimbia kujificha eti wanasubiri JW waje wafanye usaili dadek acha WANYOOKE na WATANYOOKA TU
 
“Tarehe 8 Aprili 2021, vijana wa Jeshi la kujenga Taifa wapatao 2,400, walio haidiwa kupewa ajira na Mhe. Rais kwa kutekeleza ujenzi wa ofisi za ikulu ya Chamwino waliamua kugoma, kukataa kufanya Kazi eneo jingine na kuandamana kwenda Ikulu kumuona Mhe. Rais kushindikiza kuandikishwa Jeshi. Mkuu wa Jeshi la kujenga Taifa Meja Jenerali Charles Mbunge kawasihi kusitisha mgomo huo na kutoandamana hawakusikiliza.

Kitendo hiki haikikubaliki, kugoma au kuandamana Jeshini ni kosa la Uasi , wangekua askari wangefikishwa mahakamani kwa sababu hiyo Jeshi la kujenga Taifa limesitisha mkataba wa vijana hao 854 wa kujitolea na kurudishwa makwao.” Jen. Mabeyo


Karibu kitaa walio rudishwa
 
Vijana wajinga sana, Jeshi linahitaji uvumilivu. Ajira kwao lilikuwa ni jambo la muda tu. Huku jeshini kosa la kugoma tu hata dkk moja unakuwa umedisco. Tena bado vijana wadogo sana. Nendeni mkajifunze nidhamu
 
Anzeni kujifunza kutuma post bila kumtaja hayati. Ni ngumu ila mtazoea tu. Inavyoonesha legacy yake imepanga bure vichwani mwenu.

Viva JPM. Haters wako hawaachi kukutaja kwenye post zao huku mitandaoni.
Wajane mna tabu sana.
Naona na wewe umepost bila kumtaja marehemu pombe🤣🤣🤣
 
Nimesoma habari moja kuwa JKT imesitisha mikataba na kuwafukuza vijana zaidi ya 800 baada ya kuandamana Ikulu wakinishinikiza kuajiriwa

Baada ya hao vijana kuja mtaani,wanajua kushika silaha na mafunzo ya awali ya kujihami,je hao vijana hawawezi kujiunga na vikundi vya kigaidi kama cha ISS huko Msumbiji?

Je serikali inawafuatilia hao vijana zaidi 800 mienendo yao mitaani kama sio rahisi kushawishika kujiunga na vikundi vya kigaidi kwa ukosefu wa ajira na kuleta majanga nchini?

Au unaweza ukawa mtego,wakashawishiwa kugoma wadai ajira ili watimuliwe wakajiunga na ISS huko Msumbiji


Serikali ibuni mikakati ya kuajiri vijana au kuwawezesha kupata mazingira rahisi kujiajiri ili kuepuka kushawishika kuvuka mpaka kule kusini na kujiunga na ISS

Narudia kuwatimua vijana 800 JKT ni hatari zaidi kwa usalama uliopo kusini mwa Afrika
Kwani ISS Mozambique wing wametangaza nafasi za kazi?
 
Kwa yoyote aliyepita jeshini anafahamu kuwa kosa la KUGOMA AU KUANDAMANA jeshini ni KOSA KUBWA. Ni UASI. Na kila siku tunawaambia kwamba mafunzo ya JKT ni ya kujitolea na sio sehemu ya ajira. Na kwa taarifa yenu vijana waliotumikia jkt na kurudi mtaani baada ya kumaliza muda wao ni wengi zaidi ya hao na wanaendelea na maisha mengine. Watumie skills za jkt kujiajiri na kuzalisha mali. Jeshini ni amri,subra,ukakamavu,uzalendo na uvumilivu
Naona mkono wa chadema au TLS au wa askofubagonza. I cannot imagine mwanajeshi afanye maandamano unless wamepikwa wakapikika wakadai "haki zao za kikatiba", askofu huziita uhuru na maendeleo. Mlete tundulissu awatetee
 
Hawa kwakuwa tayari wana mafunzo wanaweza kuunda vikosi vya kuasi na wakasumbua sana jeshi na amani ya nchi.Wawe makini sana.Hawa ni hatari kwa usalama wa taifa
JKT wanapewa sehemu ndogo sana ya mafunzo ya kijeshi ndiomaana hata wale wanaopata bahati ya kuajiliwa jeshini lazima waende mafunzo tena

Kumbuka wale vijana waliokufa wakati wa mafunzo pale pwani mwaka Jana tukaambiwa walikula vyakula vyenye sumu mtaani....wale ni miongoni mwa wale vijana wa JKT waliojenga ukuta wa mererani
 
Shida kubwa wengine wanaongea bila kuangalia uhalisia wa mambo na hawajui kinachoendelea kisa uongo uongo adi jeshini. Makosa ya namna ya kuajiri vijana toka jkt ilianza baada ya uongozi wa awamu ya tano kuingia.
Vijana wanapmaliza mafunzo ya miezi sita ya awali walikua wanatawanyishwa kwenye makambi mbalimbali yaliyopo chini ya jwtz kwa ajili ya uzalishaji mali na ulinzi kama sehemu ya malezi.

Wakiwa kwenye makambi ya malezi ndipo jeshi..magereza..usalama..bot..takukuru n.k wanakwenda kufanya recruitment wa vijana hawa kulingana na sifa wanazohitaji pindi wakiwa na uhitaji na kwa kwenda kwenye makambi yote ya malezi.

Shida ikaanzia kipindi cha magufuli; yeye alitoa amri wa kuajiriwa waliojenga Ukuta Marerani lakini waliokua wanalima mpunga Chita..wanaolinda mipaka huko Kigoma na Uganda na Rwanda hakuona kama wanasifa ya kuajiriwa..waliokua wanalima mahindi huko Mgambo Tanga hakuona kama wanastahili kuajiriwa sijui alifikiri wote waje Mererani kujenga ukuta bila kuwepo mgawanyo wa ki majukumu.
CDF na mkuu wa jkt wakajikalia kimya bila kuona kuna upendeleo kwenye ajira.

Watu wenye uwezo wakawapanyika vijana wao humo humo na ikawa rushwa ndani ya jeshi.
Ujenzi ulipoanza tena Chamwino stori ikawa ile ile waajiriwe wanaojenga ukuta..hao CDF na mkuu wa jkt wakawa kimya tu; vijana waliopo makambi ya mbali wakawa na vilio mbona wanaajiriwa wa Dodoma tu? then wenye michongo wakafanya wanavyojua vijana wao wakaja nao Dodoma kwenye ujenzi.

Uchaguzi ulipowadia pia wanachukuliwa vijana kwenda kuaribu uchaguzi kwa upendeleo huohuo kua wataajiriwa.

Sasa leo wanawaona kama wanaketa uasi. Swali ni je kwanini hawakushauri Magufuli kipindi hicho kuhusu ajira? wamwambie kua wao wanataratibu zao za kuwapatia vijana wa jkt ajira?
Mambo ni mengi ngoja niishie hapa.
Umewaza vizuri sana mkuu.
Kuna watu humu kazi yao kuwaponda vijana wameasi wameasi bila kufikiri chanzo cha tatizo.
Alaf askari akiasi harudishwi nyumbani si kuna adhabu za kuuwawa na kufungwa? Mbona hawajafanya ivo?
Hapa ilitafutwa mbinu ya kuwatimua tu.
Walijua kabisa 2400 nafasi hamna kwa vyovyote hawa 800+ tukiwarudisha vikosini lazima wataleta kelele kwahiyo kelele zao zitatupatia mwanya wa kuwafukuza kwa justification ya kuasi.

Jkt imekuwa tofauti sana kama hujaenda kwenye ujenzi basi sahau ajira ilihali kuna watu walibaki vikosini kulima, wako sawa na waliokwenda kujenga sasa kwanini waliojenga ndo wapewe kipaumbele? Shida ilianzia hapa
 
Gharama kubwa zilizotumika kuwaandaa hao vijana ili kuja kulitumikia taifa zinarejeshwa vipi?
Kwani hata ukisoma mpaka kuwa Professor halafu ukafanya makosa unaweza futwa kazi na hata kufungwa .Haijalishi ulitumia gharama kiasi gani mpaka kufikiwa kuwa professor!
 
Wenye madaraka wana roho mbaya sana sijui ni damu za wapi hizo...wakipata wao ajira hawawafikirii wengine hata kidogo zaidi wanatamani kuongeza miaka ya kufanya kazi bila hata kutaka kustaafu ubinafsi tuu umewajaa...
 
Tatizo la mifumo mingi ya kijeshi na kiusalama hasa katika bara la africa huwa hawataki kuhojiwa wala kutaka watu wapate taarifa za ukweli au upande wa pili, Uasi ni suala pana sana hapo ni kwamba walikiuka taratibu za kinidhamu, lakini pia hawa vijana wametumika sana katika mambo mengi, Ukweli ni kwamba pamoja na hili jeshi kuonekana mbele za watu wana sifa mzuri sana, ila ukija ndani yake wao kwa wao kuna michezo yao mingi huwa wanaicheza tatizo hakuna chombo huru kinachoweza kuhoji au kuuliza ila yapo mambo yanahitaji majibu kwa kina pia mabadiliko makubwa yanahitajika katika mfumo wa hili jeshi ili kuendena na dunia ya sasa ilipo kuanzia jkt mpak JWTZ
 
Jambo jingine linalonishangaza ni kuwa vijana hawajui kuwa kuingia jeshini ni kusaini kuwa wakati wowote upo tayari kufa kwa risasi au bomu. Wao nadhani wanafikiri kujiunga na jeshi ni kwenda kula bata ndiyo maana wanalazimisha kuajiliwa.
Wao si wanawaona wenzao wanavyokula bata?
Anyway,wamewarahisishia wenzao waliobaki,kupata ajira fasta.
Jeshi liimarishe intelijensia ya kubaini mambo kama hayo kabla hayajatokea.
 
Back
Top Bottom